Jumanne Mkota
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 2,917
- 1,660
Nimekaa nimefikiria mpaka sasa nachanginyikiwa tusaidiane kutafakari hili
Hivi karibuni Rais wa Zanzibar na aliapishwa hadharani kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri(tukio hili sikuwahi kuliona tangu nimepata ufahamu wa mambo ya siasa ) .Sasa hivi kuna malumbano yanaendelea hasa upande wa pili wa Muungano juu ya Tanzania kuongeza eneo la kiuchumi bahari ya Hindi . Nadhani kikao kilichopitisha hiyo proposal ni Baraza la mawaziri ambapo Shein ni Mjumbe.
Humu ndani kuna thread moja imeandikwa TIBAIJUKA LAZIMA AJIUZULU. sikujisumbua kuisoma kwa sababu nilijua tu inatoka kwa wazee wa GUBU (wazanzibar). Swali hivi hiyo mipaka inayoongezwa haina faida kwa zanzibar!
swali la pili: pale baraza la mawaziri kuna wazanzibar 4(Shein,Mwinyi,Nahodha na Bilal) kazi yao ni nini hapo kwenye baraza kama hoja ya kuongeza mipaka imeletwa na Tibaijuka wakaijadili na hatimae kuipitisha. Halafu viongozi wa SMZ ambao kimsingi wapo chini ya Shein wanaanzisha mapambano na Tibaijuka kwanini wasiipinge mle kikaoni kama haina manufaa kwa Zanzibar?
Na kwa nini Shein hawambii ukweli wazazibar kuhusu hilo andiko la Tibaijuka.
Maana ya baraza la mawaziri nini?
Kiukweli napata tabu sana niavyoona hii serikali inavyooendeshwa kihuni yaani kama vile kijiwe cha wala poda!
Hivi karibuni Rais wa Zanzibar na aliapishwa hadharani kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri(tukio hili sikuwahi kuliona tangu nimepata ufahamu wa mambo ya siasa ) .Sasa hivi kuna malumbano yanaendelea hasa upande wa pili wa Muungano juu ya Tanzania kuongeza eneo la kiuchumi bahari ya Hindi . Nadhani kikao kilichopitisha hiyo proposal ni Baraza la mawaziri ambapo Shein ni Mjumbe.
Humu ndani kuna thread moja imeandikwa TIBAIJUKA LAZIMA AJIUZULU. sikujisumbua kuisoma kwa sababu nilijua tu inatoka kwa wazee wa GUBU (wazanzibar). Swali hivi hiyo mipaka inayoongezwa haina faida kwa zanzibar!
swali la pili: pale baraza la mawaziri kuna wazanzibar 4(Shein,Mwinyi,Nahodha na Bilal) kazi yao ni nini hapo kwenye baraza kama hoja ya kuongeza mipaka imeletwa na Tibaijuka wakaijadili na hatimae kuipitisha. Halafu viongozi wa SMZ ambao kimsingi wapo chini ya Shein wanaanzisha mapambano na Tibaijuka kwanini wasiipinge mle kikaoni kama haina manufaa kwa Zanzibar?
Na kwa nini Shein hawambii ukweli wazazibar kuhusu hilo andiko la Tibaijuka.
Maana ya baraza la mawaziri nini?
Kiukweli napata tabu sana niavyoona hii serikali inavyooendeshwa kihuni yaani kama vile kijiwe cha wala poda!