Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,758
Science is a systematic enterprise that builds and organizes knowledge in the form of testable explanations and predictions about the universe.
Aristotle: Science refers to the body of reliable knowledge itself of the type that can be logically and rationally explained.
Technology is the making, modification, usage, and knowledge of tools, machines, techniques, crafts, systems, methods of organization, in order to solve a problem, improve a preexisting solution to a problem, achieve a goal or perform a specific function.
Mind is the faculty or complex of faculties that enables conscious thinking, reasoning, perception, and judgement.
Nimeandika kwa lugha hiyo kutokana na ukweli kuwa maana ya maneno hayo yanapatikana kwa ufasaha kwenye hiyo lugha husika.
Kwangu mimi, teknolojia ni sehemu ya sayansi. Sayansi ni ufumbuzi na uvumbuzi wakati teknolojia ni njia ya kufikia ufumbuzi/uvumbuzi.
Sijui kwa ufasaha maana halisi ya neno 'mind' kwa kiswahili. Labda tuseme ni 'fikra'. Fikra ya mwanadamu inapokuwa na ujinga (ujinga si tusi bali ni hali ya kutojua kitu-ignorance), ni rahisi kushambuliwa na madhara mbalimbali ambayo yatayadhuru maisha yake kwa namna ambayo kwa asilimia kubwa ni hasi. Fikra sahihi hutoa uamuzi/hukumu sahihi. Hukumu sahihi huja kutokana na ushahidi uliothibitishwa kisayansi.
Fikra na imani (belief) vinaendana. Fikra huitangulia imani. Fikra ikipotoka kwa kukosa uamuzi sahihi, huathiri maamuzi juu ya namna ya kuamini jambo fulani.
Mfumo wa maisha katika jamii fulani huathiriwa na kiasi cha sayansi na teknolojia iliyopo. Jamii yenye uelewa wa kutosha juu ya mazingira waliyomo haina matatizo yaliyokosa angalau ufumbuzi kutokana na tatizo lililo mbele yao. Kuwa na sayansi na teknolojia pekee haitoshi. Ni kiasi gani jamii imeerevuka kutokana na hizo variable mbili?
Mathalani ni kwa kiwango gani tunajua kuwa maji na chakula haviendani kwa wakati mmoja? Huo ni mfano mdogo sana. Tunawezaje kutumia sayansi na teknolojia kuwaelewesha jamii za wakeketaji kuwa wanachofanya si sahihi? Kuwaambia tu kuwa kitendo hicho ni kinyume na haki za binadamu, kiafya si nzuri, ni kosa la jinai inatosha? Ni kwa vipi utamweleza kisayansi kuwa kiafya si nzuri na akuelewe? Ni jambo ambalo limeshathiri 'Mind' yake. Kuwa mwanamke asiyekeketwa hawezi kuolewa. Kwamba mwanamke asiyekeketwa hana thamani wakati sio?
Inatosha kumwambia mtu kuwa macho mekundu ni dalili ya kuathirika na moshi? Imefikaje hapo hadi kuamini kuwa ajuza mwenye macho mekundu ni mchawi? Utatumiaje sayansi na teknolijia kumwelewesha huyu mtu kuwa fikra zake si sahihi hivyo hukumu anayotoa si sahihi pia? Inakuwaje haya yanaendelea kutokea wakati nguvu ya dola inatumika na elimu inatolewa? Hiyo ni mifano michache sana!
Hii ni dalili tosha kuwa jamii zetu hazijafikiwa vya kutosha na sayansi na teknolojia, hivyo fikra zetu zinatoa hukumu zisizo sahihi kwa mambo mengi sana ambayo tunakutana nayo katika maisha yetu ya kila siku. Nawasilisha.
Aristotle: Science refers to the body of reliable knowledge itself of the type that can be logically and rationally explained.
Technology is the making, modification, usage, and knowledge of tools, machines, techniques, crafts, systems, methods of organization, in order to solve a problem, improve a preexisting solution to a problem, achieve a goal or perform a specific function.
Mind is the faculty or complex of faculties that enables conscious thinking, reasoning, perception, and judgement.
Nimeandika kwa lugha hiyo kutokana na ukweli kuwa maana ya maneno hayo yanapatikana kwa ufasaha kwenye hiyo lugha husika.
Kwangu mimi, teknolojia ni sehemu ya sayansi. Sayansi ni ufumbuzi na uvumbuzi wakati teknolojia ni njia ya kufikia ufumbuzi/uvumbuzi.
Sijui kwa ufasaha maana halisi ya neno 'mind' kwa kiswahili. Labda tuseme ni 'fikra'. Fikra ya mwanadamu inapokuwa na ujinga (ujinga si tusi bali ni hali ya kutojua kitu-ignorance), ni rahisi kushambuliwa na madhara mbalimbali ambayo yatayadhuru maisha yake kwa namna ambayo kwa asilimia kubwa ni hasi. Fikra sahihi hutoa uamuzi/hukumu sahihi. Hukumu sahihi huja kutokana na ushahidi uliothibitishwa kisayansi.
Fikra na imani (belief) vinaendana. Fikra huitangulia imani. Fikra ikipotoka kwa kukosa uamuzi sahihi, huathiri maamuzi juu ya namna ya kuamini jambo fulani.
Mfumo wa maisha katika jamii fulani huathiriwa na kiasi cha sayansi na teknolojia iliyopo. Jamii yenye uelewa wa kutosha juu ya mazingira waliyomo haina matatizo yaliyokosa angalau ufumbuzi kutokana na tatizo lililo mbele yao. Kuwa na sayansi na teknolojia pekee haitoshi. Ni kiasi gani jamii imeerevuka kutokana na hizo variable mbili?
Mathalani ni kwa kiwango gani tunajua kuwa maji na chakula haviendani kwa wakati mmoja? Huo ni mfano mdogo sana. Tunawezaje kutumia sayansi na teknolojia kuwaelewesha jamii za wakeketaji kuwa wanachofanya si sahihi? Kuwaambia tu kuwa kitendo hicho ni kinyume na haki za binadamu, kiafya si nzuri, ni kosa la jinai inatosha? Ni kwa vipi utamweleza kisayansi kuwa kiafya si nzuri na akuelewe? Ni jambo ambalo limeshathiri 'Mind' yake. Kuwa mwanamke asiyekeketwa hawezi kuolewa. Kwamba mwanamke asiyekeketwa hana thamani wakati sio?
Inatosha kumwambia mtu kuwa macho mekundu ni dalili ya kuathirika na moshi? Imefikaje hapo hadi kuamini kuwa ajuza mwenye macho mekundu ni mchawi? Utatumiaje sayansi na teknolijia kumwelewesha huyu mtu kuwa fikra zake si sahihi hivyo hukumu anayotoa si sahihi pia? Inakuwaje haya yanaendelea kutokea wakati nguvu ya dola inatumika na elimu inatolewa? Hiyo ni mifano michache sana!
Hii ni dalili tosha kuwa jamii zetu hazijafikiwa vya kutosha na sayansi na teknolojia, hivyo fikra zetu zinatoa hukumu zisizo sahihi kwa mambo mengi sana ambayo tunakutana nayo katika maisha yetu ya kila siku. Nawasilisha.