ScanLink likitoka Mwanza kuja Dar lapinduka Gairo - Morogoro

Poleni majeruhi wote
Na MUNGU alaze roho za marehemu mahali pema peponi. Amen
 
aaaaaaarrrhg jamani loh imefikia hatua nikipanda magari siku hizi huwa nasali kabisa sala ya toba manake najua madereva wetu siku hizi ni mawakala wa israel. na ukishuka salama unashukuru Mungu, mbona tunaandamwa hivi, nakosa la kusema kwa kweli. RIP marehem wote
 
Basi limetoka Dar kwenda Mwanza na sio Mwanza kuja Dar.
Nimepewa taarifa na jamaa yangu ambaye yuko ktk basi aneniambia basi hilo walikuwa wanaongozana tangu Ubungo na hapo Gumira kuna ajali 2 hiyo ya Basi ambalo hadi sasa wmeshaopowa maiti 8 na zoezi linaendelea. na mbele kidogo kuna ajali nyingine ya basi ya abiria na lori la mafuta ambapo kwenye hiyo ajali pili ya lori na basi kuna majeruhi tu hakuna watu waliopoteza maisha.

Jamani hii inasikitisha sana, hivi ni nani huwa anatenga maiti na majeruhi? wengine wanacheleweshwa kwenda hosp kwa kudhaniwa wamekufa kumbe majeruhi. Mambo ya uokozi yanahitaji umakini sana.
 
Jamani hii inasikitisha sana, hivi ni nani huwa anatenga maiti na majeruhi? wengine wanacheleweshwa kwenda hosp kwa kudhaniwa wamekufa kumbe majeruhi. Mambo ya uokozi yanahitaji umakini sana.
Ni kazi nzito sana hiyo ndugu yangu, wee acha tu, hiyo kuchanganya majeruhi na maiti ni kutokana na ugumu wa kazi yenyewe
 
POLENI WAFIWA,sasa haya mambo had ini?tusisafir au?well pia mwendo wa haya magari ya abria i wa kasi sana ukilinganisha na infrastructure.majuzi hapa nipo naendesha kuelekea Arusha katika gari binafsi,nipo speed 140 kabla hujafika segera,ilinipta basi ya abria hadi ikatoka nje ya barabara,nakuymba kam thice then ikarudi barabarani.korogwe nikamfuata yule driver why aende that speed na abiria 70?akaniambia niulize waliopanga muda wa kupita vituoni,gari yenyewe tyre threads zishaanza kufifia,kuna cracks zinaonekana,derva ni wale type wasiojali,anajisifia na kusema wewe ndo ulikuwa na ile Nisan nyekundu?bahati yako ningekupanda kwa nyua shukuru munu wako.sasa hii tpe ya drivers ndo tunao wengi sana,je tufanyeje?abiria nao wanalazimisha kuwahishwa no sooner wanamwagwa!! hatari nchi hii au lada ndo ecology tunapungua kwa AIDS,Ajali,Malaria etc
 
nini kinachoendelea kuhusu hizi ajali kila siku? ni barabara mbovu au ni madereva wazembe? inasikitisha sana kuona watu wanapoteza maisha kila siku kutokana na ajali za mabasi.najua kwamba ajali ni kazi ya mungu lakini nadhani kuna uwezekano wa kuzipunguza kama watu husika wakiwa makini.nawatakia pole wafiwa wote na majeruhi nawaombe mpone haraka sana.
mkuu wa emirates hapo barabara mbovu ndio chanzo kikubwa cha ajali zimazoendelea kutokea hapa nchini
 
aaaaaaarrrhg jamani loh imefikia hatua nikipanda magari siku hizi huwa nasali kabisa sala ya toba manake najua madereva wetu siku hizi ni mawakala wa israel. na ukishuka salama unashukuru Mungu, mbona tunaandamwa hivi, nakosa la kusema kwa kweli. RIP marehem wote

Hii kauli imeniacha hoi,sasa hivi wanajijua kweli kama wao wanatumika kama mawakala wa Israel?
 
kufika mapema tunapo kwenda tunapenda..ila gharama yake muda mwingine ni kubwa...
 
kufika mapema tunapo kwenda tunapenda..ila gharama yake muda mwingine gharama yake ni kubwa...tuwe wakali kwa madereva wanaoendesha mwendo kasi hatarishi,....
 
Tajiri Mtu Mzima,

Mabasi yanayotoka Mwanza au Ziwa Magharibi uwa yanapambazua either Dodoma au Morogoro. Kwa hiyo yawezekena kabisa SkyLink ili-LALA Dodoma na kudamka kuja Dar es Salaam na nikitizama muda yawezekana ilikuwa imefika Gairo. There are chances kuwa Bus lilikuwa lina "Mechanical fault" na ndio maana liko nyuma sana ya "ETA".

Nakubaliana nawe. Watu wanaofanya biashara za mabasi njia ya kati(dar -Mwanza) wana tendency ya kuyalazimisha mabasi yao kutembea hata yakiwa na mechanical faults. Uchunguzi wa kina ufanywe ktk hili. Nimewahi safiri na mabasi haya,ubabaishaji na ubishi mtupu!
 
Nadhani namuunga mkono JK kuwa sheria zetu zifanyiwe marekebisho na kuweka adhabu kali sana.


Tatizo hapa sio sheria, barabara wala nini, kiini cha haya yote ni rushwa kuanzia TBS na Police ikichagizwa na uzembe wa madereva.
 
kufika mapema tunapo kwenda tunapenda..ila gharama yake muda mwingine gharama yake ni kubwa...tuwe wakali kwa madereva wanaoendesha mwendo kasi hatarishi,....

Ni kweli,mara nyingi abiria wenyewe ndio tatizo.Hasa wafanyabiashara.Wanachangia sana dereva kwenda mwendo kasi sababu huwa wanamwambia aongeze mwendo,akipunguza wanamtukana.Hii ipo hata kwenye daladala,dereva akikatiza njia zisizo rasmi abiria wanafurahia ili wawahi kufika.Imefika kipindi hatua za kisheria zichukuliwe hata kwa abiria na sio madereva pekee.
 
MOja ya sababu ni matajiri kutaka faida kubwa na kupunguza gharama za uendeshaji, kwani badala ya kununua tairi nzuri zenye kiwango wao hukimbilia tairi substandard za bei ya chini ambazo ndizo zinapasuka mara kwa mara barabarani, pia huwa hafanyi service kable za safari kungalia usalama wa gari, wao gari ikipiga start tu wanaona ni nzima na kupeleka safari. Chanzo kingine ni hawa TBS kuruhusu tairi substandard kuingia nchini na kutumika kwenye vyombo vya usafiri.
 
Katika kipindi hicho JK ametoa wito kwamba wanaosababisha hizi ajali wafungiwe maisha kuendesha magari, na si hivyo tu na hata adhabu ziwe kali mpaka kifungo cha maisha maana kwa kweli wote tuna kuwa ni ni majeruhi watarajiwa...

Nadhani namuunga mkono JK kuwa sheria zetu zifanyiwe marekebisho na kuweka adhabu kali sana.

Mimi siungani na jk na wewe mchaga tena nawapinga sana hadharani. Ifike mahali tuyaangalie mambo kwa upana zaidi. Si kweli na narudia si kweli kwamba ni madereva wazembe pekee ndio wanaosababisha ajali. Issue ya ajali ni kubwa kuanzia kwa traffic na serikali yenyewe. I'm sure traffic wakifanya kazi yao vile inavyotakiwa ajali zitapungua kwa kiwango kikubwa.Serikali nayo ikiboresha miundimbinu vifo vya ajali vitapungua tu. Ni kweli kwamba madereva wanachangia katika hili lakini tukitaka kuwa fair hatupaswi kuishia kwa madereva pekee.
 
Tatizo hapa sio sheria, barabara wala nini, kiini cha haya yote ni rushwa kuanzia TBS na Police ikichagizwa na uzembe wa madereva.

Mkuu, nakubaliana na wewe 100%. Rushwa ni tatizo kubwa katika mchakato mzima wa kumpatia dereva leseni hadi anapoendesha barabarani.

Lakini rushwa itaisha vipi ikiwa polisi anapokea Tsh 200,000 kwa mwezi?? Jamani tunahitaji re-formation ya hali ya juu ktk jeshi la polisi.
Kazi ipo!!
 
I think hawa madereva itabidi wawe wanapewa mvua 30 kila wanaposababisha ajali yenye vifo. Na wenye magari wapewe onyo kali.

These buses kills more people kuliko aids hapo TZ. lol

That will bring discipline kwa madereva na wenye magari.
 
siye abiria nao tunatofautiana, nilipanda basi la scandnavia kwenda mombasa, yani dereva alikuwa anatembea vizuri anafuata sheria, kwenye mashimo anapunguza mwendo, weeee, wengine wakalipuka siye hatusindikizi harusi sijui tunataka kurudi pia kama huwezi pisha, yani hili neno la kufa ni ahadi siyo zuri sana, yani kuna watu wanaamini eti kama hajaandikiwa kufa haufi hata ukianguka toka juu kabisa katika jengo la kitega uchumi.

R.I.P. mliotangulia
 
Ajali zimezidi kwa kuwa sheria zilizopo hazisimamiwi na kisa ni rushwa iliyokithiri. Weka adhabu kubwa sana upandishe dau la rushwa. Hiyo ni neema tu kwa askari wa barabarani. Hivi hatutakaa tupate Sokoine mwingine wa kupambana na rushwa? Bila kuondoa rushwa sheria hazina maana
 
Back
Top Bottom