Sungurampole
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 984
- 205
Kuna taarifa kuwa wanafunzi wanaosoma katika shule ya sekondari ya Mgololo iliyoko Wilaya ya Mufindi, Iringa hawajui kusoma wala kuandika
Mkuu wa shule amemwandikia barua Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kumlalamikia kupelekewa wanafunzi ambao hawajui kujua kusoma wala kuandika na akapendekeza wapelekwe shule ya msingi. Habari hizi zimeeleza kuwa watoto hawa 10 wako kati ya kidato cha pili na cha nne. Maelezo yanasema kuwa jitihada za kuwa rudisha shule ya msingi limekuwa kuwa gumu kwani sera ya elimu hairuhusu mwanafunzi aliyehitimu shule ya na 'kufaulu' kurudi tena shule ya msingi. Mmoja wa watoto hao aliyepata alama 166 kati ya 250 katika mtihani wake wa darasa la saba hakuweza kusoma sentensi zifuatazo- "Bibi anakula chakula" au "Mama analima bustani" . (Habarileo 18.9. 2011)
Naomba tutafakari hili kwa kina. Hivi hapa shida ni nini?
Mkuu wa shule amemwandikia barua Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kumlalamikia kupelekewa wanafunzi ambao hawajui kujua kusoma wala kuandika na akapendekeza wapelekwe shule ya msingi. Habari hizi zimeeleza kuwa watoto hawa 10 wako kati ya kidato cha pili na cha nne. Maelezo yanasema kuwa jitihada za kuwa rudisha shule ya msingi limekuwa kuwa gumu kwani sera ya elimu hairuhusu mwanafunzi aliyehitimu shule ya na 'kufaulu' kurudi tena shule ya msingi. Mmoja wa watoto hao aliyepata alama 166 kati ya 250 katika mtihani wake wa darasa la saba hakuweza kusoma sentensi zifuatazo- "Bibi anakula chakula" au "Mama analima bustani" . (Habarileo 18.9. 2011)
Naomba tutafakari hili kwa kina. Hivi hapa shida ni nini?