Sasa hili ni balaa. Tafakari chukua hatua

Jumanne Mkota

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
2,917
1,660
Nimekaa nimefikiria mpaka sasa nachanginyikiwa tusaidiane kutafakari hili

Hivi karibuni Rais wa Zanzibar na aliapishwa hadharani kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri(tukio hili sikuwahi kuliona tangu nimepata ufahamu wa mambo ya siasa ) .Sasa hivi kuna malumbano yanaendelea hasa upande wa pili wa Muungano juu ya Tanzania kuongeza eneo la kiuchumi bahari ya Hindi . Nadhani kikao kilichopitisha hiyo proposal ni Baraza la mawaziri ambapo Shein ni Mjumbe.

Humu ndani kuna thread moja imeandikwa TIBAIJUKA LAZIMA AJIUZULU. sikujisumbua kuisoma kwa sababu nilijua tu inatoka kwa wazee wa GUBU (wazanzibar). Swali hivi hiyo mipaka inayoongezwa haina faida kwa zanzibar!

swali la pili: pale baraza la mawaziri kuna wazanzibar 4(Shein,Mwinyi,Nahodha na Bilal) kazi yao ni nini hapo kwenye baraza kama hoja ya kuongeza mipaka imeletwa na Tibaijuka wakaijadili na hatimae kuipitisha. Halafu viongozi wa SMZ ambao kimsingi wapo chini ya Shein wanaanzisha mapambano na Tibaijuka kwanini wasiipinge mle kikaoni kama haina manufaa kwa Zanzibar?

Na kwa nini Shein hawambii ukweli wazazibar kuhusu hilo andiko la Tibaijuka.
Maana ya baraza la mawaziri nini?

Kiukweli napata tabu sana niavyoona hii serikali inavyooendeshwa kihuni yaani kama vile kijiwe cha wala poda!
 
uko sahihi mkubwa lkn si kuna shaka Jusa hivi kawa kisemeo cha mtu,no wonder! maana kimsingi huyo mtu haingii kwenye baraza
 
Usihangaike na hao watu wa SMZ kaka, we waache siku Muungano ikivunjika ndo watalia na kusaga meno.Fuatilia kwenye idara muhimu za serikari kama TRA uambiwe SMZ kule wafanyakazi wa idara hiyo wanafanya nini, hamna kitu kabisa mpaka wasaidiwe.Btw,wanaoanzisha hizo hoja za kuupinga muungano ni wale wenye undugu zaidi na Omani, lilkitokea la kutokea hutawaona Pempa wala Unguja.
 
Nimesha soma na hatua ni kumwita Shein arudi bara na kule uwe Mkoa na Mahita apewe mkoa ule .
 
linalo takiwa kuwa na serikali moja hapo tuwaone wanavyo sema wana unguruma utadhani si Watanzania
 
nadhani, ni wakati mwafaka wa kuwaachia nchi yao wazanzibari, ili yatimie maneno ya baba wa taifa yanayosema nje ya muungano hakuna wazanzibari, kutakuwa na unguja na pemba
 
uko sahihi mkubwa lkn si kuna shaka Jusa hivi kawa kisemeo cha mtu,no wonder! maana kimsingi huyo mtu haingii kwenye baraza

Nina mashaka na uraia wa Jussa. Na huenda ametumwa rasmi kuja kuuvuruga muungano, amekaa kibaguzi baguziiiiii!!!!
 
Back
Top Bottom