Selelii awazima Lowassa na Rostam

mkuu kumbuka ripoti ya Mwakyembe ilionyesha kuwa Rostam alikataa kutokea na alipuuza 'samansi'. Bila shaka Rostam alisha jiapiza kutohojiwa na Kamati ya Mwakyembe.

RA alikataa kutokea kwa hiari yake; kamati ya bunge ilikuwa na nguvu na uwezo wa kutumia njia zingine halali kisheria kuwalazimishiwa watuhumiwa kuhojiwa.

Kama wahusika wakubwa kwenye hili ni Lowassa na RA, ninashangaa kweli hii kamati ilishindwa kutumia nguvu zake kisheria kuwahoji hawa watu. Maneno ambayo wangeyasema mbele ya hicho kikao, yangelikuwa na nguvu na ingelikuwa hata rahisi kuwachukulia hatua za kisheria.
 
Nadhani itafikia wakati inabidi tuchague watu wa kuwajibu au kuwaelimisha.

Bob, angalia wewe na Bubu ataka kusema msije mkawa mnapoteza muda wenu bure. Angalia unajadiliana na nani.

Bubu usiyumbishwe na mtu hapa..Wape hao..Mwiba mkubwa kabisa kwao ni kuendelea kusema kama hivi!

Ishu ya mtu `ni nani` si kazi yetu, yeye anatakiwa kujijua ni nani na anafanya nini kwa Mtanzania ...basi!..Achana na waoga!
 
Ndugu zangu tukiondoa Ushabiki hakika tutaiona kweli na kweli itatuweka Huru Daima

1: Si vizuri mtu akipingana na Hoja na mtu basi apewe kundi like Fisadi, this is not fair na tusipoangalia tutakuwa tu discriminate mawazo mazuri hapa kwa Jamvi.

2: Hivi tujiulize

a:Mambo haya yanayozungumzwa sasa hivi kwa nini hayakujumuishwa kwenye Ripoti ya Kamati? Unajua kusema kwamba aliitwa kwenye kamati akakataa na hakuchukuliwa hatua yeyote ni kumpa RA uwezo/ujiko ambao hana kabisa unless yuko juu ya Sheria.

b: Je Serikali kutoteleza maazimio 23 ya Bunge, bunge limechukua hatua gani au limeamua kusalimu amri.

c: Ina maana huo ushahidi mwningine ni siri ya wajumbe wa kamati? hawa si walilipwa pesa na kutokana na hilo walipaswa kuwasilisha kila kitu walichokipata, sasa wao wakaamua kuficha baadhi ya Taarifa ili wamuokoe nani?

d: Kama ikitokea EL na RA wanaponyoka hapa ni wao ambao watakaokuwa wamewaponya na hao akina Mwakyembe kwa Kuwafichia baadhi ya Ushahidi

Kila kitu kinahitaji Timing wakuu, walikwa na nafasi nzuri sana ya Kuwamaliza Mafisadi ila wakaamua kuwasetiri sasa yamewafika shingoni wanalialia

Au wanataka RA ajipeleke mwenyewe Mahakamani?

Hivi ni kwa nini wasiwaandame akina AG na DPP kwa kushindwa kuwafungulia mashitaka
 
Huyu Seleli ndiye anayepaswa kuwa waziri wa ofisi ya Rais na Takukuru, maana alizoitoa ndio tunaita facts, hapa chini hakuna mipasho hizi ni facts au ushahidi kamili na unajisema wenyewe kama ulivyo, soma tena hizi facts hapa chini:-


Adai Kikwete alikabidhiwa mapema ripoti ya Richmond Asema kama kumuokoa ni yeye aliyepaswa kufanya hivyo

Selii alizima ndoto za Rostam na Lowassa baada ya kuanika ushiriki mzima wa wanasiasa hao wawili katika mkataba huo. Akiongea kwa kujiamini na kuchambua hoja moja baada ya nyingine,

1. Selelii alisema Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa Richmond ambapo yeye alikuwa mmoja wa wajumbe wake inaoushahidi kwamba Richmond ni mali ya Rostam.


2. Kwa upande wa Lowassa, Selelii alisema alibeba kampuni hiyo kwa maslahi ya binafsi ya rafiki yake huyo.

3. Selelii alisema
"Rostam amewadanganya kwa kusema hahusiki na Richmond."


4. "Huyu Rostam ndiye aliyetafuta nyumba kwa ajili ya matumizi ya ofisi ya Richmond. Ni yeye aliyelipia pango la nyumba hiyo," alisema Selelii huku akitolea macho Rostam.

5. Alisema, "Kamati yetu ilihakikishiwa na mtoto wa Mucadam (Hussen Mucadam) ambaye ndiye mwenye nyumba kwamba nyumba iliyotumiwa na Richmond ilipangwa na Rostam."


6. Selelii alisema "hata jopo la waadishi wa habari lililofanya kazi ya kusafisha Richmond lilitafutwa na Rostam."

7. Alisema Rostam alifikia hatua ya kutumia waandishi hao wa habari mara baada ya vyombo vya habari kuanza kueleza utata wa mkataba.

8. "Ni huyu Rostam aliyekodisha jopo la waandishi wa habari watatu mashuhuri nchini kwa ajili ya kupoza makali. Tumezungumza na waandishi wa habari hawa mmoja baada mwingine na wote wametuthibitishia hili," alisema Selelii.


9 Alitaja hata majina ya waandishi hao kuwa ni Gideon Shoo, Jimmy Mdoe na Salva Rweyemamu ambaye sasa ni mkurugenzi wa mawasiliano ya rais.

10. "Kama hahusiki kwa nini aliwatafuta hawa waandishi wa habari? Kwa nini aliwapa kazi," alihoji Selelii.

Alisema mbali na waandishi wa habari na utafutaji wa nyumba, Kamati Teule iliweza kuthibitisha kwamba baada ya Richmond kuhuisha mkataba wake kwa Dowans, wafanyakazi watatu wa Caspian walionekana katika Dowans.

11. "Kwa maana nyingine, Dowans, Richmond na Caspian ni baba mmoja mama mmoja." Alisema Kamati Teule imepata ushahidi kwamba "fedha za Dowans zilihamishiwa katika akaunti ya Caspian; Rostam alikuwa akifuatilia mwenyewe fedha hizo hazina," alisisitiza Selelii.


- Waziri Sophia anahitaji kujfunza from this, yaani kuongea na facts sio mipasho ya kitchen party, hizi juu ni facts ambazo ndio huwa tunalilia sana kwamba viongozi wetu na sisi wanachi tujifunze kuongea namna hiyo believe me itapunguza mabishano yote ya kitoto tunayopotezea muda nayo kila wakati hapa JF, Sophia angeweza kuongea namna hii bila tatizo angekwua my hero,

- Bravo Mheshimiwa Seleli, maneno haya hayafutiki na tutayatunza sana, maana ni adimu sana kuyapata katika siasa zetu Tanzania, tumezoea mipasho tu na blah! blah! hapa Mbunge ameweka wazi ukweli sasa ni clear hapa lawama iko kwa nani, iko kwa Rais na Waziri Mkuu wake maana kamati imefanya kazi yake imeweka facts wazi na mapendekezo, lakini hao wawili wameshindwa ku-deal na mapendekezo sasa tatizo ni lao, kuna waliooza CCM lakini sio wote, saafi sana Seleli tunahitaji viongozi 11 tu wanaotusimamia wananchi, na wasiobabaika na hizo Shillingi Millioni 50 zinazogaiwa na mafisadi huko bungeni sasa hivi, Bravo Seleli!

Respect.


Field Marshall Es!
 
Kama TZ wenye akili ndio wako hivyo, no wonder Tanzania tuna matatizo.

Au ndio ile ile ya kujifanya kwasababu unafundisha chuo kikuu basi una akili kuliko wengine?

Yeyote mwenye mawazo tofauti na yako ni fisadi, hayo ndio mawazo ya msomi, tena mwalimu majuu, inatia aibu kama sio kichefuchefu.

Mkuu vipi bwana mbona waenda personal.....halafu unataka kuwa mbunge kweli? Nadhani anzia kwanza udiwani! Mzee hunifahamu kabisa acha kunihusisha na mtu mwingine......sitaki andika habari za dada yako SUA na wewe! Ila ukiendelea na huu ujinga wakati watu wanakata issue za taifa hapa sina simile nitamwaga upupu vile vile
 
Ndugu zangu tukiondoa Ushabiki hakika tutaiona kweli na kweli itatuweka Huru Daima

1: Si vizuri mtu akipingana na Hoja na mtu basi apewe kundi like Fisadi, this is not fair na tusipoangalia tutakuwa tu discriminate mawazo mazuri hapa kwa Jamvi.

2: Hivi tujiulize

a:Mambo haya yanayozungumzwa sasa hivi kwa nini hayakujumuishwa kwenye Ripoti ya Kamati? Unajua kusema kwamba aliitwa kwenye kamati akakataa na hakuchukuliwa hatua yeyote ni kumpa RA uwezo/ujiko ambao hana kabisa unless yuko juu ya Sheria.

b: Je Serikali kutoteleza maazimio 23 ya Bunge, bunge limechukua hatua gani au limeamua kusalimu amri.

c: Ina maana huo ushahidi mwningine ni siri ya wajumbe wa kamati? hawa si walilipwa pesa na kutokana na hilo walipaswa kuwasilisha kila kitu walichokipata, sasa wao wakaamua kuficha baadhi ya Taarifa ili wamuokoe nani?

d: Kama ikitokea EL na RA wanaponyoka hapa ni wao ambao watakaokuwa wamewaponya na hao akina Mwakyembe kwa Kuwafichia baadhi ya Ushahidi

Kila kitu kinahitaji Timing wakuu, walikwa na nafasi nzuri sana ya Kuwamaliza Mafisadi ila wakaamua kuwasetiri sasa yamewafika shingoni wanalialia

Au wanataka RA ajipeleke mwenyewe Mahakamani?

Hivi ni kwa nini wasiwaandame akina AG na DPP kwa kushindwa kuwafungulia mashitaka

- With all due respect, hili sio tatizo la wapiganaji au anybody huko bungeni wao wametimiza walichotakiwa kukifanya na facts zimetolewa hizo juu, sasa ni tatizo letu wanachi kuwashinikiza Rais na Waziri Mkuu kuchukua hatua kutokana na mapendekezo ya bunge ambalo liliridhia kazi ya hii kamati.

- Haya maelezo yote aliyoyatoa Seleli yamo kwenye ripoti yao ya kamati, unless hukuiona tusidanganyane hapa!

Respect.


FMEs!
 
RA alikataa kutokea kwa hiari yake; kamati ya bunge ilikuwa na nguvu na uwezo wa kutumia njia zingine halali kisheria kuwalazimishiwa watuhumiwa kuhojiwa.

Kama wahusika wakubwa kwenye hili ni Lowassa na RA, ninashangaa kweli hii kamati ilishindwa kutumia nguvu zake kisheria kuwahoji hawa watu. Maneno ambayo wangeyasema mbele ya hicho kikao, yangelikuwa na nguvu na ingelikuwa hata rahisi kuwachukulia hatua za kisheria.

- Wala hawakuhitajika kuwepo mkuu, ushahidi upo wazi kuhusu uhusika wao na crime against jamhuri sasa serikali ndiyo ilitakiwa sasa kuwashika na kuwahoji kama suspects lakini sio tatizo tena la kamati ya wabunge, mbona tunajribu sana kukwepa ukweli? Kuna nini hasa kinachotafutwa?

Respect.


FMEs!
 
Ndio hapo napochoka na Wadanganyika.. yaani mnapewa ukweli na Mpiganaji badala yake mnamtazama yeye kumwondoa uhalali wa maelezo yake. atakwenda vipi mbele ya sheria ikiwa wananchi wenyewe hamridhiki na ushahidi huu..
Jamani someni maandishi kwanza kisha jukumu la kumhukumu Rostam mnalo nyie wananchi na sii Seleli. Maadam kisha wakilisha kazi yake ni jukumu lenu kuipokea na kuifanyia kazi, leo mnataka tena yeye ndiye akafungue mashtaka! mfanyiwe kila kitu....
Ama kwelim maneno ya MkamaP naanza kuyaamini kwamba ni kazi kubwa sana kuongoza Umma wa Kitanzania.

- Bob saafi sana hili taifa tuna matatizo makubwa sana na kama Mungu alivyosema watu wangu waneteketea kwa kukosa knowledge, unajua ni recently tu ndio nimegundua kuwa kusoma sana haina maana yoyote mtu anaweza kusoma na bado akawa mjinga tu yaani nimegundua hivi karibuni tu!

- Na tatzio letu kubwa Tanzania ni umasikini ndio unatusumbua sana, wengine tumeuruhusu kuingia mpaka kwenye ubongo wetu, hatuwezi ku-think right pamoja ni mi-elimu mikubwa mikubwa lakini ni bure ya ghali!

Respect.



FMEs!
 
Mkuu vipi bwana mbona waenda personal.....halafu unataka kuwa mbunge kweli? Nadhani anzia kwanza udiwani! Mzee hunifahamu kabisa acha kunihusisha na mtu mwingine......sitaki andika habari za dada yako SUA na wewe! Ila ukiendelea na huu ujinga wakati watu wanakata issue za taifa hapa sina simile nitamwaga upupu vile vile

Na wewe mpumbavu mkubwa wa JF unaona wenzako wanaenda personal wakati wewe ndio umekuwa ukimtukana Mtanzania kila anapoandika hapa JF? Search posts zako na utaona zaidi ya theluthi mbili ni matusi yako dhidi ya Mwakalinga.

Eti nini? Wewe ni mwalimu chuo kikuu? labda kama Mtanzania kakosea, kama mtu mwenye mawazo ya chuki kama yako ni mwalimu wa chuo kikuu, basi na mimi inabidi niombe hiyo kazi.

Mtanzania, achana na mjinga huyu, tuachie sisi tuponde bichwa lake. Hana lolote zaidi ya kuona wivu. Mitanzaania mingine inataka kila jambo ifanye yenyewe, ikishindwa inaanza majungu. Mara fisadi, mara kagawa laptop na upuzi mwingine ambao hata muuza mitumba wa kariakoo hatakiwi kuurudia.

Umeshatoa maelezo ya kutosha juu ya siasa za Kyela, wanaoelewa, wameshaelewa. Mjinga Masanilo hayuko hapa kuelewa, yuko kuchafua wengine ili na wenyewe wasifanikiwe kama yeye. Chaki imemchosha na amebaki kujaza wivu. Mwache mpaka apasuke mwaka huu.
 
RA alikataa kutokea kwa hiari yake; kamati ya bunge ilikuwa na nguvu na uwezo wa kutumia njia zingine halali kisheria kuwalazimishiwa watuhumiwa kuhojiwa.

Kama wahusika wakubwa kwenye hili ni Lowassa na RA, ninashangaa kweli hii kamati ilishindwa kutumia nguvu zake kisheria kuwahoji hawa watu. Maneno ambayo wangeyasema mbele ya hicho kikao, yangelikuwa na nguvu na ingelikuwa hata rahisi kuwachukulia hatua za kisheria.

Ahsante sana kwa mchago wako murua. Naomba utufahamishe kamati ya Bunge ilikuwa na nguvu zipi na ilipewa na nani nguvu hizo ili kuhakikisha watuhumiwa wote wanahojiwa? Shukrani.
 
Na wewe mpumbavu mkubwa wa JF unaona wenzako wanaenda personal wakati wewe ndio umekuwa ukimtukana Mtanzania kila anapoandika hapa JF? Search posts zako na utaona zaidi ya theluthi mbili ni matusi yako dhidi ya Mwakalinga.

Mhhhh! Niliwahi kusoma hapa siku za nyuma kwamba Mtanzania ndiyo Mwakalinga lakini sikuwa na uhakika sasa nimepata uhakika. JF watu mnatisha! Duh!
 
- With all due respect, hili sio tatizo la wapiganaji au anybody huko bungeni wao wametimiza walichotakiwa kukifanya na facts zimetolewa hizo juu, sasa ni tatizo letu wanachi kuwashinikiza Rais na Waziri Mkuu kuchukua hatua kutokana na mapendekezo ya bunge ambalo liliridhia kazi ya hii kamati.

- Haya maelezo yote aliyoyatoa Seleli yamo kwenye ripoti yao ya kamati, unless hukuiona tusidanganyane hapa!

Respect.


FMEs!

Mkuu Wananchi hawaendi Bungeni, Bunge ndio wananchi wenyewe so wananchi wajibu wao wamekabidhiwa Wabunge wautekeleze kwa niaba yao

Juzi Mwanakijiji alitoa somo zuri sana hapa kuhusu Mihimili mitatu ya Dola, unless wabunge wetu hawajui power waliyo nayo, Bunge lina uwezo wa Kuishinikiza Serikali pale ambapo linaona Matakwa ya Wananchi hayatekelezwi

Sasa sijui unataka Wananchi wafanye sasa mkuu
 
Na wewe mpumbavu mkubwa wa JF unaona wenzako wanaenda personal wakati wewe ndio umekuwa ukimtukana Mtanzania kila anapoandika hapa JF? Search posts zako na utaona zaidi ya theluthi mbili ni matusi yako dhidi ya Mwakalinga.

Eti nini? Wewe ni mwalimu chuo kikuu? labda kama Mtanzania kakosea, kama mtu mwenye mawazo ya chuki kama yako ni mwalimu wa chuo kikuu, basi na mimi inabidi niombe hiyo kazi.

Mtanzania, achana na mjinga huyu, tuachie sisi tuponde bichwa lake. Hana lolote zaidi ya kuona wivu. Mitanzaania mingine inataka kila jambo ifanye yenyewe, ikishindwa inaanza majungu. Mara fisadi, mara kagawa laptop na upuzi mwingine ambao hata muuza mitumba wa kariakoo hatakiwi kuurudia.

Umeshatoa maelezo ya kutosha juu ya siasa za Kyela, wanaoelewa,wameshaelewa. Mjinga Masanilo hayuko hapa kuelewa, yuko kuchafua wengine ili na wenyewe wasifanikiwe kama yeye. Chaki imemchosha na amebaki kujaza wivu. Mwache mpaka apasuke mwaka huu.


Great thinker mwingine wa JF!
 
Mkuu Wananchi hawaendi Bungeni, Bunge ndio wananchi wenyewe so wananchi wajibu wao wamekabidhiwa Wabunge wautekeleze kwa niaba yao

Juzi Mwanakijiji alitoa somo zuri sana hapa kuhusu Mihimili mitatu ya Dola, unless wabunge wetu hawajui power waliyo nayo, Bunge lina uwezo wa Kuishinikiza Serikali pale ambapo linaona Matakwa ya Wananchi hayatekelezwi

Sasa sijui unataka Wananchi wafanye sasa mkuu

- Bunge limetimiza kazi yake, sasa wewe utueleze unataka nini hasa? The only thing wananchi we can do hapa ni kuandamana kuwashinikiza Rais na Waziri Mkuu kuchukua hatua kufuatilia mapendekezo ya bunge, ikibidi kuwazomea na kuwarushia mawe unakumbuka last time haya yalipofanyika Mramba na Yona wakapelekwa Rumande kutunyamazisha!

- Sasa wewe utueleze unataka nini maana bunge limemaliza kazi yake tayari on the ishu?


FMEs!
 
Kuandamana?? nani afanye huo ujinga wa kupigwa mabomu kwa kumsemesha kiziwi JK asiyeona hata nchi inakokwenda yeye anaona sawa tu
 
Back
Top Bottom