Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
SERIKALI IMENYWEA..................................Gazeti la MwanaHALISI
SERIKALI imeshindwa kusema lolote kuhusiana na kushiriki katika wizi wa mabilioni ya shilingi kupitia kampuni ya Kagoda Agriculture Limited.
Taarifa za gazeti hili, toleo la wiki iliyopita, zilimnukuu wakili mmoja wa mjini Dar es Salaam akisema, chini ya kiapo, kwamba aliambiwa na Rostam Aziz kuwa fedha hizo zaidi ya Sh. 40 bilioni zilikuwa ni za kugharamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa 2005.
Wakili huyo, Bhyidinka Michael Sanze, ananukuliwa akiwasiliana na Kamati ya Rais ya Kushughulikia wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwamba miongoni mwa wahusika wakuu katika wizi huo, ni rais mstaafu Benjamin Mkapa.
Wengine aliowataja ni Rostam, Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula, gavana wa BoT, Dk. Daud Ballali, Mkurugenzi wa Mipango na Uchumi BoT, Peter Noni na wakili wa kujitegemea, Bered Malegesi.
Mwanasheria mashuhuri nchini, Mabere Marando alipotakiwa maoni yake juu ya kigugumizi hiki cha serikali, alisema, (Serikali) hawawezi kusema kitu.
Alisema, Mimi nadhani serikali imepigwa na butwaa. Hawakujua kama vitu hivi vitaibuliwa. Hawakujua haya! Inawezekana wameshangaa haya mliyoandika.
Sanze, wakili katika kampuni ya mawakili ya Malegesi Malegesi Law Chambers ya Dar es Salaam, anasema katika andishi lake kuwa alishuhudia mikataba ya uchotaji fedha alipokuwa katika ofisi za kampuni ya Caspian Construction Limited ambayo inamilikiwa na Rostam, mfanyabiashara na mbunge wa Igunga.
Sanze, katika hati ya kiapo, anadai kuelezwa na Rostam kuwa alikuwa kwenye kikao cha Mkapa, Mangula na Ballali ambapo anasema alishuhudia Mkapa akitoa amri kwa Ballali ya kutoa fedha hizo na kumkabidhi yeye (Rostam).
Siku nane tangu taarifa hizo zitoke, serikali haijesema lolote na viongozi mbalimbali ambao gazeti hili limejitahidi kuwasiliana nao, ama wamesema hawataki kuzungumza lolote au hawana la kusema.
MwanaHALISI ilimtafauta Waziri Mkuu Mizengo Pinda ili kutaka kujua msimamo wa serikali baada ya ushahidi huo kuanikwa hadharani, lakini hakuweza kupatikana.
Msaidizi wake, Ole Kuyani alimtaka mwandishi kuwasiliana na msaidizi mwingine alimyetaja kwa jina moja la Ibambiro, kwa maelezo kwamba huyo ndiye yupo karibu zaidi na bosi wake kwa wakati huo.
Ibambiro alipatikana na baada ya kuelezwa kile ambacho MwanaHALISI inahitaji kutoka kwa waziri mkuu, aliahidi kupiga simu baada ya kuwasiliana na Pinda.
Gazeti lilipoona kimya kimekuwa kirefu, lilipiga tena simu ofisini kwa waziri mkuu, lakini aliyepokea alijibu kwa ufupi. Tumekuahidi kukupigia. Subiri utapigiwa.
Hadi tunakwenda mitamboni, ofisi ya waziri mkuu haikupiga simu MwanaHALISI.
Waziri mkuu Pinda aliahidi wananchi kupitia vyombo vya habari Desemba mwaka jana, kwamba Serikali haigopi Kagoda na kwamba masuala yote yanafuatiliwa na yataelezwa bayana uchunguzi utakapokamilika.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba alipoulizwa Polisi inachukua hatua gani baada ya kupatikana ushahidi wa Sanze kuhusika kwa Kagoda na vigogo wengine katika ukwapuaji wa fedha BoT, alisema hilo aulizwe Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).
Nimekuelewa. Lakini kwa ujumla, sisi hatujadili ushahidi hadharani. Ushahidi unajadiliwa mahakamani, alisema Manumba.
Juhudi za gazeti kumpata DPP hazikuweza kuzaa matunda. Awali alipopigiwa simu juzi Jumatatu, DPP Eliezer Feleshi alipokea na baada ya mwandishi kujitambulisha alisema, nipo kwenye kikao, nipigie baadaye.
Alipoulizwa apigiwe baada ya muda gani, Feleshi alisema, ni baada ya saa moja. Gazeti liliendelea kumtafuta Feleshi juzi Jumatatu lakini simu yake ilikuwa inaita bila kupokelewa. Hadi tunakwenda mitamboni Feleshi alikataa kujibu simu.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika hakupatikana, lakini msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba, Omega Ngole, alipoulizwa juu ya msimamo wa ofisi yake, kuhusiana na waliotajwa na wakili Sanze katika sakata la Kagoda, alisema hayo ni mambo ya kujadili ofisini.
Simu ya Mwanyika Na. 0713 324854 kila ilipopigwa ilitoa jibu, simu unayopiga haipatikani, jaribu tena baadaye. Ilipigwa tena na tena, lakini jibu bado lilikuwa ni hilohilo.
Kwa mujibu wa andishi la Sanze, alishuhudia mikataba hiyo kwa kusaini baada ya kuthibitishiwa na Malegesi kuwa alishakwenda kujiridhisha kwa Ballali na Mangula. Sanze alisisitiza, Rostam mwenyewe alisema, system yote inajua.
Alipoulizwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba amepokeaje taarifa zilizotolewa na Sanze kuhusu sakata la Kagoda hasa kwa kuwa zimetaja viongozi wa CCM, aliingia kati na kusema, Kama ni masuala ya Kagoda, mimi sina la kuzungumza.
Mwandishi alipomueleza kuwa inajulikana wakati wa sakata la Kagoda yeye hakuwa katibu mkuu wa CCM, isipokuwa Sanze anasema fedha zimewasilishwa katika chama, Makamba alisisitiza, Kama ni Kagoda hilo sina jibu.
Makamba akakata simu. Gazeti linamtafuta Makamba ili pamoja na mambo mengine, ajibu swali: Zipo taarifa zozote katika chama zinazoonyesha kwamba Rostam Aziz aliingiza fedha zilizochotwa EPA, katika kampeni za CCM?
Inspekta Jenerali wa Polisi nchini (IGP), Said Mwema hakupatikana. Simu yake Na. 0754 785557 ilikuwa inaita bila kupokelewa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hoseah, alipoitwa kwa simu yake Na. 0784 763741, simu yake ilikaa kimya. Baadaye ilipopigwa tena ilijibu, samahani simu unayopiga haipatikani kwa sasa.
Mwanyika ndiye alikuwa mwenyekiti wa Timu ya Rais ya kufuatilia yaliyogunduliwa na maodita wa Ernst & Young katika ukaguzi wa akaunti ya EPA kwa mwaka 2005/2006. Wajumbe wengine wa timu hiyo ni IGP Mwema na Hoseah.
MwanaHALISI iliwasiliana na Dk. Willibrod Slaa, mbunge wa Karatu na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ili kutoa maoni yake ambapo alisema serikali haiwezi kujibu lolote kwa sababu inajua kila kitu kuhusu Kagoda.
Nyaraka mlizotumia, hata mimi ninazo. Nimejiridhisha kwamba haya mliyosema ni sahihi, na kwamba serikali inayajua. Lakini haitaki kusema ukweli huu kwa sababu, inahusika katika wizi huu, alisema Dk. Slaa.
Wakili Marando anafika mbali zaidi. Anasema, Serikali haijapuuza, tatizo hawajui la kufanya. Nimeiona affidavit (hati ya kiapo) ya Sanze ni sahihi.
Anasema, Mimi sioni kama Watanzania watasahau haya. Serikali na CCM wanajua kwamba viongozi wa vyama vya upinzani watatumia hoja hizo katika kampeni.
Hii ni mara ya kwanza Mkapa kutajwa katika sakata la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, lakini ni mara nyingi Rostam amehusishwa na ukwapuaji huo ndani ya BoT.
Hadi sasa, watuhumiwa 20 wamefikishwa mahakamani kuhusiana na sakata la ufisadi wa fedha za EPA, lakini kumekuwa na ugumu kwa serikali kushughulikia wahusika wa Kagoda:
My opinion:
Haya mambo yaliongelewa sana sana hapa JF na nnadhani wakuu walipuuza kwa kujua anywayz ni watanzania wangapi wana access na internet? Lakini inapotokea kwenye public tena kwenye gazeti siamini akina Mkamba, Chiligati kama kawaida yao kukaa kimya kwa wiki nzima. RA naye vp si alishatishia kulishtaki gazeti hili aliishia wapi?
SERIKALI imeshindwa kusema lolote kuhusiana na kushiriki katika wizi wa mabilioni ya shilingi kupitia kampuni ya Kagoda Agriculture Limited.
Taarifa za gazeti hili, toleo la wiki iliyopita, zilimnukuu wakili mmoja wa mjini Dar es Salaam akisema, chini ya kiapo, kwamba aliambiwa na Rostam Aziz kuwa fedha hizo zaidi ya Sh. 40 bilioni zilikuwa ni za kugharamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa 2005.
Wakili huyo, Bhyidinka Michael Sanze, ananukuliwa akiwasiliana na Kamati ya Rais ya Kushughulikia wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwamba miongoni mwa wahusika wakuu katika wizi huo, ni rais mstaafu Benjamin Mkapa.
Wengine aliowataja ni Rostam, Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula, gavana wa BoT, Dk. Daud Ballali, Mkurugenzi wa Mipango na Uchumi BoT, Peter Noni na wakili wa kujitegemea, Bered Malegesi.
Mwanasheria mashuhuri nchini, Mabere Marando alipotakiwa maoni yake juu ya kigugumizi hiki cha serikali, alisema, (Serikali) hawawezi kusema kitu.
Alisema, Mimi nadhani serikali imepigwa na butwaa. Hawakujua kama vitu hivi vitaibuliwa. Hawakujua haya! Inawezekana wameshangaa haya mliyoandika.
Sanze, wakili katika kampuni ya mawakili ya Malegesi Malegesi Law Chambers ya Dar es Salaam, anasema katika andishi lake kuwa alishuhudia mikataba ya uchotaji fedha alipokuwa katika ofisi za kampuni ya Caspian Construction Limited ambayo inamilikiwa na Rostam, mfanyabiashara na mbunge wa Igunga.
Sanze, katika hati ya kiapo, anadai kuelezwa na Rostam kuwa alikuwa kwenye kikao cha Mkapa, Mangula na Ballali ambapo anasema alishuhudia Mkapa akitoa amri kwa Ballali ya kutoa fedha hizo na kumkabidhi yeye (Rostam).
Siku nane tangu taarifa hizo zitoke, serikali haijesema lolote na viongozi mbalimbali ambao gazeti hili limejitahidi kuwasiliana nao, ama wamesema hawataki kuzungumza lolote au hawana la kusema.
MwanaHALISI ilimtafauta Waziri Mkuu Mizengo Pinda ili kutaka kujua msimamo wa serikali baada ya ushahidi huo kuanikwa hadharani, lakini hakuweza kupatikana.
Msaidizi wake, Ole Kuyani alimtaka mwandishi kuwasiliana na msaidizi mwingine alimyetaja kwa jina moja la Ibambiro, kwa maelezo kwamba huyo ndiye yupo karibu zaidi na bosi wake kwa wakati huo.
Ibambiro alipatikana na baada ya kuelezwa kile ambacho MwanaHALISI inahitaji kutoka kwa waziri mkuu, aliahidi kupiga simu baada ya kuwasiliana na Pinda.
Gazeti lilipoona kimya kimekuwa kirefu, lilipiga tena simu ofisini kwa waziri mkuu, lakini aliyepokea alijibu kwa ufupi. Tumekuahidi kukupigia. Subiri utapigiwa.
Hadi tunakwenda mitamboni, ofisi ya waziri mkuu haikupiga simu MwanaHALISI.
Waziri mkuu Pinda aliahidi wananchi kupitia vyombo vya habari Desemba mwaka jana, kwamba Serikali haigopi Kagoda na kwamba masuala yote yanafuatiliwa na yataelezwa bayana uchunguzi utakapokamilika.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba alipoulizwa Polisi inachukua hatua gani baada ya kupatikana ushahidi wa Sanze kuhusika kwa Kagoda na vigogo wengine katika ukwapuaji wa fedha BoT, alisema hilo aulizwe Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).
Nimekuelewa. Lakini kwa ujumla, sisi hatujadili ushahidi hadharani. Ushahidi unajadiliwa mahakamani, alisema Manumba.
Juhudi za gazeti kumpata DPP hazikuweza kuzaa matunda. Awali alipopigiwa simu juzi Jumatatu, DPP Eliezer Feleshi alipokea na baada ya mwandishi kujitambulisha alisema, nipo kwenye kikao, nipigie baadaye.
Alipoulizwa apigiwe baada ya muda gani, Feleshi alisema, ni baada ya saa moja. Gazeti liliendelea kumtafuta Feleshi juzi Jumatatu lakini simu yake ilikuwa inaita bila kupokelewa. Hadi tunakwenda mitamboni Feleshi alikataa kujibu simu.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika hakupatikana, lakini msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba, Omega Ngole, alipoulizwa juu ya msimamo wa ofisi yake, kuhusiana na waliotajwa na wakili Sanze katika sakata la Kagoda, alisema hayo ni mambo ya kujadili ofisini.
Simu ya Mwanyika Na. 0713 324854 kila ilipopigwa ilitoa jibu, simu unayopiga haipatikani, jaribu tena baadaye. Ilipigwa tena na tena, lakini jibu bado lilikuwa ni hilohilo.
Kwa mujibu wa andishi la Sanze, alishuhudia mikataba hiyo kwa kusaini baada ya kuthibitishiwa na Malegesi kuwa alishakwenda kujiridhisha kwa Ballali na Mangula. Sanze alisisitiza, Rostam mwenyewe alisema, system yote inajua.
Alipoulizwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba amepokeaje taarifa zilizotolewa na Sanze kuhusu sakata la Kagoda hasa kwa kuwa zimetaja viongozi wa CCM, aliingia kati na kusema, Kama ni masuala ya Kagoda, mimi sina la kuzungumza.
Mwandishi alipomueleza kuwa inajulikana wakati wa sakata la Kagoda yeye hakuwa katibu mkuu wa CCM, isipokuwa Sanze anasema fedha zimewasilishwa katika chama, Makamba alisisitiza, Kama ni Kagoda hilo sina jibu.
Makamba akakata simu. Gazeti linamtafuta Makamba ili pamoja na mambo mengine, ajibu swali: Zipo taarifa zozote katika chama zinazoonyesha kwamba Rostam Aziz aliingiza fedha zilizochotwa EPA, katika kampeni za CCM?
Inspekta Jenerali wa Polisi nchini (IGP), Said Mwema hakupatikana. Simu yake Na. 0754 785557 ilikuwa inaita bila kupokelewa.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hoseah, alipoitwa kwa simu yake Na. 0784 763741, simu yake ilikaa kimya. Baadaye ilipopigwa tena ilijibu, samahani simu unayopiga haipatikani kwa sasa.
Mwanyika ndiye alikuwa mwenyekiti wa Timu ya Rais ya kufuatilia yaliyogunduliwa na maodita wa Ernst & Young katika ukaguzi wa akaunti ya EPA kwa mwaka 2005/2006. Wajumbe wengine wa timu hiyo ni IGP Mwema na Hoseah.
MwanaHALISI iliwasiliana na Dk. Willibrod Slaa, mbunge wa Karatu na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ili kutoa maoni yake ambapo alisema serikali haiwezi kujibu lolote kwa sababu inajua kila kitu kuhusu Kagoda.
Nyaraka mlizotumia, hata mimi ninazo. Nimejiridhisha kwamba haya mliyosema ni sahihi, na kwamba serikali inayajua. Lakini haitaki kusema ukweli huu kwa sababu, inahusika katika wizi huu, alisema Dk. Slaa.
Wakili Marando anafika mbali zaidi. Anasema, Serikali haijapuuza, tatizo hawajui la kufanya. Nimeiona affidavit (hati ya kiapo) ya Sanze ni sahihi.
Anasema, Mimi sioni kama Watanzania watasahau haya. Serikali na CCM wanajua kwamba viongozi wa vyama vya upinzani watatumia hoja hizo katika kampeni.
Hii ni mara ya kwanza Mkapa kutajwa katika sakata la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, lakini ni mara nyingi Rostam amehusishwa na ukwapuaji huo ndani ya BoT.
Hadi sasa, watuhumiwa 20 wamefikishwa mahakamani kuhusiana na sakata la ufisadi wa fedha za EPA, lakini kumekuwa na ugumu kwa serikali kushughulikia wahusika wa Kagoda:
My opinion:
Haya mambo yaliongelewa sana sana hapa JF na nnadhani wakuu walipuuza kwa kujua anywayz ni watanzania wangapi wana access na internet? Lakini inapotokea kwenye public tena kwenye gazeti siamini akina Mkamba, Chiligati kama kawaida yao kukaa kimya kwa wiki nzima. RA naye vp si alishatishia kulishtaki gazeti hili aliishia wapi?