Lukwangule
Senior Member
- May 25, 2009
- 157
- 2
Kutakuwapo na mgao wa umeme katika mikoa yote ya Tanzania Bara kuanzia saa 12 jioni hadi saa nne usiku kila siku,Kaimu Mkurugenzi wa Tanesco Stephen Mabada amesema leo.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari alieleza sababu ya kuwepo mgao huo kuwa ni kuharibika kwa baadhi ya mitambo katika vituo mbalimbali vya kuzalishia umeme.
Mitambo iliyotajwa kuharibika iko katika vituo vya kuzalisha umeme vya Kidatu, Kihansi, Pangani na kile cha Ubungo Gas Power Plant. Hata hivyo tarifa hiyo haikueleza kiasi cha megawati kitakachokosekana baada ya mitambo hiy kuharibika.
Athari za upungufu huo zimelilazimu shirika kuanza mgao wa umeme kwa maeneo mbalimbali wakati wa matumizi makubwa ya umeme kuanzia saa 12 jioni hadi saa nne usiku, ilisema taarifa hiyo.
Ofisa mmoja wa tanesco alikiri kuwa mgao ulishaanza wiki kadhaa zilizopita na walisita kutangaza kwa kuamini kuwa matengenezo hayo yangechukua siku chache.
Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alipoulizwa lini mgao huo utamalizika alisema hajui ila akasisitiza kuwa mafundi wako site usiku na mchana kuhakikisha hali inatengemaa.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari alieleza sababu ya kuwepo mgao huo kuwa ni kuharibika kwa baadhi ya mitambo katika vituo mbalimbali vya kuzalishia umeme.
Mitambo iliyotajwa kuharibika iko katika vituo vya kuzalisha umeme vya Kidatu, Kihansi, Pangani na kile cha Ubungo Gas Power Plant. Hata hivyo tarifa hiyo haikueleza kiasi cha megawati kitakachokosekana baada ya mitambo hiy kuharibika.
Athari za upungufu huo zimelilazimu shirika kuanza mgao wa umeme kwa maeneo mbalimbali wakati wa matumizi makubwa ya umeme kuanzia saa 12 jioni hadi saa nne usiku, ilisema taarifa hiyo.
Ofisa mmoja wa tanesco alikiri kuwa mgao ulishaanza wiki kadhaa zilizopita na walisita kutangaza kwa kuamini kuwa matengenezo hayo yangechukua siku chache.
Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja alipoulizwa lini mgao huo utamalizika alisema hajui ila akasisitiza kuwa mafundi wako site usiku na mchana kuhakikisha hali inatengemaa.