KIGENE
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,552
- 813
Kwa mjibu wa taarifa ya habari ya saa moja leo asubuhi Kamishna wa Sensa amesema sheikh Ponda pamoja na makeke ya kupinga zoezi la sensa alisalimu amri na kukubali kuhesabiwa.
Kwanini hakutumia jukwaa lilelile kuwambia wafuasi wake wakahesabiwe ili kuwaepushia karaha na kadhia za kukumatwa na kufunguliwa kesi na wengine kuwapiga wake zao walikubali kuhesabiwa achilia mbali waliokimbilia porini kuwakimbia makarani wa sensa?
>>>>>>>>>>>>>>>>>
Habari kamili hii:
Chanzo: Mtanzania | JUMAPILI, SEPTEMBA 02, 2012 | Mwandishi - ELIZABETH MJATTA
VINARA waliokuwa wakihamasisha waumini wa dini ya Kiislamu wasishiriki Sensa ya Watu na Makazi, akiwamo Sheikh Issa Ponda wamehesabiwa. Kauli hiyo, imetolewa na Kamishna Mkuu wa Sensa, Amina Mrisho mjini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari.
Alisema hadi jana mchana idadi ya watu ambao walikuwa hawajahesabiwa walikuwa chini ya asilimia tano.
Aliwataka watu ambao hawajahesabiwa wajitokeze kuanzia leo hadi Septemba 8.
"Tulianza kuhesabu watu Jumapili na ilipofika Jumatatu asubuhi vinara wote waliokuwa wakipinga Sensa walikuwa wamehesabiwa akiwamo Sheikh Ponda.
Alisema makarani walifika nyumbani kwake ambako walikuta hayupo lakini walielezwa kuwa amekwenda katika Msikiti wa Mtambani.
"Lakini katika jambo la kufurahisha mke wake alitoa ushirikiano wote kwa makarani, baada ya kutoa taarifa zote za familia yake.
"Lakini baada ya wakarani kumaliza kuihesabu familia yake, alirudi kuungana na familia yake…kwa hiyo yeye alihesabiwa sasa wale wengine ambao walikuwa wanalishwa kaa la moto wajue wamepotoshwa,wapo ambao tayari wamekamatwa na jeshi la polisi.
"Sina takwimu sahihi ni wangapi, lakini mkoani Kagera watu 15 walikamatwa, Kiteto watano ambao wanaume ni wanne na mwanamke mmoja, mkoa wa Kilimanjaro ambao wamekataa kuhesabiwa ni wengi mno… lakini mkoa kwa kushirikiana na jeshi la polisi, wanafahamu ni hatua gani wanazochukua,"alisema.
Alisema mkoani Kagara, ndiko kulikuwa na vituko vingi kwa sababu wanaume walikuwa wakifanya mañosa makusudi kwa nia ya kutaka kutelekeza familia zao.
Mrisho alisema pia kuwa ili kuondoa migongano katika suala la kipengele cha dini, taasisi hiyo iko katika mchakato wa kupeleka bungeni Sheria ya Takwimu Sura ya 351 ifanyiwe marekebisho.
"Novemba tutaipeleka bungeni ifanyiwe marekebisho kusiwe na sheria inayoruhusu mtu kutoa takwimu bila kupitia kwetu kwa sababu kuruhusu vitu kama hivi ndiyo vinaleta mkanganyiko.
"Katika nchi ambazo zimeruhusu suala la dini na kabila kuingia kwenye Sensa, kumetokea machafuko makubwa na hata watu kupoteza maisha, hatutakia haya yafike kwetu," alisema.
Akizungumzia malipo kwa makarani na wasimamizi wa Sensa, alisema fedha kwa ajili ya wenyeviti wa Serikali za Mitaa ziliwasilishwa katika mikoa na wilaya siku nyingi na yalitolewa maelekezo ya jinsi ya kuzigawa.
"Natumia fursa hii kutoa tahadhari kwa wale wenye mpango wa kuchakachua malipo haya sheria itachukua mkondo wake na tutamhusisha Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuwapata wachakachuaji," alisema.
Kwanini hakutumia jukwaa lilelile kuwambia wafuasi wake wakahesabiwe ili kuwaepushia karaha na kadhia za kukumatwa na kufunguliwa kesi na wengine kuwapiga wake zao walikubali kuhesabiwa achilia mbali waliokimbilia porini kuwakimbia makarani wa sensa?
>>>>>>>>>>>>>>>>>
Habari kamili hii:
Chanzo: Mtanzania | JUMAPILI, SEPTEMBA 02, 2012 | Mwandishi - ELIZABETH MJATTA
VINARA waliokuwa wakihamasisha waumini wa dini ya Kiislamu wasishiriki Sensa ya Watu na Makazi, akiwamo Sheikh Issa Ponda wamehesabiwa. Kauli hiyo, imetolewa na Kamishna Mkuu wa Sensa, Amina Mrisho mjini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari.
Alisema hadi jana mchana idadi ya watu ambao walikuwa hawajahesabiwa walikuwa chini ya asilimia tano.
Aliwataka watu ambao hawajahesabiwa wajitokeze kuanzia leo hadi Septemba 8.
"Tulianza kuhesabu watu Jumapili na ilipofika Jumatatu asubuhi vinara wote waliokuwa wakipinga Sensa walikuwa wamehesabiwa akiwamo Sheikh Ponda.
Alisema makarani walifika nyumbani kwake ambako walikuta hayupo lakini walielezwa kuwa amekwenda katika Msikiti wa Mtambani.
"Lakini katika jambo la kufurahisha mke wake alitoa ushirikiano wote kwa makarani, baada ya kutoa taarifa zote za familia yake.
"Lakini baada ya wakarani kumaliza kuihesabu familia yake, alirudi kuungana na familia yake…kwa hiyo yeye alihesabiwa sasa wale wengine ambao walikuwa wanalishwa kaa la moto wajue wamepotoshwa,wapo ambao tayari wamekamatwa na jeshi la polisi.
"Sina takwimu sahihi ni wangapi, lakini mkoani Kagera watu 15 walikamatwa, Kiteto watano ambao wanaume ni wanne na mwanamke mmoja, mkoa wa Kilimanjaro ambao wamekataa kuhesabiwa ni wengi mno… lakini mkoa kwa kushirikiana na jeshi la polisi, wanafahamu ni hatua gani wanazochukua,"alisema.
Alisema mkoani Kagara, ndiko kulikuwa na vituko vingi kwa sababu wanaume walikuwa wakifanya mañosa makusudi kwa nia ya kutaka kutelekeza familia zao.
Mrisho alisema pia kuwa ili kuondoa migongano katika suala la kipengele cha dini, taasisi hiyo iko katika mchakato wa kupeleka bungeni Sheria ya Takwimu Sura ya 351 ifanyiwe marekebisho.
"Novemba tutaipeleka bungeni ifanyiwe marekebisho kusiwe na sheria inayoruhusu mtu kutoa takwimu bila kupitia kwetu kwa sababu kuruhusu vitu kama hivi ndiyo vinaleta mkanganyiko.
"Katika nchi ambazo zimeruhusu suala la dini na kabila kuingia kwenye Sensa, kumetokea machafuko makubwa na hata watu kupoteza maisha, hatutakia haya yafike kwetu," alisema.
Akizungumzia malipo kwa makarani na wasimamizi wa Sensa, alisema fedha kwa ajili ya wenyeviti wa Serikali za Mitaa ziliwasilishwa katika mikoa na wilaya siku nyingi na yalitolewa maelekezo ya jinsi ya kuzigawa.
"Natumia fursa hii kutoa tahadhari kwa wale wenye mpango wa kuchakachua malipo haya sheria itachukua mkondo wake na tutamhusisha Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuwapata wachakachuaji," alisema.