kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,305
- 12,600
Kujua idadi ya watu unaowahudumia ni muhimu sana kuliko kitu chochote unachopaswa kukifamu. Hata mama nyumbani anahitaji kufahamu watu (idadi, umri, jinsia, afya zao) walioko nyumbani kwake ili ajue apike chakula kiasi gani na cha aina gani, ajue idadi ya sahani, vijiko, mashuka ya kujifunika, na mahitaji mengine yatakayowatosha watu wake.
Serikali pia inahitaji kufahamu idadi na aina ya watu wake ili iweze kupanga mipango ya kuwahudumia wananchi wake. Mfano, idadi ya watu kwenye wilaya husika ni kigezo kimojawapo katika kugawanya fedha (keki ya taifa) katika mawilaya, uchapishaji wa fedha/sarafu za nchi, kujenga shule, zahanati/hospitali, vituo vya police katika eneo fulani. Kuna njia tatu za namna ya kujua idadi ya watu nchini: 1. kuhesabu watu wote (sensa) kila baada ya miaka 10, kukadiria kulingana na idadi ya kuongezeka kwa watu kwa mwaka (growth rate) ambayo unatumia (waliozaliwa kwa mwaka - waliokufa kwa mwaka) + (waliohamia - waliohama nchi)+ Idadi ya watu mwaka uliopita, na njia ya tatu ya kujua idadi ya watu ni kwa kutumia takwimu (vital statistics) kwa kuweka kumbukumbu sahihi za vizazi na vifo, wahamiaji na wanaohama. Njia hii ya tatu ndiyo inayotumiwa na mataifa yaliyoendelea kwakuwa wana mfumo mzuri wa kusimamia vizazi, vifo, uhamiaji na uhamaji. Lakini sisi bado tuhahitaji sensa ili tujuane tuko wangapi.
Sasa kama wako watu ambao wanasema hawatashiriki sensa kwa sababu ya aina yoyote ile basi wanahitaji kuelimishwa na kuombewa, maana baada ya sensa kukamilika pesa, na huduma mbalimbali zitagawanywa kulingana na idadi ya watu kwa mujibu wa sensa 2012 kwenye eneo husika, watu watanza kushangaashangaa na kulalamika tena huduma nyingi zitakapoelekezwa sehemu zenye "watu wengi".
Serikali pia inahitaji kufahamu idadi na aina ya watu wake ili iweze kupanga mipango ya kuwahudumia wananchi wake. Mfano, idadi ya watu kwenye wilaya husika ni kigezo kimojawapo katika kugawanya fedha (keki ya taifa) katika mawilaya, uchapishaji wa fedha/sarafu za nchi, kujenga shule, zahanati/hospitali, vituo vya police katika eneo fulani. Kuna njia tatu za namna ya kujua idadi ya watu nchini: 1. kuhesabu watu wote (sensa) kila baada ya miaka 10, kukadiria kulingana na idadi ya kuongezeka kwa watu kwa mwaka (growth rate) ambayo unatumia (waliozaliwa kwa mwaka - waliokufa kwa mwaka) + (waliohamia - waliohama nchi)+ Idadi ya watu mwaka uliopita, na njia ya tatu ya kujua idadi ya watu ni kwa kutumia takwimu (vital statistics) kwa kuweka kumbukumbu sahihi za vizazi na vifo, wahamiaji na wanaohama. Njia hii ya tatu ndiyo inayotumiwa na mataifa yaliyoendelea kwakuwa wana mfumo mzuri wa kusimamia vizazi, vifo, uhamiaji na uhamaji. Lakini sisi bado tuhahitaji sensa ili tujuane tuko wangapi.
Sasa kama wako watu ambao wanasema hawatashiriki sensa kwa sababu ya aina yoyote ile basi wanahitaji kuelimishwa na kuombewa, maana baada ya sensa kukamilika pesa, na huduma mbalimbali zitagawanywa kulingana na idadi ya watu kwa mujibu wa sensa 2012 kwenye eneo husika, watu watanza kushangaashangaa na kulalamika tena huduma nyingi zitakapoelekezwa sehemu zenye "watu wengi".