Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 56,278
- 92,340
Yes its pay back time,
Matola siku zote unafiki kwangu mwiko, mimi ni miongoni mwa watu tuliofurahishwa na ninaendelea kufurahishwa huku nikicheka meno yote 32 nje.
Kwanini nafurahi? Ni kwa sababu kwa miaka nenda rudi CCM imeigeuza jamii ya Waislamu na hasa BAKWATA kama chombo chao cha kufanikishia maslahi yao, na pale linapokuja swala la waislamu kuomba madai yao basi huishia kwenye ghiriba tu.
Twende taratibu:
Mahakama ya kadhi: Huu ni mkenge CCM waliingizwa na Augustine Mrema ambaye aliwaahidi Waislamu kama angeshinda Urais basi angerudisha Mahakama ya kadhi, nao CCM kwa sababu ni mabingwa wa kuiga bila hata ya kufikiri nao wakaingiza kwenye ilani yao swala hili na mbaya zaidi Rais ni Mwislamu lakini anashindwa kutimiza ahadi halali iliyomo ndani ya chama chake.
Igunga:
Baada ya CCM kuona maji yapo shingoni waliamuwa kununuwa Bakwata na kuendesha kampeni za kidini eti Chadema kisipigiwe kura na Waislamu kwa sababu kimedhalilisha Mwanamke wa Kiislamu anayedhini na Mkristo Fatuma Kimario.
CCM kana kwamba hakielewi madhara ya Propaganda hizi chafu imekuwa ni silaha yake kusema Cuf ni chama cha Waislamu na Chadema ni Chama cha Wakristo, ila tu wao ndio hawajajitambulisha bado je ni chama cha shetani?
Kwa uchache tu niseme hili swala la Waislamu kugomea Sensa mimi nawaunga mkono kwa 100% angalau labda linaweza kuwa fundisho la kufungamanisha dini na siasa, kama CCM isingekuwa inaendesha Propaganda za kidini haya yasingekuwepo ndio maana nasema Yes is pay back time.
Tukumbuke hata kule Congo kwa kuendekeza ujinga kama huu kanisa Katoliki nalo lilikuwa na waangalizi wake kwenye ule uchaguzi na mpaka leo Kanisa katoliki Congo halimtambui Joseph Kabila kama Rais halali, na kanisa linayo matokeo yake ya ule uchaguzi. huu ndio uppuzi ambao CCM wanataka kutufikisha.
Tujadili.
Matola siku zote unafiki kwangu mwiko, mimi ni miongoni mwa watu tuliofurahishwa na ninaendelea kufurahishwa huku nikicheka meno yote 32 nje.
Kwanini nafurahi? Ni kwa sababu kwa miaka nenda rudi CCM imeigeuza jamii ya Waislamu na hasa BAKWATA kama chombo chao cha kufanikishia maslahi yao, na pale linapokuja swala la waislamu kuomba madai yao basi huishia kwenye ghiriba tu.
Twende taratibu:
Mahakama ya kadhi: Huu ni mkenge CCM waliingizwa na Augustine Mrema ambaye aliwaahidi Waislamu kama angeshinda Urais basi angerudisha Mahakama ya kadhi, nao CCM kwa sababu ni mabingwa wa kuiga bila hata ya kufikiri nao wakaingiza kwenye ilani yao swala hili na mbaya zaidi Rais ni Mwislamu lakini anashindwa kutimiza ahadi halali iliyomo ndani ya chama chake.
Igunga:
Baada ya CCM kuona maji yapo shingoni waliamuwa kununuwa Bakwata na kuendesha kampeni za kidini eti Chadema kisipigiwe kura na Waislamu kwa sababu kimedhalilisha Mwanamke wa Kiislamu anayedhini na Mkristo Fatuma Kimario.
CCM kana kwamba hakielewi madhara ya Propaganda hizi chafu imekuwa ni silaha yake kusema Cuf ni chama cha Waislamu na Chadema ni Chama cha Wakristo, ila tu wao ndio hawajajitambulisha bado je ni chama cha shetani?
Kwa uchache tu niseme hili swala la Waislamu kugomea Sensa mimi nawaunga mkono kwa 100% angalau labda linaweza kuwa fundisho la kufungamanisha dini na siasa, kama CCM isingekuwa inaendesha Propaganda za kidini haya yasingekuwepo ndio maana nasema Yes is pay back time.
Tukumbuke hata kule Congo kwa kuendekeza ujinga kama huu kanisa Katoliki nalo lilikuwa na waangalizi wake kwenye ule uchaguzi na mpaka leo Kanisa katoliki Congo halimtambui Joseph Kabila kama Rais halali, na kanisa linayo matokeo yake ya ule uchaguzi. huu ndio uppuzi ambao CCM wanataka kutufikisha.
Tujadili.
Wakuu hapa JF
Kama ambavyo tayari kuna baadhi ya members wametoa taarifa hapa jamvini juu ya mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika leo katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, umemalizika saa 12 jioni ambapo viongozi mbalimbali na wabunge kadhaa wa CHADEMA, wote wakiongozwa na Katibu Mkuu, Dkt. Willibrod Slaa wamehutubia maelfu ya wakazi wa mji wa Igunga na vitongoji vyake.
Kama ilivyo kawaida kwa Watanzania, mwitikio wa wana-Igunga pia kwa chama chao, kinachobeba matumaini yao na ya Watanzania wenzao ndani na nje ya nchi ulikuwa mkubwa, wakiendelea kudhihirisha utayari wao wa kushiriki na kumiliki mchakato wa mapambano haya ya awamu ya pili, ambapo kupitia M4C, Watanzania wanajiandaa kwa mabadiliko makubwa ya kimfumo na kikatiba.
Dkt. Slaa ametoa shukrani kwa wananchi wa Igunga kwa mshikamano mkubwa waliouonesha kwa chama chao CHADEMA na kwa mwanachama mwenzao, Joseph Kashindye (aliyekuwa mgombea ubunge Igunga), pia shukrani za dhati kwa mawakili, Profesa Abdallah Safari na Gasper, walioonesha na kudhihirisha hazina ya utaalam mbalimbali ambao chama hicho kinao.
Kisha akatoa salaam za pekee kutoka kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Kamanda Freeman Mbowe ambaye yuko nje ya nchi (Houston Marekani) kikazi, akisema yuko pamoja na wana Igunga katika harakati za kudai haki zao, salaam kutoka kwa Mjumbe wa Kamati Kuu, Prof. Safari ambaye hakuwepo (akisema anawapenda sana watu wa Igunga) na salaam kutoka kwa wanachama wa tawi la Reading, Uingereza.
Baada ya shukrani na salaam hizo, Dkt. Slaa akarudia kauli yake ambayo ameitumia katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Morogoro katika mikutano ya Operesheni Sangara-M4C, kuwasisitiza wananchi, bila kujali tofauti zao za kiitikadi, kushiriki katika zoezi la sensa litakalofanyika kuanzia usiku wa leo, Agosti 26, huku akirusha kombora kuwa mvurugano unaondelea juu ya suala hilo, ni matokeo ya 'sera' ya CCM na Rais Kikwete, kupandikiza udini, wakati kwa Watanzania hiyo haijawahi kuwa 'issue' kwao.
"Wananchi na Watanzania wenzetu wa Igunga napenda kutumia fursa hii kuwasihi Watanzania wote kushiriki zoezi la sensa ya watu na makazi ambalo litafanyika usiku wa leo. Natoa mwito wa Watanzania wote bila kujali tofauti zao zozote zile, zikiwemo za dini, kushiriki shughuli hii muhimu. Ni muhimu tukajua idadi ya watu na makazi yao ili iwe rahisi kuweza kupanga mipango yetu.
"Itakuwa rahisi kuibana serikali hii inayoelekea siku zake za mwisho mwisho, kwa mfano kila eneo lenye idadi ya watu 5000 inatakiwa kuwa na zahanati, kila eneo lenye watu wanaofikia 25,000, linatakiwa kuwa na kituo cha afya, hivyo ni rahisi kuweza kuwabana na kuhoji kwa nini wananchi hawa hawana huduma muhimu za jamii.
"Lakini pia wananchi, sisi au watoto wetu wakikosa huduma muhimu kama elimu, maji au afya, haitaangalia dini, sote tutakosa bila kujali dini zetu, elimu yetu, wala huduma za afya hazitolewi kwa kufuata misingi ya dini, tukikosa tunakosa wote bila kujali wewe ni dini gani, bila kujali wewe ni shehe au wewe ni askofu, tukikosa tutakosa wote.
"Haya yanayotokea hivi sasa katika suala la sensa, masuala ya dini ni matokeo ya sera za CCM na akina Kikwete kupandikiza udini kwa Watanzania. Tunawaambia CCM na Kikwete kuwa suala la udini wamelilea sasa linawapata vizuri. Kikwete ameendekeza udini sasa yamempata mwenyewe, wakati sisi tunakemea udini, CCM walikuwa wanaupalilia kwa propaganda zao.
"Kuendekeza udini ni kukiuka misingi yenyewe ya dini maana hakuna dini yoyote, hata katika Quran inazuia mtu kumbagua mwenzake kwa sababu ya dini yake, nimesoma juu ya comparative religion, hakuna dini inakubali ubaguzi, kuendekeza ubaguzi wa kidini ni kukiuka misingi ya dini yenyewe, vitabu vitakatifu vinazuia. Haya ni matokeo ya CCM kumomonyoa misingi yetu ya utaifa, huko nyuma sisi hatukuzoea haya, Watanzania wote tuliitana ndugu, hakuna mtu aliuliza au kujali dini ya mwenzake," amesema Dkt. Slaa.
More to come...