Serikali haina kauli moja katika mambo mazito yanayogusa wananchi

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
Siku chache zilizopita Waziri Kombani alitoa kauli isiyounga mkono kuhusu mabadiliko ya katiba, na kujitetea kuwa serikali haina pesa za kushughulikia mabadiliko ya katiba na kwamba suala la madai ya Katiba ni ya akina Tundu Lisu.

Leo Waziri Mkuu anaelezea kuhusu uwezekano wa kuiandika upya au kufanyia mabadiliko baadhi ya vifungu vya Katiba.

Kwa maana hiyo kauli ya serikali inakinzana, na inatoa dalili ya kwamba kila kiongozi anaropoka anavyoona yeye bila kujadiliana na jopo la viongozi ambapo wangekuwa wanatoa kauli moja inayoeleweka. Katika uongozi huu utaratibu wa kila kiongozi binafsi kutoa kauli inayogusa utaifa ni udhaifu kwani mara kadhaa viongozi tofauti kila mmoja kutoa kauli kadiri ya maoni yake bila kuzingatia kauli inayoungwa mkono na wengi katika uongozi. Labda maana yake cheo ni dhamana?
 
Back
Top Bottom