Serikali iingilie kati tiba ya Dr. Ndodi wananchi wanaliwa fedha nyingi na hawaponi

Kingcobra

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
1,000
309
Ndugu zangu wanaJF,

Mengi yameongelewa humu JF juu ya mtu anayejiita Dr. Ndodi kuhusu utapeli wake. Mwanzoni nilidhani wanamwonea lakini mimi mwenyewe nimeshuhudia kwa macho yangu. Kuna kijana mmoja wa kiarabu ni jirani yangu anasumbuliwa sana na pumu. Baada ya kumwona na kumsikia ndodi kupitia vipindi vyake vya TV na radio nilimshauri huyo kijana amwone ndodi. Alipofika kwenye zahani magomeni mwembechai aliambiwa dawa inauzwa sh. 70,000 na utaratibu ni kwamba unanunua kwanza ndipo upate maelezo ya namna ya kutumia. Aliponunua akaenda kumwona ndodi. Maelezo aliyopata ni kwamba dawa aliyonunua ataitumia kwa wiki moja tu. Baada ya hapo itabidi afuate dawa nyingine kwa bei hiyohiyo na ataendelea kufanya hivyo kwa wiki kumi. Yule kijana alishangaa sana. Alitaka kuacha dawa ili arejeshewe fedha lakini ilishindikana. Aliporudi nyumbani, mimi pamoja na jirani wengine tulimshauri asikate tamaa bali atafute namna ya kupata fedha ili ahakikishe kuwa anamaliza dozi nzima. Bahati nzuri ndugu zake ambao wapo Oman walimchangia kiasi kikubwa cha fedha na akamudu kulipa fedha yote yaani sh. 700,000 mpaka akamaliza dozi. Kinachosikitisha ni kwamba mpaka sasa hakuna nafuu yoyote aliyopata. Pumu bado inamsumbua vilevile. Mbaya zaidi alipokwenda kwa ndodi aliambiwa kuwa eti inawezekana hakuwa anazingatia muda wa kunywa. Kwa hiyo, itabidi aanze dozi upya kwa bei ya sh. 600,000 kwa dozi nzima. Jambo hilo ndilo lililoniuma kiasi cha kuamua kuleta humu jamvini. Ukweli ni kwamba kijana wa watu alikuwa anazingatia sana muda. Mimi mwenyewe nilimsisitiza sana tangu mwanzoni kwamba dozi ya muda mrefu huwa ni muhimu sana kuzingatia muda na nilimshauri aiseti simu yake ya mkononi iwe inamkumbusha na alifanya hivyo.

My take:
Kuna wimbi kubwa limejitokeza katika miaka ya hivi karibuni ya watu kugeuza afya za binadamu wenzao kuwa mitaji. Wengi wao kama ilivyo kwa ndodi wanatumia hata misahafu kama biblia kuvuta wateja wengi. Madhara yake ndiyo hayo yaliyomkumba kijana wa kiarabu. Fedha nyingi zinatumika na hakuna nafuu inayopatikana. Ebu fikiri, katika hali ya sasa ya maisha magumu, mgonjwa analipa zaidi ya shilingi milioni moja na haponi, inaumiza kiasi gani. Ifike mahali Serikali iwaonee huruma watu wake kwa kuchukua hatua madhubuti ya kuwabana akina ndodi. Kwanza wachunguzwe kama kweli tiba zao ni za kweli. Pili wachunguze uhalali wa bei wanazowatoza wagonjwa.
 
Huyu ndodi mbona analalamikiwa na watu wengi sasa! Inawezekana kuna ukweli. WanaJF wenye influence kwenye system watusaidie kumfuatilia huyu tapeli. Nasikia kuna wakati serikali ilitaka kumfuatilia na yeye alishtuka na kuacha kujitangaza. Lakini hivi karibuni naona amerejea kwa kasi kubwa.
 
Ndugu yangu, kama nawe una amini katika dini zetu 2 zinazo2eleza kuna maisha baada ya kifo, basi tutashangaana sana huko tuendapo. Watu wamegeuza dini zetu mtaji, kwa kufungua vitabu vyetu vya dini wanatutapeli na kufanya ndio nyenzo ya maisha yao. Tulaani vitendo hvi na hatua za haraka za kisheria zichukuliwe.
 
Ndugu zangu wanaJF,

Mengi yameongelewa humu JF juu ya mtu anayejiita Dr. Ndodi kuhusu utapeli wake. Mwanzoni nilidhani wanamwonea lakini mimi mwenyewe nimeshuhudia kwa macho yangu. Kuna kijana mmoja wa kiarabu ni jirani yangu anasumbuliwa sana na pumu. Baada ya kumwona na kumsikia ndodi kupitia vipindi vyake vya TV na radio nilimshauri huyo kijana amwone ndodi. Alipofika kwenye zahani magomeni mwembechai aliambiwa dawa inauzwa sh. 70,000 na utaratibu ni kwamba unanunua kwanza ndipo upate maelezo ya namna ya kutumia. Aliponunua akaenda kumwona ndodi. Maelezo aliyopata ni kwamba dawa aliyonunua ataitumia kwa wiki moja tu. Baada ya hapo itabidi afuate dawa nyingine kwa bei hiyohiyo na ataendelea kufanya hivyo kwa wiki kumi. Yule kijana alishangaa sana. Alitaka kuacha dawa ili arejeshewe fedha lakini ilishindikana. Aliporudi nyumbani, mimi pamoja na jirani wengine tulimshauri asikate tamaa bali atafute namna ya kupata fedha ili ahakikishe kuwa anamaliza dozi nzima. Bahati nzuri ndugu zake ambao wapo Oman walimchangia kiasi kikubwa cha fedha na akamudu kulipa fedha yote yaani sh. 700,000 mpaka akamaliza dozi. Kinachosikitisha ni kwamba mpaka sasa hakuna nafuu yoyote aliyopata. Pumu bado inamsumbua vilevile. Mbaya zaidi alipokwenda kwa ndodi aliambiwa kuwa eti inawezekana hakuwa anazingatia muda wa kunywa. Kwa hiyo, itabidi aanze dozi upya kwa bei ya sh. 600,000 kwa dozi nzima. Jambo hilo ndilo lililoniuma kiasi cha kuamua kuleta humu jamvini. Ukweli ni kwamba kijana wa watu alikuwa anazingatia sana muda. Mimi mwenyewe nilimsisitiza sana tangu mwanzoni kwamba dozi ya muda mrefu huwa ni muhimu sana kuzingatia muda na nilimshauri aiseti simu yake ya mkononi iwe inamkumbusha na alifanya hivyo.

My take:
Kuna wimbi kubwa limejitokeza katika miaka ya hivi karibuni ya watu kugeuza afya za binadamu wenzao kuwa mitaji. Wengi wao kama ilivyo kwa ndodi wanatumia hata misahafu kama biblia kuvuta wateja wengi. Madhara yake ndiyo hayo yaliyomkumba kijana wa kiarabu. Fedha nyingi zinatumika na hakuna nafuu inayopatikana. Ebu fikiri, katika hali ya sasa ya maisha magumu, mgonjwa analipa zaidi ya shilingi milioni moja na haponi, inaumiza kiasi gani. Ifike mahali Serikali iwaonee huruma watu wake kwa kuchukua hatua madhubuti ya kuwabana akina ndodi. Kwanza wachunguzwe kama kweli tiba zao ni za kweli. Pili wachunguze uhalali wa bei wanazowatoza wagonjwa.

Kwanza nampa pole sana kijana wa watu kwa kutapeliwa kiasi hicho. Kwa kweli inatia uchungu sana hasa kwa mwanachi ambaye hana uwezo wa kuchukua hatua yoyote ile zaidi ya kuendelea kuumia.

Mimi nashauri ianzishwe operation maalum ya kuwapitia watu wote wanaojiita madaktari na kuwakagua kwa kina uhalisia na uhalali wa tiba zao na zichukuliwe hatua za kisheria tena kali ili kutoa funzo kwa matapeli wengine. Ndodi ni tapeli tena mkubwa. Anawavuta wananchi wengi kwa porojo zake anazoongea kama cherehani. Mimi ni mmoja wa watu waliotapeliwa na ndodi na niliandika thread kulaani kitendo hicho na kutoa wito kwa serikali imfuatilie ili wananchi wengi zaidi wasitapeliwe.
 
Pole sana; nakubaliana na wewe sasa hivi watu wanatumia matatizo ya watu kuwa mtaji! Inasikitisha sana. Sasa ushauri wangu, mwambie huyo rafiki yako atafute mmea uitwao (scientific name) Euphorbia hilta (mziwaziwa- Swahili au Athma weed- English) na majani ya mpapai, akaushie ndani then:-
-Asokote sigara avute au
-Aunguze chumbani wakati wa kulala (kama udi)
Inatuliza; haiponyeshi!
 
Ndodi!Ndodi!Ndodi!
Huyu mjomba ni Tapeli wa Kimataifa.Kuna siku 1 kwenye STARTV,alimkodi maza mmoja hv kuja kutoa ushuhuda wa tiba ya huyo TAPELI.Mtangazaji wa STAR akamuuliza yule MAZA,kwamba alitumia aina gani ya MATUNDA na kufanikiwa kupona mwanaye?Yule Maza akajitafuma sana na akashindwa kujua hata tunda gani lililo mponyesha mwanaye!Huyu Mjomba kifupi ni Mwizi Mkubwa huyu.Wananchi inabidi wawe na Mwamko!Vinginevyo wataliwa fedha zao bure.
 
Serikali inashindwa kumchukulia hatua kwa vile Dr Ndodi analindwa na sheria ya Tiba asilia na tiba mbadala ambayo inawatambua waganga wa kienyeji wote. TFDA wamejitahidi kumdhibiti kwa kutumia sheria namba 1 ya mwaka 2003 ya kudhiditi vyakula, dawa na vipodozi lakini wamegonga mwamba
 
Makanisa yamekuwa mitaji ya kutapeli watu siku hizi. Ndo yale yale ya vikombe vya babu loliondo, bibi tabora, ndodi wa mahotelini makubwa, kina DECI nk. Yote hayo matunda ya makanisa.
 
Sasa hivi anahamasisha watu waende wakapate dawa bure ila waende na pesa ya kumuona daktari (yeye ndodi). Sababu ya kutoa dawa bure anadai kuna mtu mmoja alimlipia pesa ya vipindi vya kwenye tv. Inawezekana hata hakulipiwa chochote ila alipanga dili na huyo mama mtoa ushuhuda ili kuwavuta watu maana nasikia hata hiyo pesa ya kumuona daktari nasikia haishikiki.
 
Makanisa yamekuwa mitaji ya kutapeli watu siku hizi. Ndo yale yale ya vikombe vya babu loliondo, bibi tabora, ndodi wa mahotelini makubwa, kina DECI nk. Yote hayo matunda ya makanisa.

Kwani Ndodi anatumia Kanisa au Biblia? Jaribuni kujua kutofautisha mambo? Ukweli matapeli wapo na lazima wajaribu kutumia maeneo yanayoaminika ili wawapate! Taadhari ni kwamba yalitabiriwa na kwa sababu watu hawataki mafundisho ya kweli na wanataka mambo rahisi ya kufanikiwa kwa Shortcut lazima wadanganywe. Ila nawasihi watumishi wa kweli wawafundishe wtu wao na pia wakemee jambo hili hadharani maana ukimya wao ndiyo maumivu yetu
 
Sasa hivi anahamasisha watu waende wakapate dawa bure ila waende na pesa ya kumuona daktari (yeye ndodi). Sababu ya kutoa dawa bure anadai kuna mtu mmoja alimlipia pesa ya vipindi vya kwenye tv. Inawezekana hata hakulipiwa chochote ila alipanga dili na huyo mama mtoa ushuhuda ili kuwavuta watu maana nasikia hata hiyo pesa ya kumuona daktari nasikia haishikiki.

Nilivyousikia ushuhuda wa yule mama startv, alafu ndodi nae akatangaza ofa ya kupata dawa bure isipokuwa uende na kiingilio tu, ilibidi nami niende kesho yake hapo magomeni kufukuzia ofa. Kichonistua ni ukubwa wa hicho kiingilio chake nikaambiwa sh.50,000. kwa kweli sikuamini ikabidi niondoke haraka sana. Afu huwa hatangazi ktk media hicho kiingilio ni mpaka uende ili akakutapeli hukohuko. Kweli huu ni wizi jaman.
 
Nilivyousikia ushuhuda wa yule mama startv, alafu ndodi nae akatangaza ofa ya kupata dawa bure isipokuwa uende na kiingilio tu, ilibidi nami niende kesho yake hapo magomeni kufukuzia ofa. Kichonistua ni ukubwa wa hicho kiingilio chake nikaambiwa sh.50,000. kwa kweli sikuamini ikabidi niondoke haraka sana. Afu huwa hatangazi ktk media hicho kiingilio ni mpaka uende ili akakutapeli hukohuko. Kweli huu ni wizi jaman.
Ukosefu wa elimu unaiangamaiza Tanzania! Bado tumejifunika kwenye blanketi la ujinga na umbumbumbu!
 
Ndodi ni kiboko niliwahi kwenda siku moja kumwona,nikaambiwa kuongea nae ni TSHS 50,000/=hapo bado sijaambiwa dawa,Eeeh niligeuka faster na kuondoka,huyu jamaa yuko kimaslahi zaidi na sio kuwasaidia watu kama anavyodai.
 
pole mwarabu me nakushauri uje loliondo kwa babu na jero yako tu upate kikombe cha uzima na kama hutak utaendelea kutapeliwa tu maana hapo bado hujaenda kwa sheik yahya atakwambia kuita jini moja laki 2. magomen ni makaz ya matapeli,wakabaji, walaghai ht mafisadi wapo take care bro.
 
Ndodi!Ndodi!Ndodi!
Huyu mjomba ni Tapeli wa Kimataifa.Kuna siku 1 kwenye STARTV,alimkodi maza mmoja hv kuja kutoa ushuhuda wa tiba ya huyo TAPELI.Mtangazaji wa STAR akamuuliza yule MAZA,kwamba alitumia aina gani ya MATUNDA na kufanikiwa kupona mwanaye?Yule Maza akajitafuma sana na akashindwa kujua hata tunda gani lililo mponyesha mwanaye!Huyu Mjomba kifupi ni Mwizi Mkubwa huyu.Wananchi inabidi wawe na Mwamko!Vinginevyo wataliwa fedha zao bure.

nakumbuka yule mama baada ya kumsikiliza majibu yake mimi niligundua kuwa sio shuhuda bali ni mtu wa karibu na ndodi. Jinsi alivyo anza kujieleza ilionesha hajui ila alimshukuru ndodi,jinsi alivyobanwa kwa maswali na mtangazaji basi alianza kujichanganya na hatimaye nikagundua ni mtaalam wa
Ndodi pia katika zahanati yake.Sio huyu mama tu bal hata chanel 5(eatv) aliwahi kuleta mabinti wawili na mambo nikaona ni yaleyale kuwa ni wahudumu wake.Naamini wafuatiliaji wa vipindi vyake wanaweza kuongezea juu ya hao mashuhuda.
 
pole mwarabu me nakushauri uje loliondo kwa babu na jero yako tu upate kikombe cha uzima na kama hutak utaendelea kutapeliwa tu maana hapo bado hujaenda kwa sheik yahya atakwambia kuita jini moja laki 2. magomen ni makaz ya matapeli,wakabaji, walaghai ht mafisadi wapo take care bro.
Magomeni ni makazi ya SHEIKH-TWAIN
 
jaman huyu bwana ni msabato mwenzangu na mimi na msifu kwa mafundisho yake tu lakini kwa uganga wake sijakubaliana nao mpka kesho kwa sababu navyo wajua wasabato huwa ni watu wa huruma sana na wanapenda kusaidia sana lakini kwa ndondi sijamkubali na sijaona usabato wake kwa watu wenye kuteseka na magonjwa mbali mbali pia kama Mungu ndiye aliyemjalia kuwa na uwezo wa kutibu basi ilitakiwa atumie nafasi hyo kuwasaidia watu kwa ghalama kidogo
 
Ndugu zangu wanaJF,

Mengi yameongelewa humu JF juu ya mtu anayejiita Dr. Ndodi kuhusu utapeli wake. Mwanzoni nilidhani wanamwonea lakini mimi mwenyewe nimeshuhudia kwa macho yangu. Kuna kijana mmoja wa kiarabu ni jirani yangu anasumbuliwa sana na pumu. Baada ya kumwona na kumsikia ndodi kupitia vipindi vyake vya TV na radio nilimshauri huyo kijana amwone ndodi. Alipofika kwenye zahani magomeni mwembechai aliambiwa dawa inauzwa sh. 70,000 na utaratibu ni kwamba unanunua kwanza ndipo upate maelezo ya namna ya kutumia. Aliponunua akaenda kumwona ndodi. Maelezo aliyopata ni kwamba dawa aliyonunua ataitumia kwa wiki moja tu. Baada ya hapo itabidi afuate dawa nyingine kwa bei hiyohiyo na ataendelea kufanya hivyo kwa wiki kumi. Yule kijana alishangaa sana. Alitaka kuacha dawa ili arejeshewe fedha lakini ilishindikana. Aliporudi nyumbani, mimi pamoja na jirani wengine tulimshauri asikate tamaa bali atafute namna ya kupata fedha ili ahakikishe kuwa anamaliza dozi nzima. Bahati nzuri ndugu zake ambao wapo Oman walimchangia kiasi kikubwa cha fedha na akamudu kulipa fedha yote yaani sh. 700,000 mpaka akamaliza dozi. Kinachosikitisha ni kwamba mpaka sasa hakuna nafuu yoyote aliyopata. Pumu bado inamsumbua vilevile. Mbaya zaidi alipokwenda kwa ndodi aliambiwa kuwa eti inawezekana hakuwa anazingatia muda wa kunywa. Kwa hiyo, itabidi aanze dozi upya kwa bei ya sh. 600,000 kwa dozi nzima. Jambo hilo ndilo lililoniuma kiasi cha kuamua kuleta humu jamvini. Ukweli ni kwamba kijana wa watu alikuwa anazingatia sana muda. Mimi mwenyewe nilimsisitiza sana tangu mwanzoni kwamba dozi ya muda mrefu huwa ni muhimu sana kuzingatia muda na nilimshauri aiseti simu yake ya mkononi iwe inamkumbusha na alifanya hivyo.

My take:
Kuna wimbi kubwa limejitokeza katika miaka ya hivi karibuni ya watu kugeuza afya za binadamu wenzao kuwa mitaji. Wengi wao kama ilivyo kwa ndodi wanatumia hata misahafu kama biblia kuvuta wateja wengi. Madhara yake ndiyo hayo yaliyomkumba kijana wa kiarabu. Fedha nyingi zinatumika na hakuna nafuu inayopatikana. Ebu fikiri, katika hali ya sasa ya maisha magumu, mgonjwa analipa zaidi ya shilingi milioni moja na haponi, inaumiza kiasi gani. Ifike mahali Serikali iwaonee huruma watu wake kwa kuchukua hatua madhubuti ya kuwabana akina ndodi. Kwanza wachunguzwe kama kweli tiba zao ni za kweli. Pili wachunguze uhalali wa bei wanazowatoza wagonjwa.

poleni unaweza kuspendi hela nyingi pasipo kujua wakati ulitakiwa usitumie hata laki moja, kama uko dar ndio rahisi kabisa tafuta simbi nikuelekeze ni dozi ya siku 3, achana na matapeli hao
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom