mwankuga
JF-Expert Member
- Aug 30, 2010
- 334
- 120
Hatuko mwanzo,wala hatuko mwisho,inawezekana tuko mwanzo wa mwisho.Hapa nazungumzia safari ya taifa hili la Tanzania kuelekea kwenye ukweli,kuelekea kwenye mwanga.Ukiona giza totolo limetanda kila kona ujue asubuhi inakaribia.Bila shaka Watanzaniawengi hawajawahi kuona mwanga,hawajawahi kuiona asubuhi,ni watu wachache ambao hawafiki hata nusu ya wananchi wote wanaoimiliki asubuhi na wanaoitawala nuru ya nchi hii,wakiamua leo hii mvua inyeshe wanaweza,lakini kwa muda mrefu sas wameamua jua liangaze,mazao yetu yananyauka,ngozi zetu zinangua,mama zetu wamekuwa wajane,wadogo zetu wamekuwa yatima.
Lakini sasa angalau mwanga unaanza kuonekana,wale watu waliokufa wanaonyesha dalili za kufufuka,wakina mama sasa wanaanza kung'amua kuwa waume zao hawakufa bali walipelekwa utumwani,hapa ni pazuri kwa kuanzia.Yale yanayodaiwa kuwa ni maisha bora kwa kila mwana kaya sasa yameyeyuka,hayapo na wala hayakuwahi kuwepo,sasa wananchi wanatambua kuwa hakujawahi kuwepo na mipango yoyote ya kuwakomboa zaidi ya sanaa za maonyesho na mbwembwe za vin'ola vya watawala,vinginevyo utaongoleaje tabia ya watawala wetu kuiendesha kaya kwa press conference?
Waziri mtanashati aliyevalia mavazi ya gharama hasa suti nadhifu ambazo zinapatikana London na Paris pekee,aliyependeza kisawasawa,ambaye mwonekano wake unaonyesha ana siha nzuri na bongo safi,anajitokeza mbele ya wandishi wa habari kuja kutoa majibu ya maswali magumu,mwisho wa mkutano hakuna alichokieleza zaidi ya majisifu na majigambo,"serikali yangu itawachukulia hatua kali wale wote watakaohatarisha amani na usalama wa taifa".Waandishi wanapotaka kumuuliza maswali anagoma,yuko bize na shughuli za serikali.Huyu ni mtu aliyepita skuli nyingi wao wanamwita Profesa,sawa lakini si kila Profesa ana bongo safi na pia huwezi kujua huo uprofesa aliupataje,si unajua katika kaya yetu chochote kinawezekana,wewe hujaona au hata kusikia vyeti vinauzwa au watu kofoji vyeti?.
Hapa ndipo tulipofika na hatukufika kwa bahati mbaya,na wala hatukufika kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu.Tumefika hapa kwa mapenzi ya watu wachache wateule na watoto wa mfalme wanaoishi mitaa ya ng'ambo ya DARE ES SALAAM.Hawa ni wateule weusi wenzetu kwa rangi na wageni kwa tabia na matendo yao,hawa tulikuwa nao enzi za kutafuta uhuru,tulikunywa na kula kwa pamoja,tuliishi wote kwenye nyumba za udongo,tulikunywa mvinyo na sifongo kwa pamoja,lakini wenzetu Mungu kawasaidia,wamebadili zile nafasi za wale tuliokuwa tunawapinga,ujamaa waliokuwa wanauhubiri haupo tena,sasa kila mtu na atakufa na chake.Usaliti!Usaliti!Usaliti mkubwa huu unaofanywa na ndugu zet wa damu tuliokuwa tunachunga wote ng'ombe na kukamata vindege kule Bagamoyo,Rombo,Kantalamba,Uvinza,Tundur na kwingineko.
Nasema hapa tulipofikia ni pazuri,maana hamna ambaye sasa amelala,kila mtu najua usaliti huu mtakavitu,wanajua kuwa nchi hii inahitaji ukombozi wa pili ambao ni mgumu kuliko ule wa mara ya kwanza.Ukombozi wa kwanza tulikuwa tunagombana na na wale weupe wa ng'amboambao hatukuwa na nasaba nao,sasa tunagombana na ndugu zetu,walioshiba hasa na wenye miili ya watu wawili ndani ya mwili mmoja na walevi wa madaraka wa kupindukia ambao wako radhi kununua ndege mbovu ya rais kwa gharama ya wananchi kula nyasi.Nasema tulipofika ni pazuri sana kwa kuanzia harakati,kuwa nasubira nitakuambia,na nitakachokuambia tafathali sana wambie na wengine ila usiwambie nani kakuambia maana wakubwa hawachelewi kusema nina hatarisha amani ya nchi,waulize MwanaHalisi nini kiliwapata,wakati kwa upande wa wabaka uchumiwanatesa mitaani kwa sababu kuwakamata ni sawa na kuiangusha serikali,sasa ingawaje si sawasawa.
Katika vita ya kuzikomboa nchi zetu kutoka mikononi mwa mazanuni wa kikoloni bila shaka adui yetu alikuwa anaonekana hata kwa kumtazama kwa macho,tulifanikiwa kwa sababu lengo letu lilikuwa moja,tukawaondoa wakoloni ambao tulikuwa hatuwajui vizuri.Kama Halmashauri yako ya ubongo inafanya kazi kwa ushirikiano mzuri,si tu utakubaliana na mimi bali utaamini kuwa uhuru tuliupata hatuwezi kujivunia kwani matunda yake hayaonekani,maana tumeyasubiria sana,na sas ni jioni na tunaenda kulala bila ya hata kula.
Kama haujui basi naomba kubaliana na mimi kuwa uhuru si kila mara ni mwisho wa utumwa,inawezekana sera ya assimilation na assimilado zimetuathiri kiasi kisichopimika,vinginevyo unazungumziaje tabia ya viongozi wengi wa bara hili lililoitwa bara la giza na wakoloni.BViongozi wetu wa bara hili ni walevi na walavi wa madaraka kwa kiasi kisichoelezeka.Inawezekana hatukufahamu kuwa wakati tunapata uhuru wazungu walikuwa wametuzidi akili,wakafanya kile ambacho ndicho kinatutesa hadi leo hii.
Uhuru tulioupata una maana moja tu,kuwa wajanja wachache kujimilikisha madaraka na mali na kubadili nafasi za wazungu kufaidi neema za nchi.Ikulu sas zinakaliwa na weusi wenzetu kwa ranmgi na tofauti kwa matendo.Weusi haya ni hatari kulio weupe tuliowafukuza.Angalia sasa Ikulu zetu zimetekwa,zimekuwa sehemu zinazokaliwa na wachuzi au madalali wa soko huria au wajasiliamali kwa lugha tamu za kimagharibi.Watu tunaowaheshimu sana na pengine tunaowaamini sana kama ndugu zetu,ni haohao wanaotusaliti na kushirikiana na wanyang'anyi wa ng'ambo kupora rasilimali zetu.
Baba wa taifa,Hayati Mwalimu Nyerere amewahi kusema kuwa ikilu ni sehemu takatifu,ambayo haina kitu zaidi ya kubeba matatizo ya watu,pia amepata kuwauliza vijana waliokuwa wanakimbilia ikulu,kuwa wanafuata nini Ikulu.Bila shaka sasa tunaona kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa anawajua vizuri vijana hawa(kwa sasa wazee0,na sisi pia tumeona kuwa vijana hawa walikuwa wanataka nini.Wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu mwaka 1995,pamoja na Kikwete kuonekana akimshinda Benjamini Mkapa,Baba wa Taifa aliingilia kati na kumwambia Kikwete kuwa alikuwa mdogo(sijui kiumri au kiakili)Uamuzi huo ulionekana kama ubabe,lakini sasa tunaona kuwa Nyerere kuwa alikuwa sahihi.
Lakini kwa kutenda haki zaidi,pia tumeshuhudia jinsi chaguo la Nyerere,Mkapa alivyosaidia kuchonga jeneza la nchi kuelekea kwenye utumwa.PAMOJA NA KUIMARISHA UCHUMI,KUONGEZA MAPATO YA SERIKALI NA KUONGEZA NIDHAMU YA KAZI SERIKALINI,zoezi lake la ubinafshaji mali za umma umeleta gharika kuu ndani ya nchi hii.Ubnafishaji wa mali umma unaweza usiwe tatizo maana tumeshuhudia nchi nyingine zoezi hili likienda vizuri,lakini zoezi hili kuliendesha ndani ya nchi yetu ni sawa na kuuza nchi kwani watendaji wengi wa serikali sio waaminifu hata chembe.
Katika nchi ambayo watendaji wake hawajulikani wametokea wapi,wanachaguliwa kwa ujanjaujanja kutokana na kiasi cha pesa walizonazo,na wengine wanateuliwa kushika nyadhifa kubwa serikalini kutokana na michango yao waliyoitoa wakati wa uchaguzi,vinginevyo mtandao una maana gani au una faida gani kwa wananchi?Vi9nginevyo jiulize kwanini nchi za Asia kama vile China wamesonga mbele sana kimaendeleo wakati miaka ya 1970 tulikuwa almost at the same level,lakini kwa sasa hawa watu wako mbele sana kiasi kwamba hata watu wa maghariby wameanza kuogopa.Nchi kama China inasonga mbele kwa sababu ya uzalendo wa juu kabisa,mipango inayoendana a utekelezaji,elimu nusu masomo na nusu kazi na uaminifu wa ajabu kwa watendaji wa serikali.
Lakini kwa Afrika ni tofauti sana,uhuru ulikuwa una maana moja tu,kuhamisha neema walizokuwa wanapata wazungu kwa weusi wenzetu.Angalia wenzetu hawa walivyokuwa maharamia,wakiua watu wetu wasiokuwa na hatia,usishituke sana,vinginevyo unasemaje kuhusu ufisadi wa kutisha unaofanywa na watendaji wa serikali,angalia wakina mama wanavyopoteza maisha pamoja na vitoto vyao,huduma za afya ni duni,na watu wengine wanakufa kwa kukosa chakula katikati ya ardhi yenye rutuba.
Sidhani kama wananchi waliowengi kama hawajui kinachofanywa na watendaji na wanasiasa wetu.Kwa maoni yangu wengi wanajua kuna kuna baadhi ya watu ambao zamani tuliwaita wenzetu jinsi wanavyoneemeka na kunawili kwa kutumia rasilimali za taifa.Wanachi wanatambua haya,tena ukiwakuta wanaongea kwenye vijiwe vyao,kama unapenda kuchekacheka na kutopenda kufikiri sana utawapuza lakini kama unapenda kufikiria,utaumia sana na utachukua hatua.
Mwishojapo si kwa umuhimu ni kwamba Watanzania tuna nafasi moja tu ya kurekebisha makosa yetu hapo ifikapo Octoba 2010.Japo wengi hawaamini kuwa kuwa katika Afrika inaweza kubadilisha maisha,hakika tunaweza kusonga mbele kama tutawapigia kura watu makini na wanaokerwa na umasikini wetu.Ni nafasi yetu pekee kuonyesha ukomavu wetu na uzalendo wetuTuchague watu makini na si vyama,vyama vinapita lakini Tanzania itabaki milele.Tuchague viongozi kwa umakini mkubwa ili tuitimishe ngwe ya kwanza ambayo ni MWISHO WA MWANZO.
Lakini sasa angalau mwanga unaanza kuonekana,wale watu waliokufa wanaonyesha dalili za kufufuka,wakina mama sasa wanaanza kung'amua kuwa waume zao hawakufa bali walipelekwa utumwani,hapa ni pazuri kwa kuanzia.Yale yanayodaiwa kuwa ni maisha bora kwa kila mwana kaya sasa yameyeyuka,hayapo na wala hayakuwahi kuwepo,sasa wananchi wanatambua kuwa hakujawahi kuwepo na mipango yoyote ya kuwakomboa zaidi ya sanaa za maonyesho na mbwembwe za vin'ola vya watawala,vinginevyo utaongoleaje tabia ya watawala wetu kuiendesha kaya kwa press conference?
Waziri mtanashati aliyevalia mavazi ya gharama hasa suti nadhifu ambazo zinapatikana London na Paris pekee,aliyependeza kisawasawa,ambaye mwonekano wake unaonyesha ana siha nzuri na bongo safi,anajitokeza mbele ya wandishi wa habari kuja kutoa majibu ya maswali magumu,mwisho wa mkutano hakuna alichokieleza zaidi ya majisifu na majigambo,"serikali yangu itawachukulia hatua kali wale wote watakaohatarisha amani na usalama wa taifa".Waandishi wanapotaka kumuuliza maswali anagoma,yuko bize na shughuli za serikali.Huyu ni mtu aliyepita skuli nyingi wao wanamwita Profesa,sawa lakini si kila Profesa ana bongo safi na pia huwezi kujua huo uprofesa aliupataje,si unajua katika kaya yetu chochote kinawezekana,wewe hujaona au hata kusikia vyeti vinauzwa au watu kofoji vyeti?.
Hapa ndipo tulipofika na hatukufika kwa bahati mbaya,na wala hatukufika kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu.Tumefika hapa kwa mapenzi ya watu wachache wateule na watoto wa mfalme wanaoishi mitaa ya ng'ambo ya DARE ES SALAAM.Hawa ni wateule weusi wenzetu kwa rangi na wageni kwa tabia na matendo yao,hawa tulikuwa nao enzi za kutafuta uhuru,tulikunywa na kula kwa pamoja,tuliishi wote kwenye nyumba za udongo,tulikunywa mvinyo na sifongo kwa pamoja,lakini wenzetu Mungu kawasaidia,wamebadili zile nafasi za wale tuliokuwa tunawapinga,ujamaa waliokuwa wanauhubiri haupo tena,sasa kila mtu na atakufa na chake.Usaliti!Usaliti!Usaliti mkubwa huu unaofanywa na ndugu zet wa damu tuliokuwa tunachunga wote ng'ombe na kukamata vindege kule Bagamoyo,Rombo,Kantalamba,Uvinza,Tundur na kwingineko.
Nasema hapa tulipofikia ni pazuri,maana hamna ambaye sasa amelala,kila mtu najua usaliti huu mtakavitu,wanajua kuwa nchi hii inahitaji ukombozi wa pili ambao ni mgumu kuliko ule wa mara ya kwanza.Ukombozi wa kwanza tulikuwa tunagombana na na wale weupe wa ng'amboambao hatukuwa na nasaba nao,sasa tunagombana na ndugu zetu,walioshiba hasa na wenye miili ya watu wawili ndani ya mwili mmoja na walevi wa madaraka wa kupindukia ambao wako radhi kununua ndege mbovu ya rais kwa gharama ya wananchi kula nyasi.Nasema tulipofika ni pazuri sana kwa kuanzia harakati,kuwa nasubira nitakuambia,na nitakachokuambia tafathali sana wambie na wengine ila usiwambie nani kakuambia maana wakubwa hawachelewi kusema nina hatarisha amani ya nchi,waulize MwanaHalisi nini kiliwapata,wakati kwa upande wa wabaka uchumiwanatesa mitaani kwa sababu kuwakamata ni sawa na kuiangusha serikali,sasa ingawaje si sawasawa.
Katika vita ya kuzikomboa nchi zetu kutoka mikononi mwa mazanuni wa kikoloni bila shaka adui yetu alikuwa anaonekana hata kwa kumtazama kwa macho,tulifanikiwa kwa sababu lengo letu lilikuwa moja,tukawaondoa wakoloni ambao tulikuwa hatuwajui vizuri.Kama Halmashauri yako ya ubongo inafanya kazi kwa ushirikiano mzuri,si tu utakubaliana na mimi bali utaamini kuwa uhuru tuliupata hatuwezi kujivunia kwani matunda yake hayaonekani,maana tumeyasubiria sana,na sas ni jioni na tunaenda kulala bila ya hata kula.
Kama haujui basi naomba kubaliana na mimi kuwa uhuru si kila mara ni mwisho wa utumwa,inawezekana sera ya assimilation na assimilado zimetuathiri kiasi kisichopimika,vinginevyo unazungumziaje tabia ya viongozi wengi wa bara hili lililoitwa bara la giza na wakoloni.BViongozi wetu wa bara hili ni walevi na walavi wa madaraka kwa kiasi kisichoelezeka.Inawezekana hatukufahamu kuwa wakati tunapata uhuru wazungu walikuwa wametuzidi akili,wakafanya kile ambacho ndicho kinatutesa hadi leo hii.
Uhuru tulioupata una maana moja tu,kuwa wajanja wachache kujimilikisha madaraka na mali na kubadili nafasi za wazungu kufaidi neema za nchi.Ikulu sas zinakaliwa na weusi wenzetu kwa ranmgi na tofauti kwa matendo.Weusi haya ni hatari kulio weupe tuliowafukuza.Angalia sasa Ikulu zetu zimetekwa,zimekuwa sehemu zinazokaliwa na wachuzi au madalali wa soko huria au wajasiliamali kwa lugha tamu za kimagharibi.Watu tunaowaheshimu sana na pengine tunaowaamini sana kama ndugu zetu,ni haohao wanaotusaliti na kushirikiana na wanyang'anyi wa ng'ambo kupora rasilimali zetu.
Baba wa taifa,Hayati Mwalimu Nyerere amewahi kusema kuwa ikilu ni sehemu takatifu,ambayo haina kitu zaidi ya kubeba matatizo ya watu,pia amepata kuwauliza vijana waliokuwa wanakimbilia ikulu,kuwa wanafuata nini Ikulu.Bila shaka sasa tunaona kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa anawajua vizuri vijana hawa(kwa sasa wazee0,na sisi pia tumeona kuwa vijana hawa walikuwa wanataka nini.Wakati wa mchakato wa uchaguzi mkuu mwaka 1995,pamoja na Kikwete kuonekana akimshinda Benjamini Mkapa,Baba wa Taifa aliingilia kati na kumwambia Kikwete kuwa alikuwa mdogo(sijui kiumri au kiakili)Uamuzi huo ulionekana kama ubabe,lakini sasa tunaona kuwa Nyerere kuwa alikuwa sahihi.
Lakini kwa kutenda haki zaidi,pia tumeshuhudia jinsi chaguo la Nyerere,Mkapa alivyosaidia kuchonga jeneza la nchi kuelekea kwenye utumwa.PAMOJA NA KUIMARISHA UCHUMI,KUONGEZA MAPATO YA SERIKALI NA KUONGEZA NIDHAMU YA KAZI SERIKALINI,zoezi lake la ubinafshaji mali za umma umeleta gharika kuu ndani ya nchi hii.Ubnafishaji wa mali umma unaweza usiwe tatizo maana tumeshuhudia nchi nyingine zoezi hili likienda vizuri,lakini zoezi hili kuliendesha ndani ya nchi yetu ni sawa na kuuza nchi kwani watendaji wengi wa serikali sio waaminifu hata chembe.
Katika nchi ambayo watendaji wake hawajulikani wametokea wapi,wanachaguliwa kwa ujanjaujanja kutokana na kiasi cha pesa walizonazo,na wengine wanateuliwa kushika nyadhifa kubwa serikalini kutokana na michango yao waliyoitoa wakati wa uchaguzi,vinginevyo mtandao una maana gani au una faida gani kwa wananchi?Vi9nginevyo jiulize kwanini nchi za Asia kama vile China wamesonga mbele sana kimaendeleo wakati miaka ya 1970 tulikuwa almost at the same level,lakini kwa sasa hawa watu wako mbele sana kiasi kwamba hata watu wa maghariby wameanza kuogopa.Nchi kama China inasonga mbele kwa sababu ya uzalendo wa juu kabisa,mipango inayoendana a utekelezaji,elimu nusu masomo na nusu kazi na uaminifu wa ajabu kwa watendaji wa serikali.
Lakini kwa Afrika ni tofauti sana,uhuru ulikuwa una maana moja tu,kuhamisha neema walizokuwa wanapata wazungu kwa weusi wenzetu.Angalia wenzetu hawa walivyokuwa maharamia,wakiua watu wetu wasiokuwa na hatia,usishituke sana,vinginevyo unasemaje kuhusu ufisadi wa kutisha unaofanywa na watendaji wa serikali,angalia wakina mama wanavyopoteza maisha pamoja na vitoto vyao,huduma za afya ni duni,na watu wengine wanakufa kwa kukosa chakula katikati ya ardhi yenye rutuba.
Sidhani kama wananchi waliowengi kama hawajui kinachofanywa na watendaji na wanasiasa wetu.Kwa maoni yangu wengi wanajua kuna kuna baadhi ya watu ambao zamani tuliwaita wenzetu jinsi wanavyoneemeka na kunawili kwa kutumia rasilimali za taifa.Wanachi wanatambua haya,tena ukiwakuta wanaongea kwenye vijiwe vyao,kama unapenda kuchekacheka na kutopenda kufikiri sana utawapuza lakini kama unapenda kufikiria,utaumia sana na utachukua hatua.
Mwishojapo si kwa umuhimu ni kwamba Watanzania tuna nafasi moja tu ya kurekebisha makosa yetu hapo ifikapo Octoba 2010.Japo wengi hawaamini kuwa kuwa katika Afrika inaweza kubadilisha maisha,hakika tunaweza kusonga mbele kama tutawapigia kura watu makini na wanaokerwa na umasikini wetu.Ni nafasi yetu pekee kuonyesha ukomavu wetu na uzalendo wetuTuchague watu makini na si vyama,vyama vinapita lakini Tanzania itabaki milele.Tuchague viongozi kwa umakini mkubwa ili tuitimishe ngwe ya kwanza ambayo ni MWISHO WA MWANZO.