Serikali haina hoja juu ya uwezo huu wa Mahakama

Hii makala imejaa ufundi wa kisheria kiasi kwamba kwa sisi tusokuwa wanasheria ukimaliza kuisoma inabidi umeze panadol!

Mimi bado ningependa kueleweshwa zaidi juu ya uwezo wa mahakama kutengua kipengele cha katiba kwa katiba. Kama nimemuelewa vizuri Lula, mahakama inaweza tu kutangaza uamuzi fulani au hatua fulani ya serikari kuwa kinyume cha katiba ( "Ni rahisi zaidi kwa mahakama kutengua sheria au kipengele fulani cha sheria kwa kutumia Katiba. Na ni rahisi vile vile kusema kuwa uamuzi au hatua fulani ya serikali ni kinyume na Katiba").

Kwakuwa tunajua kuwa swala la mgombea kuwa lazima awe mwanachama wa chama cha siasa tayari lilikwisha ingizwa kwenye katiba, je si wajibu wetu wananchi kupeleka shauri mahakani la kuiomba mahakama itangaze kuwa hatua ile ya serikari ya kuingiza kwenye katiba kifungu kinachokandamiza haki za raia ilikuwa kinyume cha sheria na hivyo kuishauri serikali kurekebisha? Kwa sababu kwa sasa sioni kama Mahakama itaweza kuruhusu mgombea binafsi kabla kipengele kinachotaka mgombea kuwa na chama hakijoka kwenye katiba.

Kama niko sahihi, mahakama haiwezi tu kutangaza, mpaka mtu apeleke shauri hilo mahakamani. ( Kwani haiwezi kushtaki na kusikiliza kesi wakati huo huo.)
 
.. ndio maana nimeshangaa yule Profesa kujenga hoja zisizo na msingi kabisa.. na kama kuna wanafunzi waliopitia chini yake wenye msimamo kama huo basi tuna matatizo makubwa zaidi.
.
Mzee Mwanakijiji, mimi sio tuu ni mmoja wa wanafunzi wa Prof. Kabudi, bali pia ndiye supervisor wangu wa research. Jamaa ni kichwa cha ukweli kwenye sheria, ni mmoja wa 1st Class 3 pekee za UDSM, katika kipindi cha miaka 20, yeye Dr. Migiro na Dr. Majamba.

Tangu nikiwa UD, niligundua, walimu walikuwa vichwa sana, bahati mbaya wanatokea kuwa bomu mahakamani. Vichwa vyote hivyo vitatu, hakuna hata kimoja kinaweza kusimama mahakamani kuargue kesi, kazi yao ni lecturing tuu.

Kitu kizuri kuhusu Prof. Kabudi, hana majungu, bifu bifu wa uonevu wowote katika somo lake, ukifeli somo lake, umefeli kihalali, ila pia kitu cha ziada kuhusu huyu jamaa, ni mtu wa msaada sana kwa mwanafunzi unapokwama na kumwambia mwalimu nimekwama. Mimi nilikwama sana na reseach, infact nilisha give -up, to hell with their LL.B, lakini alinipatia usaidizi wa hali ya juu kama baba na mtoto mpaka ikakamilika.

Ushauri alioutoa mahakamani naamini sio yeye, yaani sio Kabudi ninayemfahamu mimi, yule ni Kabudi mwingine kabisa. Kwanza kitendo cha kuchaguliwa yeye na Jwan, kuna maswali ya kuijiuliza, kuna vichwa vya ukweli vya katiba pale UD, Kabudi ndiyo ni kichwa, lakini kuna vichwa wala havina 1st Class, katiba vinaijua kinyume nyume, kwanini walimpick Kabudi, sababu ni moja tuu, very compromising. System imetapakaa kila kona, jamaa lazima ni mtu wa huko, na pale alichokuwa anafanya ni kupindisha ukweli delibarately ili kuibeba serikali, namsikitikia sana, ataaibika na usomi wake wote utaonekana si lolote, si chochote!
 
Heshima yako Mzee.
Kama kawaida yako, mara nyingi hutupikia chakula ambacho hata kama mdomo ni mchungu kwa homa lakini kitakutia hamu ya kula japo kidogo.
Vijana, haya mzee ametusaidia sana na sasa jukumu letu siyo kuwa na jazba bali ku-analyse hayo aliyotuandikia na tutoe maoni yetu. Ninaamini Wakubwa huingia JF na hamuezi jua pengine kuna mambo mengine huanzia hapa hapa jamvini na yakaishia peponi.
Ahsante sana mzee
 
Hii ni moja ya makala bora sana niliyokutana nayo kwa 2010. Hizi shule ni hadi tuache kupumua. Asante na hongera sana Lula
 
Mzee Mwanakijiji, ni suala moja tuu ndilo linalosubiriwa kutolewa uamuzi na sio mawili. Suala lenyewe ni la uwezo wa Mahakama Kuu kwenye masuala ya Katiba, yaani High Court Jurisdiction, ina nguvu zinazoitwa inherent powers kuhusiana na jambo lolote.

Suala la Mgombea binafsi lilishaamuliwa na Mahakama Kuu, serikali haikukata rufani kupinga kulichoamuliwa na Mahakama Kuu, bali imekata rufani kupinga uwezo wa Mahakama Kuu kuamua ilichoamua.

Hivyo uamuzi wa sasa, labda wataamua kutoa uamuzi wa kukazia hukumu ya Mahakama Kuu, tena Jaji Mkuu akiamua kuuma kama Lord Denning, anaweza akaisulubu serikali kwa Contempt of the court kwanini haikufanya chochote kutekeleza hukumu halisi, hata kama ilikata rufani, kwa vile rufani zote ni probability, baada ya hukumu, utekelezaji huanza unless kama serikali ingeomba 'Stay Order', kusitisha utekelezaji, kitu ambacho serikali haukufanya. Kukata rufani pekee siyo 'Stay Order'.


Kama suala ni moja "mamlaka ya mahakama kuu kusikiliza/kuamua hii kesi" kwa nini Serikali iliendelea na hii kesi kwenye Mahakama Kuu...hakuna kipengele cha Sheria kinachowaruhusu kugomea kuendelea na kesi katika Mahakama ambayo hawana imani nayo?
 
Na. Lula wa Ndali Mwananzela (Raia Mwema)



Kutengua sheria au kipengele cha Katiba kwa Katiba?
Ni rahisi zaidi kwa mahakama kutengua sheria au kipengele fulani cha sheria kwa kutumia Katiba. Na ni rahisi vile vile kusema kuwa uamuzi au hatua fulani ya serikali ni kinyume na Katiba.



Kwa mfano, Bunge likiamka siku moja na kutunga sheria inayosema kuwa kuanzia sasa hakutaruhusiwa kuwepo kwa dini yoyote nchini Tanzania na Rais akaridhia na ikawa sheria, wananchi watakimbilia mahakamani na kudai kuwa serikali imevunja Katiba kwa sababu Katiba inatambua haki ya wananchi kuwa na imani na dini zao. Hivyo, mahakama inaweza kutangaza kwa urahisi tu kuwa sheria hiyo mpya ni kinyume na Katiba na papo hapo sheria hiyo inakosa nguvu au kwa muda ambao mahakama itakuwa imeweka kwa serikali kujisahihisha.



Hata hivyo, hili siyo rahisi pale ambapo serikali badala ya kutunga sheria inaamua kuingiza kwenye Katiba kitu ambacho kinapingana na haki zile za msingi. Yaani, serikali inatambua kuwa ikitunga sheria juu ya jambo hilo inaweza kufutwa kwa hiyo inaamua kuliingiza jambo hilo kwenye Katiba.


Hivi ndivyo ilivyofanya kwenye suala la mgombea binafsi mara ya kwanza; kwani wakati wanasubiri kusikiliza rufaa ambayo wameipoteza, serikali ikaenda Bungeni na kufanya mabadiliko ya Katiba kwa kutumia sheria namba 34 ya 1994 (Mabadiliko ya 11 ya Katiba) na kuingiza kwenye Katiba kitu ambacho hakikuwapo mwanzoni kwa uwazi huo.



Mabadiliko hayo yakafanya ni lazima kuwa wagombea wote wa ngazi zote ni lazima wawe wanatokana na vyama vya kisiasa, na matokeo yake ni mara moja kufuta wagombea huru na binafsi. Hili lilimkorofisha Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere na kuita kuwa ulikuwa ni uamuzi wa kipumbavu – nakubaliana naye.


Mbinu hii ikikubaliwa ni hatari kwa demokrasia
Sasa kama tutakubali kama serikali inavyotaka kuwa jambo likishaingizwa kwenye Katiba haliwezi kupitiwa (judicial reviewed) na mahakama matokeo yake yatakuwa ni yale yale. Serikali itaanza kukwepa kuleta sheria na itakuwa inafanya mabadiliko ya haraka ya Katiba na kuziba midomo wakosoaji. Hili halipaswi kukubaliwa.


lulawanzela@yahoo.co.uk

Wakuu,

Naombeni mnielimishe hapo kwenye Bold na hasa kwenye Red. Mwandishi anaposema Serikali ilingiza Jambo kwenye Katiba ana maana gani...hii sheria/ kifungu kipya si kilipelekwa Bungeni na kupigiwa kura na Wabunge? Au
 
.
Mzee Mwanakijiji, mimi sio tuu ni mmoja wa wanafunzi wa Prof. Kabudi, bali pia ndiye supervisor wangu wa research. Jamaa ni kichwa cha ukweli kwenye sheria, ni mmoja wa 1st Class 3 pekee za UDSM, katika kipindi cha miaka 20, yeye Dr. Migiro na Dr. Majamba.

Tangu nikiwa UD, niligundua, walimu walikuwa vichwa sana, bahati mbaya wanatokea kuwa bomu mahakamani. Vichwa vyote hivyo vitatu, hakuna hata kimoja kinaweza kusimama mahakamani kuargue kesi, kazi yao ni lecturing tuu.

Kitu kizuri kuhusu Prof. Kabudi, hana majungu, bifu bifu wa uonevu wowote katika somo lake, ukifeli somo lake, umefeli kihalali, ila pia kitu cha ziada kuhusu huyu jamaa, ni mtu wa msaada sana kwa mwanafunzi unapokwama na kumwambia mwalimu nimekwama. Mimi nilikwama sana na reseach, infact nilisha give -up, to hell with their LL.B, lakini alinipatia usaidizi wa hali ya juu kama baba na mtoto mpaka ikakamilika.

Ushauri alioutoa mahakamani naamini sio yeye, yaani sio Kabudi ninayemfahamu mimi, yule ni Kabudi mwingine kabisa. Kwanza kitendo cha kuchaguliwa yeye na Jwan, kuna maswali ya kuijiuliza, kuna vichwa vya ukweli vya katiba pale UD, Kabudi ndiyo ni kichwa, lakini kuna vichwa wala havina 1st Class, katiba vinaijua kinyume nyume, kwanini walimpick Kabudi, sababu ni moja tuu, very compromising. System imetapakaa kila kona, jamaa lazima ni mtu wa huko, na pale alichokuwa anafanya ni kupindisha ukweli delibarately ili kuibeba serikali, namsikitikia sana, ataaibika na usomi wake wote utaonekana si lolote, si chochote!

Ushauri wa upi wa Kabudi usiokubaliana nao wewe? nina wasi wasi kuwa watu hatujui kwa undani nini Prof.Kabudi na wenzake waliishauri mahakama zaidi ya mistari michache tuliyoiona magazetini. Ukifuatilia sana, utagundua kuwa kwa kiasi kikubwa wote watatu hawakutofautiana sana ktk ushauri. .

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananci la tar 10/04/2010, iliripotiwa kuwa marafiki wote wa mahakama walitamka kuwa Mahakama haina uwezo wa kutengua kifungu chochote cha katiba. Hili nadhani ndo ukweli ambao hata tusokuwa wanasheria tunauona.

Aidha Prof Mwaikusa anaripotiwa na Mwananchi hivi...."Naye Profesa Mwaikusa alisema kuwa Mahakama Kuu ilikuwa na mamlaka kusikiliza shauri hilo na kwamba kama inapewa jukumu la kuzilinda haki za msingi zilizoainishwa kwenye katiba hiyo, haiwezi kunyamaza pale inapoona kuwa haki hizo zinaondolewa na kifungu chochote kilichotungwa hata na Bunge. Hata hivyo, alisema ingawa mahakama ina mamlaka ya kutamka kuwa kifungu fulani cha katiba ni kinyume cha katiba, lakini haipaswi kwenda mbali zaidi ya kutamka hivyo. Katika kesi ya msingi Mahakama Kuu ilikwenda zaidi na kuipa serikali muda wa miezi sita kuingiza kifungu kinachoruhusu kuwepo kwa mgombea binafsi kabla ya uchaguzi uliokuwa unafuata. Hapa haikuwa na mamlaka haya,” alisema Profesa Mwaikusa nje ya mahakama." Sasa mbona huyu hakushambuliwa kama Kabudi?

Naona watu wameamua kumponda Prof. bila hoja za msingi. Naamini watu wengi wanataka haki ya mgombea binafsi irudishwe, bila shaka Prof Kabudi naye angependa hivyo, lakini pale alikuwa anatoa ushauri wake kama msomi na kwa kuzingatia sheria zilizopo, tumtofautishe na wakili anayesimamia upande fulani. Tuwe fair
 
Wakuu,

Naombeni mnielimishe hapo kwenye Bold na hasa kwenye Red. Mwandishi anaposema Serikali ilingiza Jambo kwenye Katiba ana maana gani...hii sheria/ kifungu kipya si kilipelekwa Bungeni na kupigiwa kura na Wabunge?
Serikali na Bunge la chama gani?
 
Naona watu wameamua kumponda Prof. bila hoja za msingi. Naamini watu wengi wanataka haki ya mgombea binafsi irudishwe, bila shaka Prof Kabudi naye angependa hivyo, lakini pale alikuwa anatoa ushauri wake kama msomi na kwa kuzingatia sheria zilizopo, tumtofautishe na wakili anayesimamia upande fulani. Tuwe fair

Consigliori, kwa kulinganisha ushauri alioutoa Prof Kabudi (ambao kwa maoni yako hatujauelewa!) na hii mada aliyoandika Lula (sina hakika kama nae ni Professor!) kuhusiana na jambo hilohilo bado unaona Prof Kabudi alikuwa na hoja ambazo tungezitegemea kutoka kwa msomi wa calibre yake?
 
Hoja sio Chama...hoja si Serikali imeundwa na Chama gani au Wabunge ni wa Chama gani. Hoja hapa ni Serikali kama Mhilimi mmoja na Bunge kama mhilimili mwingine.

Ni kweli ni bunge ndio lililopitisha hayo mabadiliko ya kwenye katiba na si serikali. Lakini kumbuka muswada unapelekwa bungeni na serikali. Kama una serikali ya sisiemu na bunge ambalo kwa sehemu kubwa ni sisiemu, effectively tunaweza kusema ni 'serikali' ndio iliyobadilisha katiba. Katika hili la kubadili katiba kulazimisha raia kugombea kupitia chama cha siaia hata Mwl Nyerere hakusita kuinyooshea kidole serikali ya sisiemu (na sio bunge!).
 
Naam. Mkuu mwanakiji nimekupata.Umesema vema kwamba CCM ILIVUNJA katiba kwa kutunga sheria inayowanyima wananchi "Sacred rights". Ilifanya hivyo kwa makusudi ya kulinda madaraka yake kwa sababu waliofia Nyerere alipowaonya mwanzo kwamba upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM. kwaiyo wakawaziba. NINA haki ya KUCHAGUA na kama mimi SINA haki ya KUCHAGULIWA. Haki hiyo iliondolewa na CCM. Je majaji watumie katiba kurejesha haki hiyo?? Na Je wasipofanya hivyo je watakuwa wanatekeleza jukumu lao KUU ya kutafsiri na Kulinda haki na wajibu wa raia? kwani ndo jukumu lao. LAKINI HAKI HIZO ni zilizo orodheshwa kwenye Katiba.Haki ya mimi kama mimi kusimama na kuchaguliwa haipo kwenye katiba.Mbona wakina Msekwa hawakuninyima haki hiyo wakati wanatunga katiba? kwa sababu inavunja haki za raia. Hivi kipindi kifungu hichi kinajadiliwa bungeni na hatimaye kupitishwa kuwa katiba wanasheria, wabunge na hata hawa maprofessa waliona ni sawa tu? Umetoa angalizo je kama mahaka haiwezi kutumia katiba kutengua katiba na CCM wapo madarakani na wameamua kutunga sheria zinazowabana wale wasio na madaraka ili wasiyapata na kuziingiza sheria hizo kwenye katiba ambapo mahakama haiwezi kuzigusa je nini kitafuata baada ya hapo. Tanzania haitakuwa nchi inayoongozwa kwa misingi ya demokrasia. Je wapo tayari? Nadhani CCM ingependa iwe. Something must be done.
 
Ushauri wa upi wa Kabudi usiokubaliana nao wewe? nina wasi wasi kuwa watu hatujui kwa undani nini Prof.Kabudi na wenzake waliishauri mahakama zaidi ya mistari michache tuliyoiona magazetini. Ukifuatilia sana, utagundua kuwa kwa kiasi kikubwa wote watatu hawakutofautiana sana ktk ushauri. .

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananci la tar 10/04/2010, iliripotiwa kuwa marafiki wote wa mahakama walitamka kuwa Mahakama haina uwezo wa kutengua kifungu chochote cha katiba. Hili nadhani ndo ukweli ambao hata tusokuwa wanasheria tunauona.

Aidha Prof Mwaikusa anaripotiwa na Mwananchi hivi...."Naye Profesa Mwaikusa alisema kuwa Mahakama Kuu ilikuwa na mamlaka kusikiliza shauri hilo na kwamba kama inapewa jukumu la kuzilinda haki za msingi zilizoainishwa kwenye katiba hiyo, haiwezi kunyamaza pale inapoona kuwa haki hizo zinaondolewa na kifungu chochote kilichotungwa hata na Bunge. Hata hivyo, alisema ingawa mahakama ina mamlaka ya kutamka kuwa kifungu fulani cha katiba ni kinyume cha katiba, lakini haipaswi kwenda mbali zaidi ya kutamka hivyo. Katika kesi ya msingi Mahakama Kuu ilikwenda zaidi na kuipa serikali muda wa miezi sita kuingiza kifungu kinachoruhusu kuwepo kwa mgombea binafsi kabla ya uchaguzi uliokuwa unafuata. Hapa haikuwa na mamlaka haya,” alisema Profesa Mwaikusa nje ya mahakama." Sasa mbona huyu hakushambuliwa kama Kabudi?

Naona watu wameamua kumponda Prof. bila hoja za msingi. Naamini watu wengi wanataka haki ya mgombea binafsi irudishwe, bila shaka Prof Kabudi naye angependa hivyo, lakini pale alikuwa anatoa ushauri wake kama msomi na kwa kuzingatia sheria zilizopo, tumtofautishe na wakili anayesimamia upande fulani. Tuwe fair
.
consigliori asante, hoja ya Prof. Kabudi kuwa Mahakama Kuu haina mamlaka kuingilia katiba. Hoja hiyo ameibase kwenye 'The Constitutionalism of Consititution', wakati anaelewa wazi kuwa hii katiba yetu tumeiunda bila kufuata misingi sahihi ya constitutional, hivyo tuna katiba consitutitional isiyo na constutionalism, kwa serikali kuamua kufanya mabadiliko itakavyo na bado anaitetea?!.

Hukumu ya Mahakama Kuu, haikuingilia uhuru wa Bunge, ilichofanya ni kuamuru kuwa kifungu kinachomlazimisha mtu kudhaminiwa na chama, ni kifungu batili, na ikaiamuru serikali ipeleke Bungeni marekerbisho muhimu. Kwa mujibu wa Kabudi, ingetakiwa Mahakama Maalum ya Katiba ndio ifanye hayo. Hizo inherent powers za Mahakama Kuu ni zipi?.
 
.
consigliori asante, hoja ya Prof. Kabudi kuwa Mahakama Kuu haina mamlaka kuingilia katiba. Hoja hiyo ameibase kwenye 'The Constitutionalism of Consititution', wakati anaelewa wazi kuwa hii katiba yetu tumeiunda bila kufuata misingi sahihi ya constitutional, hivyo tuna katiba consitutitional isiyo na constutionalism, kwa serikali kuamua kufanya mabadiliko itakavyo na bado anaitetea?!.

Hukumu ya Mahakama Kuu, haikuingilia uhuru wa Bunge, ilichofanya ni kuamuru kuwa kifungu kinachomlazimisha mtu kudhaminiwa na chama, ni kifungu batili, na ikaiamuru serikali ipeleke Bungeni marekerbisho muhimu. Kwa mujibu wa Kabudi, ingetakiwa Mahakama Maalum ya Katiba ndio ifanye hayo. Hizo inherent powers za Mahakama Kuu ni zipi?.

Asante Pasco, ila bado naona hatukutakiwa kumlaumu Prof. Kabudi kwa kuietetea katiba ( hata kama ni consitutitional isiyo na constutionalism kama unavyodai) kwa sababu hii ndo katiba tuliyonayo; unless you are telling me that haitakiwi kutambulika.

Katika par yako ya pili, si Prof. Kabudi tu aliyesema mahakama haikuwa na mamlaka kuimuru(Kuiambia) serikali kifungu fulani cha katiba kibadilishwe, this is also shared by Prof. Mwaikusa kama alivyoripotiwa na Mwananch (Hata hivyo, alisema ingawa mahakama ina mamlaka ya kutamka kuwa kifungu fulani cha katiba ni kinyume cha katiba, lakini haipaswi kwenda mbali zaidi ya kutamka hivyo. Katika kesi ya msingi Mahakama Kuu ilikwenda zaidi na kuipa serikali muda wa miezi sita kuingiza kifungu kinachoruhusu kuwepo kwa mgombea binafsi kabla ya uchaguzi uliokuwa unafuata. Hapa haikuwa na mamlaka haya,” alisema Profesa Mwaikusa nje ya mahakama." ). Sasa vipi Prof. Mwakusa hasemwi ila na Prof. Kabudi tu?
 
Wakuu,

Naombeni mnielimishe hapo kwenye Bold na hasa kwenye Red. Mwandishi anaposema Serikali ilingiza Jambo kwenye Katiba ana maana gani...hii sheria/ kifungu kipya si kilipelekwa Bungeni na kupigiwa kura na Wabunge? Au

S.S. Phares.. labda nikurudishe nyuma kidogo. Hukumu ya Manento in 2005 iliangalia nyuma suala kidogo na kuelezea mkorogano ambao mwandishi hapa ana urefer:

[FONT=Times New Roman, serif]Aggrieved by this declaration, the Respondent filed an appeal to the Court of Appeal while the Petitioner also cross appealed against certain decisions made adverse to him. This was Civil Appeal No. 3 of 1995. It cannot also be disputed that while the appeal was pending the Respondent processed a bill and proceeded to enact a law which had the effect of rendering the ruling of the High Court ineffective and/or a nullity.[/FONT]




[FONT=Times New Roman, serif] On that ground the Respondent applied to withdraw the appeal. The Court of Appeal of course had to grant the application for withdrawal but speaking through [/FONT][FONT=Times New Roman, serif]KISANGA Ag. [/FONT][FONT=Times New Roman, serif]C[/FONT][FONT=Times New Roman, serif].J. [/FONT][FONT=Times New Roman, serif]the Court of Appeal lamented at p. 3 of the typed judgment:[/FONT]


[FONT=Times New Roman, serif]"... We are constrained to have to point out some aspects in the handling of this matter by the appellant which cause great concern. While the ruling was being awaited, the Government on 16/10/94 presented a Bill in Parliament seeking to amend the Constitution so as to deny the existence of that right, thus pre-emptying the Court Ruling should it go against the Government. This is where things started going wrong. The Government was now adopting parallel causes of action towards the same end by asking Parliament to deal with the matter simultaneously with the High Court. That was totally wrong for reasons which will be apparent presently.[/FONT]




[FONT=Times New Roman, serif]Thus the government consciously and deliberately drew the judiciary into a direct clash with Parliament by asking the two organs to deal with the same matter simultaneously. Such a state of affairs was both regrettable and most undesirable. It was wholly incompatible with the smooth administration of justice in the country and every effort ought to be made to discourage it."[/FONT]




[FONT=Times New Roman, serif] The Court then went on to observe in conclusion:[/FONT]




[FONT=Times New Roman, serif]"In the instant case had the amendment been initiated and passed after the Court process had come to a finality that in law would have been alright procedurally, the soundness of the amendment itself, of course, being entirely a different matter. Then the clash would have been avoided. Indeed that would be in keeping with good governance which today constitutes one of the attributes of a democratic society. "[/FONT]




[FONT=Times New Roman, serif] The amendments referred to in the judgment of the Court of Appeal are those made by Act No. 34 of 1994 which as observed, was passed by the Parliament on 16/10/94 while the Ruling of Lugakingira J (as he then was) was handed down on 24/10/94, as it was still pending when the Parliament enacted the law. As a matter of procedure, we must, at once condemn this act of the Respondent as being contrary to the dictates of good governance, and for which we can do no more than quote the above cited passage from the judgment of the Court of Appeal. We shall leave it at that and now go to the substance of the petition which is before us.[/FONT]

Kwa hiyo, serikali ikiamini kuwa nyongeza yoyote ya kwenye Katiba haiwezi kuhojiwa mahakamani iliamua kubypass mahakama na kuleta mabadiliko. Sasa, endapo mahakama itakubaliana kuwa kipengele cha Katiba hakiwezi kutenguliwa pale kinapoingizwa kutishia haki za wananchi au haki za binadamu basi serikali itaweza kufanya hivi. Imagine.. Serikali inaamua kuingiza kipengele kwenye Katiba (kwa kupitia sheria) na kusema kuwa hakuna uhuru wa kutoa maoni. Je mtu ataweza kulalamika mahakamani? Jibu la serikali litakuwa "hapana" kwa sababu mahakama haina uwezo wa kutengua kipengele cha Katiba! Hili ni wazo la hatari.
 
Asante Pasco, ila bado naona hatukutakiwa kumlaumu Prof. Kabudi kwa kuietetea katiba ( hata kama ni consitutitional isiyo na constutionalism kama unavyodai) kwa sababu hii ndo katiba tuliyonayo; unless you are telling me that haitakiwi kutambulika.

Katika par yako ya pili, si Prof. Kabudi tu aliyesema mahakama haikuwa na mamlaka kuimuru(Kuiambia) serikali kifungu fulani cha katiba kibadilishwe, this is also shared by Prof. Mwaikusa kama alivyoripotiwa na Mwananch (Hata hivyo, alisema ingawa mahakama ina mamlaka ya kutamka kuwa kifungu fulani cha katiba ni kinyume cha katiba, lakini haipaswi kwenda mbali zaidi ya kutamka hivyo. Katika kesi ya msingi Mahakama Kuu ilikwenda zaidi na kuipa serikali muda wa miezi sita kuingiza kifungu kinachoruhusu kuwepo kwa mgombea binafsi kabla ya uchaguzi uliokuwa unafuata. Hapa haikuwa na mamlaka haya,” alisema Profesa Mwaikusa nje ya mahakama." ). Sasa vipi Prof. Mwakusa hasemwi ila na Prof. Kabudi tu?

Nakusikia lakini tatizo ni kuwa mahakama mara zote imekuwa ikitoa agizo kutokana na nguvu zake kutaka wahusika wasahihishe walichoharibu. Lakini serikali inajaribu kujiweka nje ya maagizo ya mahakama. Mahakama isipokuwa na uwezo wa kuagiza kilichoharibiwa (baada ya kukikuta hivyo) kitengenezwe ni jinsi gani wahusika watatekeleza? Kwenye suala la Valambhia ilikuwa hivi hivi.. Hivi majuzi sehemu moja huko US mahakama imetaka school district kuondoa sera za kibaguzi kwa wanafunzi na kuwapa vipimo vya kutumia. Hiyo ni sehemu ya judicial review.

sehemu ya hukumu ya Manento inasema hivi:

[FONT=Times New Roman, serif]We shall also declare in the present case that in principle it shall be lawful for private candidates to contest for the posts of President and Member of Parliament along with candidates nominated by political parties. However unlike the learned late judge we will not just leave it at that. Exercising our powers under any other relief as prayed in the petition and cognizant of the fact that a vacuum might give birth to chaos and political pandemonium we shall proceed to order that the Respondent in the true spirit of the original Article 21 (1) and guided by the Fundamental Objectives and Principles of State Policy contained in Part 11 of the Constitution between now and the next general elections, put in place, a legislative mechanism that will regulate the activities of private candidates. So as to let the will of the people prevail as to whether or not such candidates are suitable. As this is a public interest litigation the parties shall bear their own costs.[/FONT]


[FONT=Times New Roman, serif]It is so ordered.[/FONT]

Huo msisitizo ni wa kwangu. Mahakama haikuweka utaratibu wa wagombea binafsi uwe vipi hapo ingekuwa inatunga sheria kama maprofesa wanavyodai. Mahakama haikufanya hivyo... imeweka muda (kitu ambacho inauwezo wa kufanya) na kutaka Bunge litengeneze mazingira ya kuwahusisha wagombea binafsi. Hii ilikuwa in 2005. Kumbuka alisema hivyo kwa sababu katika hukumu ya Lugakingira licha ya kuruhusu wagombea binafsi lakini kulikuwa na ombwe, serikali haikufungwa kulazimishwa kuweka mazingira ya wagombea binafsi ndio maana in 2000 na 2005 hakukuwa na utaratibu huo. Manento ameremedy tatizo hilo kwa kuwaambia serikali waandae utaratibu huo by 2010. Sasa leo serikali ikisema haina muda mimi naona ni wapuuzi kwa sababu they have had 4 years to take heed ya agizo hilo la mahakama na wamekataa defiantly.
 
Mzee Mwanakijiji,

Marafiki wa mahakama wote wanne wamesema mahakama haina uwezo wa kwenda mbali zaidi ya kutamka kwamba kifungu fulani ni batili. Kwenye hilo wote wanakubaliana ikiwa ni pamoja na Prof. Mwaikusa, lakini mnachosahau ni kwamba mahakama ilienda mbali mbali zaidi na kuiamuru serikali kupitia bunge ifanye utaratibu wa kuruhusu mgombea binafsi.

Hata kama hicho kifungu ni batili haina maana kwamba ubatili huo unaweza kuondolewa kwa kuruhusu mgombea binafsi tu. What if serikali ikiamua kubadili kile kifungu kingine kinachompa kila raia haki ya kuchagua au kuchaguliwa? Vifungu viwili vinapogongana kunakuwa na njia zaidi ya moja kuondoa huo mgongano.

Mahakama kwenye hukumu yao wametamka kifungu ni batili na wakatoa option moja tu ya kuondoa ubatili huo, je hilo ni sawa?

Tatizo kubwa la mjadala huu ni watu kuujadili kwa kufuata common sense badala ya kujadili kwa kufuata katiba ya nchi. Kwenye sheria common sense inachukua nafasi ndogo sana. Ukiangalia common sense, utaona Zombe aliua au huyu wa BOT utaona ana case ya kujibu lakini mahakama haiendeshiw hivyo.
 
Mzee Mwanakijiji,

Marafiki wa mahakama wote wanne wamesema mahakama haina uwezo wa kwenda mbali zaidi ya kutamka kwamba kifungu fulani ni batili. Kwenye hilo wote wanakubaliana ikiwa ni pamoja na Prof. Mwaikusa, lakini mnachosahau ni kwamba mahakama ilienda mbali mbali zaidi na kuiamuru serikali kupitia bunge ifanye utaratibu wa kuruhusu mgombea binafsi.

Mahakama haikwenda mbali; ilifanya kitu kilicho ndani ya uwezo wake (hapa ndio natofautiana na maprofesa wetu na ninaamini mahakama ikitoa uamuzi itakuwa upande wangu). Mahakama inauwezo wa kuamuru remedy. Kwa mfano, kama haki ya mtu imevunjwa na chombo cha serikali mahakama haiwezi kuishia tu nakusema tendo hilo la serikali ni "kinyume na katiba" lakini ni jukumu lake kuhakikisha kuwa haki hizo zinakuwa restored. Inafanya hivyo kwa kuagiza chombo husika kufanya hivyo na wakati mwingine hata kuwabana kwa muda ili wakishindwa iwe nii contempt of court.

Hata kama hicho kifungu ni batili haina maana kwamba ubatili huo unaweza kuondolewa kwa kuruhusu mgombea binafsi tu. What if serikali ikiamua kubadili kile kifungu kingine kinachompa kila raia haki ya kuchagua au kuchaguliwa? Vifungu viwili vinapogongana kunakuwa na njia zaidi ya moja kuondoa huo mgongano.

Sheria inaweza kufanya vyovyote inavyotaka as long as kwamba wagombea binafsi wanaruhusiwa kushiriki uchaguzi huu; Katika kufanya hivyo, serikali haipaswi kuwapa mzigo mkubwa wagombea binafsi kushiriki kuliko wagombea wa vyama kwa hivyo, tusipoangalia serikali isipokuwa makini tutarudi tena hili kwa sababu inaweza kutunga sheria ya kuruhusu wagombea binafsi lakini ikawa ni sheria ambayo practically haiwezekani. Kwa mfano, tukiambiwa mgombea binafsi lazima awe na wadhamini 2000 wakati mgombea wa chama anatakiwa awe na wadhamani 10.. hii itamfanya mgombea binafsi kuwa na kazi ngumu zaidi na hivyo kesi nyingine itafunguliwa kupinga sheria hiyo mpya na tutarudi kwenye gurudumu hili hili.

Mahakama kwenye hukumu yao wametamka kifungu ni batili na wakatoa option moja tu ya kuondoa ubatili huo, je hilo ni sawa?

Una maanga wametoa option moja? itakuwaje kama option NI moja tu?

Tatizo kubwa la mjadala huu ni watu kuujadili kwa kufuata common sense badala ya kujadili kwa kufuata katiba ya nchi. Kwenye sheria common sense inachukua nafasi ndogo sana. Ukiangalia common sense, utaona Zombe aliua au huyu wa BOT utaona ana case ya kujibu lakini mahakama haiendeshiw hivyo.

Hili ni kweli.. ukiangalia Katiba hii kesi wala isingefika hapa wagombea binafsi wangekuwa wamesharuhusiwa kushiriki kuanzia 2000 na 2005! lakini ndiyo hivyo sometimes common sense is not that common after all.
 
Kamakabuzi.. ndio maana nimeshangaa yule Profesa kujenga hoja zisizo na msingi kabisa.. na kama kuna wanafunzi waliopitia chini yake wenye msimamo kama huo basi tuna matatizo makubwa zaidi.

Profesor Kabudi hakuna kitu na alidhalilisha tasnia yote ya sheria....i'm ashamed of him
 
Na. Lula wa Ndali Mwananzela (Raia Mwema)


.............................................. [Snip]

Kama tunavyofahamu serikali inaundwa kwa mihimili mitatu; yaani Utendaji (Rais na wote wanaotekeleza majukumu mbalimbali kwa mujibu wa sheria na ofisi zao – mara kwa mara tunawaita hawa ni “serikali”), Mahakama; yaani Jaji Mkuu na vyombo vyote vinavyoshughulikia suala la upatikanaji na utoaji wa haki na Bunge; yaani Spika na wabuneg na vyombo vyote vinahusiana na mchakato wa kutunga sheria na usimamizi wa serikali pamoja na ushauri.
Katika demokrasia vyombo hivi vitatu vinahusiana sana na wakati huo huo vinaachiana madaraka mbalimbali. Wakati wowote vyombo hivi vinapogongana au kushindwa kufanya kazi kwa pamoja, basi, demokrasia yenyewe inakuwa mashakani. ........................................ etc

lulawanzela@yahoo.co.uk

Hapo kwenye red font. Nahisi kwamba lulawanzela alimaanisha dola? Yaani Dola inaundwa kwa mihimili mitatu; Serikali, Mahakama na Bunge
 
Back
Top Bottom