Serikali: CHADEMA inapewa pesa kutoka nje kuleta machafuko Tanzania

Ni kweli, ana uelewa mfinyu sana. Wiki iliyopita alitamka bila ya aibu kuwa Misri imekuwa ikiongozwa kijeshi tangu mapinduzi ya gamal Abdel Nasser ya mwaka 1952 -- hakujua kwamba Misri ilianza kuwa na demokrasia ya vyama vingi tangu wakati wa Sadat 1971 na kuwa na chaguzi ambazo kila mra chama tawala NDP ndiyo kilikuwa kinashinda, kwa kuchakachua (kama vile CCM tu) hadi 2011 Tahrir ilipotokomeza uchakachuaji huo!

Labda angesema Misri ilikuwa inatawaliwa na wanajeshi, au waliokuwa wanajeshi -- lakini siyo kijeshi!!!

MNembe afahamu kuwa tuko wengi tu ambao tuna uelewa wa historia na mambo ya ulimwengu kwa hiyo achunge sana kauli zake hasa pale, inaposemekana ana mikakakti ya kuingia Ikulu 2015.

Hivi kwa nini haya mazungumzo na hasa linapokuja suala la kumjadili Membe watu wanakosa focus. Watashika hili na baada ya muda kidogo topic inabadilishwa.

Hoja hapa ni kwamba kuna balozi zinazoshukiwa kukisaidia chama fulani cha upinzani na hadi sasa hatujui na TLP, NRA, CUF au NCCR Mageuzi. Sasa kujadili mada kwa hisia kwamba chama hicho ni kile kilicho maarufu kwa wengi humu, hazina msingi wowote. Sasa kama kuna ushahidi kwamba alichoeleza yeye hakina ukweli basi watu watoe data za kumkosoa siyo kurukia lile au hili kwa nia tu ya kujaribu kuonyesha kwamba mtu huyo haaminiki.

Kuhusu suala la utawala wa Misri yeye alitamka wazi kabisa kwamba nchi ile imekuwa chini ya utawala wa kijeshi kwa msingi kwamba wale waliofanya mapinduzi mwaka 1952 ndiyo hao hao wamekuwa wakibadilishana uongozi.

Hicho unachoita wewe mfumo wa vyama vingi kama aivyofanya Sadat ni kiini macho na ndiyo maana vyama vyote hivyo kikiwemo Muslim Brotherhood vimekuwa vinapata misukosuko na hata viongozi wao kuwekwa kizuizini.

Hicho kinachoitwa demokrasia si demokrasia na ndiyo maana hata leo ni military junta ileile ndiyo iliyopo madarakani. Kwa ujumla ukosoaji huu ni ule ule uliochochewa na chuki za mtoa mada bila kujali kile alichoongea na ndiyo maana kuna kurukia rukia mada. Wenye akili wanajua kiini cha ukosoaji huu holela!
 
Kwa ujumla mie huwa simpendagi huyu. Namwona ana majidai sana na maringo -- kama vile yule Lukuvi. Tena nasikia aliwahi kuwatesa na kuwauwa askari wa Uganda waliokuwa wakikamatwa mateka na kupelekwa kwake kuhojiwa.

Anyway, haya yote na mengine itabidi yawekwe hadharani ikifika 2015 ikiwa kweli atataka kugombea kwenda Ikulu.

Saafi sana kwa kuusemea moyo wako hadharani. Natoa changamoto kwa wengine wenye chuki binafsi kama wewe kutangaza msimamo wao bayana ili tujue na tuwasamehe kwa waliyoyaongea na yale watakayoyaongea huko mbele ya safari!
 
Mkuu salaam:
Sasa mbona unajichanganya? Hiyo miaka penye wekundu ni upi unaotangulia? Maana unaonekana umekerwa kwamba amesema ilitawaliwa kijeshi tangu 1952 na hajui kwamba Misri ilianza kuwa na mfumo wa vyama vingi tangu 1971 wakati wa Anwar Saadat? Mbona sasa 1952 inatangulia kabla ya 1971? Na ni kweli mwaka huo 1952 kulikuwa na mapinduzi ya kijeshi ambayo yaliongozwa na Meja General Mohamed Naguib ambaye akawa Rais wa kwanza kabla ya Abdel Nasser kuwa Rais wa pili kunako 1954. Hukumsikiliza kwa makini Mh.Membe. Huyu ni mwana Diplomasia na hizi data ndogondogo anazo kwenye finger tips.
Nilimsoma W.Slaa katika thread moja akisema kwamaba mara nyingi viongozi wapoongea sicho kinachoripotiwa na wana habari. Kuna upotoshwaji mwingi hapo katikati. Na alikuwa akisema haya kufuatia kauli yake tata juu ya kifo cha mkuu wa mkoa Shinyanga. Sasa je na hapa tumhukumu Dr. Slaa kwamba si makini na hatufai,, tayari keshatangaza habari za kifo huku mtu yu hai?? Je tuseme ana uelewa finyu?? kwa hilo?
Napita fasta.

Heshima kwako mkuu! Hapa umewatoa watu tongotongo lakini wale wenye chuki zao binafsi wacha wachonge lakini sisi wenye utimamu wa akili tunajua thamani ya kile alichokizungumza.
 
Most of us w think twiceon each speech.

JK please talk to team members. they should be extra careful on their words.
Wanachochea machafuko





Fumbo mfumbie mjinga mwelevu na mimi tutata........................
 
Nimewasiliana na Afisa Habari Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje kupata ufafanuzi, alichonijulisha ni kuwa Membe aliulizwa swali na Mwandishi wa Habari ikiwa Wizara inafahamu kuwa ziko tuhuma kuwa nchi za magharibi (bila kutaja jina) zinafadhili upinzani nchini. Jibu la Waziri lilikuwa fupi sana nalo ni " Serikali imesikia pia tuhuma hizo na inazifanyia kazi".

Je, Waziri alitakiwa kujibu nini? Kwanini upinzani udhaniwe kuwa ni CHADEMA tu? Wale mnaosema awataje, atawatajaje kama tuhuma hazijathibitika na pengine ni uzushi tu? Na kwa kuwa watuhumiwa ni serikali za nchi za nje zenye mahusiano ya kidiplomasia na Tanzania chini ya Mkataba wa Viena wa 1961, je nani angetakiwa kujibu swali hilo?

Mwalimu Nyerere aliwahi kuelekeza "Argue don't Shout". Angelikuwa ametaja Chama na kuthibitisha ukweli wa tuhuma hizo, thread hii ingekuwa na msingi.

Si, sahihi na itaendelea kuwa si sahihi kwa chama chochote cha siasa cha nchi hii iwe CCM au chochote kile kufadhiliwa kutoka nje kwa kuwa ni hatari kwa ustawi na usalama wa nchi yetu. Pengine ningetegemea mjadala humu ungejikita kuhusu athari za Chama cha siasa kufadhiliwa na Serikali ya Nje na nini kifanyike. Nawapongeza CHADEMA kwa kupata ufadhili wa ndani wa Sabodo wa wazi , lile linakubalika, napinga ufadhili wa kificho wa ama serikali kutoka nje au wafanyabiashara wa ndani kwa chama chochote. Kama ufadhili wa kificho wa wafanyabiashara wa ndani umetuletea ufisadi tuliokuwa nao leo, ufisadi wa nje utatuletea madhila gani?

Tanzania ni muhimu zaidi kuliko vyama vyetu. Tusijifunge kwenye box la ushabiki wa vyama.

Sheba Mkuu wangu!

Watu hapa wanajaribu kutafuta justification ya kumuadhibu huyu bwana hata asipostahili kuhukumiwa. The response was given in the passing na jibu hilo lilisadifu swali lililoulizwa. Tuache kuwafanya watu ni mbumbumbu kwa sababu ile taarifa sisi wote tuliiona na alichojibu pengine wala hakikuhitaji kupata ufafanuzi kutoka kwa afisa habari, lakini kwa sababu ya mkanganyiko huu wa makusudi ndo sasa umeingia gharama ya kupata ukweli wa ziada ambao haukuhitajika.

Lakini kwa vile kinachotafutwa hapa ni namna ya kumnyonga "mtuhumiwa " huyu hata kama hana hatia ndo maana tunajikuta tuko hapa tulipo. Sinema ndo kwanza inaanza, nilitabiri kwamba mradi huyu bwana anaonekana ni kikwazo kwa mradi wa wakubwa, haya yataendelea mpaka lengo litimie.
 
Jana waziri wa mambo ya nje benard membe amesema wana taarifa kwamba kuna nchi za magharibi kupitia balozi zao hapa nchi ambazo zinakifadhili chama kimoja cha siasa ili kuchochea machafuko. Hizi ni tuhuma nzito sana ambazo hazipaswi kufumbiwa macho. Kama ni kweli mpango huo upo serikali inapaswa kujiuliza mara mbilimbili kulikoni mabalozi hao wasaliti uhusiano wa kibalozi uliodumu miaka mingi kipindi hiki? Pili, kwa nini mabalozi waache kufadhiri miradi ya maendeleo waende wakafadhiri machafuko??? TAFAKARI!!!!

Kama ni kweli kwanini asiweke majina ya nchi hizo hadharani? Ni kipi kinachowaogopesha kufanya hivyo?

Mimi naona huu ni usanii tu wa kujaribu kuzikwepa lawama chungu nzima dhidi ya Serikali hii katika utendaji wake ambao umekuwa si wa kuridhisha hata kidogo.
 
Hivi ni nani alizua uongo kwamba Maalim Seif alikuwa anafadhiliwa na nchi za kiarabu na kupanga shehena ya uongo ya silaha alizosingizia Maalim Seif kaletewa toka Arabuni kutumia kuangusha serikali ya Zanzibar wakati maalim seif alipokuwa waziri kiongozi wa Zanzibar?

Baadaye ukweli ulijulikana lakini maalim seif naye alikuwa mtu hatari kwa fitna, kwani aliendesha fitna za uongo kumtoa Abdu Jumbe madarakani. Hivyo hakuonewa huruma, ukizingatia kwamba aliyefanya fitna dhidi yake alikuwa ni kijana mdogo tu ndani ya TISS.

Nani aliasisi fitna za uongo dhidi ya Sali Ahmed Salim mwaka 2005 ili asiwe tishio kwa JK?

Haya Chadema, msiangalie miguuni kwenu bali mwisho wa upeo wa macho yenu 360 degrees!
 
Back
Top Bottom