Samweli sitta ni zaidi ya raisi kikwete

Ndio ni jasiri tena sana, ukiwa na Profile zuri ndani ya nchi hiii husiti kusema chochote maana hao CCM hawawezi kukukamatia chini
 
No body swims in a muddy pond and get out of it clean!!!!! Provided yuko CCM.... I still have doubts about him....
 
Siku zote nimekuwa nikimuunga mkono Samuel Sitta kwa mtazamo wake kuhusu maendeleo ya nchi yetu. Kuna wakati nilitafuta fursa ya kukutana naye na kufanya naye mazungumzo. Kwa kweli ni mtu anayeonesha kukerwa na ufisadi kutoka moyoni kabisa. Ni mtu ambaye anaamini nchi yetu inaweza kusonga mbele iwapo raslimali za nchi zitatumika ipasavyo. Kwa mtazamo wangu, Sitta ni kama mpiganaji Dr Slaa. Naamini wawili hawa wangeunganisha nguvu na na hata ikatokea kwamba wanaunda serikali nchi yetu ingepaa sana kimaendeleo. Tuache kuiga majungu yanayoenezwa na akina Lowasa, Chenge na Rostam kuhusu mpiganaji huyu shupavu. Angalia, yupo ndani ya serikali lakini anakosoa yale ambayo anaona hayaendi sawa. Big up Mzee Sitta!
 
Sitta ni mwanasiasa mjanja (smart) anayesoma alama za nyakati na kutumia fursa kutoa kauli muafaka kulingana na mazingira yaliyopo. Ana uchungu na nchi? Hii ni kauli ya kuitumia kwa tahadhari sana linapokuja suala la wanasiasa. Ni wachache sana unaoweza kuwaamini kwa hilo. Kuhusu kumzidi Kikwete - sijui tunapimaje hapo. Maana Sitta zake ni kauli wakati Kikwete tunaangalia maamuzi - vitu viwili tofauti.
 
Tangiapo na itabaki hivyo sikuzote.

Wana Jamvi, kwa mtazamo wangu sita ni mzalendo wa kweli mwenye uchungu na nchi yake
kwasababu kuu zifuatazo:
-Uwezo wake kama spika kuruhusu mijadala ambayo imeweza kutishia uhai wa ccm.
-Kuto wogopa mafisadi wenye fedha ambao wanaogopewa.
-Kukataa kuwaangukia mafisdi.

Nani asiyekumbuka jinsi ndugu Sitta alivyoweza kuruhusu mjadala wa richmond bungeni, ambao umeleta kitimutimu kufikia hatua ya EL kujiuzuru? kutoka na mkasa huu ndipo tulipojua udhaifu wa ccm, wengine tulikuwa hatujuhi.
Sitta aliweza kushikilia msimamo wake wa kuwashambulia mafisadi bil kuigopa, inahitaji ujasiri kwa kweli kwani kama waziri mkuu mizengo pinda mwenye ulinzi madhubuti aliwagwaya mafisadi kwa kusema ni watu hatari, lakini Sitta aliendeleza mapambano nao.
Kitendo cha Sitta kukataa kuwaomba radhi mafisadi mbele ya kamati ya usuluishi wa ccm ni kitendo cha ujasiri.
Kweli sitta ni mzalendo mwenye uchungu na nchi yake na ni zaidi ya raisi, kitendo cha kikwete mtu ambaye yupoyupo asiyejali chochote kumpa uwaziri sitta ni ukweli tosha kuwa sitta ni zaidi y raisi.
 
Hata huyo Dr Slaa sio msafi mkienda kwenye database ya kanisa mtaona madudu yake, na ni aibu kwa mtu mzima mwenye umri kama Dr Slaa mwenye kuijua dini awe anavunja amri ya sita!

Binafsi kila mmoja anamawaa yake na kila mtu ana sifa zake.
Mkuu Zimwi la DR Slaa bado linakuandama, Hapa anasemwa sitta wewe unamuingiza Dr Slaa. Madrasa bwana!
 
Hamna mwana ccm hata mmoja ambaye ni mzalendo na ana machungu na taifa letu. hao wote ni wezi wanaopiga kelele ni wale waliokosa njia za kuiba.
 
Back
Top Bottom