MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
Gasper Andrew ,Singida MBUNGE wa Jimbo la Singida mjini, Mohamed Gullam Dewji, ameahidi kutumia zaidi ya Sh50 milioni kugharamia uwekaji wa mtandao wa intaneti (Internet) kwa shule zote 17 za sekondari za Serikali, jimboni humo ili kusaidia wanafunzi na walimu kujisomea zaidi. Mpango huo wa aina yake,utaanzia na shule tano ambazo tayari zina umeme, shule hizo ambazo ni pamoja na Mitunduruni, Mwenge, Dk Salmini Amour, Chief Senge,na Kindai,kila moja itapewa kompyuta 20 ili kufungua darasa maalumu kwa ajili ya wanafunzi na walimu kujifunzia. Dewji maarufu kwa jina la MO alitoa ahadi hiyo wakati akizungumza kwenye kikao cha pamoja na walimu wa shule za sekondari za Manispaa ya Singida uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kanisa la Katoliki Misuna mjini hapa. Alisema amefikia uamuzi huo kutokana na ukweli kwamba kupitia mtandao wa intaneti wanafunzi au mtu ye yote utamsaidia kujifunza mambo mengi.Aidha, alisema uamuzi huo umesukumwa pia na shule nyingi za sekondari za Serikali kukabiliwa na matatizo mengi yakiwamo vitabu vya kujisomea/kujifunzia. Kutokana na upungufu/uhaba wa vitabu vya kujisomea na mengine mengi, mimi mbunge wenu, nimeleta wataalamu wa intaneti kutoka Marekani ili watufungulie mtambo utakaowezesha shule zote za sekondari za Serikali zilizo na umeme, ziweze kujiunga na mtandao wa intaneti. Dewji alisema hapo ndipo walimu na wanafunzi wanaweza kupata mambo mengi yatakayowasaidia kwenye masomo yao . Source Mwananchi Gazeti |