Serikali inataka nini ndipo taa za Mbeya Intl Airport zijengwe?

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,240
4,466
Uwanja wa Songwe Mbeya, ambao hauishi kujengwa, umekosa taa za njia ya kurukia na kutua kwa ndege mpaka sasa. Hizi taa (runway edge lights) hutumika kuonesha mwisho mwa pembe za barabara ya ndege wakati wa kiza na pale panapokuwa na shida ya kuona hususani kuwapo na mvua au ukungu.

Mwanzoni mwa mwaka huu Fastjet ilishindwa kutua katika uwanja huu na kurejea Dsm mara mbili (nilikuwa mmoja wa abiria katika safari moja, usipime)!!! Gazeti la Mwananchi liliandika habari hii (FastJet yashindwa tena kutua Uwanja wa Songwe)

Ikiwa serikali imeamua kujenga uwanja mkubwa kama ule, na kuufungua bila taa unategemea nini?

Wahusika wanasubiri siku moja kutokee maafa, ndipo taa zijengwe?
 
Mkuu ule uwanja ni "jipu" kubwa sana,watu wamepiga sana pesa pale hasa hapo TANZANIA AIRPORT AUTHORITY,kuanzia Meneja wa mradi mpaka Management ya TAA na Bodi yake.

Na kiukweli Mbeya sio "International Airport", hii inabaki tu kuitwa "Airport",hauwezi kuiita "International" wakati ndege kutua na kuruka mwisho saa kumi na mbili jioni,kutua kwa ndege kunategemea "Sun rise and Sun set".

Hauwezi kuwa uwanja wa Kimataifa wakati hauna mitambo ya kuongozea ndege nyakati za usiku,wakati wa mvua kali na wakati wa ukungu,hauna hadhi hiyo sababu Mbeya sio "Mpaka' yani hauwezi kuwa na International flight ikatua Mbeya na watu wakaonekana wameshafika Tz, sababu pale hakuna "Uhamiaji wala Custom".

Hadhi hiyo haina sababu Songwe hakuna "Jet A-1 Depot",Fastjet ikienda Mbeya ni lazima ijaze "full tank" maana Mbeya hakuna visima vya refueling,sasa haiwezi kuwa hata "Technical Landing" ya ndege zinazopita.

Ndege nyingi zinazopita kwenda kusini mwa Afrika zikipata matatizo ni lazima zije zitue Dsm,wakati zingewez kutua Mbeya na kumaliza matatizo yake.Ule uwanja ni jipu,watu wamepiga hela na wakaufungua kisiasa tu.
 
Wakuu, hata mimi najiuliza: hivi taa za uwanja zinagharimu kiasi gani? maana kuna wakati fastjet wanapata shinda sana kutua hasa nyakati za asb kutokana na ukungu. Kama kawaida yetu, tunasubiri majanga yatokee kisha tuanze kusema "ni mapenzi ya Mungu". Kweli wameshindwa kuweka taa?
 
Back
Top Bottom