Matamshi haya ya Sophia yanaonesha kuwa serikali ya Kikwete inaamini kuwa foreign governments are funding CHADEMA ili kifanye maandamano na kuleta vurugu nchini.Waziri wa Jakaya Kikwete, Sophia Simba, akiongea kwenye TBC leo asubuhi amesema kuwa viongozi wa CHADEMA wanapewa pesa nyingi kutoka nje ili kufanya maandamano kwa lengo la kuifanya nchi isitawalike.
Sophia amesema kuwa CHADEMA wamekuwa wakiwapa wananchi pesa ili washiriki maandamano hayo.
"Eti wanaandamana kuhusu DOWANS na uchumi. Kwa kuwa kesho ni siku ya kimataifa ya wanawake, nachukua fursa hii kuwasihi wanawake wasishiriki maandamano ya kikundi hiki. Kwanza wanakupa pesa za siku moja tu, huko kwenye maandamano kuna uchumi?" Alisema.
"Haya maandamano hayana tija."
Sophia aliwataka wananchi, hasa wanawake, wasipoteze muda kwenda kwenye maandamano ya CHADEMA kwani muda huo wangeutumia kufanya ujasiriamali.
"Kama kuna matatizo yoyote, serikali itayashuhulikia," alisema.
Watawala wanajiaminisha kuwa eti CHADEMA inawalipa wale maelfu ya Watanzania wanaojitokeza kwenye maandamano.
Msimamo wa serikali ya Kikwete imenikumbusha ya Gadaffi wa Libya ambaye US President Ronald Reagan alimuita kama "The Mad Dog of the Middle East" way back in 1986.
Gaddafi alisema: "Wananchi wa Libya wananipenda sana. Wanaoshiriki maandamano wamelishwa madawa ya kulevya na Al Qaeda na Marekani."
Pia kwa kusema "Kama kuna matatizo yoyote, serikali itayashuhulikia," hii ina maana kuwa watawala hawatambui matatizo lukuki ya wananchi wa Tanzania ambao ni kama kila mmoja kabeba gunia la misumari -- mgao wa umeme, Dowans, ufisadi, umasikini, ukosefu wa ajira, mfumuko wa bei, maisha magumu, kuporomoka kwa elimu, afya duni, ukosefu wa maji, maradhi, viongozi serikalini kutokuwa na maadili, wananchi kunyimwa haki zao, na mengineo mengi.
The CCM government is in denial.