Sauti hizi hospitali ya taifa muhimbili haziwezi tafutiwa ufumbuzi?

Mnyamahodzo

JF-Expert Member
May 23, 2008
1,932
985
Kama ulikwisha wahi kwenda katika Hospitali yetu, kubwa kuliko zote hapa nchini Tanzania,yaani Hospitali ya Taifa Muhimbili muda wa saa saba mchana au saa kumi kasoro jioni utakuwa umekutana na hili nalolitaka kulisema.

Ndiyo! Ziko sabababu nyingi zinzoweza mfanya mtu akaenda Muhimbili, yawezekana ugonjwa au unasindikiza mgonjwa, kuchukuliwa kipimo,kumwona mgonjwa ama kuweka au kuchukua maiti.

Karibu na chumba cha maiti pana nyumba mbili kubwa za ibada, yaani msikiti na kanisa. sasa ukiwepo Muhimbili masaa hayo niliyoyataja wakati ibada inaanza msikitini, inapigwa adhana. Sauti yake yakuzwa na kipaza sauti. Inatupwa mbali sana.

Sasa tatizo hapa ni hili, nikijua ile ni hospitali yenye wagonjwa wanaolazwa na wasiolazwa na nikijua kuwa hata magari hayaruhusiwi kupiga honi ndani ya eneo la hospitali;iweje sauti hizi katika kipaza sauti ziwe zinaendelea kuwa kero kwa wagonjwa hasa wa zile wodi za wazazi na watoto(maana zipo umbali wa chini ya mita 100 toka msikitini)?

Hivi adhana ikipigwa bila ya kutumia kipaza sauti, ibada inakuwa batli? Kama hilo ni kweli. Je! Maeneo ambako hakuna umeme wala kipaza sauti ibada zao ni batili? Je! Ibada walizofanya wakina Mtume Mohamad (S.A.W) bila kutumia kipaza sauti zilikuwa batili?

Kama ibada inaendelea kuwa halali hata kama adhana itapigwa bila kipaza sauti,kwanini basi tuendeleee kuwasumbua wagonjwa? Hivi inamaana hata wanaokwenda kuswali hapo miaka yote hiyo, wameshindwa kuliona au wanaifurahia hiyo hali?

Kama hujawahi kuwa na mgonjwa Muhimbili katika masaa hayo huwezi jua ni kwa kiasi gani sauti hizo ni karaha;hili linawahusu watu wote bila kujali dini wala rangi yake.

Wana-jamvi hebu tulijadili na watu wa Muhimbili wachukue maoni yetu.
 
Kama ulikwisha wahi kwenda katika Hospitali yetu, kubwa kuliko zote hapa nchini Tanzania,yaani Hospitali ya Taifa Muhimbili muda wa saa saba mchana au saa kumi kasoro jioni utakuwa umekutana na hili nalolitaka kulisema.

Ndiyo! Ziko sabababu nyingi zinzoweza mfanya mtu akaenda Muhimbili, yawezekana ugonjwa au unasindikiza mgonjwa, kuchukuliwa kipimo,kumwona mgonjwa ama kuweka au kuchukua maiti.

Karibu na chumba cha maiti pana nyumba mbili kubwa za ibada, yaani msikiti na kanisa. sasa ukiwepo Muhimbili masaa hayo niliyoyataja wakati ibada inaanza msikitini, inapigwa adhana. Sauti yake yakuzwa na kipaza sauti. Inatupwa mbali sana.

Sasa tatizo hapa ni hili, nikijua ile ni hospitali yenye wagonjwa wanaolazwa na wasiolazwa na nikijua kuwa hata magari hayaruhusiwi kupiga honi ndani ya eneo la hospitali;iweje sauti hizi katika kipaza sauti ziwe zinaendelea kuwa kero kwa wagonjwa hasa wa zile wodi za wazazi na watoto(maana zipo umbali wa chini ya mita 100 toka msikitini)?

Hivi adhana ikipigwa bila ya kutumia kipaza sauti, ibada inakuwa batli? Kama hilo ni kweli. Je! Maeneo ambako hakuna umeme wala kipaza sauti ibada zao ni batili? Je! Ibada walizofanya wakina Mtume Mohamad (S.A.W) bila kutumia kipaza sauti zilikuwa batili?

Kama ibada inaendelea kuwa halali hata kama adhana itapigwa bila kipaza sauti,kwanini basi tuendeleee kuwasumbua wagonjwa? Hivi inamaana hata wanaokwenda kuswali hapo miaka yote hiyo, wameshindwa kuliona au wanaifurahia hiyo hali?

Kama hujawahi kuwa na mgonjwa Muhimbili katika masaa hayo huwezi jua ni kwa kiasi gani sauti hizo ni karaha;hili linawahusu watu wote bila kujali dini wala rangi yake.

Wana-jamvi hebu tulijadili na watu wa Muhimbili wachukue maoni yetu.

...mnh, huenda wanawakumbushia wagonjwa wazidi kuwa karibu na muumba wao, si umesema ni karibu na chumba cha maiti?

Kwani lile kanisa pale nao hawagongi kengele?
 
hii kali adhana leo hii inakuwa kelele, sasa na sie wa uswahilini tunaoamshwa usiku bila ridhaa yetu na hizo adhana tusemeje au tuandamane
 
hii kali adhana leo hii inakuwa kelele, sasa na sie wa uswahilini tunaoamshwa usiku bila ridhaa yetu na hizo adhana tusemeje au tuandamane

Mkuu wewe si uko home. Hapa inasemewa wagonjwa ambao hawapo mbali na maiti zilizopo mochwari. Inawezekana sauti zinazotoka kanisani/msikitini zisiwe kelele, kwa waumini. Lakini kuna wagonjwa ambao si wakristo au waislam, kwao hizo ni kelele. Kwangu mimi kwa mfano, adhana ni kelele ila kengele si kelele. Ukweli ni kuwa, vyote viwili (kengele na adhana) ni kelele kwa wagonjwa. Vipigwe marufuku hospitalini.
 
...mnh, huenda wanawakumbushia wagonjwa wazidi kuwa karibu na muumba wao, si umesema ni karibu na chumba cha maiti?

Kwani lile kanisa pale nao hawagongi kengele?

Mkuu, ukweli ni kuwa wale wakiristu wamekuwa wastaarabu,hapana kengele wala alama ya kengele(maana waweza sema zamani ilikuwapo).

Wasio wakiristu wala waislamu sijui wanafanyia wapi ibada zao. Kwanza, sijawahi liona jengo lao lakini pili, kama lipo inamaanisha wanafanya bila ya kutoa sauti zinazoweza wasumbua wagonjwa.
 
Mkuu angalia usije pondwa mawe.

Mkuu, huu utakuwa wendawazimu unaozidi kichaa kinachotokana na dini. Yaani, kusema jambo jema na kufanya marejeo ya ilivyokuwa huko nyuma lakini nikifikiria mustakabali wa afya za watu walioletwa eneo maalumu kwa matibabu ndiyo waje kunipiga mawe kama kafiri(mpinga maneno ya Mwenyezi Mungu).

Jamani, tusiseme kwasababu tu wazima tunakula, tunakunywa na kupata usingizi mzuri. Hebu jaribuni kujiweka katika nafasi ya ugonjwa, nakwambia si redio tu utakayoichukia bali hata kengele.
 
Kusema ukweli kupiga kelele ya aina yoyote ile kwenye hospital yoyote ile duniani huwa ahiruhusiwi, wagonjwa wanatakiwa kukaa sehemu yenye utulivu ili waweze kupumzika sasa ukipiga kelele tena inakuwa tabu kidogo wengine wanamatatizo yasiyohitaji kelele za aina yoyote hapo tunawasaidia aje hawa wagonjwa??

Ningependa kuwashauri hawa ndugu zetu kwenye huo msikiti mdogo waendeshe ibada zao bila ya kupiga hiyo adhana mathalani inajulikana pale ni hospital hivyo kutoweka spika kwa ajili ya adhana haitoleta maana mbaya, wawafikiria wagonjwa kwanza hata mwenyezi mungu ataona ni haki pia kutoweka hizo spika
 
...Karibu na chumba cha maiti pana nyumba mbili kubwa za ibada, yaani msikiti na kanisa. sasa ukiwepo Muhimbili masaa hayo niliyoyataja wakati ibada inaanza msikitini, inapigwa adhana. Sauti yake yakuzwa na kipaza sauti. Inatupwa mbali sana.

Sasa tatizo hapa ni hili, nikijua ile ni hospitali yenye wagonjwa wanaolazwa na wasiolazwa na nikijua kuwa hata magari hayaruhusiwi kupiga honi ndani ya eneo la hospitali;iweje sauti hizi katika kipaza sauti ziwe zinaendelea kuwa kero kwa wagonjwa hasa wa zile wodi za wazazi na watoto(maana zipo umbali wa chini ya mita 100 toka msikitini)?

Wana-jamvi hebu tulijadili na watu wa Muhimbili wachukue maoni yetu.
Aslm'Alykm...!
Mnyamahodzo, swala lako ni zuri sana ila wakati mwingine sisi raiya huwa hatuangalii haki zetu za msingi na huwa tunapenda kulalamika kabla hatujachuwa hatua zinazopaswa kwanza.

Wewe ukiwa ni raiya mwenye mgonjwa au Mwenye kuelewa haki wagonjwa kule Muhimbili au Hospitali yoyote ile, na wakati wa Swala au kwa sababu yoyote ile utokea sauti yenye kusababisha kero au usumbufu kwa wagonjwa, wewe ulipaswa kuwaona au kuzungumza kwa uzuri uongozi wa huo Msikiti na kuwafahamisha hiyo kero wanayo ipata wagonjwa wanao fikiwa na hiyo Sauti ya Adhana.

Kulalamika tu kwenye tovuti utakuwa ujawasaidia bado ndugu zetu wanao pata usumbuvu na hiyo Sauti ya Adhana.

Waislam wanaweza kuadhini Bila kipaza sauti na Swala ika-sihi.

Basi fanya hima kuwasiliana na uongozi wa msikiti wa hapo Muhimbili, ni matumaini yangu kuwa watakusikiliza na kufanyia kazi malalamiko yako Insha'Allah.

X-Paster.
 
Aslm'Alykm...!
Mnyamahodzo, swala lako ni zuri sana ila wakati mwingine sisi raiya huwa hatuangalii haki zetu za msingi na huwa tunapenda kulalamika kabla hatujachuwa hatua zinazopaswa kwanza.

Wewe ukiwa ni raiya mwenye mgonjwa au Mwenye kuelewa haki wagonjwa kule Muhimbili au Hospitali yoyote ile, na wakati wa Swala au kwa sababu yoyote ile utokea sauti yenye kusababisha kero au usumbufu kwa wagonjwa, wewe ulipaswa kuwaona au kuzungumza kwa uzuri uongozi wa huo Msikiti na kuwafahamisha hiyo kero wanayo ipata wagonjwa wanao fikiwa na hiyo Sauti ya Adhana.

Kulalamika tu kwenye tovuti utakuwa ujawasaidia bado ndugu zetu wanao pata usumbuvu na hiyo Sauti ya Adhana.

Waislam wanaweza kuadhini Bila kipaza sauti na Swala ika-sihi.

Basi fanya hima kuwasiliana na uongozi wa msikiti wa hapo Muhimbili, ni matumaini yangu kuwa watakusikiliza na kufanyia kazi malalamiko yako Insha'Allah.

X-Paster.
Mkuu, you have nailed it!!!! umeeleza haswa jinsi ya jama'a inavyotakiwa kuwa. sijui nikushukurje.... nikiwa pale muhimbili nilikuwa na the same questions, lakini nikajua kwamba hata viongozi wa pale [au na penginepo kama hapo, wale wa LAKAIRO MNANISIKIA!], hawajui kinachotakiwa

nakupa tano mkuu
 
Last edited:
Karibu na chumba cha maiti pana nyumba mbili kubwa za ibada, yaani msikiti na kanisa. sasa ukiwepo Muhimbili masaa hayo niliyoyataja wakati ibada inaanza msikitini, inapigwa adhana. Sauti yake yakuzwa na kipaza sauti. Inatupwa mbali sana.

Sasa tatizo hapa ni hili, nikijua ile ni hospitali yenye wagonjwa wanaolazwa na wasiolazwa na nikijua kuwa hata magari hayaruhusiwi kupiga honi ndani ya eneo la hospitali;iweje sauti hizi katika kipaza sauti ziwe zinaendelea kuwa kero kwa wagonjwa hasa wa zile wodi za wazazi na watoto(maana zipo umbali wa chini ya mita 100 toka msikitini)?

Hivi adhana ikipigwa bila ya kutumia kipaza sauti, ibada inakuwa batli? Kama hilo ni kweli. Je! Maeneo ambako hakuna umeme wala kipaza sauti ibada zao ni batili? Je! Ibada walizofanya wakina Mtume Mohamad (S.A.W) bila kutumia kipaza sauti zilikuwa batili?

Kama ibada inaendelea kuwa halali hata kama adhana itapigwa bila kipaza sauti,kwanini basi tuendeleee kuwasumbua wagonjwa? Hivi inamaana hata wanaokwenda kuswali hapo miaka yote hiyo, wameshindwa kuliona au wanaifurahia hiyo hali?

Kama hujawahi kuwa na mgonjwa Muhimbili katika masaa hayo huwezi jua ni kwa kiasi gani sauti hizo ni karaha;hili linawahusu watu wote bila kujali dini wala rangi yake.

Wana-jamvi hebu tulijadili na watu wa Muhimbili wachukue maoni yetu.

Ndugu Mnyamahodzo shukran kwa kutuletea habari yenye kuwakera wagonjwa wa Hospitali ya Muhimbili.

Mimi kama Mwislamu nachangia maoni kama ifuatayo.

Kama Kweli sauti ya adhana inawakera wagonjwa wa pande yeyote ya Muhimbili basi lazima Viongozi wa hiyo Msikiti wa arifiwe kwa njia ya ustaarabu ili wafanye juhudi ya kuondoa kero ya kipaza sauti kwa wagonjwa hao wa karibu na mbali.

Napenda ifahamike sio lazima adhana isemwe kupitia kipaza sauti wala sio moja wapo ya nguzo za Ibada kuadhini kupitia kipaza sauti.Kwahiyo adhana ikiadhiniwa bila kipaza sauti Ibada haitakuwa batili wala kupata dosari yeyote.

Adhana inaweza kuadhiniwa bila kipaza sauti kama kweli inawakera wagonjwa au

kipaza sauti itumiwe kwa sauti ya chini isiyo weza kukera wagonjwa wa karibu na mbali ya Muhimbili.

Nataraji mpaka hapa maoni yangu niliyo changia italeta manufaa japo kidogo.

Wako katika Utu
Mpenzi wa Islam
 
Ndugu Mnyamahodzo shukran kwa kutuletea habari yenye kuwakera wagonjwa wa Hospitali ya Muhimbili.

Mimi kama Mwislamu nachangia maoni kama ifuatayo.

Kama Kweli sauti ya adhana inawakera wagonjwa wa pande yeyote ya Muhimbili basi lazima Viongozi wa hiyo Msikiti wa arifiwe kwa njia ya ustaarabu ili wafanye juhudi ya kuondoa kero ya kipaza sauti kwa wagonjwa hao wa karibu na mbali.

Napenda ifahamike sio lazima adhana isemwe kupitia kipaza sauti wala sio moja wapo ya nguzo za Ibada kuadhini kupitia kipaza sauti.Kwahiyo adhana ikiadhiniwa bila kipaza sauti Ibada haitakuwa batili wala kupata dosari yeyote.

Adhana inaweza kuadhiniwa bila kipaza sauti kama kweli inawakera wagonjwa au

kipaza sauti itumiwe kwa sauti ya chini isiyo weza kukera wagonjwa wa karibu na mbali ya Muhimbili.

Nataraji mpaka hapa maoni yangu niliyo changia italeta manufaa japo kidogo.

Wako katika Utu
Mpenzi wa Islam

Mkuu, umenipa faraja kubwa kwa uelewa na wisdom yako!!!! i wish wengi tungekuwa kama wewe
 
Ndugu Mnyamahodzo shukran kwa kutuletea habari yenye kuwakera wagonjwa wa Hospitali ya Muhimbili.

Mimi kama Mwislamu nachangia maoni kama ifuatayo.

Kama Kweli sauti ya adhana inawakera wagonjwa wa pande yeyote ya Muhimbili basi lazima Viongozi wa hiyo Msikiti wa arifiwe kwa njia ya ustaarabu ili wafanye juhudi ya kuondoa kero ya kipaza sauti kwa wagonjwa hao wa karibu na mbali.

Napenda ifahamike sio lazima adhana isemwe kupitia kipaza sauti wala sio moja wapo ya nguzo za Ibada kuadhini kupitia kipaza sauti.Kwahiyo adhana ikiadhiniwa bila kipaza sauti Ibada haitakuwa batili wala kupata dosari yeyote.

Adhana inaweza kuadhiniwa bila kipaza sauti kama kweli inawakera wagonjwa au

kipaza sauti itumiwe kwa sauti ya chini isiyo weza kukera wagonjwa wa karibu na mbali ya Muhimbili.

Nataraji mpaka hapa maoni yangu niliyo changia italeta manufaa japo kidogo.

Wako katika Utu
Mpenzi wa Islam

Wakuu Mpenzi wa Islam, X-PASTER na MTM mmenifurahisha sana kwa kulijadili swala hili kwa ustaarabu, hekima na uungwana wa hali ya juu. Muendelee hivyo hivyo katika mijadala mbali mbali hapa ukumbini. Mwenyezi Mungu awajalie wote katika kila mlitakalo~AMIN.
 
Aslm'Alykm...!
Mnyamahodzo, swala lako ni zuri sana ila wakati mwingine sisi raiya huwa hatuangalii haki zetu za msingi na huwa tunapenda kulalamika kabla hatujachuwa hatua zinazopaswa kwanza.

Wewe ukiwa ni raiya mwenye mgonjwa au Mwenye kuelewa haki wagonjwa kule Muhimbili au Hospitali yoyote ile, na wakati wa Swala au kwa sababu yoyote ile utokea sauti yenye kusababisha kero au usumbufu kwa wagonjwa, wewe ulipaswa kuwaona au kuzungumza kwa uzuri uongozi wa huo Msikiti na kuwafahamisha hiyo kero wanayo ipata wagonjwa wanao fikiwa na hiyo Sauti ya Adhana.

Kulalamika tu kwenye tovuti utakuwa ujawasaidia bado ndugu zetu wanao pata usumbuvu na hiyo Sauti ya Adhana.

Waislam wanaweza kuadhini Bila kipaza sauti na Swala ika-sihi.

Basi fanya hima kuwasiliana na uongozi wa msikiti wa hapo Muhimbili, ni matumaini yangu kuwa watakusikiliza na kufanyia kazi malalamiko yako Insha'Allah.

X-Paster.

Ndugu, ushauri wako ni mzuri ninauafiki. Lakini suala la kuweka mawazo/maoni ambayo ni KERO YANGU katika JF haimaanishi kuwa ni kulalamika hapa. Ukiwauliza web-moderators hivi imliiweka forum ya kero ilikupokea malalamiko ya watu tu, jibu, si kweli. Ndiyo sababu katika KERO YANGU wanapofafanua wanataja kero/malalamiko na dukuduku. Haimaanisha kila kero na dukuduku ni malalamiko.

Pamoja na hili hilo ninaamini wapo viongozi na wadau wa Muhimbili wanaosoma hapa, hivyo wao watakua miongoni mwa watu watakaolifikisha hili kama marudio kwa viongozi wenzao wa juu wanapojadili masuala ya maendeleo ya Hospitali na mahusiano na jamii ya watanzania.
 
Ndugu, ushauri wako ni mzuri ninauafiki. Lakini suala la kuweka mawazo/maoni ambayo ni KERO YANGU katika JF haimaanishi kuwa ni kulalamika hapa. Ukiwauliza web-moderators hivi imliiweka forum ya kero ilikupokea malalamiko ya watu tu, jibu, si kweli. Ndiyo sababu katika KERO YANGU wanapofafanua wanataja kero/malalamiko na dukuduku. Haimaanisha kila kero na dukuduku ni malalamiko.

Pamoja na hili hilo ninaamini wapo viongozi na wadau wa Muhimbili wanaosoma hapa, hivyo wao watakua miongoni mwa watu watakaolifikisha hili kama marudio kwa viongozi wenzao wa juu wanapojadili masuala ya maendeleo ya Hospitali na mahusiano na jamii ya watanzania.
Nashukuru mtu wangu kwa maelezo yako, ila mimi binafsi nilimaanisha kuwa Sisi wananchi tunapaswa kuwa majasiri zaidi na kuyashughurikia mambo yetu ya kijamii kwanza kabla ya kulalamika, ila nashukuru tena kwa maelezo yako, wakati mwingine inawezekaa sifahamu haswa nafasi yako kiasi ya kwamba inaweza kuwa si rahisi kwako kuwasiliana na uongozi husika, ili kutatua ilo jambo ulilo liweka hapa.

Nami ni matumaini yangu kuwa wale wahusika wanweza kulitatua hilo tatizo.

Kila la kheri mkuu, tupo pamoja.
 
Wakuu Mpenzi wa Islam, X-PASTER na MTM mmenifurahisha sana kwa kulijadili swala hili kwa ustaarabu, hekima na uungwana wa hali ya juu. Muendelee hivyo hivyo katika mijadala mbali mbali hapa ukumbini. Mwenyezi Mungu awajalie wote katika kila mlitakalo~AMIN.
Dua yako iwe makbur, kwa sote Insha'Allah

Jazakallah Khair

'May Allah grant you goodness'.
 
Kama ulikwisha wahi kwenda katika Hospitali yetu, kubwa kuliko zote hapa nchini Tanzania,yaani Hospitali ya Taifa Muhimbili muda wa saa saba mchana au saa kumi kasoro jioni utakuwa umekutana na hili nalolitaka kulisema.

Ndiyo! Ziko sabababu nyingi zinzoweza mfanya mtu akaenda Muhimbili, yawezekana ugonjwa au unasindikiza mgonjwa, kuchukuliwa kipimo,kumwona mgonjwa ama kuweka au kuchukua maiti.

Karibu na chumba cha maiti pana nyumba mbili kubwa za ibada, yaani msikiti na kanisa. sasa ukiwepo Muhimbili masaa hayo niliyoyataja wakati ibada inaanza msikitini, inapigwa adhana. Sauti yake yakuzwa na kipaza sauti. Inatupwa mbali sana.

Sasa tatizo hapa ni hili, nikijua ile ni hospitali yenye wagonjwa wanaolazwa na wasiolazwa na nikijua kuwa hata magari hayaruhusiwi kupiga honi ndani ya eneo la hospitali;iweje sauti hizi katika kipaza sauti ziwe zinaendelea kuwa kero kwa wagonjwa hasa wa zile wodi za wazazi na watoto(maana zipo umbali wa chini ya mita 100 toka msikitini)?

Hivi adhana ikipigwa bila ya kutumia kipaza sauti, ibada inakuwa batli? Kama hilo ni kweli. Je! Maeneo ambako hakuna umeme wala kipaza sauti ibada zao ni batili? Je! Ibada walizofanya wakina Mtume Mohamad (S.A.W) bila kutumia kipaza sauti zilikuwa batili?

Kama ibada inaendelea kuwa halali hata kama adhana itapigwa bila kipaza sauti,kwanini basi tuendeleee kuwasumbua wagonjwa? Hivi inamaana hata wanaokwenda kuswali hapo miaka yote hiyo, wameshindwa kuliona au wanaifurahia hiyo hali?

Kama hujawahi kuwa na mgonjwa Muhimbili katika masaa hayo huwezi jua ni kwa kiasi gani sauti hizo ni karaha;hili linawahusu watu wote bila kujali dini wala rangi yake.

Wana-jamvi hebu tulijadili na watu wa Muhimbili wachukue maoni yetu.

Why not borrow a leaf from Rwanda that these disturbing noises are stopped forthwith.
 
Back
Top Bottom