Serikali: CHADEMA inapewa pesa kutoka nje kuleta machafuko Tanzania

Kweli Chadema naiaminia ina maana leo asubuhi wanawake walikuwa studio walikuwa wanashusha nondo zilizoooza kwa Chadema manake Channel Ten Kipindi cha Baragumu alikuweko Letisia Masori sijui jina lake kama nilisikia vizuri (NCCR) formal Mwenyekiti wanawake Chadema na yeye alikuwa anasema viongozi wa chadema wamekurupuka kuendesha maandamano nchi nzima ajabu tunasikia NCCR wanaanza mikitano kigoma then nchi nzima huko sio kujikanyaga kweli
 
Huyu Sophia Simba si ndiye aliyekacha kujieleza kwa kingereza bungeni wakati akiomba kura kuwa mwakilishi kwenye bunge la SADC? Lakini kwa uzezete wa wabunge wa CCM wakampigia kura 100%.

Sasa mnategemea nini kutoka kwa mtu kama huyo?

Hivi hakutokea mwannchi yeyote akamuuliza swali kwa kingereza ili tusikie vioja?
 
Wenzako hatukurupuki. Majibu ya maswali yako ya kizushi haya hapa:

Friend of Gaddafi named to head Libyan parliament

Hii ndio njia maridhawa ya kuwaumbuwa mijitu inayojifanya kujuwa kila kitu kumbe hakuna wanalojuwa, wakati kila kitu kimo humuhumu kwenye internet.

Mohamed shossi tunakuomba na wewe mwaga data kama hizi au kubali kwamba nia yako ilikuwa ni kupotosha watu au upo humu kazi yako ni ubishi bila kuwa na data.
 
Kinamuuma nini msaada unakuja kwa CDM kwawaambie marafiki wa chadema wasitoe msaada,uwe wa ndani na nje ni msaada,
Hili libibi mdomomdomo tu,.natamani nili.........
 
Waukaye binti simba ucha myangu.
wanaandamana kwa ajili yako wewe mwanangu, ili uwagawie kidogo hilo pilau la taifa.

Uwaziri wewe.
ubunge wa kuteuliwa wewe.
ubunge sadeki wewe.
mjumbe nec wewe.
Hukatai aaah una nini zaidi ya wenzio acha ubinafsi.

Wewe ni roboti ili uyaweze yote hayo?
Haya ucha lelo wanakuja hao nguvu ya uma wamesha changanyikiwa wasije wakakutunisia! achia mapema ukalime hogo.

Nakukumbusha sembe la muhogo lile jeusi mboga pandu ima ndimu chumvi na pilipili kiswasa! kwabaho?
 
Hizi porojo zimepikwa maksudi ili kupoteza lengo, na kamwe mtu hasifikirie ya kwamba huyo mama ajuhi ukweli kwamba hakuna cha fedha za kutoka nje katika shughuli hii, na vile vile kwamba hakuna anayelipwa kwaajili ya kushiriki kwenye maandamano.

Hapana shaka yeyote mwitikio wa wananchi kwenye maandamano hayo umeifanya serikali kuwa na hofu na ndiyo maana inajaribu kutafuta visingizio vya kuielezea hali hiyo
 
Natamani hata kumg'ata huyo Sophia, anasema kama kuna tatizo inamaana kuwa hawajui kuwa sisi tuna matatizo kiasi gani?

kumbe tunaweza kuwa tuna walaumu jama kila siku kumbe hawajui kama sisi tuna matatizo eti??

Hayo sio matusi na kejeli kwa wananchi waliowaweka madarakani??
Matamshi haya ya Sophia yanaonesha kuwa serikali ya Kikwete inaamini kuwa foreign governments are funding CHADEMA ili kifanye maandamano na kuleta vurugu nchini.

Watawala wanajiaminisha kuwa eti CHADEMA inawalipa wale maelfu ya Watanzania wanaojitokeza kwenye maandamano.

Msimamo wa serikali ya Kikwete imenikumbusha ya Gadaffi wa Libya ambaye US President Ronald Reagan alimuita kama "The Mad Dog of the Middle East" way back in 1986.

Gaddafi alisema: "Wananchi wa Libya wananipenda sana. Wanaoshiriki maandamano wamelishwa madawa ya kulevya na Al Qaeda na Marekani."

Pia kwa kusema "Kama kuna matatizo yoyote, serikali itayashuhulikia," hii ina maana kuwa watawala hawatambui matatizo lukuki ya wananchi wa Tanzania ambao ni kama kila mmoja kabeba gunia la misumari -- mgao wa umeme, Dowans, ufisadi, umasikini, ukosefu wa ajira, mfumuko wa bei, maisha magumu, kuporomoka kwa elimu, afya duni, ukosefu wa maji, maradhi, viongozi serikalini kutokuwa na maadili, wananchi kunyimwa haki zao, na mengineo mengi.

The CCM government is in denial.
 
vyeo namadaraka ni mengi sana ndio maana walishajisahau kabisa kama wananchi wana matatizo.
to me I count her comment as such an insult.
Waukaye binti simba ucha myangu.
wanaandamana kwa ajili yako wewe mwanangu, ili uwagawie kidogo hilo pilau la taifa.
Uwaziri wewe.
ubunge wa kuteuliwa wewe.
ubunge sadeki wewe.
mjumbe nec wewe.
Hukatai aaah una nini zaidi ya wenzio acha ubinafsi.
Wewe ni roboti ili uyaweze yote hayo?
Haya ucha lelo wanakuja hao nguvu ya uma wamesha changanyikiwa wasije wakakutunisia! achia mapema ukalime hogo.
Nakukumbusha sembe la muhogo lile jeusi mboga pandu ima ndimu chumvi na pilipili kiswasa! kwabaho?
 
hizo ni kelele za chura huyu mama mama ni feki sana sijui katumwa au inakuwaje maana kila siku anaongea matope tu, bora angeongea pumba maana ni chakula cha mifugo! angekuwa amefanya la maana kama angetoa ushahidi wa alichokwa anazungumza vinginevyo akapimwe akili huyu!
 
Huyu mama nilimsikia juzi akiongea nilishangaa.. hana tofauti na Khadija Kopa enzi zile walivyokuwa wakipashana na Mwanahamisi Kidogo (sorry najua kwa sasa ni marehemu).

Nilijiuliza mtu anayeongea pumba hivi amekuwaje waziri??? Huwezi kuwa na mategemeo ya maendeleo kupitia mama huyu na mawaziri wengine wanaokalia mipasho badala ya kuchapa kazi.:A S 13:
 
Badala ya kujibu hoja anatafuta mchawi, tulisema loong time ago kwamba something is not very right na the thinking za huyu mama!, Hivi huko TBC hakukuwa na mtu wa kumuuliza yeye zile Billions za kampeni yake ya Mwenyekiti wa UWT alizipata wapi?

Kwani Tanzania tuna sheria inayokataza chama cha siasa kupokea hela toka nje? Je CCM haipokei hela toka nje? CCM wangejibu hoja badala ya kutafuta wachawi wao ambao ni wao wenyewe!

CCM bwana kweli ni kichwa cha ajabu sana, Wapiganaji walipowapigia kelele huyu huyu mama na Anna Abdallah walikuwa kimbele mbele kuwaponda, sasa kelele zile zile zinatokea Chadema, wanalia hela kutoka nje! ha! ha! ha! ha! what a joke na huu uongozi!
 
Maneno ya Simba yana mantiki, si rahisi kuandaa maandamano kila kukicha, unahitaji bajeti nono. Jee fedha zinatoka wapi?

Bajeti nono kufanya lipi!

Wananchi wanakuja wenyewe, wanatembea kwa miguu yao! Wakipata kiu wananunua maji kwa waleti zao!

Hakuna posho za kushiriki maandamano.

Viongozi/wabunge wa Chadema wanaoshiriki maandamano si wengi CDM kushindwa kuwalipia nauli, kama inahitajika lkn.
Majimshindo na Sofia Simba. Chadema haiitaji malori kuleta watu, hailipi wananchi, haihitaji bendi, haiwahitaji ze comedy wala vivutio vya kuwavuta waTZ kushiriki mikutano.
Siwashangai Sofia na majiMshindo, C** bila haya mambo hayaendi.
 
- Badala ya kujibu hoja anatafuta mchawi, tulisema loong time ago kwamba something is not very right na the thinking za huyu mama!, Hivi huko TBC hakukuwa na mtu wa kumuuliza yeye zile Billions za kampeni yake ya Mwenyekiti wa UWT alizipata wapi? Kwani Tanzania tuna sheria inayokataza chama cha siasa kupokea hela toka nje? Je CCM haipokei hela toka nje? CCM wangejibu hoja badala ya kuatfuta wachawi wao ambao ni wao wenyewe!

- CCM bwana kweli ni kichwa cha ajabu sana, Wapiganaji walipowapigia kelele huyu huyu mama na Anna Abdallah walikuwa kimbel mbele kuwaponda, sasa kelele zile zile zinatokea Chadema, wanalia hela kutoka nje! ha! ha! ha! ha! what a joke na huu uongozi!


FMeS!

Kuna tatizo kubwa sana broda! Hatupendi kusikia ukweli tunakwepa hoja kwa mipasho. Watanzania kila siku wanazidi kujua ukweli na uongo wa wanasiasa wetu. Ifike wakati maslahi ya nchi yawekwe mbele.

Ni aibu miaka 50 baada ya uhuru hatuna cha kujivunia kama taifa. Hatuna maji, umeme, elimu inazidi kushuka, rushwa na ufisadi vyashamili kwa kisingizo cha utulivu na amani!
 
Maneno ya Simba yana mantiki, si rahisi kuandaa maandamano kila kukicha, unahitaji bajeti nono. Jee fedha zinatoka wapi?

Nyie mnavyokwiba kura na kumuweka mkwere madarakani kilazima hela mmepata wapi???mtalijua jiji mwaka huuu
 
Wenzako hatukurupuki. Majibu ya maswali yako ya kizushi haya hapa:

Friend of Gaddafi named to head Libyan parliament

Friend of Gaddafi named to head Libyan parliament | Top News | Reuters

Hii ndio njia maridhawa ya kuwaumbuwa mijitu inayojifanya kujuwa kila kitu kumbe hakuna wanalojuwa, wakati kila kitu kimo humuhumu kwenye internet. Mohamed shossi tunakuomba na wewe mwaga data kama hizi au kubali kwamba nia yako ilikuwa ni kupotosha watu au upo humu kazi yako ni ubishi bila kuwa na data.

Sipo kwa ajili ya kubishana nipo kwa kutaka kuelimika samahani kama hapa Jf wanatakiwa wanaojua tu.
 
Kuna tatizo kubwa sana broda! Hatupendi kusikia ukweli tunakwepa hoja kwa mipasho. Watanzania kila siku wanazidi kujua ukweli na uongo wa wanasiasa wetu. Ifike wakati maslahi ya nchi yawekwe mbele. Ni aibu miaka 50 baada ya uhuru hatuna cha kujivunia kama taifa. Hatuna maji, umeme, elimu inazidi kushuka, rushwa na ufisadi vyashamili kwa kisingizo cha utulivu na amani!

Well, tumewaruhusu kwa muda mrefu sana na hii tabia, lakini now it is coming to an end na ni ishu kama hizi ndio unaona uwezo wa kufikiri wa viongozi wetu ulipo, badala ya kujibu hoja anajaribu kuuondoa mjadala na kuupeleka kwenye hela kutoka nje as if chama cha siasa kupokea hela toka nje ni kuvunja sheria ya Jamhuri, ndio huwa tunaita ma-viongozi magoi goi!
 
Back
Top Bottom