Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 116,476
- 215,295
Magufuli alishawahi kuyakataa malori kwa vile yanaharibu barabara , sasa kama alimaanisha kweli ni wakati wa kuifufua reli .Waifutilie mbali PPRA kutokana na ukosefu wao wa UZALENDO, kitengo hicho kisitumiwe na wafanya biashara wa malori ya kubebea mizigo kipiga vita ujenzi wa reli ya kati?? Wanakuja na horror stories za kutunga tu - mbona katika utawala wa JK hatukuwai kusikia ngonjera za namna hiyo - kumetokea nini hapa katikati, yaani Taifa suddenly tunajifanya hivi sasa reli haina umuhimu wowote!!!
Kuna wakati fulani Mh.Kinana na wengine waliwahi kuwa sceptical na kitengo hiki cha manunuzi ya UMMA, kama Dk.Magufuli anataka kufanikiwa katika malengo yake kwenye sekta nyeti, basi kuna ulazima wa kukifutilia mbali kitengo hiki au kukifanyia reform ya haraka sana - linapo kuja suala nyeti kama ujenzi wa reli watu hawa wasishirikishwe kabisa.
Dk.Magufuli azungumze na Serikali ya China moja kwa moja waone watatusaidia vipi, binafsi nina imani na Wachina kuliko Mataifa ya magharibi, hata Kenya kuna waswahili/viongozi walikuwa wanawapiga vita Wachina wasijenge reli, walikuwa wanatoa visingizio kama vya PPRA lakini Kenyatta aliwapuuzia ndio maana reli inajengwa kwa kasi ya kutisha - ujenzi wa reli ya kati una umuhimu wa pekee Nchini - Dk.Magufuli husikubali watu wenye ajenda zao kukwamisha ujenzi wa reli kwa kutoa visingizio vya kutunga,kila siku wana move/shift goal posts - na mchezo huu umekuwa more pronouced kwenye utawala wako - WHY?
Dk.Magufuli amuombe ushauri Rais Kenyatta au Raila watampa mbinu walizotumia kupata msaada wa Serikali ya China - our lifeline ya kutuwezesha kujenga reli ya kati itapatikana Uchina si pengine - tuwe wakweli hapa, yaani tunashindwa Nchini za Africa magharibi zinazo jenga reli kwa msaada/wataalamu wa China - mfano Nigeria na Cameroon/B.Faso kama sikosei - sisi tuna matatizo gani lakini? We don't seem 2 get our priorities right!!