Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
SIKU moja baada ya magari matano ya Ikulu kuzima baada ya kuwekwa mafuta machafu mkoani Kilimanjaro wananchi wa kada mbalimbali, wakiwamo wanasiasa wameijia juu serikali na hasa Idara ya Usalama wa Taifa kwa hatua hiyo, huku wakihoji ilikuwaje magari ya serikali yajaze mafuta kwenye vituo binafsi.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Freeman Mbowe Bw. Mbowe alisema kuwa huo ni uzembe wa hali ya juu na kwamba Rais asifumbie macho uzembe huo hata kidogo, kwani kufanya hivyo anayaweka maisha yake rehani.
Pia alisema matukio yanayomwandama Rais Jakaya Kikwete yakiwemo ya gari zake kuzimika ghafla na tairi kupata kuchomoka hivi karibuni na hili la kuwekewa mafuta machafu ni ishara ya kuwa usalama wake uko hatarini, hivyo akashauri 'serikali iazime walinzi wa CHADEMA (Red Brigade) wasaidie katika eneo hilo'.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Freeman Mbowe Bw. Mbowe alisema kuwa huo ni uzembe wa hali ya juu na kwamba Rais asifumbie macho uzembe huo hata kidogo, kwani kufanya hivyo anayaweka maisha yake rehani.
Pia alisema matukio yanayomwandama Rais Jakaya Kikwete yakiwemo ya gari zake kuzimika ghafla na tairi kupata kuchomoka hivi karibuni na hili la kuwekewa mafuta machafu ni ishara ya kuwa usalama wake uko hatarini, hivyo akashauri 'serikali iazime walinzi wa CHADEMA (Red Brigade) wasaidie katika eneo hilo'.