Serikali Dar es Salaam yafuatilia kuchanwa mabango ya CCM

Safari_ni_Safari

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
23,268
17,097
PICHA za mgombea wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizobandikwa katika eneo baadhi ya maeneo zimechanwa na watu wasiojulikana hali ambayo ofisi ya Mkuu wa Mkoa imesema inafuatilia kubaini wanaofanya vitendo hivyo.

Eneo ambalo gazeti hili limeshuhudia picha hizo zikiwa zimechanwa ni katika chuo cha teknolojia Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema, "tutalifanyia kazi suala hilo na ngoja tuanze kulishughulikia kwa kuwa lipo ndani ya mkoa wangu ina maana lipo chini yangu pia," alisema Lukuvi.


Gazeti hili lilipita katika maeneo hayo na kushuhudia picha za mgombea huyo zilizobandikwa katika mabati na kuta zilizozunguka eneo hilo zikiwa zimechanwa hali iliyoleta maswali mengi kwa watu wengine waliokatisha katika eneo hilo.


Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya watu hao ambao hata hivyo hawakupenda majina yao yaandikwe gazetini walisema kinachotakiwa kufanywa kwa sasa ni kwa mamlaka zinazohusika kuwatafuta waliofanyakitendo hicho ili wafunguliwe mashitaka.

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba alipozungumza na gazeti hili, alisema, "kwa sasa siwezi kusema neno lolote kwa kuwa si mhusika wa mkoa huu, ingekuwa hapo zamani wakati huo mkoa unatambulika kama mkoa wa Mmakamba ningeweza kulisemea suala hilo," aliongeza katibu huyo.


Maoni
Acheni hizo na nyie bwana mambo ya CCM yaenze kutumia fedha za serikali kuyashughulikia. CCM watafute namna yao watakayoweza kuyalinda mabango yao. Kama zingechanwa za chadema au CUF serikali ingezishughulikia? Mambo ya nchi ndo yanaponichoshaga hapo.
 
Hiyo "Thanks" yangu nimekugongea ni kwa ajili ya yale maoni yako ya font nyekundu.
 
Hizo ndizo kampeni, Bwana, nani kakuambia wana chuo wote wanamuunga mkoni jamaa!!! Msilazimishe watu, acha watu waamue wenyewe. Watashughulikia wangapi wakati najua zitachanwa nyingi tuu? Haya ni mambo pet pet sana!! Shughulikieni ya maana!! Kwanza hayo mabilioni ya kampeni yangesaidia sekta ya afya, elimu, kilimo, you name all!!
 
Hiyo "Thanks" yangu nimekugongea ni kwa ajili ya yale maoni yako ya font nyekundu.

Huyu Makamba muppet kweli....yaani mali yako inaharibiwa unasema wewe huhusiki au anathibitisha kuwa ni kweli ikulu imelipia hayo mabango kwa yule mdosi wa Canada?

Lukuvi ni muppetx2...anakurupuka tu hili si swala ala kipolisi zaidi....Makamba anatakiwa kushitaki Polisi ili waanze kulifanyia kazi...hii kutu itawatoka lini hawa watu kuwa CCM na serikali ni vitu tofauti kimaslahi??...Argh kamatakamata itaanza na as usual innocents ndio wataumia
 
Damu ni nzito ndungu zangu.
Luvuvi ni Mbuge wa CCM, ameteuliwa pia kuwa mkuu wa mkoa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la ulinzi na Usalama wa Jiji la Dar.
Alipe fadhila gani tena kwa CCM??
 
Kama mgombea wa CCM anakubalika kwa nini wametandaza mabango kila kona mpaka yamekuwa uchafu.
Nimeamini kizuri cha jiuza kibaya cha jitembeza.
 
Damu ni nzito ndungu zangu.
Luvuvi ni Mbuge wa CCM, ameteuliwa pia kuwa mkuu wa mkoa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la ulinzi na Usalama wa Jiji la Dar.
Alipe fadhila gani tena kwa CCM??

Sasa anafanya kazi kupitia magazeti?....Mwenye mali (Makamba) hajui uharibifu huu...yeye Lukuvi atachomaamafuta toka Ilala Boma mpaka DIT kwa kodi zetu?.....Mbona Ngwasuma na Akudo wanachaniana hayo mabango kila siku na yeye hafuatilii?...AISEE... AM VERY ANGRY UNAJUA!!!!!!:mad2::mad2:
 
Hiyo "Thanks" yangu nimekugongea ni kwa ajili ya yale maoni yako ya font nyekundu.

Na mimi pia. Ombwe la uongozi kweli lipo.

Nimeamini ule msemo wa 'Chama kushika hatamu na serikali kuwa mtekelezaji' bado upo hai.
 
Sasa uwanja sawa wa kiushindani ktk siasa uko wapi? Ya chadema na vyama vingine yanalindwa na nani? Nadhani pia hata Aliyeyachana namuunga mkono yanarundikwa mpaka unakuwa uchafu! Kituo kizima kinajazwa bango la aina moja lenye ujumbe huohuo. Mbona jiji wanangoa matangazo ya biashara ya watu wengi tu ambao wanaleseni za biashara na wanalipa kodi. Vp c c m wanayalipia hayo mabango yanayobandikwa kwenye kuta za majengo na vituoni?
 
Hizo ni salamu tu angoje 31/10/2010 labda wachakachue kura.
 
PICHA za mgombea wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizobandikwa katika eneo baadhi ya maeneo zimechanwa na watu wasiojulikana hali ambayo ofisi ya Mkuu wa Mkoa imesema inafuatilia kubaini wanaofanya vitendo hivyo.

Eneo ambalo gazeti hili limeshuhudia picha hizo zikiwa zimechanwa ni katika chuo cha teknolojia Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema, “tutalifanyia kazi suala hilo na ngoja tuanze kulishughulikia kwa kuwa lipo ndani ya mkoa wangu ina maana lipo chini yangu pia,” alisema Lukuvi.


Nasikia Manispaa za Dar Es Salaam zilipitisha sheria kuwa kubandika posters katika kuta za nyumba ni kosa la jinai. Anachoshughulikia Lukuvi ni kipi waliondoa hizo posters au waliobandua.

Kama kweli hiyo sheria ipo naona waliofanya kosa ni wale waliobandika na wala sio waliondoa.

Hebu tulijadili hilo
 
Mrema (wa TLP) last week alilalamika mabango yake yamen'golewa huko Vunjo na watu anaoamini ni wafuasi wa CCM. Jee waliofuatilia suala hili, Polisi walichukua hatua gani?
 
Nasikia Manispaa za Dar Es Salaam zilipitisha sheria kuwa kubandika posters katika kuta za nyumba ni kosa la jinai. Anachoshughulikia Lukuvi ni kipi waliondoa hizo posters au waliobandua.

Kama kweli hiyo sheria ipo naona waliofanya kosa ni wale waliobandika na wala sio waliondoa.

Hebu tulijadili hilo

Kosa kwa wengine woote - lakini siyo kwa CCM!
 
Kinachonichosha ni yule aliyekuwa Rais kutofahamika licha tu ya Tanzania nzima bali hata eneo lisilozidi kilometre tatu kutoka Ikulu. Wanaanza kukimbizana mitaani na watu wanaotoa mabango. Hayana jipya hayo. Kwani wanachuo hawajui sera zenu kandamizi kwa watoto wa maskini wanaosoma elimu ya juu.

Tumieni mabavu yenu haitawasaidia sana. Usitegemee mabango yenu yapendwe na wahanga wa utawala wenu. Sawa na kubandika picha ya Osama msikitini hiyo
 
Kinachonichosha ni yule aliyekuwa Rais kutofahamika licha tu ya Tanzania nzima bali hata eneo lisilozidi kilometre tatu kutoka Ikulu. Wanaanza kukimbizana mitaani na watu wanaotoa mabango. Hayana jipya hayo. Kwani wanachuo hawajui sera zenu kandamizi kwa watoto wa maskini wanaosoma elimu ya juu.

Tumieni mabavu yenu haitawasaidia sana. Usitegemee mabango yenu yapendwe na wahanga wa utawala wenu. Sawa na kubandika picha ya Osama msikitini ubalozi wa marekani hiyo
 
PICHA za mgombea wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizobandikwa katika eneo baadhi ya maeneo zimechanwa na watu wasiojulikana hali ambayo ofisi ya Mkuu wa Mkoa imesema inafuatilia kubaini wanaofanya vitendo hivyo.

Eneo ambalo gazeti hili limeshuhudia picha hizo zikiwa zimechanwa ni katika chuo cha teknolojia Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema, "tutalifanyia kazi suala hilo na ngoja tuanze kulishughulikia kwa kuwa lipo ndani ya mkoa wangu ina maana lipo chini yangu pia," alisema Lukuvi.


Gazeti hili lilipita katika maeneo hayo na kushuhudia picha za mgombea huyo zilizobandikwa katika mabati na kuta zilizozunguka eneo hilo zikiwa zimechanwa hali iliyoleta maswali mengi kwa watu wengine waliokatisha katika eneo hilo.


Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya watu hao ambao hata hivyo hawakupenda majina yao yaandikwe gazetini walisema kinachotakiwa kufanywa kwa sasa ni kwa mamlaka zinazohusika kuwatafuta waliofanyakitendo hicho ili wafunguliwe mashitaka.

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba alipozungumza na gazeti hili, alisema, "kwa sasa siwezi kusema neno lolote kwa kuwa si mhusika wa mkoa huu, ingekuwa hapo zamani wakati huo mkoa unatambulika kama mkoa wa Mmakamba ningeweza kulisemea suala hilo," aliongeza katibu huyo.


Maoni
Acheni hizo na nyie bwana mambo ya CCM yaenze kutumia fedha za serikali kuyashughulikia. CCM watafute namna yao watakayoweza kuyalinda mabango yao. Kama zingechanwa za chadema au CUF serikali ingezishughulikia? Mambo ya nchi ndo yanaponichoshaga hapo.

Hapo kwenye red natumaini ikitokea kwa vyama vingine watafanya hivyo hivyo pia
 
Back
Top Bottom