Serikali ipeleke hela zaidi seta za uzalishaji sio sekta za huduma.

Tikerra

JF-Expert Member
Sep 3, 2008
1,702
146
Katika siku hizi za karibuni tumeshuhudia trends ambazo ziko disturbing sana.Kwamba sasa sekta za huduma kama elimu ndizo zinazotengewa fedha nyingi zaidi na serikali kuliko sekta za uzalishaji kama kilimo nk.Mambo hayawezi kwenda hivyo.Ninachojiuliza ni kwamba hivi hizo hela za ku-support service sectors zinatoka wapi,maana sekta zetu za uzalishaji ziko hoi?Ni wazi kabisa kwamba ni hivi vimikopo mikopo tunavyopewa na World Bank nk.Sasa nchi haiwezi kutegemea pesa ya mikopo,pesa isiyo zalisha.Ni lazima tuendeleze sekta zetu za uzalishaji,halafu hizi ndizo zitegemeze sekta za huduma.System yeyote inayotegemea mikopo haiko sustainable kabisa.Uchumi wa dunia ume anguka kwa sababu ya mikopo.Tulidanganywa mno na matapeli wa nchi za magharibi kwamba mikopo itatutoa,na kwa ujinga wetu tukakubali,kwamba kweli itatutoa,huu nu utapeli wa kutisha! Mikopo haiwezi kuitoa nchi wala mtu binafsi!Mkopo ni hela hewa.Uchumi wa Iceland uko taabani kwasababu ya kutegemea mikopo.Lazima tuzalishe.Sasa tunataka na sisi tuwe kama Iceland?As a loan bubble grows,it eventually collapses.The loan bubble of the world has collapsed.Tusisubiri zaidi,naomba sasa tuanze kuwa positive thinkers,badala ya kumwaga hela kwenye service sectors,tuanze sasa kumwaga kwenye sekta za uzalishaji,ama sivyo loan buble yetu ita collapse and that is extremely dangerous.
 
Back
Top Bottom