Serikali imetangaza zabuni kwa kampuni za ujenzi nje ya nchi kubomoa jengo la ghorofa 16 Dar

Chipsi yaipembeni

Senior Member
Jan 8, 2015
128
90
Wakuu,

Katika kupitia mitandao mbalimbali ili kupata habari mbili tatu, nilikutana na hii ambayo imeandikwa na Gazeti Mtandao la FikraPevu.

Eti hapa nchini Serikali imekosa kampuni inayoweza kubomoa majengo marefu ikiwemo lile lililopo katikati ya Jiji la Dar es salaam ambalo liliamriwa na Serikali yenyewe kuwa libomolewe kwa muda wa karibu miaka mitatu sasa.

Ninajiuliza kuwa, hivi kama hili jengo lingebomoka jana au leo, hiyo hasara ya raslimali watu na mali zilizopo pale zitalipwa na nani? Kwanini miaka yote hiyo tangu walivyounda tume yao haikulishughulikia hili jambo kwa kina hadi sasa tunaona danadana za Serikali?

===================
attachment.php

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amesema Serikali imelazimika kutangaza tenda kwa kampuni zilizo nje ya nchi zenye wataalamu wenye vifaa vinavyoweza kutumika kubomoa majengo marefu ili kubomoa jengo la ghorofa 16, lililopo makutano ya barabara za Indira Gandhi na Morogoro, katikati ya jijini la Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Waziri Lukuvi, hatua hiyo inafuata baada ya Tanzania kukosa wataalamu hao kwa kipindi kirefu, baada ya jengo hilo lililobaki likiwa limesimama baada ya jengo pacha lingine kuporomoka mwaka 2013 na Serikali kuagiza jengo hilo pia libomolewe kutokana na kujengwa chini ya viwango.

Jengo hilo bado limeendelea kusimama hali inayozidi kuwatia hofu wananchi wanaoishi pamoja na kufanya shughuli zao za kiuchumi katika maeneo yanayozunguka jengo hilo.

Amesema kutokana na tatizo hilo, Serikali imeamua kutangaza zabuni kwa kampuni za mataifa mengine ili kuepuka madhara kwa jamii wakati wa ubomoaji wa jengo hilo.

Amesema jengo hilo lipo katika kiwanja kinachomilikiwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) jirani na jengo lililoanguka na kuua watu 21 hivyo lazima libomolewa na wataalamu kwa kutumia vifaa maalumu.

Alifafanua kuwa, licha ya jengo hilo kuwa chini ya kiwango, pia liko karibu na majengo mengine matatu pamoja na Msikiti hivyo ubomoaji wake unahitaji utaalamu wa hali ya juu na vifaa vinavyoweza kumtahimili uzito wa mabaki ya jengo hilo.

Waziri Lukuvi, amekaririwa na FikraPevu akisema ukosefu wa vifaa mbalimbali vya kubomoa majengo marefu nchini umekuwa ukiigharimu Serikali kiasi kikubwa cha fedha, kutokana na kulazimika kutafuta wataalamu wa vifaa kutoka mataifa mengine.

Taarifa kutoka ndani ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, zinaeleza kwamba, ipo kampuni ambayo ilipewa dhamana ya ubomoaji wa jengo hilo tangu mwanzoni mwa mwaka huu lakini haieleweki ni kwanini utekelezaji wake umesuasua – sua hadi Waziri mwenye dhamana alipoamua kuingilia kati suala hilo.

Jengo-hilo-lipo-katika-Mtaa-wa-Indira-Gandhi-Dar-linatarajiwa-vuvunjwa-wakati-wowote-kuanzia-sasa.jpg


Jengo hili lipo katika Mtaa wa Indira Gandhi Dar es Salaam linatarajiwa vuvunjwa wakati wowote kuanzia sasa

Kampuni kutoka China inayojulikana kwa jina ERJE imetajwa na Afisa mmoja kutoka katika Ofisi hiyo ya Mkuu wa Mkoa (hakutaja jina lake litajwe) kuwa miongoni mwa kampuni ya 5 zilizotuma maombi katika mamlaka husika kuomba kufanya kazi hiyo, ingawa alishindwa kuithibitishia FikraPevu kwamba ni kwanini kampuni hiyo haikuanza kufanya kazi hiyo tangu makubaliano hayo yafanyike.

Soma zaidi | =>Serikali yatangaza Zabuni kwa Kampuni za Ujenzi Nje ya Nchi kubomoa Jengo la Ghorofa 16 Dar
 

Attachments

  • Muonekano wa jengo hilo jinsi linavyoonekana na majengo yaliyopo jirani yake.jpg
    Muonekano wa jengo hilo jinsi linavyoonekana na majengo yaliyopo jirani yake.jpg
    59 KB · Views: 3,112
Mkuu, hii habari tuliipata tukajicheka sana...! Kuna mdau mmoja akasema UDSM hawajawahi kuzalisha mhandisi Mwenyezi ujuzi wa kubomoa jengo lenye ghorofa zaidi ya nne.
 
Hapo hakuna cha wataalam wa kubomoa wala nini, watakuja wachina na kubomoa kwa winch zilizoko hapa hapa Tz na hata ikitokea huo msikiti na nyumba za jirani kuharibiwa na ubomoaji huo bado hakutakuwa na kelele kwa hao wabomoaji wa kigeni.

Hilo ghorofa lilitakiwa kuwa ndio sehemu ya field kwa wahandisi wetu kufanya mazoezi ya jinsi ya kubomoa majengo marefu.

Tatizo viongozi hawana maono, hata ukienda China au marekani kusomea uhandisi wa majengo bado wataona hufai.

Hilo jengo hata vijana wa mataani wakipewa ajira ya mwaka mzima watalibomoa tu, kwani lilijengwaje?
 
Yule waziri mbabe alikuwa sana kusema uwezo wa matajiri wa Tanzania ni kuwekeza kwenye juice,chapatii na maji
 
[Q UOTE=TeamCCM-2015;14147800]Mkuu suala si ujuzi tu bali vitendea kazi vipo/wanavyo?[/QUOTE]
Wewe gamba akili is hakuwa tegemezi imenock kabisa!kwanza u nafahamu ni vitendea kazi gani vinavyohitajika wakati wa kubomoa Gorofa?
Usitake kusema eti tz hakuna wataalam wala vitendea kaZi.
 
kuna njia ya kubomoa majengo marefu bila kuadhira majengo na mali zilizoko jirani na jengo husika kwa kutumia milipuko ya baruti inaitwa buiding implosion inayofanywa na controlled demolion industry ie check youtube!!! Kwa hapa tz hiyo industry haipo kabisa au niseme sijaona ikifanyika
 
Nimewahi ona jinsi wenzetu nchi za mbele (ktk Geographic Channel) jinsi wanavyobomoa majengo marefu kwa kutumia xplosives, maeneo yaliyo naajengo na watu wengi kubomoa kiholela holela unaweza leta majanga mengine, hivyo kama nchini hamna wa kubomoa kwa utaratibu ambao hautasababisha majanga sioni tatizo hapo!
 
Wala halita bomolewa hii ni kampeni ya ccm kuwahadaa wananchi kwamba ni watekelezaji, ikipita octoba 25, habari inawekwa kapuni jamaa anaenda kuweka zuio mahakamani anaendelea na ujenzi wake.
 
Nadhani kwenye mtaala au sylabus inayotumika kufundisha makandarasi wa majengo iwe inatoa pia mafunzo ya kubomoa. Kama wewe ni mkandarasi, unajua kujenga majumba kama haya basi ujue kuyabomoa pia!
 
Tukisema UKAWA tunaanza na Elimu kwanza Jamani mtu elewe.... CCM ni zaidi ya Laana kwa Watanzania
 
Sijaona tatizo la notice ya waziri ..hii inabaki ni changamoto kwa vyuo hapa nchini
 
Nadhani kwenye mtaala au sylabus inayotumika kufundisha makandarasi wa majengo iwe inatoa pia mafunzo ya kubomoa. Kama wewe ni mkandarasi, unajua kujenga majumba kama haya basi ujue kuyabomoa pia!
Mi najua ukijua namna ya kuingia basi ujue na namna ya kutoka. Sasa na supplementary na disco zote za engineering kumbe kubomoa hamjui???
 
Nadhani kwenye mtaala au sylabus inayotumika kufundisha makandarasi wa majengo iwe inatoa pia mafunzo ya kubomoa. Kama wewe ni mkandarasi, unajua kujenga majumba kama haya basi ujue kuyabomoa pia!
Mi najua ukijua namna ya kuingia basi ujue na namna ya kutoka. Sasa na supplementary na disco zote za engineering kumbe kubomoa hamjui???
 
Nadhani kwenye mtaala au sylabus inayotumika kufundisha makandarasi wa majengo iwe inatoa pia mafunzo ya kubomoa. Kama wewe ni mkandarasi, unajua kujenga majumba kama haya basi ujue kuyabomoa pia!

Wanafundishwa kubomoa ila mwisho ni jengo la ghorofa5, juzi tu jengo la nssf ubungo limeshushwa na kampuni ya wazawa
 
Kuna nyumba ngapi Dar es Salaam zilizoonekana zimejengwa chini ya viwango ni kwanini hiyo moja tu ibomolewe?
 
Back
Top Bottom