Kama kunawakati Kanisa linatakiwa lijitambue ni sasa, kwa nyakati tofauti kanisa limekuwa likisinzia kwa kile kilichukuwa kinaelezwa kuwa nchi hii ni kisiwa cha amani. Kanisa la Tanzania limekuwa sio moja na ndiyo maana hata matamko huenda kila dhehebu likatoa tamko lake. Kila dhehebu limejitahidi sana kujiangalia kivyake, na ndiyo maana likichomwa kanisa la Anglikana, Katoliki wamekuwa akidhani hawahusiki. Kimsingi watu wasio wakristo hawajua kuwa kanisa la Tanzania sio moja, hawajui kuwa kinachofanyika Anglikana Katoliki hakijui, hili ni tatizo ambalo naamini sasa litaisha, ni wakati sasa kanisa la Tanzania likajiangalia kama Kanisa Moja, Kanisa lijitambue kuwa linahitaji liwe moja katika mshikamano, kanisa linatakiwa kuaminiana na kamwe anachofanyiwa kibaya mpentekoste KKKT akilaani kwa nguvu zote.
Pamoja na ubaya wa yote yanayotokea dhidi ya Kanisa nafikiri, huku ni kuwaamsha wakristo ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisinzia na kusahau mambo ya msingi, Kanisa sasa livae silaha za imani na kuishindania imani ya Kristo kwa kufunga na kuomba ili Mungu adhihirike kuwa huyo ndiye Mungu wa kweli.
Kanisa la Tanzania liungane bila kujali udhehebu, waangalie ukristo, msaba uwe mbele, udhehebu utumike kuwafundisha wakristo njia ya kuendea wokovu, ila inapofika suala la Kanisa udhehebu uwekwe pembeni. Bila kanisa kuwa moja, adui atapenya na kusumbua. KANISA LA TANZANIA NI WAKATI WA KUAMKA NA KUWA KITU KIMOJA
Pamoja na ubaya wa yote yanayotokea dhidi ya Kanisa nafikiri, huku ni kuwaamsha wakristo ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisinzia na kusahau mambo ya msingi, Kanisa sasa livae silaha za imani na kuishindania imani ya Kristo kwa kufunga na kuomba ili Mungu adhihirike kuwa huyo ndiye Mungu wa kweli.
Kanisa la Tanzania liungane bila kujali udhehebu, waangalie ukristo, msaba uwe mbele, udhehebu utumike kuwafundisha wakristo njia ya kuendea wokovu, ila inapofika suala la Kanisa udhehebu uwekwe pembeni. Bila kanisa kuwa moja, adui atapenya na kusumbua. KANISA LA TANZANIA NI WAKATI WA KUAMKA NA KUWA KITU KIMOJA