Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,928
Robo tatu ya Tanzania inakabiliwa na upungufu mkubwa wa chakula. Kuna watu wanakabiliwa na njaa katika nusu ya wilaya zote nchini na hali haionekani kutengemaa sasa hivi. Serikali inajitahidi kuhamisha nafaka kutoka sehemu mbalimbali zenye chakula kupeleka kwenye sehemu zenye upungufu wa chakula. Kwenye soko la dunia nchi nyingi zaidi zinazidi kugombea chakula kidogo kilichopo na kama kawaida mataifa makubwa yatakuwa na uwezo wa kupata vyakula vingi kuliko nchi maskini.
Kwa vile chakula ni limited resources ni wazi kuwa itahitajika uamuzi wa makusudi wa kuanza kufikiria jinsi ya kuration chakula aidha kwa mikoa, wilaya na hata kwa kaya. Japo kuration chakula kwa kaya ni uamuzi wa mwisho kabisa wa hali ngumu ya njaa yawezekana kuanza kuration chakula kwenda kwenye miji mikubwa na hasa kupunguza vyakula vya anasa katika miji hiyo hasa vitu kama nyama, mchele na baadhi ya matunda. Hii yote ni katika kuhakikisha kuwa hakuna sehemu ya Tanzania ambayo inakabiliwa na uhaba kupita kiasi. Wasiwepo watu wanaoishi katika anasa ya kula na kusaza katika taifa la watu wengine ambao hawajui watakula nini.
Kama ilivyokuwa wakati wa Mwalimu ambapo matajiri na maskini waligawana njaa ili kuhakikisha watu wote wanapata vyakula vya msingi yawezekana uamuzi kama huo tusipoangalia unaweza kuchkuliwa tena. Je, wale walioshiba watakuwa tayari kula pungufu ya wanavyokula sasa? Je, mashule ya boarding yanaweza kuhitaji kufungwa kwa ajili ya upungufu wa chakula (hii ikiwa ni pamoja na vyuo)? Je, italazimika kupiga marufuku baadhi ya sherehe na mikutano ambayo ambayo inatumia vyakula vingi kama starehe?
Je suala hili la mgao lianze na Jiji la Dar mahali ambapo watu wachache hata wanajua kuwa sehemu nyingine Tanzania kuna uhaba wa njaa? Jibu langu ni ndio. Nimekuwa nikifuatilia suala hili kwa miaka mitatu na naweza kusema kwa uhakika mkubwa tu, hakuna kitu kinachoweza kusababisha migongano ya kisiasa na kijamii kama hili suala la chakula. Wakati wa Nyerere japo kulikuwa na nidhamu ya watu kujali kuwa sote tuko pamoja katika hili; je chini ya viongozi wetu hawa Watanzania watakuwa pamoja kukubali kushare kidogo au Ufisadi ndio utajionesha kustahili kwake zaidi kuliko watu wengine?
nawaza tu.
Kwa vile chakula ni limited resources ni wazi kuwa itahitajika uamuzi wa makusudi wa kuanza kufikiria jinsi ya kuration chakula aidha kwa mikoa, wilaya na hata kwa kaya. Japo kuration chakula kwa kaya ni uamuzi wa mwisho kabisa wa hali ngumu ya njaa yawezekana kuanza kuration chakula kwenda kwenye miji mikubwa na hasa kupunguza vyakula vya anasa katika miji hiyo hasa vitu kama nyama, mchele na baadhi ya matunda. Hii yote ni katika kuhakikisha kuwa hakuna sehemu ya Tanzania ambayo inakabiliwa na uhaba kupita kiasi. Wasiwepo watu wanaoishi katika anasa ya kula na kusaza katika taifa la watu wengine ambao hawajui watakula nini.
Kama ilivyokuwa wakati wa Mwalimu ambapo matajiri na maskini waligawana njaa ili kuhakikisha watu wote wanapata vyakula vya msingi yawezekana uamuzi kama huo tusipoangalia unaweza kuchkuliwa tena. Je, wale walioshiba watakuwa tayari kula pungufu ya wanavyokula sasa? Je, mashule ya boarding yanaweza kuhitaji kufungwa kwa ajili ya upungufu wa chakula (hii ikiwa ni pamoja na vyuo)? Je, italazimika kupiga marufuku baadhi ya sherehe na mikutano ambayo ambayo inatumia vyakula vingi kama starehe?
Je suala hili la mgao lianze na Jiji la Dar mahali ambapo watu wachache hata wanajua kuwa sehemu nyingine Tanzania kuna uhaba wa njaa? Jibu langu ni ndio. Nimekuwa nikifuatilia suala hili kwa miaka mitatu na naweza kusema kwa uhakika mkubwa tu, hakuna kitu kinachoweza kusababisha migongano ya kisiasa na kijamii kama hili suala la chakula. Wakati wa Nyerere japo kulikuwa na nidhamu ya watu kujali kuwa sote tuko pamoja katika hili; je chini ya viongozi wetu hawa Watanzania watakuwa pamoja kukubali kushare kidogo au Ufisadi ndio utajionesha kustahili kwake zaidi kuliko watu wengine?
nawaza tu.