Elections 2010 Serikali: Bei za saruji, nondo zishushwe (maji ya shingo sisiem)

Geza Ulole

JF-Expert Member
Oct 31, 2009
58,779
78,450
20th October 10
Serikali: Bei za saruji, nondo zishushwe

Richard Makore

Serikali imeviagiza viwanda vya saruji na nondo nchini kuhakikisha vinapunguza bei ya bidhaa hizo kwa kuwa hakuna sababu yoyote ya msingi inayochangia zipande mara kwa mara.
Agizo hilo lilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara Viwanda, Biashara na Masoko, Joyce Mapunjo, alipozungumza na NIPASHE kuhusu upandaji holela wa bidhaa hizo.
Alisema uzalishaji wa saruji na nondo ni mkubwa lakini hajui kwanini wazalishaji hao wanazipandisha na kuwafanya wananchi wa kawaida kushindwa kuzinunua.
Aliahidi kufuatilia kwenye viwanda hivyo ili aelezwe sababu zinazowafanya wazidi kupandisha bidhaa zao kwa mauzo ya jumla na hivyo kuwafanya wauzaji wa rejareja nao kupandisha bei.
Bei ya nondo yenye milimita 10 yenye urefu wa futi 40 kwa sasa ni Sh.10,000 kutoka Sh. 8,000 milimita 12 Sh. 13,000 badala ya Sh. 12,000 na bei ya mfuko mmoja wa saruji hivi sasa ni Sh. 13,000 badala ya Sh. 12,000.
Na katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa Wakala wa Serikali Biashara na Leseni nchini (Brela), Esteriamo Mahingila, aliwataka wazalishaji na wakulma kujiwekea malengo ili kuhakikisha wanaziwekea nembo bidhaa zao zote wanazozalisha.
Mahingila alikuwa akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo wataalamu wa masuala ya hakimiliki duniani ambao wanahakikisha bidhaa zinakuwa na nembo na alama kabla ya kuuzwa.

NIPASHE
Serikali: Bei za saruji, nondo zishushwe

MY TAKE
Sitashangaa Mzugaji wetu kubadili sera na kusema elimu bure toka chekechea mpk chuo!!
 
Uyo punjo analeta masihara kwenye business viwanda ivyo vimepandisha saruji bse of increasing cost of prodution but of latest ni kuongezeka kwa dola rate.
 
Duhh! serikali gani hii ya kihuni? Tumfuate Waziri Kamala au Katibu mkuu?? - Upuuzi gani huu!!:mmph::biggrin1:
 
Hayo angewaambia watu wa Bukoba alafu wakamchagua tungemwamini kumbe kapigwa chini kisa Pumba na kuwa na PHD fake na porojo nyingi.
Kwani tukijitoa EAC tutakufa?
Umekamua uchumi hujui tofauti ya ushuru na ruzuku?
Oh poor Kamala unaruhusiwa kupitia pitia vitabu vyako.
Sandstone,limestone,clay na gypsum vyote vyapatikana nchini isipokuwa Coal ambayo inatoka nje has baada ya kukabizi Kiwira kwa Mkapa.
Tukianza chimba mkaa kule Ngaka/songea na Mchuchuma/Liganga then angalau tukaanza kutumia umeme wa uranium toka Namtumbo au wa gas bei ya cement lazima ishuke aache sound huyu.

Kuna viwanda vinalipa umeme mpka 400mil a month sasa kwa nini saruji isiwe ghali.
Alafu akumbuke sometimes sarauji inakuwa ghalama bse of poor infrastructure imagine maeneo kama Mbinga,Mbambaay,Kigoma,Singida,Kasanga na maeneo mengine yenye rough road pamoja na kuwa mbali na maeneo ya viwanda ivyo ni kero namba moja.
 
Dr.Slaa alisema atashusha bei ya vifaa vya ujenzi wakabisha ..Kiko wapi sasa.serikali ya kihuni kabisa?yaani huyu Joyce Mapunjo ndo asiongee kabisa kazi kunywa mi konyagi tu kule trinity
 
Kiuaminifu, bei za vitu vinategemea gharama za uzalishaji, hakuna uchawi..Ila kwa bongo, ambapo commonsense is not the order of the day, anything is possible.
 
Hawa watu kweli ni vilaza ..ni bora tu wakae kimya tusijue mapungufu yao ya akili..sasa mtu anasema viwanda vipunguze bei saabu hawana sababu yeyote ya msingi ya kupandisha bei..hapohapo anakuja kusema inabidi afanye ziara aangalie kitu gani kinasababisha kupanda...Sasa kwanini asingeanza kwanza kufanya ziara apate data za kutosha ndio aweze kusema lolote kuhusu bei za hizo bidaa za ujenzi?? Mtu mkubwa kama huyo aliye na mamlaka makubwa kabisa katika wizara ambayo inasimamia sekta hiyo kuzungumza kama a layman niaibu kubwa na nachelea kusema huyu mama ha fit katika hiyo position. Kama katumwa basi ana shida huyu...Bei ya sementi kupanda zanasabishwa na serikali yenyewe....gharamakubwa ya uzalishaji wa sementi ukiondoa gharama za manpower huletwa na Umeme wa Tanesco ambayo kwa mwezi ni si chini ya Mil 300,na hapo bado Tanesco wanaomba EWURA kuongeza gharama za umeme na hapo hapo bado serikali inasema hawa watu wamshushie bei ya sement mwananchi..Hivi serikali ya Tanesco na ya viwanda hivi ni Tofauti?>? na bado umeme wenyewe sio reliable haya kuna HFO, Petrol and diesel ya kuendeshea mitambo mbalimbali ya kiwanda..kila leo bei inapanda na kamwe haishuki...je serikali inajua kua kupanda kwa mafuta pia kunaathiri bei ya vitu kama sementi??? haya tena Makaa ya Mawe ( coal) ambayo ndio huchangia gharama kubwa zaidi ya uzalishaji wa sementi..serikali imeshaua viwanda vya ndani vya kuchimba makaa hayo kama Kiwira Coal Mine...ambayo uwepo wake ungesababisha upunguaji mkubwa wa gharama za upatikanaji wa hii Nishati..sasa Coal inayotumika zaidi hupatikana South Africa na ni ya gharama kubwa ukilinganisha na ya hapa sababu ina components nyingi ..Purchasing Price + All TRA clearing duties +All landed costs.Na ubaya zaidi components nyingi zinakua determened na foreign currency ( USD ) ambayo ndio Purchasing Currency ,so dolla Ikipanda na gharama ya coal pia kwa hela ya kikwetu hupanda na hivyo kusababisha gharama za uzalishaji kuwa kubwa na mwishowe bei ya sementi kupanda...sasa tuchukulie suala kama hilo je huyu mzalishaji ana influece yeyote na suala la kupanda au kushuka kwa dola???au je Mzalishaji huyu ana influence yeyote ya kuanzishwa kwa kiwanda chakuzalishia makaa ya mawe hapa nchini?? Mimi ndhani mwenye influence na vitu vyote ivyo ni serikali na siyo mzalishaji wa sementi au Nondo....yenyewe Serikali ndio itakayoweza kushusha bei za sementi mpaka TZS 5,000 kama ikiwa serious na kuvalia njuga hayo matatizo yote...Kajipange vizuri KATIBU
 
Duhh! serikali gani hii ya kihuni? Tumfuate Waziri Kamala au Katibu mkuu?? - Upuuzi gani huu!!:mmph::biggrin1:

Kweli kabisa upuuzi gani huu! Juzi tu Kamala kamwita rais Mtarajiwa mbumbumbu kwa kusema kwamba atashusha bei ya saruji na mabati leo serikali inadandia sera za Dr Slaa na Chadema ambazo tuliambiwa hazitekelezeki!! Matumbo moto. Pigia kura chadema na Dr Slaa.
 
Sometimes sio lazima mtu akuone mjinga bali matendo yako yanaweza kudhihirisha una matatizo ya akili hivi kukataa kwamba Cement haishuki bei then ukapiga u turn kusema inaweza kushuka si mambo ya ajabu jamani? Inamaana basi kumbe kuna mambo mengi yanawezekana but either yameepuuzwa au zilikuwa nyanza za ufisadi kwa watu fulani. Tanzania hii ni Tanzania nyengine jamani wasomi wapo wengi hatutawaliki kijinga namna hivyo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom