Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,269
Roketi la Soyuz lilifyetuliwa leo kutoka kituo cha misafara ya anga za juu ya Ulaya katika Guiana ya Ufaransa katika eneo la Karibian, ikiwa inabeba satelite mbili za mwanzo za mfumo wa Galilleo wa uongozi wa safari za angani. Mradi huo wenye gharama ya euro bilioni 5.4 unatarajiwa kuwa na setalite 27 zenye kufanya kazi pamoja na tatu nyingine za kutumiwa wakati wa dharura, ifikapo mwaka 2020. Mfumo huo utakuwa unashindana* na ule wa Kimarekani wa GPS. Mfumo huu wa Ulaya utagunduwa usahihi wa mkao wa dunia hadi ukubwa wa eneo la mita moja, wakati mfumo wa Marekani wa GPS usahihi wake unafikia ukubwa wa eneo la mita tatu hadi nane.