Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,063
- 22,755
Pathetic. Pamoja na kuwahifadhia bure, gharama za kuendesha kesi hawatachangia, na kama tukishindwa kwenye kulipa damages wataturuka kimanga! Halafu wakitubeza kuwa tunajipendekeza tunakasirikia nini?
Amandla.........
Aliyezoea vya kunyonga, vya kuchinja ataviweza ? Ngekewa ananikumbusha hadithi ya Maimuna wa bara !
Maimuna nenda kachange kuni
(Akiwa kajilaza)Haka mama naumwa mkono
Maimuna hebu kateke maji
(Akiendelea kulala)Hapana mama naumwa mguu
Maimuna kawashe jiko
Kweli mama naumwa mwili mzima
Maimuna kasonge ugali
Hakika mama simwezi hata kunyanyuka
Maimuna karibu mezani ule
(Akitoka mbio)Haya mama nakuja
Ngekewa kwa kupenda ngekewa naona hayuko peke yake ! Eti wanalilia samaki - labda kitakachofuata ni maandamano !