Elections 2010 Samuel Sitta: Kura Zihesabiwe Mitaani

Ng'wanangwa

JF-Expert Member
Aug 28, 2010
10,827
4,172
Nimeskiza mahojiano ya kati ya watu wa radio one na Bwana Samuel Sitta.

Analalama utaratibu wa NEC wa kutaka "matokeo yajumuishwe kwenye majengo imara ya serikali". Anasema ndo chanzo cha ucheleweshaji matokeo. Anatoa ushauri kuwa kura zihesabiwe kwa mtindo wa kuweka uzio wa makuti, kuzungusha kamba, na kuweka askari kadhaa. Kuweka meza katikati, kumwaga kura juu ya hiyo meza na kuanza kuhesabu.

My take:
Sitta anataka kuturudisha enzi za mwaka 47. Tulishatoka huko. Majengo yanavamiwa na nguvu ya umma, sembuse makuti??
 
mzee hapo alikuwa na point, tatizo kubwa linalotokea hapo ni siri inayofanyika ndani ya hizo nyumba imara za kuhesabia kura, hapo nipo kwenye ugonvi mkubwa na ndipo kwenye wizi wa kura,

kama nchi yetu ingekuwwa inafanya mambo mengi kwa usawa na haki hilo la kuhesabia kura ndani wala lisingekuwa tatizo, Chaguzi nyingi za nyuma ilikuwa watu wanaenda kwenye mikutano na hawapigi kura sahihi, lakini sasa watu wameamka, jiulize kwa nini maeneo mengi CCM waliposhinda hakuna anaelalalmika na kwa nini pale kwenye upinzani wa kwel;i ndipo kwenye malalmiko?

NEC hawako huru na watu hawana imani nao, na ili kutoa mzizi wa fitina kura zinapaswa kuhesabiwa hadharani kila mtu aone, kama kushindwa ama kushinda iwe hadharani
 
Nadhani anachotaka kusema ni kuwa hakuna uwazi wakati wa majumuisho na hiyo inaweza ikakaribisha wizi wa kura.
Analenga kutetea vyama vya upinzani kwamba kura zao zinaibiwa .... nahasa analenga kura za urais!!
 
Nadhani anachotaka kusema ni kuwa hakuna uwazi wakati wa majumuisho na hiyo inaweza ikakaribisha wizi wa kura.
Analenga kutetea vyama vya upinzani kwamba kura zao zinaibiwa .... nahasa analenga kura za urais!!


Bravoooooo! inside of his option there is the TRUTH which he want us to know and ukiwa na akili ya kumsoma vizur utamwelewa!:smile-big::smile-big:
 
Katusaidia njia mbadala ya kuondokana na hili balaa la uchakachuaji.
 
Nadhani anachotaka kusema ni kuwa hakuna uwazi wakati wa majumuisho na hiyo inaweza ikakaribisha wizi wa kura.
Analenga kutetea vyama vya upinzani kwamba kura zao zinaibiwa .... nahasa analenga kura za urais!!

Labda tuanze na hili la tume huru.

Lakini suala la kuhesabu kura 'ugani' tutakuwa tunasikia visa vya kuchomana visu na kukatana mapanga kila leo.

Bado nina shaka kidogo.
 
Labda tuanze na hili la tume huru.

Lakini suala la kuhesabu kura 'ugani' tutakuwa tunasikia visa vya kuchomana visu na kukatana mapanga kila leo.

Bado nina shaka kidogo.

jana kura zimehesabiwa ndani na ofice za mafisadi zimechomwa moto pia, kwenye haki weka haki
 
Hapo suruhisho ni Katiba mpya ambayo itaunda Tume huru ya Uchaguzi, Otherwise hakuna kitu.
 
Hana lolote. anataka kujipendekeza kwa upinzani wamchague tena kuwa spika
 
Nimeskiza mahojiano ya kati ya watu wa radio one na Bwana Samuel Sitta.

Analalama utaratibu wa NEC wa kutaka "matokeo yajumuishwe kwenye majengo imara ya serikali". Anasema ndo chanzo cha ucheleweshaji matokeo. Anatoa ushauri kuwa kura zihesabiwe kwa mtindo wa kuweka uzio wa makuti, kuzungusha kamba, na kuweka askari kadhaa. Kuweka meza katikati, kumwaga kura juu ya hiyo meza na kuanza kuhesabu.

My take:
Sitta anataka kuturudisha enzi za mwaka 47. Tulishatoka huko. Majengo yanavamiwa na nguvu ya umma, sembuse makuti??

HIZO STANDARDS ZILIWEKWA NA MAFIUSADI KATIKA JIMBO LAKE TU ILI WAPIGA KURA WAKE WASIJITOKEZE KUMPIGA KURA, NA HATIAMYE WAMWANGUSHE KISIASA. KATIKA MKOA WA DAR ES SALAAM JIMBO LA UBUNGO KUNA ENEO VITUO SABA VILIWEKWA KATIKA UWANJA WA WAZI HAUNA HATA FENCE WAKAWEKA MAHEMA MAWILI AU MATATU KWA VITUO VYOTE SABA, AND THE TERRRAIN WAS NOT GOOD.

KURA ZIKAPIGA HAPO NA KUHESABIWA HAPO HAPO. HAPAKUWEPO VITI WALA KITU CHOCHOTE CHA ZIADA. ILIBIDI VITI VIAZIMWE BAA YA JIRNAI NDIPO SHUHULI IANZE.

TUME YA UCHAGUZI KUPITIA KWA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI AMBAO NI WAKURUGENZI WA HALAMASHAURI ZA WILAYA AMBAO NI WATEULE WA SERIKALI YA CCM HUPANGA VITUO VYA KUANDIKISHA WAPIGA KURA NA KUPIGA KURA KATIKA NAMNA YA KUHUJUMU WAPINZANI AU BAADHI YA WABUNGE WAA CCM WASIOTAKIWA KAMA SPIKA SITTA.

MATHALANI MOJA YA MBINU ILIYOKUWA IMEPANGWA KWA NIA YA KUMUANGISHA MHE JOHN MNYIKA NI WA JIMBO LA UBUNGO NI KUPANGA KITUO KIMOJ TU CHA KUJIANDIKISHA NA KUPIGA KURA KWA KWA ENEO LENYE UREFU WA KILOMITA 10 KWA UPANA WA KILOMITA 10 NA LIKIWA LIMESHONANA MAKAZI YA WATU KWA VIWANJA VYA MITA 20x20; KUTOKANA NA WAINGI WA WAPIGA KURA WALIOJIANDIKISHA KATIKA KITUO HICHO KITUO HICHO KIKAGAWANYWA KUWA VITUO SABA VYA KUPIGA KURA VYOTE VIKIWA SEHEMU MOJA TU KATIKA MAHEMA MAWILI TU.

HIVYO KUWALAZIMU WANANCHI KUTUMIA VYOMBO VYA USAFIRI KWA GHARAMA K.M DALADALA, TEKSI, PIKIPIKI NA HATA KUTEMBEA KWA MIGUU KWA KATI YA KILOMITA 5 HADI 10 KUJA KUJIANDIKISHA NA KUPIGA KURA.MATOEKO YAKE WASTANI WA WAPIGA KURA WALIKUWA NI KATI YA 140 NA 150 KATI YA WAPIGA KURA 500 KATIKA KILA KITUO KATIA YA HIVYO VITUO SABA VILIVYOWEKWA SEHEMU MOJA TUU.



INSHALAAHA JOHN MNYIKI AMEIBUKA KIDEDEA LICHA YA NJAMA ZA AINA HII.

KWA MAONI YANGU SPIKA SITTA HANA MORAL AUTHORITY KUZUNGUMZIA MATENDO HAYA YA SERIKALI YA CCM KWA KUWA NI JUZI JUZI TU ALIKUWA AKIITETEA
.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom