Serikali ilipokosea katika madai ya madaktari

mgomo haukuwa na SHURUTI, ila HIARI..then if so, iweje leo wajitokeze na kusema "walidanganywa", hoping that we are a great thinkers, does it ring a bell anyhow with their reason?..i dont think so...na hapa ndio walipokosea, kuchanganya kati ya SUBIRA na UKIMYA!!




Nadhani;

WIVU na KUTOJIAMINI:
Mkuu, takribani madaktari 400ambao watahitimu mwaka huu wamepangwa katika hospitali tayari, "wakichukua" nafasi yao, sasa nashindwa kuelewa kwanini baada ya kuona jambo hili likitokea ndio wakumbuke "msamaha" unapaswa kutoka...nisingependa kutoa maneno ya kashfa kwa madaktari wenzangu kwa kiwa ni wanafamilia(kitaaluma), lakini nina uhakika msamaha si wa DHATI ila kurudishwa.


SUBIRA:
Kwa daktari wa kitanzania akaaye masaa 30 macho kabla ya kukabidhi shift nyingine akiwa sehemu mbali mbali (wodini,chumba cha upasuaji,kliniki nk) ambaye amekwishazoea "kutingwa" na utitiri wa kazi, kusubiri bila kufanya kazi, ni MATESO, na hasa inapokuja suala la kimahakama...tofauti na hospitali, mahakama hutaja kesi kwa mpango wake, na huitaji SUBIRA ya hali ya juu kupata kusikilizwa kwa kesi yako..hii imetafsiriwa kuwa ni UKIMYA wa MAT hata mara baada ya MAT kutamka "tusubiri jambo hili lipo kisheria" katika mtandao wao kutokana na wengi(madaktari WALIOFUKUZWA kuwa nje ya jiji na hivyo kuwa ngumu katika kuitisha mkutano physically)


KIBURI:
Ilikuwa ni shida kwao(madaktari "WALIOATHIRIWA" na mgomo kuendelea kusubiri mtaani baada ya kushindwa kwenda nje au kuwa katika ajira binafsi but above all nielewavyo mimi...madaktari wa kitanzania "tuna viburi" at times..na ninasema hivi kwasababu ANTICIPATION before war/battle or any crisis for that matter it's not questionable, lakini kwa baadhi ya madaktari wakitambua kuwa mgomo unaweza kuwatoa kazini.

Kuna msemo unasema "usichague nguo ya kujisitiri ikiwa uko uchi" ..kama mtu aliondoshwa kazini, nijuavyo mimi katika kujisitiri angekuwa na vijikazi vidogo vidogo vimtunze kwa muda hadi pale maamuzi ya mahakama yatapotoka...lakini jambo hili lilikuwa next to impossible kwa baadhi ya madaktari..wakijifariji kwa maneno, "utaua fani", lakini ninachoshindwa kuelewa je fani hiyo ilikuwa "haifi" wakati ukiwa idle??!...but this was used as scapegoat, the truth being Kujishusha ili kufanya kazi hata kama ina kipato kidogo kuliko ulichokuwa unapata ni shida!! wengi walitaka kipato sawa au zaidi..na hicho ndio ninachoita KIBURI.

-lakini mtu anaweza kutafsiri ninawahukumu/kulaumu bure na kuwa sasa ndio "wamejishusha"..ofcourse they have, but is it genuine?..
ingekuwa ni jambo rahisi kuomba msamaha kama suala halipo mahakamani, na takribani wiki mbili zilizopita Mh. Hussein Mwinyi(Waziri wa Afya) alipokuwa pale MNH na MOI alisema "serikali haijawafukuza intern doctors, bali MCT itawaita mmoja mmoja kuwahoji".. sasa swali ni kwamba msamaha huu utabatilisha maamuzi ya Serikali? vipi mahakama na MCT?
 
naona wamelianzisha wenyewe.amsha aliyelala utalala wewe.

Hahaha...sasa huu undumilakuwili sijui utawapeleka wapi...wale wenzao waliowaacha(half the number) hawawezi kuwarudia, kazini hawawezi kurudi waziri ameshawaambia "mwizi akikiri" ni sheria kufata mkondo wake!!... sasa waliikejeli MAT, acha waanze mchakato wa kutafuta wanasheria kabisaaa..
 
Kama liliweza kuwa na mwazo ipo siku litafika mwisho tuu,Nchi ya ahadi ni lazima iwe isiwe nilazima tutafika tuu,inawezekana tukachelewa ila tutafika,itafika kipindi nasisi tutakuwa na vifaa vyote na haki ya madaktari itatekelezwa na kuheshimiwa damu haikumwagika bure.Warudi kazini tuu wakafanye kazi japo wanamaumivu Mungu yupo upande wao na atawatia vungu.Kila lakheri madaktari wetu.
 
Mkuu wamogori, kuna vitu vingi vilisemwa lakini hebu tujijumbushie kupitia thread hii ni vipi vya msingi na visivyo na msingi! ..yaaji madai yapi kati ya hayo hapo juu si/hayakuwa ya lazima!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Small Boy, na Mkuu Lua, ni ngumu sana kwa sisi kufikia huko wa-Afrika kusini walipofikia ikiwa bado haya tunayapuuzia!

haitakuwa ngumu kama tutaamua,tatizo tuliowapa madaraka(wanasiasa) yaani ni bumbumbu wa kutupwa, na wabinafsi wa kutupwa.
kingine ni hawa maprof na specialist doctors hawana msaada wowote katika kushinikiza mabadiliko kwani wamejaa uwoga , kutokujiamini na unafiki
 
haitakuwa ngumu kama tutaamua,tatizo tuliowapa madaraka(wanasiasa) yaani ni bumbumbu wa kutupwa, na wabinafsi wa kutupwa.
kingine ni hawa maprof na specialist doctors hawana msaada wowote katika kushinikiza mabadiliko kwani wamejaa uwoga , kutokujiamini na unafiki

Mkuu, naelewa unachokisema lakini hapa kuna vitu vya kuzingatia.Wewe kama mfanyakazi wa Sekta ya Afya una sehemu yako, lakiji pia wanachi wanasehemu yao...

Ni ukweli ndani yetu kuna kusalitiana na unafiki mwingi lakini hiyo inatokana na kiburi cha elimu, mfano uchache wa wataalamu katika specialities/super speciakity fulani n.k

Hivyo basi wote kama Wananchi, Serikali na Wahudunu wa Afya tuna sehemu ya kufanya katika hili, ..ukweki tunaujua na tunajua givi ndivyo sahihi lakini 'lini hasa' ndilo swali muhinu!
 
Wa-TZ tuache unafiki/ushabiki usio kuwa na msingi, leo muhimbili ukitemvelea (kupitia thread zilizoletwa hapa, picha) zinaonyesha hali ile ile, cha ajabu leo ndio watu wanaguswa?! wakati haya yalisemwa kitambo!!
 
kwani wewe ni raia wa nchi gani embu soma hii Ilani vizuri kwanza katika suala la AFYA

· kwa Afya: Kuhakisha kwamba kila kijiji kinakuwa na Zahanati, kila Kata inakuwa na Kituo cha Afya, kila wilaya inakuwa na Hospitali, na kila Mkoa unakuwa na hospitali ya Rufaa:
· kuwapatia mafunzo watumishi wake ndani na nje ya nchi; kwa

· kuzipatia vifaa bora na vya kisasa hospitali zetu kama vile mashine za mionzi (LINAC machine) kwa ajili ya tiba ya saratani; kununua mashine za mionzi kama vile CT-Scan na MRI kwa ajili ya upasuaji wa ubongo na mgongo.

· Lengo la kufanya hivyo ni kuwezesha upatikanaji wa huduma mahsusi zinazohitaji vifaa na ujuzi mahsusi zipatikane hapa hapa nchini na hivyo kutolazimika kupeleka watu wetu kutibiwa nchi za nje. Aidha, kuajiri wataalamu zaidi wa afya kutoka ndani na nje ya nchi pamoja na kuboresha mazingira ya kazi kwa lengo la kuongeza ubora wa huduma za afya. Hospitali za Wilaya zitaendelea kuimarishwa kwa kuzipatia madaktari, wauguzi, dawa na vifaa tiba vya kutosha. Pia tutatoa motisha kwa watumishi ambao wanafanya kazi katika maeneo yenye mazingira magumu ili kuwajengea ushawishi wa kuendelea kutoa huduma za afya katika maeneo hayo. Utaratibu pia utawekwa utakaowezesha wananchi kuwa na Bima ya Afya ili kumudu gharama za matibabu.

Hizi porojo anazozisema Magufuli zilisemwa na kudaiwa huko nyuma, three years later down the road, haya madai ndiyo mnayaona yanamantiki?


CT Scan, MRI so forth. Hivi uwe na hivi vifaa wakati hata mashine za Xray hakuna na zilizopo zinamatatizo Refer Bombo, Kigoma, Shinyanga, Bugando(Mwanza).


Hivi unahakikishaje kila kijiji kinakuwa na Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali n.k wajati gakuna wataalamu? Unajua idadi ya madaktari wote wako wangapi? Unadhani shida yao ni majengo? Majengo(magofu) yapo lakini yametumiwaje hawa!

Mafunzo ndani na nje ya nchi? Kwa kipi hicho? Ufadhili huu wa wanafunzi chini ya 100 wakati waliochaguliwa ni zaidi ya 700?

BIMA: Mifuko ya vijijini ya bima ilifutwa zamani na hawa wafanyakazi wenyewe wanakatwa gharama bila huduma stahiki.


This is Nonsense.
 
Nianze kusema kuwa mimi ni daktari, na ningependa kwa pamoja tusio madaktari na madaktari tujadiliane katika uzi huu, si kwa kuonyesha hisia (hasira,matusi,kejeli n.k), kupoteza muda, kupotosha madai na taarifa na bali kwa kuona mapungufu ya chanzo cha mgomo kabla ya kujadili madhara yake, ili wote kama watanzania(na wasio watanzania pia) kuliweka sawa hili na kulisaidia Taifa.

MADAI NA UFAFANUZI:
-Uwajibishwaji wa watendaji wakuu wa W/Afya
Ufafanuzi: Kutokana na ubadhirifu uliothibitika, hatua za kinidhamu zilipaswa kufuatwa.

-Uboreshwaji wa Huduma za Afya katika hospitali.
Ufafanuzi: Upatikanaji wa vifaa kazi, madawa na mazingira ya Hospitali ili kutoa huduma stahiki wa wagonjwa. Yaani
Upatikananji wa vitendea kazi:(machine za upimaji moyo, kifua, sukari, uzito, urefu n.k), Mashine za Oxygen, vifaa vya kuongezea maji na damu mwilini n.k .
Upatikanaji wa nyenzo(Machine kama vile CT Scan, MRI, Mashine za mionzi yaani X-ray, mashine za matibabu yaani mionzi ya kutibu saratani)
Mazingira-Kuongeza vitanda, mashuka, huduma za chakula kwa wagonjwa wasio na ndugu n.k

-Posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (Risk allowance) 30% au Chanjo
Ufafanuzi: Katika mazingira ya sasa ambapo unaweza kuambukizwa Kifua kikuu(TB), Homa ya Ini (Hepatitis), UKIMWI (HIV/AIDS) tunapaswa kujikinga dhidi ya magonjwa haya tunapokuwa tukitibu wagonjwa na hivyo ni vyema serikali kutoa chanjo au isipowezekana kutoa chanjo na itoe posho tajwa kujikinga, mfano chanjo ya Homa ya ini pekee kwa mwaka ni mara 3 na inagharimu 45,000 (30USD) kwa kila chanjo.

-Posho ya kuitwa kazini(On call allowance)-5%
Ufafanuzi: Kisheria(Sina uhakika na kifungu), Muda wa kuitwa kazini au katika kada/sekta nyingine huitwa “Overtime” ni asilimia tano(5%) ya mshahara na hivyo, sheria ifuatwe katika hili.

-Posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu(Hardship allowance)-40%
Ufafanuzi: Si madaktari wote(yaani madaktari 1500) wafanyao kazi katika hospitali za serikali wanafanya kazi katika mazingira magumu bali, wachache hasa walio vijijini na hivyo, ili kuwapa motisha na kuonyesha njia ya motisha ili madaktari wasibaki mijini tu na hivyo kuwafanya waende vijijini ili kuepuka usumbufu wa wagonjwa kusafiri toka mkoahadi mkoa kwa matibabu, posho ya mazingira magumu itolewe kwa madaktari hawa walio vijijini na si wote.

-Posho ya Usafiri(10%) au mkopo wa magari.
Ufafanuzi: Kwa madaktari wale kukaa mbali na hospitali, wapatiwe posho hii au mkopo wa gari(NA PESA HII IKATWE KATIKA MSHAHARA). Hii ikiwa na maana daktari aliye zamu na anayeishi(mfano) bunju na kufanya kazi Muhimbili, au anayeishi Vikindu na kufanya kazi Amana, anayeishi kimara mwisho na kufanya kazi Temeke nk katika mikoa mingine anayetakiwa kufika usiku saa nane na hakuna usafiri anaweza kufika kwa wakati.

-Posho ya makazi (30%) au kupatiwa nyumba.
Ufafanuzi: Kisheria (“Doctor is equal to high government officer and is entitled to a house”).Nitapokuwa na vifungu vya sheria nitathibitisha hili. Na kwa kuwa jambo hili lipo kisheria basi na sheria ifuatwe(na ndio Seriakali ilisema inajenga nyumba 700 za madaktari), lakini isipowezekana kwa daktari kupatiwa nyumba(kwa ambao hawana) basi posho ya asilimia 30% itumike kama mbadala.

-Wafanyakazi wote wa Sekta ya Afya wapewe kadi za kijani za bima ya Afya.
Ufafanuzi: Kwa wafanyakazi wa sekta ya Afya yaani madaktari, wauguzi, wafamasia, watu wa maabara, nk. Wapewe bima za Afya wakipata huduma sawa na ile wanayotoa.

-Pendekezo la mshahara kuwa mil. 3.5/=kwa mwezi.
Ufafanuzi: Kama vile mishahara katika Serikali inavyotegemea
*Muda wa masomo wa fani.
*Kiwango cha elimu.
*Ugumu wa masomo wa fani husika.
*Ugumu wa kazi.
*Muda unaotumika kazini.
Hivyo kwa kuzingatia haya, pendekezo la mshahara tajwa utolewe kwa madaktari lakini kama ikishindikana basi Mwajiri(Seerikali) na itoe pendekezo lake.

MAKOSA:
Jumla ya madaktari wote katika hospitali zaSerikali ni 1500, hii ikiwa ni takwimu ya Wizara ya Afya yam waka 2011 na ikijumuisha zaidi ya madaktari 300 waliofukuzwa na 150 waliokwenda nje tayari hadi leo trh 17.07.2012. Hivyo tafsiri iliyotumika ni ;
-Daktari hayuko entitled kupata nyumba kama high government official kama ilivyoainishwa kisheria
-Daktari hatakiwi kulipwa overtime (call allowance)mara baada ya muda wa kazi kwa aslimia tano ya mshahara
-Tafsiri ya kuwa madaktari wote huwa wanakuwa zamu za usiku (overtime) na hivyo kuwekakiasi cha posho tajwa juu kuwa ya madaktari wote na kila siku!
-Tafsiri ya pesa ya mazingira magumu kwa madaktari wote(KWANI SI MADAKTARI WOTE WAKO MAZINGIRA MAGUMU YA VIJIJINI)
-Tafsiri ya kutaka posho ya mazingira hatarishi pekee badala nyenzo za kujikinga na chanjo
-Tafsiri kuwa wafanyakazi wengine wa sekta ya afya hawakujumuishwa katika madai.
-Tafsiri ya pendekezo la mshahara tajwa kuwa ni SHURUTI ya kurudi kazini.
-Tafsiri ya kuwa PENDEKEZO la mshahara haliwezi kupungua!

Jana,Rais Magufuli amejionea taswira ya idara ya afya na huduma kwa wagonjwa. Amewaona wagonjwa wakiwa hawana tiba ila tabu hadi aibu. Amewaona wauguzi wakisema asichokiamini. Taswira inayojaza hasira.

Dr. Stephen Ulimboka alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Taasisi za Madaktari nchini Tanzania. Alikuwa na fikra,hoja na nia za kupigania ubora wa idara ya afya hasa hospitalini. Alitaka maboresho ya maslahi ya matabibu na hata vifaa-tiba viwepo.

Dr. Ulimboka alipigania ustawi. CT-Scan na vifaa vingine vya tiba hospitalini havikuwa vikikauka kinywani mwake. Maboresho na ustawi wa kwenye afya alipambania. Yakampata ya kumpata! Rais Magufuli ameona na kuguswa. Hadi atatumia mshahara wake kumtibu mgonjwa fulani pale Muhimbili, aliyelazwa miezi miwili bila tiba.

Dr. Ulimboka atumike kukumbusha hoja za kitabibu. Rais Magufuli amekuwa shahidi mzuri. Kama Muhimbili kuna hali ile,kwingineko kukoje?

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Magufuli aliijua hali ile toka zamani na anajua kwa kumbadilishia kituo cha kazi Mkurugenzi Mkuu haina manufaa yeyote, ngoja aendelee kuwachezea ngoma!
 
Wanasiasa wanacheza na akili za watanzania,na kwakuwa watanzia tuliowengi tuwapumbavu acha wafurahie huu mchezo wao.
 
Kumbe muda ni rafiki mzuri wa ukweli.
Sasa tunaweza kujua kuwa Dr. Ulimboka na waliomteka pamoja na kutaka kumuua ni nani alikuwa analinda maslahi mapana ya taifa. Na sasa ndio tuelewe kuwa 'kushughulikiana' kunalifanya taifa 'stagnant'.
 
Back
Top Bottom