Serikali ina mpango gani na waTZ huko Bondeni

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Kwa siku kadhaa sasa machafuko dhidi ya wahamiaji yamepamba moto huko Afrika ya Kusini. Hadi hivi sasa wananchi wa nchi kadhaa za Kiafrika wameuawa na idadi yao imefikia karibu 40 hivi. Miongonni mwa wanaodaiwa kuuwa ni pamoja na raia 6 wa Tanzania walioko Bondeni.

Hata hivyo ikiwa imetingwa na mambo mengine serikali yetu haijatoa msimamo wowote au juhudi zozote zinazoeleweka kuhusu kuhakikisha usalama wa wananchi wetu uko Afrika ya Kusini.

Hofu yangu ni kuwa wakati Serikali inataka watanzania walioko nje ya nchi wachangie maendeleo ya nyumbani kwa kutuma fedha, kuwakeza na hata kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo, inaonekana hamu yao inaishia hapo tu.

Serikali haina mpango wowote au sera yoyote inayoeleweka ya kuwa mtetezi wa raia wake walioko nje ya nchi. Mara kadhaa sasa watanzania wanapata matatizo nje ya nchi na serikali yetu aidha inafunga kinywa au inakuwa na attitude "si mliondoka Tanzania" au kuwaona kuwa watanzania walioko nje ya nchi ni nusu raia au wana haki kidogoo na hawana protection yoyote ya State.

Pendekezo:

Serikali ya Tanzania yenye madege makubwa ya kutosha iandae ndege kwenda Afrika ya Kusini na kumchukua Mtanzania yoyote anayetaka kurudi nyumbani. Hili linawezekana na si gumu. Serikali pia ioneshe kujali raia wake isiwafanye kama ilivyowafanyia vijana wetu kule Ukraine au ilivyojifanya imesahau suala la vijana wetu waliouawa hapa US. Serikali yetu isifumbie macho kama inavyofumbia macho suala la kijana Fupi ambaye amewekwa kwenye kundi la Maghaidi uko Guantanamo.
 
Naungana mkono na mzee mwana kijiji lakini akumbuke kuwa hilo ni ndoto. Nitakupa mfano hai tena hapahapa Tanzania na tukio hilo lilifanywa na kiongozi mkubwa wa serikali tena bila ya aibu wakati huo ni katibu kiongozi. Kulitokea ugonjwa wa ajabu huko kijijini kwao Mahenge jamaa alichofanya yeye alichukua helikopta ya serikali akamkomba mama yake mzazi huku akiwaacha wanakijiji wenzake wakiteketea. Kwa hiyo mzee Mwanakijiji hoja yako ni nzuri lakini kwa hawa mafisadi wataanza na watoto wao,vimada vyao hiyo ni first priority.
 
mpango wa nini? please give government a brake, Watanzania tuna haki ya kurudi nyumbani kama mlimpo hapana haki. Serikali didn't sent you to US or UK or SA, you decided on your own willing. Please let stop this ujamaa politics.

majority ya Watanzania walipo South Africa walikwenda kinyuma cha sheria katika miaka 1990's. Government need to focus na mambo mengine ambayo yanaitaji more attention, we can always go back home.
 
Pendekezo

Serikali ya Tanzania yenye madege makubwa ya kutosha iandae ndege kwenda Afrika ya Kusini na kumchukua Mtanzania yoyote anayetaka kurudi nyumbani. Hili linawezekana na si gumu. Serikali pia ioneshe kujali raia wake isiwafanye kama ilivyowafanyia vijana wetu kule Ukraine au ilivyojifanya imesahau suala la vijana wetu waliouawa hapa US. Serikali yetu isifumbie macho kama inavyofumbia macho suala la kijana Fupi ambaye amewekwa kwenye kundi la Maghaidi uko Guantanamo.


Watanzania wengi walio south Africa wapo pale kinyume cha sheria, hakuna takwimu zozote zinazoonyesha kwamba wapo wangapi, na wafanya nini. Wengi wamejibabu kuwa ni raia wa nchi kama Rwanda, Burundi au Somalia na wameshapata either karatasi zao au wako kwenye procidure.

Sasa serikali ya Tanzania mnataka ianzie wapi? How will the government reach unknown number of Tanzania in unknown areas? Kwa hapa mwanakijiji natofautiana na wewe 100%. Dawa ya kila anaeona ananyanyasika katika nchi aliyokwenda mwenyewe kwa hiari yake bila kulazimisha ni kurudi Tanzania. Hakuna vita South Africa kusema inabidi B56 zisecure area kabla ya kuwachukua Watanzania, no waende kwenye office za Kamata za huko south then wapande Kamata hadi Dar. Point is reduce government expenses zisizo na kichwa wala pua
 
Mtanganyika,
Kwa nini tuache ndugu zetu wafe eti tu kwa kuwa waliingia au wanaishi SA kinyume cha sheria?Serikali iwasaidie kurudi kama wapo wanaohitaji.
Kuna wengine wameingia ki halali lakini sasa maisha yao yako mashakani na wapo vituo vya polisi wamejisetiri.Ni vema wasaidiwe kurudi kama wataridhia.
Tusisikilize usemi wa siasa kwamba majeshi yameingia mtaani kusaidia kukamata waharifu,huko hakufai kabisa
Kumbuka ni hivi karibuni tu hata balozi wetu huko walimkong'oli kwenye tafrija.Sijui hata kama amepata nafuu.
Hata kama mtu ni jambazi huwa anapelekwa hospital kutibiwa ndipo mkondo wa shule ya sheria unafuata.
 
Single D
Kwa nini wasipande wenyewe mabasi wakarudi Dar? Kwani south kuna vita kusema kwamba aliyao inaweza kuwa mashakani kwenye standi ya Mabasi?
 
watoto walio zaliwa ndani ya ndoa na wale walio zaliwa nje wana haki sawa kwa baba yao !! kwahiyo watz walioko bondeni wana paswa kupatiwa msaada na serikali ya kisura
 
kama kuna wanaotaka kurudi na hawana jinsi nafikiri kitu cha kwanza wanatakiwa kuwasiliana na ubalozi ili serikali kama inataka kuwafuata ijue ni wangapi wanataka kurudi, lakini serikali haiwezi kutoa ndege kwenda african kusini bila kujua idadi kamili ya watu wanaotakiwa kurudi inawezekana wapo watanzania ambao hawataki kurudi tanzania pamoja na machafuko. My Views
 
Tena hili ni jukumu la msingi na la Kikatiba la Serikali yoyote MAKINI na inayowajibika kwa Raia wake. Tunaona serikali za wenzetu zinatuma haraka ndege zao kokote kwenye machafuko kuwachukua raia wao. Hapa kwetu hata lile ONYO au TAHADHARI kwa Wananchi wetu kuhusu hali ilivyo huko SAUZI bado Serikali yetu Tukufu inatafakari!
 
Single D
Kwa nini wasipande wenyewe mabasi wakarudi Dar? Kwani south kuna vita kusema kwamba aliyao inaweza kuwa mashakani kwenye standi ya Mabasi?

Hali si nzuri hasa mji wa Cape Town maana mashambulizi yameenea ikla sehemu.Acha kufika stendi ya mabasi yaani hata kwenda uwanja wa ndege unavamiwa njiani hata hujafika.Naamini umeona mabomu ya petrol yanatumika kuwalipua watu.
Walio vituo vya polisi ndo tu wako salama,Serikali iwasadie.
Siamini kuwa hawa ndo wa sauzi tuliowatunza pale mjini Morogoro ki eneo cha Mazimbu na ndo wameamua kutugeuka hivi.
 
Lakini jamani kule SA si kuna ubalozi pale??kwa nn wasiende kujisalimisha alafu serikali ikajua wapo wangapi ili iweze kuwapa msaada..tatizo wabongo wengi wameenda SA kwa kuzamia ndo maana wanaogopa kujisalimisha ubalozi hawajaenda kihalali kingine kama walipelekwa na serikali basi inafanya kosa kuto wapa msaada lakini kama walienda wao wenyewe ubalozi upo pale wanaweza kupata msaada pale sasa tunasikia wengine wamejiandikisha kama warundi,wanyarwanda na wasonjo hapo sasa kazi kweli kweli nani ataenda ubalozi wkt hata pass hana duhhh aibu wana JF
 
Mashambulizi yamesambaa toka J'berg hadi Capetown sasa hapo ubalozini wataendaje wakati ukionwa tu njiani unavamiwa na kushambuliwa?
 
tusiwalaumu kuwa tuliwatunza pale mazimbu, hali ya maisha imekuwa ngumu chini ya uongozi wa Thabo Mbeki kiasi kuwa ajira imekuwa issue ndo maana wameingia mtaani kutaka kuwaondoa wageni ili wabakie wao, ili linakuja hata TZ kwani hali inaendelea kuwa ngumu zaidi kila siku.
 
tusiwalaumu kuwa tuliwatunza pale mazimbu, hali ya maisha imekuwa ngumu chini ya uongozi wa Thabo Mbeki kiasi kuwa ajira imekuwa issue ndo maana wameingia mtaani kutaka kuwaondoa wageni ili wabakie wao, ili linakuja hata TZ kwani hali inaendelea kuwa ngumu zaidi kila siku.

Kwa hiyo wa TZ nao wavamie makampuni ya wa Sauzi?Maana yapo mengi tu hadi ya ulinzi ambao akina Marwa,Mwita,Chacha wamezaliwa nao damuni?
Najua hili litaleta uhasama sana ktk nchi za Afrika hasa ambazo zimeathirika na haya mashambulizi ya raia wao.
Lilianza kidogo miaka kadhaa nyumakwa kuwang'atisha mbwa wahamiaji haramu waliokamatwa njia za vichochoroni,sasa limekuwa kushambuliwa na mabomu ya petrol na kubakwa mitaani.
 
tusiwalaumu kuwa tuliwatunza pale mazimbu, hali ya maisha imekuwa ngumu chini ya uongozi wa Thabo Mbeki kiasi kuwa ajira imekuwa issue ndo maana wameingia mtaani kutaka kuwaondoa wageni ili wabakie wao, ili linakuja hata TZ kwani hali inaendelea kuwa ngumu zaidi kila siku.

SI WAIBWAGE ANC YAO? HATA HAPA ccm WAKO MATATANI
 
pressure itatoka kwa watanzania wenyewe walioko huko bondeni.
what they can do ni kuwasiliana na ubalozini kwanza. hiyo ndo step ya kwanza. then ubalozi utakapowapa jibu lenye utata( which will probably happen), wafikiriwe mbinu nyengine za msaada ikiwa ni kama hii aliyotowa mkijiji au kutafutiwa safe house kwa muda
 
Mtanganyika,

the issue in SA is very serious, na haichagui wewe umeingia kihalali wala nini, nimeongea na Cousin wangu muda si mrefu, yeye ni Engineer na yuko SA CapeTown kihalali, kaoa kule M-SA......lakini just a few minutes ago ananiambia hali si shwari na lolote laweza kutokea.......kwani hata kusafiri toka sehemu A kwenda B huna uhakika wa kufika!!...........tena Cape Town wanatumia hata snippers!!........ananiambia wala hakutegemea kwa area anayoishi kuamka asubuhi na kuambaiwa kuwa mtaa wa pili tu toka mtaa anakoishi Warundi 4 wameuawa..........

Hawa ndio wa-SA waliomuua Sokoine, and they got away with it, hawa ndio waSA ambao Mpungwe an rafiki yake BWM wanaowa-embrace.......damn!!

SA Govt inabidi ichukue hatua za nguvu na zisizo za kinafiki kama apology ya Bi Winnie Mandela.........yes i said it "apology ya kinafiki"!!
 
Field80,

sidhani kama unaifahamu Afrika Kusini, na kama unaifahamu labda majina ya miji tu! Hivi unajua ubalozi wa Tanzania uko wapi? Uko Pretoria, mtu wa Cape Town, Durban - (KwaZulu Natal, Pietmarziburg, New Castle, nk) au Mpumalanga, Limpopo, au Western cape atafikaje huko pretoria!! Hivi wewe unajua kweli Afrika Kusini, au umekaa hapo Mikindani, Mtwara unafikiri nchi zote ziko hivyo!

Watanzania hawataki msaada wowote kwasasa, BALI tamko rasmi la serikali dhidi ya raia wake wa Afrika Kusini, na hata ikiwezekana kushinikiza serikali ya Afrika Kusini tuzuia machafuko zaidi! Mbona tumekuwa tukitoa maonyo kwa Burundi, DRC, ... why not Afrika Kusini? Rais Mbeki yuko nchini Tanzania, Makamu wake yuko Nigeria, wote hawa wamefunga midomo (kama Ben Mkapa) hawataki kuzungumzia machafuko! Ni zamu ya serikali kuwakaripia kwa hili, kwani wanaokufa ni raia wa TZ, na pia inajenga uhasama ndani ya Afrika kwa waafrika wenyewe! Utajisikiaje ukisikia Mozambique wameaanza kupiga raia wasioongea kireno!!
 
hawa tuliwalinada sana wakati wa ukombozi wa bara la afrika sasa wamejisahau wanatumaliza. kweli shukurani ya punda ni mateke
 
Balozi zetu haziwasaidii Watanzania wakiwa nje hata kama walipelekwa na serikali. Tumesoma malalamiko mengi ya Wanafunzi wa Kitanzania katika nchi mbali mbali duniani, sasa hawa waliojiendea kivyao vyao sidhani kama ubalozi huo utakuwa na msaada wowote, labda itakuwa ni mara ya kwanza. Balozi zetu si za kukimbilia ukipatwa na matatizo nje ya nchi na ushahidi upo wa kutosha tu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom