Serikali ilivyotekeleza Maazimio ya Bunge Richmond-Pinda.

Watumishi wote waliohusishwa na sakata hili wamepewa haki ya kusikilizwa kwanza. WM amepata maoni na ushauri kutoka kwa Chenge, Mkono, Mwakyembe,...
 
Hiyo ndo Serikali ya awamu ya nne, kama kweli wahe. wabunge walikuwa serious siku wanatoka maazimiop hayo tutaona leo wakikataa upuuzi huu. Huwezi kuwaambia Wabunge makini eti Serikali itazidai fedha ambazo IPTL imelipwa zaidi (itazidai lini? kwanini bado hawajadaiwa?). Wahusika wameandikiwa barua za kujieleza ebo! utafikiri Afisa Mtendaji wa kata anajieleza kwa Mwenyekiti wa Wilaya kumbe PM analijibu bunge. acha tu!!!
 
Hakuna kujadili this time mpaka next bunge, kwahiyo tutajua kama wameikubali au wamekataa bunge lijalo. Lakini kuna ambao tayari wameshaikataa tayari kwa mahojiano ya juu kwa juu.
 
Hivi kweli Tanzania yetu wazalendo wamekufa wote? Vyuo vikuu vyetu vinahitimisha mabwege, ndio maana tupata viongozi mabwege, wabunge mawaziri, rais nk matapeli na mabwege. Tunaelekea wapi?
 
Itakuwa ni maajabu kwa wembe kukata na kuungusha mbuyu, tena mbuyu wenyewe ule wa pale ostaybar dar.

serikali hauna nguvu dhidi ya mafisadi wake walioiweka serikali madarakani, ndio maana katika kashfa zote za ufisadi zinazotokea serikali inaishia KUFUNIKA KOMBE MWANAHARAMU APITE. kitendo cha serikali kuchukua hatua dhidi ya mafisadi ni sawa na kukalia tawi la mti walilokalia wenyewe na matokeo yake ni kujiangusha wenyewe, they will never take action on anything, thats for sure

na katika mapendekezo ya kamati ya bunge, si kazi leo mkaambiwa kuwa rais ameunda tume nyingine ya kufuatilia kama mapendekezo ya kamati teule yanafaa kuchukuliwa hatua na serikali na waandike ripoti baada ya mwaka mmoja, hakuna cha zaidi
 
Ukila na WAZEE haliharibiki NENO!

Sure Wildcard, unajua huko vijijini Maafisa watendaji wa vijiji, Kata hata wa halmashauri wanafukuzwa kazi kila siku kwa kusababisha hasara ya za sh. 10,000, laki ikizidi sana 1 million. Hawa waliolitia Taifa hasara ya mabillioni kama wale wa EPA wanalindwa kwa kuwa wamekula na wakubwa. aibu kubwa hii.

Wiki hii pia kuna kimbembe kule kwa jirani zetu Uganda, jamaa wamekula NSSF vibaya sana tena kwa stahili za kibongo!
 
Hiyo ndo Serikali ya awamu ya nne, kama kweli wahe. wabunge walikuwa serious siku wanatoka maazimiop hayo tutaona leo wakikataa upuuzi huu. Huwezi kuwaambia Wabunge makini eti Serikali itazidai fedha ambazo IPTL imelipwa zaidi (itazidai lini? kwanini bado hawajadaiwa?). Wahusika wameandikiwa barua za kujieleza ebo! utafikiri Afisa Mtendaji wa kata anajieleza kwa Mwenyekiti wa Wilaya kumbe PM analijibu bunge. acha tu!!!

bwana weeeeeee walioambiwa wajieleze wamewaandikisha wake zao mali zao na majumba, Pinda unatupoteze tuu muda wetu
 
Je kweli tulikuwa tunategemea jipya hapa? Nadhani tuliyoyaona kuhusu EPA hatukutakiwa kuwa na mawazo tofauti na yale. Ilishasemwa CCM ni CCM tu, haitabadilika na kuyatetea maslahi ya watanzania wa kawaida, kama wao maslahi yao yanahatarishwa. Muda wa kuiondoa madarakani umefika, tena nadhani tumechelewa sana kufikia uamuzi wa kuwatoa. Wapiganaji tuanze na Tarime. (Tukiwa huko tusisahau hujuma za Kiteto, tujipange haswa)
 
Jamani tukimbilie wapi maana hawa viongozi wetu wanawaongopa sana mafisadi kiasi kwamba hawawezi kuwafanya chochote.na ndio mana maelezo ya Pinda yamejaa maneno tumewaandikia barua za kujitetea sikui kujieleza.Kwa kweli hawa watu wanacheza na akili za watz.
 
Tatizo vyama vya upinzani nao wanaganga njaa zao zao tu, hakuna upinzani wa maana Tanzania, hakuna mikakati yenye maana, wote wamekalia migogoro tu, hatuna mkombozi poor us na CCM haitakuja kubadilika kamwe. Utafikiri tunamkosi!!
 
Tatizo vyama vya upinzani nao wanaganga njaa zao zao tu, hakuna upinzani wa maana Tanzania, hakuna mikakati yenye maana, wote wamekalia migogoro tu, hatuna mkombozi poor us na CCM haitakuja kubadilika kamwe. Utafikiri tunamkosi!!

hapa wala si wakulaumiwa vyama vya upinzani,wao walishafanya kazi yao,wameulezea umma wa wadanganyika juu ya ufisadi wa nchi hii na kuwapa ushahidi wa kutosha.
Tatizo ni la wananchi ambao wao wanadhani upinzani utafanya kila kitu wakati sio kweli,wananchi wanatakiwa kuwaunga mkono wale wate wanao tetea maslahi yao.
Lakini kitu cha ajabu na ndio tatizo lilipo ni kwa wananchi kuto kujua wao wanahusika vipi ktk maamuzi ya serikali yao,madhara ya kuwa na serikali dhaifu kama hii na zilizopita ambazo zime watenga wananchi na kuwakumbuka wakati wa uchaguzi tu.
Hili tatizo ndio limepelekea hata wabunge wetu kuwa wasikilizaji tu na kupiga makofi hata kwa kitu wasichokijua.
Kwa maana hiyo basi Mizengwe K aanza Kupinda na hakutakuwa na mtu wa kumsimamia.
CCM itaendelea kushinda chaguzi zote bila wasiwasi.
 
Kwa anayejua siasa za TZ hili lilitegemewa kabisa. Kama JK ameshindwa kuwaadhibu wezi kweli Pinda angeweza kuwaadhibu waliozembea kama akina Hosea?

Haki imebaki mikononi mwa sisi wananchi hapo 2010. Kama tunataka kuwarudisha watu hawa hawa, wa kujilaumu ni sisi wenyewe.

Anzeni kutafuta majimbo mapema maana kupiga kelele hapa JF pekee haitoshi kabisa.
 
Kwa mujibu wa tangazo la spika wa Bunge alilolitoa muda mchache uliopita ni kuwa Waziri mkuu atawasilisha taarifa yake siku ya alhamisi kuhusiana na utekelezaji wa maazimio 21 ya Bunge kuhusiana na Richmond.

Hivyo basi siku hiyo itakuwa ni siku ya kusikia hatua gani zimechukuliwa na nini kinaendelea.

Huenda tukaambiwa tena kuwa serikali inataka hadi April 2009 ili kuweza kutekeleza maazimio hayo ya Bunge.

Hiki kitakuwa ni kipimo kizuri kama kweli serikali inaheshimu muhimili wa Bunge ama laa ,kwani kama itashindwa kutekeleza maazimio ya Bunge ....

"Richmond kujadiliwa 28-08-2008" Mpaka kieleweke ... anything happening my dear?? .... kwani leo ni tarehe 28, thanks for an update
 
Back
Top Bottom