Samwel Sitta ampiga bao Lowassa urais 2015

Mkuu, ujue JF sio sehemu ya porojo sasa wewe unajifungia ndani na Laptop yako unaandika tamthilia ya kihindi halafu unaleta JF..

Rudi tena ukajipange upya na tread yako nyepesi!
 
Kweli katika maisha kuna kitu kinaitwa Proffessional and Amateur, Au Kuna Kitu Kinaitwa legelege au Ukomavu...!
Kamanda Samwel Sitta Ameonyesha Ukomavu wa kiasa pamoja na uwezo mkubwa sana baada ya kuweza kuwaweka chini mahasimu wawili GODBLESS LEMA na GAUDENCE LYIMO (meya wa jiji la Arusha) Kitu ambacho hakuna kiongozi mwingine aliyedhubutu kufanya hivyo!

Na kweli kama amani itatokea tena Arusha basi SITTA ndio atakuwa amefanikisha kwa asilimia mia moja!

Napenda niseme Samwel Sitta Ndio Kiongozi kwa mambo yafuatao

+Ana Msimamo usiopindishwa,Kama ishu ya dowans Amekuwa na Msimamo thabiti
+Ni kiongozi jasiri,shupavu, kama kwenye uchaguzi 2010 alijitoa mhanga kwa CCM Ajitose kwenye mdahalo na Dk.Slaa
+Ni Kiongozi aliyewashughulikia mafisadi ipasavyo kwa kuruhusu mijadala ya bungeni ambayo iliwaaumbua mafisadi

Huyu ndio Samwel Sitta Kiongozi Jasiri Anayemnyima usingizi Ngoyai...,Sitta Anatumia Akili Wakati Ngoyai Anatumia Pesa Tutaona NANI ATAKUWA MSHINDI...

hakuna mtu mwenye akili nzuri akatokea Tabora.
 
Afadhali sasa hivi kila thread inaihusu CCM..CDM imeanza kupotea kwenye jukwaa letu la siasa.

huu ndio uzuri wa mods na ndiyo utam wa JF...............hata wanaobandika pumba wanapewa premium status.
 
upatanishi wa meya na mbunge unapatikana kanisani hii kali!au walimuogopa askofu? FF,MS mkiambiwa nchi inaendeshwa na kanisa mnabisha?

Kama serikali imekosa hekima basi kwa Mungu hekima haijaisha, na Kanisani ndipo mahali pa upatanisho, maana Biblia inasema jua lisichwe ukiwa na jambo moyoni na nduguyo. Hii ni sawa na naipenda, siyo ile ya wenzetu kutwangana bakora humohumo.
 
Mh! Ushabiki mwingine bwana?! Sifa za kijinga kabisa

mjinga mwenyewe, kama unaushabiki wa sifa za hekima zishushe tuzipime tukuambie kiwango. Sitta ndo mwenyewe ukimpambanisha na Fisadi Lowasa labda kama unataka kumpambanisha na mtu mwingine, mseme tumpime then tutakujibu. Acha hizo.
 
Mh 6 anafaa sana kuwa PRESIDENT Kwa sababu ni mtu mwenye hekima na busara pia.Tatizo linalomsumbua Mh 6 ni chama chake ccm kimejaa unafiki na majungu hakipendi mtu yeyote mpenda haki na usawa.
 
Sitta ni mnafiki namba mmoja kutokea Tanzania

ANAISHI KWENYE NYUMBA YA SPIKA
ALIONGEZA MARADUFU MARUPURUPU YA WABUNGE
ALIZIMA DOWANS
ALIUNGA MKONO POSHO
ALIANZISHA CCJ
ALIJIJENGEA JENGO LA USPIKA KWAO


acha unafiki wewe, sitta ni kiongozi shupavu anaehitajika katika nchi hii. we endelea kubaki na ulimbukeni wako wa kuwa kibaraka wa edward. huna jipya kazi yako ni kuendeleza unafiki tu, wewe pamoja na huyo lowasa wako wote ni wezi
 
hakuna mtu mwenye akili nzuri akatokea Tabora.

Acha ujinga wewe' hv watu wengine huwa mnawazanin? Ni mpumbavu tu ndiyo anaweza kutukana jamii nzima ya watu bila uchunguzi' mtemi Milambo,Mtemi Isike na Chief Fundikira unawajua hawa? Makwaiya wa Kuhenga na Prof Lipumba unawafahamu? Unajua kuwa kura tatu (UAMUZI WA BUSARA) Ulifanyika Tabora?
 
Watanzania wenzangu. Tumeingia kwenye mtego wa kushindaniana uongozi tu? Yaani leo hii badala ya watu kushughulikia mikakati ya maendeleo, tunaangalia uchaguzi wa 2015! Sikatai kuangalia uchaguzi, ni sawa, lakini sio muda muafaka. Kwa sasa tunapaswa kushughulikia miradi ya maendeleo, uchaguzi ukifikia wakati wake tutafanya tu. Jamani tutafakari, tubadilike, na tuchukuwe hatuwa. Ndio maana WaTz tunabaki kuwa omba omba tu.
 
acha unafiki wewe, sitta ni kiongozi shupavu anaehitajika katika nchi hii. we endelea kubaki na ulimbukeni wako wa kuwa kibaraka wa edward. huna jipya kazi yako ni kuendeleza unafiki tu, wewe pamoja na huyo lowasa wako wote ni wezi

Ushupavu wa kuwa na vimada labda
 
Vp kalam imeisha wino ama ndio hizo tu cfa za cta ? Pole ila utakuwa mjinga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom