Serikali ifanye haya kutokomeza mimba za utotoni. Kuwafunga watu miaka 30 siyo suluhisho

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,279
21,396
Habari za majukumu wananchi na wabunge mliomo humu JF;

''KUWAFUNGA VIJANA WA KIUME PEKEE; NI KUTUACHIA YATIMA PASIPO ULAZIMA SISI, WAZAZI NA WAJUKUU ZETU NDIO TUTAKAOUMIA NA HILO.''

Kuna mswada ule uliopelekwa bungeni kuhusu wale wanaowatia mimba watoto waliochini ya miaka 18, Napongeza kwa hatua hiyo ya dhati ya serikali kuthubutu kuonesha nia ina mpango wa kupunguza mimba za utotoni; Mswada huo ukipita na kuwa sheria bado hauta tatua moja kwa moja hili tatizo la mimba za utotoni kutokana na kwamba halitakuwa suruhisho bali Tutakuwa tunatengeneza matatizo mengine ambayo ni makubwa zaidi kuliko hata tatizo lenyewe kama ifuatavyo;

1. Hii sheria endapo mtuhumiwa atafungwa miaka 30, itasababisha ongezeko la watoto tegemezi mtaani kwakuwa majukumu ya kulea huyo mtoto yatafanywa na watu wengine.

2. Itasababisha sisi wazazi wa mabinti waliotiwa mimba tuhakikishe tunayamaliza kifamilia na wakwe zetu (watia mimba wa wanetu) kwa kuhofia kuachiwa mzigo huo mkubwa wa kulea wajukuu kwa miaka 30 bila msaada na kuongeza makali ya maisha.

3. Tunawanyima haki wajukuu zetu watakaozaliwa kuwaona baba zao kwa miaka 30 kwa kuishi kama yatima jambo ambalo ni kinyume na haki za binadamu.

4. Watoto hawa wanaweza kuwa wapo kwenye hatari kubwa ya kukosa maadili katika maisha yao yote.

5. Itachangia sana sana kwa kupunguza upendo baadhi ya wazazi kuwachukia hasa wapatapo/wazaapo watoto wa kike na kuongeza mfumo dume hapa nchini kwa kuwanyanyapaa.

6. Hao mabinti watawaficha mabwana zao kwa kuhofia kukosa misaada endapo wakifungwa jera.

7. Kwa sheria hiyo; serikali itakuwa imeongeza kwa kasi kubwa utoaji wa mimba kwa mabinti zetu kwani watalazimika kuzitoa kwa gharama yeyote ile pasipo hata kujali athari ya afya kimwili na kiimani kitu ambacho kitachangia vifo kwa mabinti zetu kupitia huu utoaji mimba.

8. Hii sheria itahitaji uthibitisho wa madaktali (DNA) kuhusu ukweli wa jambo lenyewe kwa mtuhumiwa iwapo ni kweli kahusika kumpa ujauzito au la! Ili kuepusha visasi na kubambikiana kesi hizi kimajungu.

9. Kwa uthibitisho huo wa madaktali; serikali itawajibika kutafta ukweli kwakuwa na madaktali wa kutosha nchi nzima hadi vijijini vinginevyo sheria hii itafanya kazi mjini tu.

10. Tutapoteza nguvu kazi ya vijana wetu wengi kwa kuwafunga miaka 30 jela; wakati kuna njia mbadala wa kumaliza jambo hilo Kwakuwa lengo nikutokomeza na si kukomoana.

Note; Sheria hiyo ya miaka 30 jera itumike kwa matukio maalum ya kikatili ya ubakaji bila kujali kabakwa nani, awe mtoto wa shule au mama mtu mzima ie. Kama tukio la kule morogoro n,k.. LAKINI KWA WATOTO WETU WALIOTIWA MIMBA MASHULENI KWA RIDHAA YAO SISI WAZAZI NDIO TUTAKAOUMIA.

Nashauri haya yafanyike Mbadala ili kutokomeza hizi mimba za utotoni kirahisi kabisa:


  1. Pitisheni sheria Kali (kwa watoto wa kike) za kufunga wasichana wanaobeba mimba kifungo cha inje miaka 20 na viboko 100, Hii sheria ihubiliwe hadi vijijini, Mtaona kama binti hata mmoja atakaethubutu kufanya ngono tena wakati anafaham kuna viboko na jela vinamsubili akibeba mimba.
  2. kifungo cha miaka 30 kibaki kwa wabakaji tu, bila kujali aliyebakwa ni mwanafunzi au mtu mzima.
  3. Zitolewe semina kwa walimu ili wawafundishe watoto wa kike mashuleni Athari za kujamiiana chini ya miaka 18; kiafya na kielimu.pia wazazi na jamii nzima Tupige marufuku uvaaji Wa vimini Kwa watoto kuwa endapo mtoto akionekana kavaa akamatwe na kuadhibiwa na wazazi wapigwe faini Kwa malez mabovu.
  4. Masomo ya afya ya uzazi mashuleni (reproduction system) yafundishwe kijinsia(Gender teaching) , Wanafunzi wa kike wasifundishwe wakiwa mchanganyiko na wakiume- Kwani haya masomo yanapofanyika kwa pamoja na wanaume, yanawaongezea sana watoto wa kike ujasiri wa kutokuwaogopa wanaume kihisia, pia hulahisisha sana kutongozana wao kwa wao
  5. Serikali kupitia wizara ya afya na ustawi wa jamii iweke mikakati ya kupima bikira za wanafunzi kila mara na wawe na kadi maalumu kama zilivyo za kliniki za watoto, wapimwe wakiwa darasa la 4,5 na la 7 kwa shule ya msingi. Na kabla ya kujiunga form 1 wapimwe, pia fom 2,3,4,5 na 6 wapimwe kila waanzapo na wamalizapo mhura wa masomo. Kama hilo watashindwa,basi wapime hizo bikira japo mara moja moja darasa la 7, form 2,4,5 na 6 lengo nikuongeza hofu, pia kwa watoto mabikira wapate motisha za kupewa kipaumbele kukaa hostel kuliko wengine n.k
  6. Serikali kupitia wizara ya elimu na ustawi wa jamii; iweke mikakati mathubuti mashuleni kwa kuweka mpango maalumu wa (periodic pregnant testing for student ); kwa darasa la 5 na la 7 kwa shule za msingi, kwa secondary fomu one hadi formu 4 wapimwe hata kila mwaka, hii itaongeza hofu kwa wanafunzi wenyewe na wazazi watashiriki kwa ukamilifu kusimamia zoezi hilo.

Hayo yote yataenda sambamba na wale wote wanaoonekana kujihusisha na mapenzi shuleni ili wakanywe ama waondolewe kabisa mashuleni kwa Suspension na wale wote wenye kuthibitishwa kuwa na mahusiano na mwanafunzi kimapenzi wakamatwe mara moja; hilo likifanyika litasaidia kutisha wengine kutojihusisha na mapenzi mashuleni…hilo hata sisi wazazi tutashiriki kwa hali na mali kulitekeleza.

Mpango huo wa kuwapima watoto kila mara; utatumika kama tangazo la kupinga mimba za utotoni, kwahiyo utasambaa hadi huko vijinini kupitia kwa wanafunzi wenyewe.

Maadili yatalejea kwa watoto na pengine hata wakafika chuo na bikira zao.

Taifa litapata mama bora na wenye familia na maadili.

Sisi wazazi tutajivunia pia kuzaa watoto wa kike kwa maana tutakuwa naimani wapo katika jamii salama tofauti na presha tulizo nazo sasa.

KUWAFUNGA WATIA PEKEE MIMBA HAITAONDOA TATIZO KWASABABU VITOTO VYA KIKE HAVIGUSWI NA SHERIA YA KIFUNGO HIVYO HAVITAACHA KUJIRENGESHA.

NAOMBA KUWASILISHA MSWADA HUU, KARIBUNI TUJADILI WADAU.

NB: Kama una hoja tofauti/mbadala ya kutokomeza mimba iweke hapa pia ijadiliwe.

Updates;
Tazama video ya wabunge wanaochangia juu ya hili moja kwa moja hapa;
 
Hahaha periodic pregnancy testing imenikumbusha kipindi nasoma shule flani hivi walikua wanatukurupua tu kila baada ya miezi kadhaa wanatupima ujauzito kwa mikono,wapo baadhi ya mabinti waligundulika kwa style hio wakarudishwa nyumbani mara moja,
 
Hayo yote u ayosema hayawezekani kwa kuwa sasa serikali imekuwa inatoa condom kwa wanafunzi sasa unategemea nini?

Walimu wenyewe ambao wanatakiwa kujitoa kwa kazi hiyo mishara yao ni matusi makubwa!
Hai unaowataka watunge sheria hizo ndo watuhumiwa
 
Ushauri mzuri pia condom ziongezwe radha ili wanafunzi wapende kuzitumia mana serikali imeruhusu zitumiwe mashulen
 
Kabla ya mswaada huu kwa sasa sheria ikoje kuhusu wanaowapa mimba mabinti ambao umri wao ni chini ya miaka 18?
 
Hahaha periodic pregnancy testing imenikumbusha kipindi nasoma shule flani hivi walikua wanatukurupua tu kila baada ya miezi kadhaa wanatupima ujauzito kwa mikono,wapo baadhi ya mabinti waligundulika kwa style hio wakarudishwa nyumbani mara moja,
Yote yanawezekana mbona serikali ikijipanga.
 
Hahaha periodic pregnancy testing imenikumbusha kipindi nasoma shule flani hivi walikua wanatukurupua tu kila baada ya miezi kadhaa wanatupima ujauzito kwa mikono,wapo baadhi ya mabinti waligundulika kwa style hio wakarudishwa nyumbani mara moja,
Umenikumbusha, hata mi nilisoma shule moja hiv iko Moshi, tulikuwa tunafanyiwa hilo zoezi.
 
Hoja inamantiki, subiri tusikie sisiem walio bungeni wanasemaje!
Shida ya wale utasikia wanasema wanapinga lakini ikifika wakati wa kupitisha utasikia wanasema wanaunga mkono kwa asilimia 100 na kuanza kupiga meza huku wakisema, ndiyoooooo!
 
Habari za majukumu wananchi na wabunge mliomo humu JF;

''KUWAFUNGA; NI KUTUACHIA YATIMA PASIPO ULAZIMA SISI, WAZAZI NA WAJUKUU ZETU NDIO TUTAKAOUMIA NA HILO.''

Kuna mswada ule uliopelekwa bungeni kuhusu wale wanaowatia mimba watoto waliochini ya miaka 18, Napongeza kwa hatua hiyo ya dhati ya serikali kuthubutu kuonesha nia ina mpango wa kupunguza mimba za utotoni; Mswada huo ukipita na kuwa sheria bado hauta tatua moja kwa moja hili tatizo la mimba za utotoni kutokana na kwamba halitakuwa suruhisho bali Tutakuwa tunatengeneza matatizo mengine ambayo ni makubwa zaidi kuliko hata tatizo lenyewe kama ifuatavyo;

1. Hii sheria endapo mtuhumiwa atafungwa miaka 30, itasababisha ongezeko la watoto tegemezi mtaani kwakuwa majukumu ya kulea huyo mtoto yatafanywa na watu wengine.

2. Itasababisha sisi wazazi wa mabinti waliotiwa mimba tuhakikishe tunayamaliza kifamilia na wakwe zetu (watia mimba wa wanetu) kwa kuhofia kuachiwa mzigo huo mkubwa wa kulea wajukuu kwa miaka 30 bila msaada na kuongeza makali ya maisha.

3. Tunawanyima haki wajukuu zetu watakaozaliwa kuwaona baba zao kwa miaka 30 kwa kuishi kama yatima jambo ambalo ni kinyume na haki za binadamu.

4. Watoto hawa wanaweza kuwa wapo kwenye hatari kubwa ya kukosa maadili katika maisha yao yote.

5. Itachangia sana sana kwa kupunguza upendo baadhi ya wazazi kuwachukia hasa wapatapo/wazaapo watoto wa kike na kuongeza mfumo dume hapa nchini kwa kuwanyanyapaa.

6. Hao mabinti watawaficha mabwana zao kwa kuhofia kukosa misaada endapo wakifungwa jera.

7. Kwa sheria hiyo; serikali itakuwa imeongeza kwa kasi kubwa utoaji wa mimba kwa mabinti zetu kwani watalazimika kuzitoa kwa gharama yeyote ile pasipo hata kujali athari ya afya kimwili na kiimani kitu ambacho kitachangia vifo kwa mabinti zetu kupitia huu utoaji mimba.

8. Hii sheria itahitaji uthibitisho wa madaktali (DNA) kuhusu ukweli wa jambo lenyewe kwa mtuhumiwa iwapo ni kweli kahusika kumpa ujauzito au la! Ili kuepusha visasi na kubambikiana kesi hizi kimajungu.

9. Kwa uthibitisho huo wa madaktali; serikali itawajibika kutafta ukweli kwakuwa na madaktali wa kutosha nchi nzima hadi vijijini vinginevyo sheria hii itafanya kazi mjini tu.

10. Tutapoteza nguvu kazi ya vijana wetu wengi kwa kuwafunga miaka 30 jela; wakati kuna njia mbadala wa kumaliza jambo hilo Kwakuwa lengo nikutokomeza na si kukomoana.

Note; Sheria hiyo ya miaka 30 jera itumike kwa matukio maalum ya kikatili ya ubakaji bila kujali kabakwa nani, awe mtoto wa shule au mama mtu mzima ie. Kama tukio la kule morogoro n,k.. LAKINI KWA WATOTO WETU WALIOTIWA MIMBA MASHULENI KWA RIDHAA YAO SISI WAZAZI NDIO TUTAKAOUMIA.

Nashauri haya yafanyike Mbadala ili kutokomeza hizi mimba za utotoni kirahisi kabisa:

1. Zitolewe semina kwa walimu ili wawafundishe watoto wa kike mashuleni Atthari za kujamiiana chini ya miaka 18; kiafya na kielimu.

2. Masomo ya afya ya uzazi mashuleni (reproduction system) yafundishwe kijinsia(Gender teaching) , Wanafunzi wa kike wasifundishwe wakiwa mchanganyiko na wakiume- Kwani haya masomo yanapofanyika kwa pamoja na wanaume, yanawaongezea sana watoto wa kike ujasiri wa kutokuwaogopa wanaume kihisia, pia hulahisisha sana kutongozana wao kwa wao .

3. Serikali kupitia wizara ya afya na ustawi wa jamii iweke mikakati ya kupima bikira za wanafunzi kila mara na wawe na kadi maalumu kama zilivyo za kliniki za watoto, wapimwe wakiwa darasa la 4,5 na la 7 kwa shule ya msingi. Na kabla ya kujiunga form 1 wapimwe, pia fom 2,3,4,5 na 6 wapimwe kila waanzapo na wamalizapo mhura wa masomo. Kama hilo watashindwa,basi wapime hizo bikira japo mara moja moja darasa la 7, form 2,4,5 na 6 lengo nikuongeza hofu, pia kwa watoto mabikira wapate motisha za kupewa kipaumbele kukaa hostel kuliko wengine n.k

4. Serikali kupitia wizara ya elimu na ustawi wa jamii; iweke mikakati mathubuti mashuleni kwa kuweka mpango maalumu wa (periodic pregnant testing for student ); kwa darasa la 5 na la 7 kwa shule za msingi, kwa secondary fomu one hadi formu 4 wapimwe hata kila mwaka, hii itaongeza hofu kwa wanafunzi wenyewe na wazazi watashiriki kwa ukamilifu kusimamia zoezi hilo.

Hayo yote yataenda sambamba na wale wote wanaoonekana kujihusisha na mapenzi shuleni ili wakanywe ama waondolewe kabisa mashuleni kwa Suspension na wale wote wenye kuthibitishwa kuwa na mahusiano na mwanafunzi kimapenzi wakamatwe mara moja; hilo likifanyika litasaidia kutisha wengine kutojihusisha na mapenzi mashuleni…hilo hata sisi wazazi tutashiriki kwa hali na mali kulitekeleza.

5. Mpango huo wa kuwapima watoto kila mara; utatumika kama tangazo la kupinga mimba za utotoni, kwahiyo utasambaa hadi huko vijinini kupitia kwa wanafunzi wenyewe.

6. Maadili yatalejea kwa watoto na pengine hata wakafika chuo na bikira zao.

7. Taifa litapata mama bora na wenye familia na maadili.

8. Sisi wazazi tutajivunia pia kuzaa watoto wa kike kwa maana tutakuwa naimani wapo katika jamii salama tofauti na presha tulizo nazo sasa.

KUWAFUNGA WATIA MIMBA NI KUTENGENEZA TATIZO JINGINE KUBWA ZAIDI.

NAOMBA KUWASILISHA MSWADA HUU, KARIBUNI TUJADILI WADAU.

NB: Kama una hoja tofauti/mbadala ya kutokomeza mimba iweke hapa pia ijadiliwe.
Mawazo kuntu sana mkuu inahitaji kua na akili ndefu kuona haya
 
Wasiwasi wangu ni kwamba hao watakao kuwa wanapima hizo bikra ndiyo watakuwa wanazitoa au kuwakuwadia ziende kutolewa.
 
Back
Top Bottom