Sappi yuko sahihi kuhusu uwezo wa Maximo?

Nimefurahi sana kuona wadau mbalimbali wapenda maendeleo ya soka hapa nchini kwetu wamejitokeza kwa wingi kupinga kauli za kibabaishaji zinazotolewa na watu wachache wasiopenda kuona Tanzania inapiga hatua muhimu katika maendeleo ya soka. Ni wakati muafaka sasa tujifunze kuwaheshimu wataalam na pia kujifunza kutoka kwao. Nina hakika leo hii ukipata wasaa wa kufanya mahojiano na waliowahi kuwa makocha wa Taifa Stars nadhani tunaweza kusikia mambo ya aibu zaidi ya tunavyohisi. Kelele zinazopigwa juu ya kutaka kuingilia kazi za Maximo huenda zimejitokeza baada ya kundi ambalo lilizoea kufanya hivyo huko nyuma kushindwa kujipenyeza katika ukuta mgumu unaoongozwa na beki mashuhuri na nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Rais Leodgar Tenga. Laiti kama tungekuwa na uongozi wa kubabaisha sidhani kama Maximo angekuwepo leo hii. Mwisho tumpatie ushirikiano kwa wakati maximo kama kocha wetu wa Timu ya Taifa.
 
Nimefurahi sana kuona wadau mbalimbali wapenda maendeleo ya soka hapa nchini kwetu wamejitokeza kwa wingi kupinga kauli za kibabaishaji zinazotolewa na watu wachache wasiopenda kuona Tanzania inapiga hatua muhimu katika maendeleo ya soka. Ni wakati muafaka sasa tujifunze kuwaheshimu wataalam na pia kujifunza kutoka kwao. Nina hakika leo hii ukipata wasaa wa kufanya mahojiano na waliowahi kuwa makocha wa Taifa Stars nadhani tunaweza kusikia mambo ya aibu zaidi ya tunavyohisi. Kelele zinazopigwa juu ya kutaka kuingilia kazi za Maximo huenda zimejitokeza baada ya kundi ambalo lilizoea kufanya hivyo huko nyuma kushindwa kujipenyeza katika ukuta mgumu unaoongozwa na beki mashuhuri na nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Rais Leodgar Tenga. Laiti kama tungekuwa na uongozi wa kubabaisha sidhani kama Maximo angekuwepo leo hii. Mwisho tumpatie ushirikiano kwa wakati maximo kama kocha wetu wa Timu ya Taifa.

Mkuu ni kweli hawa wababaishaji ni lazima tuwashikie kidedea, wao ndio wanaoharibu soka yetu.
 
Tuangalie na mchango wa mdau huyu jamani.Gonga hapa: MICHUZI

Mkuu Balantanda,

Huko kwa Michuzi nilikuwepo na huo hapo chini ndiyo ulikuwa mchango wangu


Nadhani moja kati ya sheria za mpira wa miguu ni kuwa uamuzi wa refa ni wa mwisho. nadhani hii sheria iliwekwa makusudi ili kulinda heshima na nidhamu ya mchezo unapochezwa. Kama hii sheria isingekuwepo basi tungeona vituko kadha wa kadha kutoka kwa wachezaji, viongozi na hata mashabiki na labda huu mchezo ungelikuwa tofauti na tunavyouona sasa.

Nia yangu ya kutanguliza maelezo hayo hapo juu ni kutaka kuweka sawa mawazo ya wadau wa soka hasa Tanzania. Kwa muda mrefu tumekuwa tukisuasua kutafuta namna ya kuleta maendeleo katika soka. Hatua kadhaa zilichukuliwa lakini hatukuweza kupiga hatua za kuridhisha kwani tulikuwa na labda na mipango mizuri lakini tukakosa mbinu (strategies) bora za kutekeleza mipango. Ili soka la Tanzania liweze kukua na kuifanya timu ya taifa iwe bora na imara, hatuna budi sisi wadau ambao tuko mstari wa mbele (Wachezaji wa zamani, viongozi, mashabiki nk) tuanze kufikiria jinsi gani ya kuwekeza katika soka la vijana wadogo. hili ndiyo suluhisho la matatizo yetu. ushauri huu umekuwa ukitolewa mara kwa mara na washauri kadhaa wa ndani na wa nje ya nchi akiwemo Maximo alipofika hapa nchi kuanza kazi. Tumekuwa tukiwapa kazi ngumu makocha ya kuweza kutengeneza timu zetu hasa za taifa kwa kuwa inabidi kocha anze kufundisha wachezaji wetu namna ya kucheza mpira katika basic level. Hii ndiyo reflection ya hali halisi iliyopo katika vilabu vyetu, kwa maana unapoona mchezaji ana behaviour mbaya kwenye timu ya taifa basi ujue huko kwenye klabu level ndiyo ameoza kabisa. Vilabu vingi havijui kulea wachezaji na matatizo haya yanachangiwa kwa kiasi kikubwa na viongozi na wanachama wenyewe. Wachezaji wanavunja maadili ya uchezaji (kama kuvuta bangi, uchelewaji kwenye mazoezi, kutofuata maelekezo ya mwalimi nk) lakini kwa viongozi na wanachama kwao hilo si tatizo, hatimaye walimu husika hushindwa kufanya kazi zao na timu kutofanya vizuri.

Ni vema basi tujifunze kumwachia mwalimu afanye kazi zake ikiwa ni pamoja na kuwa-discipline wale watovu bila ya kuwaonea aibu au kufikiria uwezo wao. kwa mfano mtoa mada anaposema kuwa Abdi Kassim alifunga goli bora, that does not have any connection with discipline, hata kama ni bora kwa maoni ya mtoa mada lakini si bora kama mchezaji. Tunataka kuona kuwa wale wote wanaopata nafasi ya kuvaa jezi za national team wanafikia na kukidhi viwango vyote muhimu kama wachezaji. Tunataka wachezaji ambaowatakuwa wanauwezo wa kufuata maelekezo ya mwalimu na ku-maintain nidhamu kwa wakati wote 100%.

Tumuache maximo afanye kazi na sisi wengine tu-msupport kwa kutayarisha vijana wadogo huku mitaani kwetu.

Ninaamini wachezaji wazuri wa taifa stars bado tunao huku mitaani kwetu na si wale walioko Simba au Yanga.
 
Mkuu Balantanda,

Huko kwa Michuzi nilikuwepo na huo hapo chini ndiyo ulikuwa mchango wangu




Ni vema basi tujifunze kumwachia mwalimu afanye kazi zake ikiwa ni pamoja na kuwa-discipline wale watovu bila ya kuwaonea aibu au kufikiria uwezo wao. kwa mfano mtoa mada anaposema kuwa Abdi Kassim alifunga goli bora, that does not have any connection with discipline, hata kama ni bora kwa maoni ya mtoa mada lakini si bora kama mchezaji. Tunataka kuona kuwa wale wote wanaopata nafasi ya kuvaa jezi za national team wanafikia na kukidhi viwango vyote muhimu kama wachezaji. Tunataka wachezaji ambaowatakuwa wanauwezo wa kufuata maelekezo ya mwalimu na ku-maintain nidhamu kwa wakati wote 100%.

Tumuache maximo afanye kazi na sisi wengine tu-msupport kwa kutayarisha vijana wadogo huku mitaani kwetu.

Ninaamini wachezaji wazuri wa taifa stars bado tunao huku mitaani kwetu na si wale walioko Simba au Yanga.

Mkuu hebu soma barua waliyoandika akina Yondani, Amiri, Godfrey, Chuji, Boban nk. halafu weka na ya kaseja ukimaliza useme muachieni mwalimu afanye kazi... [IKO MICHUZI BLOG]

hapo siafiki, kwani kocha wa mpira mwenye chuki [kama walivyoainisha wachezaji kwenye barua yao] ni sawa na mabosI wabaya maofisini WENYE CHUKI KWA BAADHI YA WATU(tunawaona kila siku) ni sawa na mawaziri au wanasiasa wenye chuki... tunao kila siku nk. NI SAWA NA NDUGU WENYE CHUKI... NA HASA PALE AMBAPO UNATAKA KILA MTU AMTENGE M'BAYA WAKO, LA HASHA

Kwa maoni yangu, Maximo has lost power over his first half team and that never brings success hata kama ingekuwa brazil, pamoja na ubora wake nafananisha na mfalme alipoteza wafuasi; none of his tactics will work

Scolari, Hullier, Hoddle, Schuster, etc
 
Mkuu MTM, nimesoma hayo maelezo yao. Kocha ni zaidi ya kufundisha, manake anatakiwa kuwa kama Mzazi. Huwezi kumchukia mchezaji sababu ni rafiki wa mtu anayefanya makosa. Hiyo ni kuweka makundi ndani ya timu. Nilisoma katika Gazeti moja Maximo akimtahadharisha Haruna Moshi "Baoban" kuwa akiendelea lalamika ataweka siri yake kubwa ambayo itamfanya hata Moshi ahame nchi. Kama kweli alitoa hiyo kauli, anaonesha udhaifu mkubwa.

Maelezo yao nimeyaweka hapa chini:-

wachezaji wa taifa stars wavunja ukimya kupitia globu ya jamii
KILICHOTOKEA IVORY COAST KATI YETU (HARUNA, ATHUMAN, KEVIN, BONI, AMIR, NURDIN) NA KOCHA MARCIO MAXIMOUTANGULIZI

Kwanza kabisa tunatoa pongezi kwa mtandao huu wa jamii na Tunaomba balozi utufikishie haya tulionayo kwa jamii ya watanzania wote.

Katika maelezo yetu haya tutaeleza kila mmoja ya walioandikwa hapo juu kilichomtokea kwa kituo kabla hatujaondoka na baada ya kuwa kwenye mashindano, tunafanya hivi kwa kuwa hatuna uwezo wa kuongea na waandishi wa habari ana na pia tunaogopa kama binadamu tusije tukatereza kitu ambacho kinaweza kikatuletea madhara katika shughuli zetu za kila siku (Kucheza Mpira).
Hivyo kwa ushauri wa ndugu na jamaa zetu tukaona ni bora tutumie tovuti yetu hii ya jamii kuwaomba msamaha watanzania wote na pia kuwapa haki ya kujua nini hasa kilichotokea na pia tunaomba wanahabari watumie ujumbe wetu huu kuwafikishia habari wananchi wote wa Tanzania ili waweze kuelewa undani wa sakata zima hili na tunaomba endapo tutakacho kieleza hapa kitakuwa sio kweli atoke mbele ya jamii na kutukosoa tuko tayari kwa hilo.

ATHUMAN IDD (Chuji)
Itakumbukwa kuwa wakati nikiwa na timu yangu ya Yanga niliumia nyama za paja kitu ambacho kilisababisha Dakitari wa timu kushauri kuwa nipumzike wakati nikiendelea na matibabu ili niweze kupona vizuri kitu ambacho nilikifanya na nikaamua kwenda kwa mama yangu Tanga kupumzika wakati nikiendelea na matibabu.
Siku chache baadae niliitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ambapo niliripoti lakini sikuweza kufanya mazoezi na timu kwa sababu ya tatizo langu la paja na hata Dakitari wa timu alithibitisha hilo, lakini baada ya muda mfupi nikaanza mazoezi mepesi pamoja na timu na mwisho nikawa sawasawa japo sio 100%.
Muda mfupi kabla ya kwenda kwenye mashindano Kocha mkuu akaniita na kuniambia kuwa ananichukua mimi kwenda Ivory Coast kwa kuogopa kelele za watu lakini sitocheza kitu ambacho sikukielewa lakini pia sikutaka kukubali kwani niliamini naendelea vizuri na baada ya siku chache nitakuwa sawasawa 100% kwahiyo kocha ataweza kunipanga.
Tulipofika kwenye mashindano niliongeza bidii ya mazoezi ili kumshawishi kocha kuwa niko sawasawa 100% lakini hilo halikueleweka nikaendelea kubaki benchi bila maelezo ya kujitosheleza kwanini niko benchi hasa mechi ya pili tuliocheza na Ivory coast nilikuwa niko tayari kimwili na hata kiakili kwa aslimia 100 kucheza mchezo ule lakini sikupangwa.

HARUNA MOSHI (Boban)
Kucheza kwenye mashindano makubwa kama yale imekuwa ni ndoto ya kila mchezaji duniani kwahiyo kupata nafasi kama ile huwa ni bahati na kila mtu huwa anajitahidi kuonyesha kiwango chake chote ili ikiwezekana apate nafasi ya kwenda kucheza mpira wa kulipwa popote duniani kwani kunakuwa na wawakilishi wa vilabu mbalimbali vya nje kuja kuangalia wachezaji wanaoweza kuwafaa.
Siku ya mechi ambayo tulicheza na Ivory Coast nilipangwa lakini nakiri nilicheza chini ya kiwango ila tu naomba watu waelewe kuwa haikuwa hivyo kwa makusudi kwani ilikuwa ni nafasi yangu ya kuonekana hivyo ilitokea kwa bahati mbaya sana na ninasikitika kwa hilo.

Baada ya mechi tukiwa kwenye mkutano wa wacheza kocha alinisema sana kupita kiasi (kwa karibu dk15 hivi) kitu ambacho hakikunifurahisha na kama hivyo haitoshi kwa muda wote toka siku hiyo nikawa hata nikimsalimia haitikii wala hataki kuniangalia machoni kwa kweli ni kitu ambacho kiliniumiza sana katika muda wote niliokuwa mashindanoni.

KEVIN YONDANI
Na mimi pia nakiri kuwa katika mechi ya kwanza nilicheza chini ya kiwango lakini kama alivyosema Boban kuwa ile ilikuwa ni jukwaa la sisi kuonekana duniani kwamba tunaweza endapo tukipewa nafasi.
Kwa hiyo kutokana na presha ambayo kwa kweli ilinizidi nikajikuta kuwa nimepania sana mpaka nashindwa kucheza kwa kiwango kile ambacho ninakifiria kichwani kwangu.

Baada ya mechi kwenye mkutano wa wachezaji kwa kweli hilo lilikuwa ni kosa kubwa sana kwa kocha wetu kiasi cha kushindwa hata kuvumilia na kunipa nafasi nyingi na hata kuongea au kusalimiana na mimi ilikuwa haiwezekani kitu ambacho nadhani haikuwa sawa nilistahili kupewa nafasi nyingine niweze kufanya kile ambacho kila mtu alikitarajia kutoka kwangu.

AMIR MAFTAH
Kwa upande wangu mimi kosa langu kubwa ni kuwa karibu na Athuman kwa hiyo na mimi nikajikuta nimeingizwa kwenye mkumbo huo, lakini ikumbukwe kuwa mimi na Athuman tumekuwa tukila na kulala pamoja toka wakati wa Serengeti Boys. Kwa hiyo n iwatu ambao yeye anapokuwa na matatizo kama haya mimi najisia angalau kumwambia neno hata moja ambalo litamfariji kwasababu ndie mtu ninemjua vizuri kuliko mtu mwingine kambini na siwezi kumtelekeza leo hasa wakati ambapo anahitaji kuwa na mtu wa karibu.
Kwangu mimi hilo lilikuwa ni kosa kubwa sana kiasi cha kutopangwa na hata kuwekwa kwenye list ya wachezaji wa akiba.

NURDIN BAKAR
Kama ilivyokuwa kwa Amir na mimi kosa langu kubwa ni hilohilo la kuwa karibu na Athuman na mimi pia nikaingizwa kwenye mkumbo huo, lakini Mimi, Amir na Athuman tulikuwa kulala pamoja Serengeti Boys, Simba na hata sasa Yanga kwahiyo niwatu ambao mmoja wetu anapokuwa na matatizo tunakaa kama kitu kimoja kuongea na pia ifahamike kuwa hata wazazi wetu wanafahamiana kwahiyo tunapoongea ni kama watoto wa familia moja, lakini baada ya kuona kuwa kocha hafurahii uhusiano huo nikaona wacha nijitoe kwa muda na ndio angalau nikapata nafasi ya kucheza.

MWINGINE
Haya yaliyotokea pia yamumuhusisha Godfrey Boni ambaye sijui ni kwanini Kocha aliamua kumuingiza kwenye sakata hili labda anaweza kueleza vizuri (Kocha) endapo akiulizwa.

MATUKIO YA IVORY COAST
Sisi wachezaji ambao tulikuwa katikati ya sakata hili yalitukuta yafuatayo:
Tulitolewa kabisa kwenye Program ya mazoezi ya timu tukawa tunafanya mazoezi wenyewe pembeni (kwa wale waliokuwepo wanaweza kuwa mashahidi wa hili).

Tulitolewa kwenye mazungumzo ya timu kwa sababu kocha alisema anataka kuzungumza na wachezaji wake tu, ikabidi sie tutoke waongee.

Kocha alimwambia Katibu kuwa sisi asiotutaka turudshwe nyumbani ndege ya kwanza itakayopatikana kitu ambacho katibu hakukubali na hata Waziri alipoambiwa kasema yeye ndio kiongozi wa msafara kwahiyo ndie anaeamua ni nani anarudi na nani anabaki kwahiyo hakuna mtu atakae rudi nyumbani kabla ya mashindano kuisha.

UWANJA WA NDEGE DAR ES SALAAM
Baada ya kufika uwanja wa ndege waziri Mkuchika alituita (Boban na Chuji) na kutuuliza kilichotokea tukamueleza yote bila kubakiza.
Baada ya hapo tukaamua kuondoka kurudi makwetu kitu ambacho watu wengi waliona kuwa sio sawa kwa hiyo kwa ajili yao tunawaomba radhi kwa hilo lakini ikumbukwe kuwa sisi ni binadamu na yote yaliyotokea Ivory Coast yalitutesa kwa kipindi chote tulichokuwa huko tukaona hatuna hata haja ya kuwa na watu ambao hawakutaka kuwa na sisi, kifupi ni kwamba hatukutaka kuwa wanafiki na kuvaa tabasamu la plastiki.

MWISHO
Tunatoa shukurani zetu za dhati kwa Katibu wa TFF Frederick Makalebela na Mkuu wa msafara Mh. Muhammad Seif Khatibu wa kutumia busara ya hali ya juu wakati wote wa mtafaruku huu na tunawaambia kuwa huo ndio moyo wa kimichezo na kizalendo.
Tunaimani endapo wakiendelea hivi basi Nchi yetu itafika mbali kwa Tanzania ni Kubwa kuliko mtu binafsi awae yeyote Yule.

Hayo ndio yaliyotokea Ivory Coast na tunaomba mzee wa tovuti ya jamii uwasilishe kilio chetu kwa watanzania na tumeamua tutoe leo kabla ya wenzetu kuondoka kwenda mashindanoni Misri na kama kuna mtu yeyote anasema kuwa haya tuliyoandika sio kweli basi awasilishe maoni yake ili watanzania wajue mbivu na mbichi.

Unaweza kuwasiliana na sisi kuhusu hili kwa email (KAPUNI) Ila tunaomba usiichapishe hii email address kwenye mtandao wa jamii.

Asanteni sana
Haruna;
Athuman;
Kevin;
Amir;
Nurdin;
Godfrey.​
Source: Michuzi Blog
 
Kireka una uwezo wa kuwaleta wafaransa au yale yale ya ku critisize hata mfanikio madogo yaliyopo. Unajua hapa tuwe wakweli, sifia kilichofanyika, kama wewe umefuzu kwenye kushauri nenda kamshauri afanyeje siyo kukimbilia kwenye vyombo vya habari kuzungumza utumbo wa kuku eti huoni mafaniko.

Kiukweli huoni mfafanikio??? Nyie ndo wale mnataka watoto wenu watembee bila kutambaa haiwezekani.
 
Mkuu hebu soma barua waliyoandika akina Yondani, Amiri, Godfrey, Chuji, Boban nk. halafu weka na ya kaseja ukimaliza useme muachieni mwalimu afanye kazi... [IKO MICHUZI BLOG]

hapo siafiki, kwani kocha wa mpira mwenye chuki [kama walivyoainisha wachezaji kwenye barua yao] ni sawa na mabosI wabaya maofisini WENYE CHUKI KWA BAADHI YA WATU(tunawaona kila siku) ni sawa na mawaziri au wanasiasa wenye chuki... tunao kila siku nk. NI SAWA NA NDUGU WENYE CHUKI... NA HASA PALE AMBAPO UNATAKA KILA MTU AMTENGE M'BAYA WAKO, LA HASHA

Kwa maoni yangu, Maximo has lost power over his first half team and that never brings success hata kama ingekuwa brazil, pamoja na ubora wake nafananisha na mfalme alipoteza wafuasi; none of his tactics will work

Scolari, Hullier, Hoddle, Schuster, etc

Barua nimeiona na kwa kifupi tu kuwa wamejidhalilisha kabisa na adhabu waliyopewa wanastahili kabisa. na vilevile sioni sababu za kuendelea na mjadala ikiwa tayari wenyewe wamekiri kufanya mambo kinyume na profession inavyotaka.

Kitendo chochote cha kuhujumu timu kinatosha kabisa kuwafukuza kwenye timu hao vijana. Haiwezekani wachezaji, wako mstari wa mbele kwenye mapambano wanafanya mashara kama wako kwenye sherehe ya kupaka hinna au kitchen party?

Maximo aendelea na wale ambao wanajua faida ya kusikiliza mwalimu nini na aendelee kututengenezea wengine.

Whoever is going to misbehave will be responsible and have to be fired immediately.

Hao vijana na nie washauri wao wengi ni muhimu kuelewa kuwa, Professionals hufanya yale wanayotakiwa na wala siyo yale wanayotaka .
 
Barua nimeiona na kwa kifupi tu kuwa wamejidhalilisha kabisa na adhabu waliyopewa wanastahili kabisa. na vilevile sioni sababu za kuendelea na mjadala ikiwa tayari wenyewe wamekiri kufanya mambo kinyume na profession inavyotaka.

Kitendo chochote cha kuhujumu timu kinatosha kabisa kuwafukuza kwenye timu hao vijana. Haiwezekani wachezaji, wako mstari wa mbele kwenye mapambano wanafanya mashara kama wako kwenye sherehe ya kupaka hinna au kitchen party?

Maximo aendelea na wale ambao wanajua faida ya kusikiliza mwalimu nini na aendelee kututengenezea wengine.

Whoever is going to misbehave will be responsible and have to be fired immediately.

Hao vijana na nie washauri wao wengi ni muhimu kuelewa kuwa, Professionals hufanya yale wanayotakiwa na wala siyo yale wanayotaka .

Duh, hii kali, watu wanasema love is blind... KWELI UNA MAPENZI NA MAXIMUM;

aliyedhalilika ni maximo, yeye kama kiongozi amepata wapinzani na wanmuweka uchi... na kauli zake za chuki wabongo wamechoka..

Kiongozi wa serikali au ofisi nyingine akisemwa kwamba anapingwa then tunasema hafai, wachezaji wakigoma then wao ndio waondoke. hatuaondokana na utumwa wa fikra mpaka tugundue kuheshimu professionals... na hata mpira ni professional these days

Sina hakika kama imewahi kutokea wachezaji sita wakaandika yaliyoandikwa katika historia ya tanganyika... ukiona kunafuka moshi ujue kuna moto
 
aliyedhalilika ni maximo, yeye kama kiongozi amepata wapinzani na wanmuweka uchi... na kauli zake za chuki wabongo wamechoka..
Mkuu tumesikia maximo hafai hafai.....crap
kma ungekuwa na mamlaka na kwa ujuvi wao wa soka ungempendekeza nani achukue mikoba ya marcio?
Sina hakika kama imewahi kutokea wachezaji sita wakaandika yaliyoandikwa katika historia ya tanganyika... ukiona kunafuka moshi ujue kuna moto
sina hakika kama imewahi kutokea timy taifa ikapendwa kama kwenye utawala wa maximo....
 
Mkuu tumesikia maximo hafai hafai.....crap
kma ungekuwa na mamlaka na kwa ujuvi wao wa soka ungempendekeza nani achukue mikoba ya marcio?

sina hakika kama imewahi kutokea timy taifa ikapendwa kama kwenye utawala wa maximo....

Nisingependekeza yeyote kwasababu kuna jopo with technical abilities and skills to do that task,

kuhusu kupendwa ni kweli... but that wouldn't mean mapenzi ya yetu kwa taifa yalete mgawanyiko; hakuna national team inayopendwa kama england lakini hata kwao discipline is two way traffic and not top-bottom
 
Ni kweli Maximo amefanya kazi kwa kiasi chake hadi hapo alipofikia, tatizo ni pale baadhi ya wadau wanaotaka tuamini kwamba Maximo ni kocha wa aina ya pekee sana ambaye watanzania tumempata kwa mara ya kwanza. Kwa mtazamo wangu tatizo la soka yetu sio mwalimu bali mazingira (miundombinu) ya kufundishia, tulisha wahi kuwa na walimu wa calibre ya Maximo na walishindwa kufanya kazi kutokana na mazingira mabovu ya kufanyia kazi yaliyokuwepo kipindi kile. Kuna tofauti gani kati ya Maximo na Clovis de Oliveira (Brazil) au na Rudi Gutendorf yule mjerumani aliyekuja nchini miaka ya 80 mwanzoni? Maximo amepata bahati ambayo makocha wetu wazawa/wageni hawakuweza kuipata. Je ni kweli hatumbuki timu yetu ya Taifa iliyokuwa inaweka kambi Salvation Army, wachezaji wanakunywa maji ya bomba yasiyochemshwa? Timu iliyo katika mazingira hayo unategemea ifanye nini katika mashindano? Serikali ya awamu ya pili ilichoweza kufanya kwa timu ya Taifa ni kuitungia jina na kuiita kichwa cha mwendazimu, kwa msingi huo mwalimu mzawa afanye nini? Tuangalie tunapokwenda tusiende tunapoangalia!
 
Serikali ya awamu ya pili ilichoweza kufanya kwa timu ya Taifa ni kuitungia jina na kuiita kichwa cha mwendazimu, kwa msingi huo mwalimu mzawa afanye nini? Tuangalie tunapokwenda tusiende tunapoangalia![/QUOTE]

Magehema, ndiyo maana kuna haja pia ya kuitafutia jina jipya hii Timu yetu ya Taifa. Wataalamu wa Masoko watakubaliana na mimi kwamba jina nalo huwa lina mchango wake kwenye mafanikio (mazuri au mabaya). Angalia mfano huu, kuna watu wanaamini kwamba Msanii wa mziki wa Bongo Fleva almaarufu kama Dudu baya amekuwa akipatwa na mikasa ya mara kwa mara kutokana na kuchagua kutumia jina Dudu Baya. Lakini kutokana na kuwa na jina jingine la Tumaini, ndilo huchagiza kumpunguzia mikasa hiyo
 
[QUOTE Kocha ni zaidi ya kufundisha, manake anatakiwa kuwa kama Mzazi.

HILI NALO NENO
 
Jamani jamani, hivi hamuoni kwamba Maximo ni failure????. nashangaa sana wachangiaji humu wanavyosema ati hatuna shukurani kwa alipotufikisha Maximo. katufikisha wapi????, Hivi wewe ikiwa safari yako ni ya kufika Dodoma na ukanunua vyote vinavyoweza kukufukisha Dodoma, na mwishowe ukaishia Chalinze hata morogoro hujafika utajisifia kufika chalinze tena kwa wiki mbili badala ya masaa tu?
nasema hivyo ajili Maximo kapewa kila alichotaka na hata zaidi kutoka kwa TFF na wadhamini na wadau wengine lakini mafanikio ni 20% ya alichostahili kufanikisha je tumsifu, hivi do we need 20% of performance from him kwa support anayopata?.
Mfano mdogo tu kama mtakumbuka enzi za Serengeti boys na Kibadeni wakitembeza bakuli kupitia ITV na matokea yalionekana kwa muda mfupi tu, sasa hivi tunawachezaji maarufu waliotokana na serengeti boys na hata maximo anawatumia baadhi.
Hakika sijaona kikubwa alichofanya Maximo.

Nadhani Mart Nooj ndo katufikisha mbali ukilinganisha na Maximo.
Tutakukumbuka Daima Maximp
 
Back
Top Bottom