NdasheneMbandu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 940
- 308
Wadau,
Tuwe wakweli, kwa hali ilivyo sasa ya kutokuwepo kwa mvua na kusababisha mabawawa yetu kukosa maji, bila shaka hivi sasa tungekuwa hoi tukiogelea kwenye lindi la mgawo mkubwa wa umeme. Wapo ambao bahati mbaya hawataki kuamini kwamba mgawo wa umeme Tanzania ulikwa ni artificial kwa maana kwamba unatengenezwa na genge la wahuni na walafi wanaoshirikiana na wenzao wa TANESCO huku wakiacha watanzania wakiumia na kuteseka sana.
Nakumbuka wakati wa sakata la kumsimamisha kazi aliyekuwa Mkurugenzi wa TANESCO Bw. Mhando ulitokea ubishani mkubwa kwamba Serikali imemwonea kwani tayari alikuwa ameruhusu umeme utolewe kwa mgawo. Mimi mwenyewe ni mojawapo ya watu waliopinga kusimamishwa kazi kwa Bw. Mhando nikiamini alikuwa ameonewa lakini sasa nimeamini kuwa mgawo wa umeme lilikuwa ni daraja la mafisadi la kupitishia fedha za walipa kodi wa nchi hii. Hapa lazima niwe mkweli, naanza kuwa na wasiwasi na credibility ya Zitto Kabwe na Kamati yake kama kweli nayo haikuwa miongoni mwa wanufaika wa mgawo wa umeme. Haiwezekani watu wachache akina Prof. Muhongo na wenzake including Katibu Mkuu Nishati na Madini waje na suluhisho la haraka kiasi hicho kama kweli mgawo ulikuwa unatokana na tatizo kubwa.
Najua hatua hiyo imemjengea Prof. Muhongo maadui wakubwa kiutendaji ikiwa ni pamoja na Zitto Kabwe mwenyewe pamoja na wabunge wenzie. Lakini sisi wananchi wa kawaida tutaendelea kumwombea Prof. Muhongo na timu yake Mungu awalinde ili waendelee kupigania haki ya watanzania kwa mapana zaidi.
Tuwe wakweli, kwa hali ilivyo sasa ya kutokuwepo kwa mvua na kusababisha mabawawa yetu kukosa maji, bila shaka hivi sasa tungekuwa hoi tukiogelea kwenye lindi la mgawo mkubwa wa umeme. Wapo ambao bahati mbaya hawataki kuamini kwamba mgawo wa umeme Tanzania ulikwa ni artificial kwa maana kwamba unatengenezwa na genge la wahuni na walafi wanaoshirikiana na wenzao wa TANESCO huku wakiacha watanzania wakiumia na kuteseka sana.
Nakumbuka wakati wa sakata la kumsimamisha kazi aliyekuwa Mkurugenzi wa TANESCO Bw. Mhando ulitokea ubishani mkubwa kwamba Serikali imemwonea kwani tayari alikuwa ameruhusu umeme utolewe kwa mgawo. Mimi mwenyewe ni mojawapo ya watu waliopinga kusimamishwa kazi kwa Bw. Mhando nikiamini alikuwa ameonewa lakini sasa nimeamini kuwa mgawo wa umeme lilikuwa ni daraja la mafisadi la kupitishia fedha za walipa kodi wa nchi hii. Hapa lazima niwe mkweli, naanza kuwa na wasiwasi na credibility ya Zitto Kabwe na Kamati yake kama kweli nayo haikuwa miongoni mwa wanufaika wa mgawo wa umeme. Haiwezekani watu wachache akina Prof. Muhongo na wenzake including Katibu Mkuu Nishati na Madini waje na suluhisho la haraka kiasi hicho kama kweli mgawo ulikuwa unatokana na tatizo kubwa.
Najua hatua hiyo imemjengea Prof. Muhongo maadui wakubwa kiutendaji ikiwa ni pamoja na Zitto Kabwe mwenyewe pamoja na wabunge wenzie. Lakini sisi wananchi wa kawaida tutaendelea kumwombea Prof. Muhongo na timu yake Mungu awalinde ili waendelee kupigania haki ya watanzania kwa mapana zaidi.