Mnyamahodzo
JF-Expert Member
- May 23, 2008
- 1,932
- 985
Kama ulikwisha wahi kwenda katika Hospitali yetu, kubwa kuliko zote hapa nchini Tanzania,yaani Hospitali ya Taifa Muhimbili muda wa saa saba mchana au saa kumi kasoro jioni utakuwa umekutana na hili nalolitaka kulisema.
Ndiyo! Ziko sabababu nyingi zinzoweza mfanya mtu akaenda Muhimbili, yawezekana ugonjwa au unasindikiza mgonjwa, kuchukuliwa kipimo,kumwona mgonjwa ama kuweka au kuchukua maiti.
Karibu na chumba cha maiti pana nyumba mbili kubwa za ibada, yaani msikiti na kanisa. sasa ukiwepo Muhimbili masaa hayo niliyoyataja wakati ibada inaanza msikitini, inapigwa adhana. Sauti yake yakuzwa na kipaza sauti. Inatupwa mbali sana.
Sasa tatizo hapa ni hili, nikijua ile ni hospitali yenye wagonjwa wanaolazwa na wasiolazwa na nikijua kuwa hata magari hayaruhusiwi kupiga honi ndani ya eneo la hospitali;iweje sauti hizi katika kipaza sauti ziwe zinaendelea kuwa kero kwa wagonjwa hasa wa zile wodi za wazazi na watoto(maana zipo umbali wa chini ya mita 100 toka msikitini)?
Hivi adhana ikipigwa bila ya kutumia kipaza sauti, ibada inakuwa batli? Kama hilo ni kweli. Je! Maeneo ambako hakuna umeme wala kipaza sauti ibada zao ni batili? Je! Ibada walizofanya wakina Mtume Mohamad (S.A.W) bila kutumia kipaza sauti zilikuwa batili?
Kama ibada inaendelea kuwa halali hata kama adhana itapigwa bila kipaza sauti,kwanini basi tuendeleee kuwasumbua wagonjwa? Hivi inamaana hata wanaokwenda kuswali hapo miaka yote hiyo, wameshindwa kuliona au wanaifurahia hiyo hali?
Kama hujawahi kuwa na mgonjwa Muhimbili katika masaa hayo huwezi jua ni kwa kiasi gani sauti hizo ni karaha;hili linawahusu watu wote bila kujali dini wala rangi yake.
Wana-jamvi hebu tulijadili na watu wa Muhimbili wachukue maoni yetu.
Ndiyo! Ziko sabababu nyingi zinzoweza mfanya mtu akaenda Muhimbili, yawezekana ugonjwa au unasindikiza mgonjwa, kuchukuliwa kipimo,kumwona mgonjwa ama kuweka au kuchukua maiti.
Karibu na chumba cha maiti pana nyumba mbili kubwa za ibada, yaani msikiti na kanisa. sasa ukiwepo Muhimbili masaa hayo niliyoyataja wakati ibada inaanza msikitini, inapigwa adhana. Sauti yake yakuzwa na kipaza sauti. Inatupwa mbali sana.
Sasa tatizo hapa ni hili, nikijua ile ni hospitali yenye wagonjwa wanaolazwa na wasiolazwa na nikijua kuwa hata magari hayaruhusiwi kupiga honi ndani ya eneo la hospitali;iweje sauti hizi katika kipaza sauti ziwe zinaendelea kuwa kero kwa wagonjwa hasa wa zile wodi za wazazi na watoto(maana zipo umbali wa chini ya mita 100 toka msikitini)?
Hivi adhana ikipigwa bila ya kutumia kipaza sauti, ibada inakuwa batli? Kama hilo ni kweli. Je! Maeneo ambako hakuna umeme wala kipaza sauti ibada zao ni batili? Je! Ibada walizofanya wakina Mtume Mohamad (S.A.W) bila kutumia kipaza sauti zilikuwa batili?
Kama ibada inaendelea kuwa halali hata kama adhana itapigwa bila kipaza sauti,kwanini basi tuendeleee kuwasumbua wagonjwa? Hivi inamaana hata wanaokwenda kuswali hapo miaka yote hiyo, wameshindwa kuliona au wanaifurahia hiyo hali?
Kama hujawahi kuwa na mgonjwa Muhimbili katika masaa hayo huwezi jua ni kwa kiasi gani sauti hizo ni karaha;hili linawahusu watu wote bila kujali dini wala rangi yake.
Wana-jamvi hebu tulijadili na watu wa Muhimbili wachukue maoni yetu.