Sasatel vs uploading speed

Iyokopokomayoko

JF-Expert Member
Sep 15, 2011
1,785
441
HABARI ma-great thinkers wote,
Mimi natumia modem ya sasatel kwa zaidi ya mwaka sasa, bali kuanzia mwezi novemba mwaka jana nilianza kushuhudia speed ya internet yangu ikiwa si stable kama awali, kwa kifupi sasatel ya sasa si ile ya zamani sijui kwa watumiaji wengine.

lakini la mhimu ni UPLOAD SPEED yake, kwa sasa file lolote lenye kuanzia 1mb ku-upload ni shida sana kwa kifupi ku-upload siyo kazi nawezafanya tena, bali sina tatizo sana downloading speed. mara ya mwisho nimetest upload speed ilikuwa 0.24 kbps. Nimemuuliza rafiki yangu mmoja ameeniambia kwa sehemu kubwa ku-upload ni tatizo linalohusu zaidi modem na siyo pc.

Naomba kuuliza wataalamu na wengine kwa uzoefu wao, hasa mnaotumia sasatel, na nyinyi mnaexperience the same problem kama ilivyo kwangu?, na kwa wale mnaotumia airtel au voda upload speed zenu ni ngapi?.

Natanguliza shukrani zangu kwa yeyote atakayepoteza muda wake kunifafanulia jambo hili.

nawasilisha
 
kaka uploading speed ya mitandao yote ni ndogo sanaaaaaa. ispokuwa TTCL TU
Mkuu nashukuru kwa muda wako, TTCL uploading speed yake ni ngapi? nijurishe kwani leo hii hii nahitaji kubadili modem, niliwaza airtel sasa kama wewe unasema ttcl ndio nzuri niambie speed yake nitashukuru sana kwa hilo.
 
nimejaribu ile ya cable. inakuwa sawa uploading and downloading. kama ile ya 45000tsh per month inakuwa 40kb per second. na ile ya 75000tsh per month inakuwa 60kb per second.
 
nimejaribu ile ya cable. inakuwa sawa uploading and downloading. kama ile ya 45000tsh per month inakuwa 40kb per second. na ile ya 75000tsh per month inakuwa 60kb per second.
Bado ni ndogo sana hata hiyo mkuu, sasatel ukinunua kifurushi cha sh 7500 unapata 1.5 GB, hivyo ukinunua hivyo kila wiki kwa mwezi ni sh 30,000 na utakuwa umepata 6 GB. 60kbps kwa sh 75000 ni ndogo mno mkuu.
 
unafahamu ukiambiwa 60kbps? hiyo ni speed tu. kwa hiyo sasa uwezo wako unaweza kudownload 100GB kwa mwezi cz hiyo ipo unlimited. also hiyo speed ya 60kbps ni sawa kwenye uploading and downloading. ukilinganisha na sasatel wao downloading inafika 300kbps lkn uploading ni ndogo sana chini ya 10kbps. na hiyo ttcl imewekwa ivo cz ni unlimited
 
Back
Top Bottom