Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Picha ya kwanza:
Mkuu wa Mkoa Dodoma akiongoza maandamano ya kuchangisha pesa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya watawa wa shirila la Mt. Gemma Galgani jimbo Katoliki dodoma.
Picha ya pili:
Mheshimiwa Swamweli Sitta aliyekuwa mgeni wa heshima katika kuchangisha pesa za ujenzi wa nyumba ya watawa akimsalimia Askofu mstaafu Mathias Isuja wa jimbo katoliki Dodoma.
Kuna kitu ambacho najifunza katika matukio haya yanayoendelea katika kuhamasisha watu kuchangia maendeleo, vyama vya siasa na mashirika mbalimbali.
Kuna dalili za wazi wafadhili ambao tulizoea kuwa nao ambao wamesaidia mengi kwa sasa hali ngumu ya uchumi inayoikumba dunia wameanza kuadimika, na njia pekee ni sisi wenyewe kushikamana na kuwasaidiana kwani uwezo tunao, sababu tunazo, tukiunganisha nguvu tutaweza.
Chadema wamekusanya mamilioni katika harambee yao pale Dar, Samweli sitta kakusanya kadhaa leo hapa Dodoma, na kwengineko tukiendelea na moyo huu huu tutafika mbali kuliko kupitisha bakuli huko nje na hivyo kupambana na masharti magumu ya mikopo yao yenye riba.
Rais Mkapa alifanikiwa kuanzisha mradi wa maji ya Ziwa Victoria kuja Shinyanga na mikoa mingine ya kati, hali kadhalika ujenzi wa Daraja la Tanzania-Msumbiji. Aliweza kwa nini tusifuate nyanyo hizo?