Serikali inapokumbuka shuka asubuhi

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Apr 17, 2009
3,517
1,360
Wakati hoja hiyo ikisugua vichwa vya wabunge, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) imesema serikali haitalitelekeza Shirika la Umeme nchini (Tanesco) iwapo litaamua kwenda Mahakama Kuu kuwasilisha pingamizi dhidi ya maombi yaliyowasilishwa Dowans.


Maombi hayo yanataka hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC) isajiliwe katika Mahakama Kuu ya Tanzania ili Tanesco iilipe fidia ya Sh. bilioni 94 kwa kuvunjiwa mkataba wake.


Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa serikali ina kila sababu ya kuisadia Tanesco katika jambo hilo kwa vile shirika hilo ni mtoto wake kwa asilimia 100. "Tanesco wakiamua kwenda mahakamani, si mtoto wa serikali, vipi tumtelekeze?" alihoji Masaju.


Masaju alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa na NIPASHE kueleza nafasi ya serikali kuhusu hatma ya maombi hayo ya Dowans dhidi ya Tanesco yaliyowasilishwa Mahakama Kuu ya Tanzania Januari 25, mwaka huu.


Swali hilo la NIPASHE kwa Masaju lilikuja baada ya Naibu Msajili Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Salvatory Bongole, kuwaambia waandishi wa habari juzi kuwa Tanesco wenyewe na mtu mwingine yeyote, wanaruhusiwa kuwasilisha pingamizi mahakamani hapo.


Masaju alisema mbali ya kuwa Tanesco ni mtoto wa serikali, pia hawawezi kupuuza maslahi ya taifa. "Vyovyote vile, hatuwezi kupuuza maslahi ya taifa hili. Kwani nani hiyo hela haimuumi?" alihoji Masaju.

Aliwataka Watanzania kusubiri kwani iwapo maamuzi ya kupinga maombi hayo ya Dowans mahakamani yatafikiwa, jambo hilo litakuwa bayana mahakamani.
NIPASHE ilipomtafuta Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, William Mhando, kueleza kama shirika lake litaweka pingamizi Mahakama Kuu dhidi ya maombi ya Dowans, juhudi zake ziligonga ukuta.


Badala yake, mwandishi alishauriwa kuwasiliana na Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud, ambaye alipotakiwa kueleza suala hilo, alisema kwa ufupi: "No comment" (Sina la kuzungumza) na alipotakiwa kueleza kwanini hana la kuzungumza, alisisitiza kusema: "No comment."

CHANZO: NIPASHE

Mambo hayo, baada ya kusema kuwa Dowans lazima ilipwe serikali yetu hiihii inabadilika ghafla na kusema kuwa itaingia kuisaidia Tanesco kwa maslahi ya taifa. Kwa nini mwandishi wa habari hakuuliza maslahi ya taifa yamejulikana lini ndani ya ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali ambaye amekuwa akisisitiza kuwa Dowans Lazima ilipwe, kiasi cha kumfanya abadili mawazo yake

Mwanzoni ofisi ilikuwa na mtazamo kuwa Dowans lazima ilipwe na kwa kuwa na msimamo huwo kulikuwa na vigezo fulani vilivyomshawishi AG kuwa na msimamo huo. Vigezo hivyo bado vipo lakini AG kabadili msimamamo AG haoni kuwa hata akishindwa kihalali Wtanzania hatutamuelewa na badala yake tutajua bayana kuwa katusaliti kutokana na msimamo wake wa awali? Kimadili AG hakutakiwa kufanya Uturn ya ghafla hivyo bila hata kujustify sababu ya hiyo U turn.

Kufanya hivyo ( kuwa na misimamo miwili katika issue moja) kimaadili ni kosa. Ndio maana scale of justice ile nembo ya sheria haiko balanced imelala upande mmoja.
 
Yaani sisi watanzania kweli ni mazuzu, serikali hiyo ilisema kwamba lazima ilipe dowans iisaidie tanesco kupinga application ya dowans ni janja tu, serikali na wabunge wa ccm, wote wanajua kwamba there is no loophole in legal techinicaliteis kuepuka kutolipa hilo deni sasa baada ya kuona watu wamechachamaa ndio wanatuuzuga kwamba wamejaribu kupinga malipo lakini wameshindwa ili wawalipe kiulaini bila kelele
 
Unajua Tanesco walishaonyesha nia ya kukata rufaa mara tu hukumu ile ilipotolewa. Lakini Hukumu ile ilipofika ofisi ya AG, Mwanasheria mkuu akasema swala hilo limefungwa, kilichobaki ni kulipa tu. Cha kujiuliza ni kwamba:

  1. AG na Tanesco nani aliyekuwa wa kwanza kuiona hukumu ile ile. Kwa vyovyote vile ni Tanesco, ndo mana walisema watapinga
  2. AG aliposema suala limefungwa, hakuna kupinga hukumu, aliwashirikisha Tanesco? ambao ndo wadaiwa
 
Unajua Tanesco walishaonyesha nia ya kukata rufaa mara tu hukumu ile ilipotolewa. Lakini Hukumu ile ilipofika ofisi ya AG, Mwanasheria mkuu akasema swala hilo limefungwa, kilichobaki ni kulipa tu. Cha kujiuliza ni kwamba:

  1. AG na Tanesco nani aliyekuwa wa kwanza kuiona hukumu ile ile. Kwa vyovyote vile ni Tanesco, ndo mana walisema watapinga
  2. AG aliposema suala limefungwa, hakuna kupinga hukumu, aliwashirikisha Tanesco? ambao ndo wadaiwa

AG anasema atawasaidia tanesco kupinga hiyo award, hatujajulishwa kuwa wao Tanesco wanataka kuipinga, ukimya wa Tanesco sio wa bure, siajabu unatokana na kauli ya mwanasheria mkuu wa serikali kuwa hakuna jinsi lazima kiasi hicho kilipwe.

CC ilipokaa alisema wanasubiri maamuzi ya mahakama walisema hivyo wakijua fika kuwa Tanesco hawana nia au wanavuta miguu kwenye hili suala kwa nini CC kama kweli inajali maslahi ya wananchi wasiiamuru Tanesco ikimbie Mahakama Kuu??
 
Mwisho wao upo karibu sana kama inavyotokea Misri na sehemu nyinginezo kwa wananchi kuingia mtaani na kudai haki zao mpaka kinaeleweka.
 
Unajua Tanesco walishaonyesha nia ya kukata rufaa mara tu hukumu ile ilipotolewa. Lakini Hukumu ile ilipofika ofisi ya AG, Mwanasheria mkuu akasema swala hilo limefungwa, kilichobaki ni kulipa tu. Cha kujiuliza ni kwamba:


  1. AG na Tanesco nani aliyekuwa wa kwanza kuiona hukumu ile ile. Kwa vyovyote vile ni Tanesco, ndo mana walisema watapinga
  2. AG aliposema suala limefungwa, hakuna kupinga hukumu, aliwashirikisha Tanesco? ambao ndo wadaiwa

Ukifuatilia sana, inaonekana CCM taratibu inaanza kuzinduka kwamba watanzania hawalikubali hilo la DOWANS, hiyo moja lakini pili, wameachana na ushauri wa akina Makamba na Sheikh Yahya, na sasa hivi wamerudi kutaka ushauri wa wasomi wao, wanaojua kuangalia alama za nyakati. inaonekana DOWANS, pamoja na machungu yake, ina jambo moja jema sana, nalo ni kuwa-mobilise watanzania wote katika issue moja. kitu ambacho CCM wanaogopa kuliko hata njaa, (kukosa ruzuku).

baada ya taarifa ya CC yao, kukaanza kuvuja taarifa za kwamba si kweli CC walisema alivyosema katibu mwenezi Chiligati!!, baadae tukasikia kwamba wabunge wa CCM wamegomea hilo na kwamba JK naye anagomea hilo la kuilipa DOWANS. na kwa taarifa hii ya AG kwamba anakumbuka kwamba TANESCO sio yatima, wakati Ngeleja alishatamka kwamba TANESCO watalipa wenyewe na sio serikali. sasa inaonekana serikali taratibu inabadili msimamo wake kujiweka mahala pa kuigomea DOWANS. hii inaonesha kwamba pressure inafanya kazi. ila wasoma alama za nyakati watakuwa wameishauri serikali kwamba iwe makini. katika mazingira ya Tunisia na Misri, na wengineo kama hao, ni hatari kuanza ubishi wa kitaifa kama huu, wakati vigezo vyote vya Tunisia na Misri vipo pia hapa Tz: kupanda gharama za maisha, hakuna ajira, ufisadi uliokithiri, ombwe la uongozi, nk.
 
inabidi wananchi waambiwe ni kitu gani kimeifanya serikali ibadili mawazo, wasipofanya hivyo itaonekana dhahiri kuwa ni fix za serikali
 
Ukifuatilia sana, inaonekana CCM taratibu inaanza kuzinduka kwamba watanzania hawalikubali hilo la DOWANS, hiyo moja lakini pili, wameachana na ushauri wa akina Makamba na Sheikh Yahya, na sasa hivi wamerudi kutaka ushauri wa wasomi wao, wanaojua kuangalia alama za nyakati. inaonekana DOWANS, pamoja na machungu yake, ina jambo moja jema sana, nalo ni kuwa-mobilise watanzania wote katika issue moja. kitu ambacho CCM wanaogopa kuliko hata njaa, (kukosa ruzuku).

baada ya taarifa ya CC yao, kukaanza kuvuja taarifa za kwamba si kweli CC walisema alivyosema katibu mwenezi Chiligati!!, baadae tukasikia kwamba wabunge wa CCM wamegomea hilo na kwamba JK naye anagomea hilo la kuilipa DOWANS. na kwa taarifa hii ya AG kwamba anakumbuka kwamba TANESCO sio yatima, wakati Ngeleja alishatamka kwamba TANESCO watalipa wenyewe na sio serikali. sasa inaonekana serikali taratibu inabadili msimamo wake kujiweka mahala pa kuigomea DOWANS. hii inaonesha kwamba pressure inafanya kazi. ila wasoma alama za nyakati watakuwa wameishauri serikali kwamba iwe makini. katika mazingira ya Tunisia na Misri, na wengineo kama hao, ni hatari kuanza ubishi wa kitaifa kama huu, wakati vigezo vyote vya Tunisia na Misri vipo pia hapa Tz: kupanda gharama za maisha, hakuna ajira, ufisadi uliokithiri, ombwe la uongozi, nk.

What if wanatumia hiyo lugha ya "Tanesco ni mtoto wa serikali" ili waweze kuweka wanasheria wa serikali watakaoipinga hiyo hukumu ili matokeo yawe yale yale? I can smell something, lakini sio kwamba wamezinduka hapana. It is just another game ambayo hatujaijua vizuri. Tanesco ikitumia wanasheria walioteuliewa na serikali kuwatetea most likely itakua imepangwa washindwe. Then watakuja nakusema hata mahakama zetu zinasema DOWANS ilipwe, so lazima tufuate sheria. I bet you hamna jema hapa.
 
Kinachotakiwa ni ajiuzulu William Ngeleja na William Mhando kw aktuletea hili balaa, na kushindwa kuli-handle
 
Khaaaaa mi siasa za TZ zimenichosha,AG lazima tulipe,naibu wake tutasaidia isilipwe,PM lzm ilipwe,waziri wa nishati lzm ilipwe,sita na mwakyembe hakuna kulipwa,uvccm hakuna kulipa,katibu mwenezi tutalipa. Naona sasa tz kuna selikali zaidi ya 2 mana kila mtu akiamka anaongea lake
Ttz la kua na rais lele mama,me nazan ts tym aseme yeye tutalipa au la mana ye ndo mwenye jukumu la mwisho,tumechoka jamani
 
Mkuu NN, hawa CCM ni wahuni tu na mafisadi wakubwa ambao waliweka mbele maslahi yao binafsi badala yale ya nchi. Walikuwa na kiburi cha kutisha hata kuanza kuifilisi nchi kwa kupitia EPA, Meremeta, Kagoda, Rada, Richmond/Dowans n.k. na baadhi yao kuweza hata kutamka kwamba CCM itatawala milele.

Wamezoeea kutuona Watanzania kama wapumbavu tu tutallamika pembeni kuhusu utendaji wa Serikali na kutofanya lolote. Sasa kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu wamestushwa mno na pingamizi kali toka kwa Watanzania wengi kuhusiana na malipo haramu wanayotaka kuyafanya kwa Dowans. Hawakutegena kabisa kana watapata uopinzani toka kwa Wananchi ndiyo maana yule Ngekeja na Werema walikuwa mstari wa mbele kuhakikisha malipo yale yanafanywa haraka haraka ila wagawane mgao wao.

Sasa na haya yaliyotokea Tunisia na Misri yamewaogopesha sana maana wanajua fika kwamba Tanzania si kisiwa na sababu za msingi zilizowafanya Watunisia na Wamisri kuingia mitaani ili kuzing'oa Serikali zao madarakani, sababu hizo zipo pia Tanzania.

Ikiwa hawana pesa za kuwalipa Wafanyakazi wa Serikali watapata wapi pesa za kuisadia TANESCO ili iweze kutoa huduma nzuri na kuondokana na kero kubwa ya mgao wa umeme miaka nenda miaka rudi inayowaathiri sana Watanzania na pia uchumi wa nchi..

Wanajibaraguza tu hawa walilewa madaraka wakajisahau sasa wanaanza kutapatapa.
 
Hawa jamaa lazima watakuwa na plan B ya kulamba izo ela inabdi tuwe makini.
Mwanzo walikataa leo wanajifanya wana uchungu na ela seriously ili litakuwa changa la macho
 
What if wanatumia hiyo lugha ya "Tanesco ni mtoto wa serikali" ili waweze kuweka wanasheria wa serikali watakaoipinga hiyo hukumu ili matokeo yawe yale yale? I can smell something, lakini sio kwamba wamezinduka hapana. It is just another game ambayo hatujaijua vizuri. Tanesco ikitumia wanasheria walioteuliewa na serikali kuwatetea most likely itakua imepangwa washindwe. Then watakuja nakusema hata mahakama zetu zinasema DOWANS ilipwe, so lazima tufuate sheria. I bet you hamna jema hapa.

Inawezekana ikawa hivyo, lakini watakuwa wajinga ziadi kuliko nilivyofikiria. unajua the wind of change inavuma tayari. lakini pengine uko right, maana wakati ule wa siasa za vyama vingi, pamoja na wind of change, ilihitaji pressure ya Nyerere kwa CCM kukubali vyama vingi. sasa nani ataipa pressure CCM kukubali katiba mpya ya kweli? wakati ule wa kukubali vyama vingi CCM waliweka mambo kwa namna ambayo maslahi yao yanalindwa. leo watathubutu kujinyonga wenyewe kwa kuweka katiba mpya inayotakiwa na watanzania? hapo kweli nakubaliana na wewe. lakini tunarudi kule kule. tunahitaji kumobilise watanzania, tupate PEOPLE'S POWER. hii ndio silaha pekee tuliyonayo. na ndio imeshinda Tunisia na ndio inatumika Misri. kule wametumia sana hizi social networking kama twitter, lakini Misri hata mobile phones hazifanyi kazi!!! mkuu kwa kweli tunahitaji kujiandaa!
 
Back
Top Bottom