Saudi Women defy drive ban

MaxShimba

JF-Expert Member
Apr 11, 2008
35,772
4,054
RIYADH (AFP) – Saudi women are set to defy a ban on driving Friday, one month after Manal al-Sharif was jailed for taking the wheel and posting footage of her rebellious act online.

The demonstrations are the climax of a two-month online campaign riding the winds of the so-called Arab spring which has spread mass revolts across the region and toppled two regimes.

But instead of organising a protest, women who have driving licences obtained abroad are being urged to get behind the wheel calmly and run their errands themselves without relying on male drivers.

The main Facebook page campaign, dubbed Women2Drive, says the action will start on Friday and keep going "until a royal decree allowing women to drive is issued."

Women in Saudi Arabia face an array of constraints, ranging from having to cover from head to toe in public and needing authorisation from a male guardian to travel, to having restricted access to jobs due to strict rules of segregation.

Due to the ban, women end up having to hire foreign drivers whose wages eat into their household incomes. If they cannot afford a driver, they have to rely on male members of their immediate families to give them a lift.

"Saudi Arabian authorities must stop treating women as second-class citizens and open the kingdom?s roads to women drivers," London-based Amnesty International said on Thursday.

More Saudi women defy drive ban - Yahoo! News
 
Hawa kina mama wa Saudi Arabia nimewapenda kwa hili walau, basi wakifanikiwa pia wachachamae kuruhusiwa kuacha nywele na sura zao tuzione
 
Hawa kina mama wa Saudi Arabia nimewapenda kwa hili walau, basi wakifanikiwa pia wachachamae kuruhusiwa kuacha nywele na sura zao tuzione

Mkuu Hawa hawana tofauti na kina mama wa Jordan, Egypt au katika nchi ambazo wanaonesha nywele na sura...au unakusudia wanapokuwa "beaches"?
 
004.034
YUSUFALI: Men are the protectors and maintainers of women, because Allah has given the one more (strength) than the other, and because they support them from their means. Therefore the righteous women are devoutly obedient, and guard in (the husband's) absence what Allah would have them guard. As to those women on whose part ye fear disloyalty and ill-conduct, admonish them (first), (Next), refuse to share their beds, (And last) beat them; but if they return to obedience, seek not against them Means (of annoyance): For Allah is Most High, great (above you all).

I have never read any verse in the Bible or Torah similar to this, although there are some pretty hairy verses in all of these fables. It seems Islam really has it out for the female. Why? What is it about a woman that is so threatening and vile to a Muslim that abuse of a woman has survived in their canon for 14 centuries?
 
Libya eti Ghadafy katawala muda mrefu.Huku Saudia wanataka kutumia gari kuleta machafuko.Wanawake vibwengo wanaotumika hata Afrika na Tanzania wapo.Ukifuatilia historia zao huwa ni wasomi wa kimarekani na wahuni.
Hii si mara ya mwanzo gari za wanawake kutumika kwa malengo hayo na kote nyuma yameshindwa.Safari hii pia itakuwa hivyo.Waislamu sasa wameamka.
 
Libya eti Ghadafy katawala muda mrefu.Huku Saudia wanataka kutumia gari kuleta machafuko.Wanawake vibwengo wanaotumika hata Afrika na Tanzania wapo.Ukifuatilia historia zao huwa ni wasomi wa kimarekani na wahuni.
Hii si mara ya mwanzo gari za wanawake kutumika kwa malengo hayo na kote nyuma yameshindwa.Safari hii pia itakuwa hivyo.Waislamu sasa wameamka.

Hebu fafanua hapo kwenye nyekundu Mkuu. Hivi Wanawake kuomba haki ya kuruhusiwa kuendesha gari ni uhuni au ukibwengo? Kuna kipengele chochote katika dini ya Kiislamu kinachokataza Wanawake kuendesha gari? Kama kipo kiweke hapa Mkuu. Kuna Wanawakewengine ambao bado hawajaolewa na hawawezi kuendesha magari yao mpaka wawe na dreva na wengine hawana uwezo wa kuajiri dreva na hawana ndugu, jamaa wa kiume kuweza kuwaendesha. Mimi naona ni haki yao Wanawake hao kudai waruhusiwe kuendesha bila pingamizi lolote lile.

Nchi chungu nzima za ME ambazo asilimia kubwa ni waislamu wanawake wanaruhusiwa kuendesha magari sioni kwanini isiwe hivyo kule Saudi Arabia.
 
Hebu fafanua hapo kwenye nyekundu Mkuu. Hivi Wanawake kuomba haki ya kuruhusiwa kuendesha gari ni uhuni au ukibwengo? Kuna kipengele chochote katika dini ya Kiislamu kinachokataza Wanawake kuendesha gari? Kama kipo kiweke hapa Mkuu. Kuna Wanawakewengine ambao bado hawajaolewa na hawawezi kuendesha magari yao mpaka wawe na dreva na wengine hawana uwezo wa kuajiri dreva na hawana ndugu, jamaa wa kiume kuweza kuwaendesha. Mimi naona ni haki yao Wanawake hao kudai waruhusiwe kuendesha bila pingamizi lolote lile.

Nchi chungu nzima za ME ambazo asilimia kubwa ni waislamu wanawake wanaruhusiwa kuendesha magari sioni kwanini isiwe hivyo kule Saudi Arabia.

BAK you are always smart.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hebu fafanua hapo kwenye nyekundu Mkuu. Hivi Wanawake kuomba haki ya kuruhusiwa kuendesha gari ni uhuni au ukibwengo? Kuna kipengele chochote katika dini ya Kiislamu kinachokataza Wanawake kuendesha gari? Kama kipo kiweke hapa Mkuu. Kuna Wanawakewengine ambao bado hawajaolewa na hawawezi kuendesha magari yao mpaka wawe na dreva na wengine hawana uwezo wa kuajiri dreva na hawana ndugu, jamaa wa kiume kuweza kuwaendesha. Mimi naona ni haki yao Wanawake hao kudai waruhusiwe kuendesha bila pingamizi lolote lile.

Nchi chungu nzima za ME ambazo asilimia kubwa ni waislamu wanawake wanaruhusiwa kuendesha magari sioni kwanini isiwe hivyo kule Saudi Arabia.
Kwa kweli vipengele vipo.Na huyu mwanamke anayetumika kuleta fujo katika nchi ya kiislamu ni kwamba anataka kuvikiuka hivyo vipengele na anapotosha hili suala.
Mwanamke wa kiislamu si kwamba haruhusiwi moja kwa moja kuendesha gari lakini haipendelewi afanye hivyo.Ikiwa ana wasimamizi kamili wa mambo yake,yaani ana mume,watoto na watu wake wengine wa karibu kumuhudumia basi anatakiwa awe mfalme na atumikiwe tu na wanaume hao.Pindi hao hawapo basi anaweza kuendesha kwa dharura na asivuke 88km kutoka anapokaa na ajisitiri vizuri.
Kinyume chake hairuhusiwi kujitokea tu ili kutembelea marafiki,kwenda beach na kuzagaa zagaa ovyo mijini na mbali kutoka anapokaa.Kitu ambacho hawa vibwengo ndilo wanalolitaka.Hili ndilo ambalo Saudi Arabia wanalipinga na ni jambo halali.
 
Kwa kweli vipengele vipo.Na huyu mwanamke anayetumika kuleta fujo katika nchi ya kiislamu ni kwamba anataka kuvikiuka hivyo vipengele na anapotosha hili suala.
Mwanamke wa kiislamu si kwamba haruhusiwi moja kwa moja kuendesha gari lakini haipendelewi afanye hivyo.Ikiwa ana wasimamizi kamili wa mambo yake,yaani ana mume,watoto na watu wake wengine wa karibu kumuhudumia basi anatakiwa
awe mfalme na atumikiwe tu na wanaume hao.Pindi hao hawapo basi anaweza kuendesha kwa dharura na asivuke 88km kutoka anapokaa na ajisitiri vizuri.
Kinyume chake hairuhusiwi kujitokea tu ili kutembelea marafiki,kwenda beach na kuzagaa zagaa ovyo mijini na mbali kutoka anapokaa.Kitu ambacho hawa vibwengo ndilo wanalolitaka.Hili ndilo ambalo Saudi Arabia wanalipinga na ni jambo halali.

Awe mfalme tena!? Na wale ambao hawajaolewa na hawana uwezo wa kuajiri dreva lakini wana uwezo wa kununua gari nao wafanyeje? Mbona sheria kama hii haiko kule Qatar, Bahrain, UAE, Iraq, Iran n.k.? Mimi kwa maoni yangu hii ni sheria ambayo haistahili kuwepo kabisa na kama Wanawake walioamua kuipingia wakipata support kubwa kutoka kwa wananchi wenzao basi si ajabu kabla ya mwaka huu kwisha ikafutwa. Nilifurahi kusikia mwanaume mmoja msaudia kule BBC leo akisema, "Wenzetu wanaenda mwezini, sisi hata kuruhusu wanawake kuendesha magari tunashindwa."

Hawa watawala wa Saudi Arabia wameyaona yale yaliyoyokea kule Misri, Tunisia, Syria na sasa Morocco kwa hiyo hili kama litapata support kubwa basi ni lazima watanywea tu maana wananchi hawaridhiki na mengi yanayofanywa na watawala wao.
 
Awe mfalme tena!? Na wale ambao hawajaolewa na hawana uwezo wa kuajiri dreva lakini wana uwezo wa kununua gari nao wafanyeje? Mbona sheria kama hii haiko kule Qatar, Bahrain, UAE, Iraq, Iran n.k.? Mimi kwa maoni yangu hii ni sheria ambayo haistahili kuwepo kabisa na kama Wanawake walioamua kuipingia wakipata support kubwa kutoka kwa wananchi wenzao basi si ajabu kabla ya mwaka huu kwisha ikafutwa. Nilifurahi kusikia mwanaume mmoja msaudia kule BBC leo akisema, "Wenzetu wanaenda mwezini, sisi hata kuruhusu wanawake kuendesha magari tunashindwa."

Hawa watawala wa Saudi Arabia wameyaona yale yaliyoyokea kule Misri, Tunisia, Syria na sasa Morocco kwa hiyo hili kama litapata support kubwa basi ni lazima watanywea tu maana wananchi hawaridhiki na mengi yanayofanywa na watawala wao.

Tatizo kwa watu wengine, ni tafsiri tu.
Chochote kitakachofanywa Saudi Arabia hata kama si sehemu ya dini, kuna watu wanatafsiri kuwa dini ndio imeamuru hivyo. Hii ndio inayoleta mambo ya kishabiki. Otherwise, mimi nafikiri sheria ya kumkataza mwanamke kuendesha gari si hitaji la kidini.
 
Awe mfalme tena!? Na wale ambao hawajaolewa na hawana uwezo wa kuajiri dreva lakini wana uwezo wa kununua gari nao wafanyeje? Mbona sheria kama hii haiko kule Qatar, Bahrain, UAE, Iraq, Iran n.k.? Mimi kwa maoni yangu hii ni sheria ambayo haistahili kuwepo kabisa na kama Wanawake walioamua kuipingia wakipata support kubwa kutoka kwa wananchi wenzao basi si ajabu kabla ya mwaka huu kwisha ikafutwa. Nilifurahi kusikia mwanaume mmoja msaudia kule BBC leo akisema, "Wenzetu wanaenda mwezini, sisi hata kuruhusu wanawake kuendesha magari tunashindwa."

Hawa watawala wa Saudi Arabia wameyaona yale yaliyoyokea kule Misri, Tunisia, Syria na sasa Morocco kwa hiyo hili kama litapata support kubwa basi ni lazima watanywea tu maana wananchi hawaridhiki na mengi yanayofanywa na watawala wao.
Bubu mbona unataka kusema mambo usiyoyajua!.
Ambae hajaolewa hakuna tofauti na aliyeolewa katika kutekeleza uislamu.Kwani yeye hana wazazi na kaka zake?.
Umesema "mimi kwa maoni yangu..... ".Nijuavyo mimi uislamu hauendi na mawazo ya watu.Wachilia mbali wewe ambaye si muislamu hata huyo msaudia uliyemsikia BBC leo kama ni muislamu hana nafasi ya kuleta ujinga wake.
Hiyo support unayoitaraji imeshindikana Libya unadhani itapatikana Saudia tena kwa jambo lenye maelezo ya kutosha juu ya uhalali na uharamu wake.
Hawa watawala wa Saudia kwa urafiki wao na Marekani wanaweza kweli kunywea lakini usidhani ndio watabadili kitu katika uislamu.Kubwa ni kuwa watakuwa na mwisho mbaya duniani na akhera watakuwa kuni za kuchomea waovu wenzao akina Firauni.Nawaangalie wenzao Yemen,Tunisia na Misri.Wale wote ilikuwa ni watu wa kunywea lakini wote Mungu hakuwatia nguvu kujitetea mbele ya raia ambao wamewafanywa wawe maadui zao.
Hizi kampeni tunajua kuwa zina malengo mengi.Baadhi yao ni kutafuta masoko ya vipodozi na kubwa ni kutaka kuuangusha uislamu kwenye shina lake kwa kudhani wamefanikiwa kwenye matawi kama vile Pakistan,Afghan,Iraq na kadhalika.
 
On a serious note wanawake wanachangia foleni barabarani as wanachukua mda mrefu kufanya maamuzi kama ban ingekuwa kwa ajili ya iyo ningewasupport.Ila nao wakomae kuacha vichwa wazi kupiga pedo vimni nk soko huria sasa
 
Kila nchi na sheria zake Saudia Arabia huo ndio utaratibu wao but sio sheria za Kislam, kwa mfano Uingereza majuzi wamepitisha sheria ya wanaume kwa wanaume mnaweza kufunga ndoa serikali ikatoa cheti cha ndoa, Marekani pia Obama kasaini sheria kuruhusu Mashoga jeshini, kwa hiyo mimi sioni tatizo kila nchi na sheria zake
 
Bubu mbona unataka kusema mambo usiyoyajua!.
Ambae hajaolewa hakuna tofauti na aliyeolewa katika kutekeleza uislamu.Kwani yeye hana wazazi na kaka zake?.
Umesema "mimi kwa maoni yangu..... ".Nijuavyo mimi uislamu hauendi na mawazo ya watu.Wachilia mbali wewe ambaye si muislamu hata huyo msaudia uliyemsikia BBC leo kama ni muislamu hana nafasi ya kuleta ujinga wake.
Hiyo support unayoitaraji imeshindikana Libya unadhani itapatikana Saudia tena kwa jambo lenye maelezo ya kutosha juu ya uhalali na uharamu wake.
Hawa watawala wa Saudia kwa urafiki wao na Marekani wanaweza kweli kunywea lakini usidhani ndio watabadili kitu katika uislamu.Kubwa ni kuwa watakuwa na mwisho mbaya duniani na akhera watakuwa kuni za kuchomea waovu wenzao akina Firauni.Nawaangalie wenzao Yemen,Tunisia na Misri.Wale wote ilikuwa ni watu wa kunywea lakini wote Mungu hakuwatia nguvu kujitetea mbele ya raia ambao wamewafanywa wawe maadui zao.
Hizi kampeni tunajua kuwa zina malengo mengi.Baadhi yao ni kutafuta masoko ya vipodozi na kubwa ni kutaka kuuangusha uislamu kwenye shina lake kwa kudhani wamefanikiwa kwenye matawi kama vile Pakistan,Afghan,Iraq na kadhalika.


Ami hapo hata wewe unakosea, aloolewa anatofauti na asieolewa kwani sasa ana nyumba yake na kufuata yale mumewe (akichanganya na zake ) kuhusiana na mambo ya maisha na ndoa.. kitu ambacho kaka au baba atakukataza/kuruhusu yaweza tofautiana na kile ambacho mume atakukataza/kukuruhusu ingawa mengine yaweza fanana..

Nafikiri wakati umefika kua kuna mambo ya kupembua.. katika kitabu cha dini (Quran) sidhani kwamba kuna sehemu inasema kua mkeo makataze kuendesha gari… NDIO Wanaweza wasikubali kirahisi lakini ni ukweli usiopingika kua eventually hii itapitishwa hata kama itachukua zaidi ya a year..
Nakubali kua kweli US ana nia mbaya na hizo nchi… lakini saa ingine tuwaluamu na wao wenyewe kua wanafiki na kukosa ushirikiano. Sipendi US afanyavyo na technique zake mbovu za kuhakikisha kashikilia kila sehemu lakini hainifanyi niwe judgemental kwa kitu ambacho naona hakina logic kuwahusisha..

Ni kweli kua Mmarekani nia yake kubwa ni ku enculturate na kuharibu mfumo mzima… lakin kumbuka Ami kua kwa upande wa vipodozi kihistoria hata kidini inaonesha ni jinsi gani mwanamke anatakiwa ajirembe na kujipodoa kwa ajili tu ya mumewe, waarabu ni wataalam na naamini wa kwanza kutumia marashi na vipodozi kabla hata ya watu wa magharibi... licha ya hivyo.. wanawake wa kiarabu kwa kujipamba na kujipodoa mzungu haoni ndani.. tofauti kati yao mzungu hujionesha mwarabu huishia kuonesha kwa mumewe.

 
  • Thanks
Reactions: BAK
Bubu mbona unataka kusema mambo usiyoyajua!.
Ambae hajaolewa hakuna tofauti na aliyeolewa katika kutekeleza uislamu.
Kwani yeye hana wazazi na kaka zake?.
Umesema "mimi kwa maoni yangu..... ".
Nijuavyo mimi uislamu hauendi na mawazo ya watu.Wachilia mbali wewe ambaye si muislamu hata huyo msaudia uliyemsikia BBC leo kama ni muislamu hana nafasi ya kuleta ujinga wake.
Hiyo support unayoitaraji imeshindikana Libya unadhani itapatikana Saudia tena kwa jambo lenye maelezo ya kutosha juu ya uhalali na uharamu wake.
Hawa watawala wa Saudia kwa urafiki wao na Marekani wanaweza kweli kunywea lakini usidhani ndio watabadili kitu katika uislamu.Kubwa ni kuwa watakuwa na mwisho mbaya duniani na akhera watakuwa kuni za kuchomea waovu wenzao akina Firauni.Nawaangalie wenzao Yemen,Tunisia na Misri.Wale wote ilikuwa ni watu wa kunywea lakini wote Mungu hakuwatia nguvu kujitetea mbele ya raia ambao wamewafanywa wawe maadui zao.
Hizi kampeni tunajua kuwa zina malengo mengi.Baadhi yao ni kutafuta masoko ya vipodozi na kubwa ni kutaka kuuangusha uislamu kwenye shina lake kwa kudhani wamefanikiwa kwenye matawi kama vile Pakistan,Afghan,Iraq na kadhalika.

Sasa kama hao wanawake wanaopinga sheria hii iliyopitwa na wakati kama wangekuwa na kaka zao na Wazazi wao kungekuwa na haja tena ya kulalamika? Huu uislamu wa kuwakataza wanawake wasiendeshe magari upo Saudia tu? Mbona katika nchi nyingine za ME ambazo zina asilimia kubwa ya Waislamu hakuna sheria kama hii. Mie nakwambia we subiri tu hawa Wanawake wakichachamaa kudai haki zao na kuungwa mkono na asilimia kubwa ya Wasaudia wenzao basi hii sheria ya mwaka 47 itafutwa tu sijui ni kipengele gani cha kiislamu ambacho kinawakataza Wanawake wasiendeshe magari. Issue hii haihitaji kuwa Muislamu au Mkristo ndio uipigie debe ni sheria ya kipumbavu ambayo haikuwa na mantiki yoyote mwaka 1970 na haina mantiki yoyote leo hii 2011.
 
Sasa kama hao wanawake wanaopinga sheria hii iliyopitwa na wakati kama wangekuwa na kaka zao na Wazazi wao kungekuwa na haja tena ya kulalamika? Huu uislamu wa kuwakataza wanawake wasiendeshe magari upo Saudia tu? Mbona katika nchi nyingine za ME ambazo zina asilimia kubwa ya Waislamu hakuna sheria kama hii. Mie nakwambia we subiri tu hawa Wanawake wakichachamaa kudai haki zao na kuungwa mkono na asilimia kubwa ya Wasaudia wenzao basi hii sheria ya mwaka 47 itafutwa tu sijui ni kipengele gani cha kiislamu ambacho kinawakataza Wanawake wasiendeshe magari. Issue hii haihitaji kuwa Muislamu au Mkristo ndio uipigie debe ni sheria ya kipumbavu ambayo haikuwa na mantiki yoyote mwaka 1970 na haina mantiki yoyote leo hii 2011.
Sikiliza nikwambie!.Hakuna sheria na agizo la kiislamu linalopitwa na wakati na wala hakuna iliyoanza mwaka 47 na 1970.Maagizo yanayoanzia kwa Allah s.w hayana mwanzo wala ukomo.
Nyinyi kwenye forums na magazeti munaong'ang'ania Saudia iachie uendeshaji wa gari huru kwa wanawake wala hamuelewi lengo kuu na hao walioanzisha ajenda hii.Wanawake na wanaume wa Saudia na kote kwengine wala hawana akili ya kupinga hekima ya Muumba wao.
Kwa kifupi nitoe fununu la kile ninachojua mimi mwenyewe.Katika Uislamu kuna kitu kinaitwa sitara ya mwanamke.Hii sitara ni mada pana sana wahadhiri wa kiislamu wanaweza wakatoa darsa mpaka ukasinzia bila kfikia mwisho.Katika sitara gari inaweza ikawa kitu kimojawapo kinachoondoa hiyo sitara.Inapoondoka kunapatikana kitu kinaitwa fitna na hii ikija nchi na dunia haikalilki.Waislamu kwa wakristo huonja chungu yake.
Wanaopinga uislamu hupendelea kuanza na kuleta fitna kwanza kabla kutumia makombora ya kutoka angani ili kurahisisha kazi.Katika uislamu wanawake ni watu muhimu sana na msingi kila jambo.Hivyo ukiweza kuwavuruga wao kwanza utakuwa umewaweza wanaume wao wa kiislamu.
Ukiwa na muda kidogo jisomee tafsiri ya Qur'an surat Ahzaab:59 na Surat Nnuur aya za 30 na 31.Vile vile jisomee mada ya Hijabu.
Wasomi wa kiislamu wa Saudia ndio wanaoelewa hayo.Wafalme na ndugu zao wanaweza wakajaribu kuridhia matakwa ya maadui lakini bado watakuwa hawajaufaa ulimwengu kwani fitna ikija itatukumba sote waislamu kwa wakristo.Mfano wa fitna inavyoenea angalia mizozo ya Libya na Iraq.
 
Back
Top Bottom