Samaki wa Magufuli wafufua mgogoro wa muungano?

Hivi mbona sikuwai kuwasikia toka siku wamekamatwa samaki hawa? iweje leo? ama kweli mchuzi mtamu jaman teh, teh, teh

bila shaka wako tayari kulipia na gharama za utunzaji kwa 40%, au sio ndugu zetu?


,,,,Kama serikali kamilifu,basi ni wajibu wa SMZ kuchukua jukumu lake hilo la kulipia pia GHARAMA za kuwatunza hao samaki kwa mgawano huohuo wa 40%, tatizo hata wakipewa percent hiyo ambayo inatambuliwa kisheria katika jumla ya tani 260 huko za hao samaki,ni mgao mkubwa kwelikweli,hivi na tatizo hili la umeme tutawatunza vipi hao,huyo waziri aache kutuhamishia "goal posts" sasa,tuna tatizo la msingi la umeme zanzibar,Serikali ya SMZ inatusaidia vipi kutoka hapa???
 
Huu Muungano una kero kweli kweli, ningekuwa na uwezo ningeuvunjilia mbali ili nchi ile cha kwao.
Hicho ndio kinachotakiwa, sio kama Zenji wanataka hao samaki waliotoka kwenye mafriza.

Zanzibar wamezungukwa na bahari, ni sehemu ambayo watu wake wako very picky kwenye masuala ya vyakula.Mwananchi ananunua samaki alietoka kwa mvuvi sasa hivi, tena anachagua hadi macho ya samaki yako vipi.Kama yamelegea anakataa, anakwambia huyo amekaa sana hamtaki.

Sema Zanzibar imechoshwa na muungano, uvunjwe tuu au tutaendelea kufanya vitimbi vya namna hii!

Na wala bado, ndio kwanza ngoma imeanza 2010!
 
samaki%20wa%20magufuli.jpg
Samaki wenyewe ndio hawa
 
Wazanzibari bwana, chao kinakuwa chao wenyewe wala hawatushirikishi, lakini chetu wanataka asilimia 40? Zanzibar kuna watu wasiozidi milioni moja, bara tuna watu milioni 40 halafu watake asilimia 40? Hivi hawa siyo wachawi kweli?
Ninachojua mimi ni kwamba watanzania wote walitangaziwa kuomba hao samaki iwapo wanawahitaji, sasa wenyewe hawakuomba, wanataka wapelekewe? Wao ni akina nani hadi tuwabembeleze hivyo? Sometimes huu muungano ni kero tupu. Uvunjike tu wala hautusaidii. Nichagueni mimi niwe Rais ili niuvunjilie mbali huo muungano.

Mawazo potofu tu tunayoyaweka mbele. Kwani mipaka ya bahari inagawiwa kwa wingi wa watu?
 
Duuh, nimetoka kupata msosi huku kitoweo kikiwa ni samaki hao wa makufuli. Naona wanaolalamika watakuwa wamechelewa kwani ndo wanaliwa hivyo !!
 
Hawa wamezungukwa na maji kila upande, na chakula chao cha kila siku ni samaki, lakini hawaridhiki hadi wawapate hao wa makufuli...huu ni utoto dizaini...huh!
Au watu wa pwani nielezeni, jodari ni mtamu kuliko CHANGU?



Mmekuwa mnakula vilivyo vyenu (madini na gesi) wao wakinyamaza basi hata hawa samaki waliovuliwa kwao wanyamazee? Mnapogosha shuka sana nyie!
 
Omba Mungu Muungano udumumu ili muendelee kunufaika na vya Bahari Kuu lakini ukivunjika leo tunarudisha mipaka-Please ielewe mipaka ya Tanganyika yako katika Bahari ya Hindi!!!!! Watu wanachojivunia ni Tanzania na siyo Tanganyika na Tanzania haiwezi kuwepo bila nchi Zanzibar. Hivi hujafahamu tu wale wa Maandalizi (Nursery)wanafahamu hivyo.

Zidumu fikita za Kada Pakacha!
 
naomba kufahamu,
Eneo la bahari ambalo ni sehemu ya Zanzibar linafikia asilimia 40?



Katika akili yako ukishatoka visiwa vya Zanzibar kuelekea baharini kuna umbali gani kabla kuingiliwa na mipaka ya nchi nyengine?

Hatafu angalia Tanganyika kuelekea baharini ina masafa gani kabla ya kukutana na nchi nyengine kama Msumbiji na Kenya. Kama ulisoma hesabu shule ya msingi hiyo inatosha kukupa jawabu.
 
Walianza kumalizana na kushikana uchawi wenyewe kwa wenyewe sasa wameshaeneza sumu mpaka bara.
Nilishasema kuwa ktk kipindi hiki kuna jambo tena la siri linaendelea kupangwa huko zenji kama tusipokuwa makini na hawa wazee wa chaza watakuja na kitu ghafla na tutashindwa pa kutokea.
Muungano kwao si mali kitu tena kwani nje ya muungano wanaweza kutengeneza usultani wa kutawala milele visiwani. hawapendi kupokezana madaraka hawa.
Yangu macho


Macho yako itabidi uyakodowe sana kwani huko kumalizana naona kuko Bara sasa, umeyasikia ya waraka orijino na waraka feki?
 
UNAWEZA KUTUSAIDIA KITU KIMOJA KAKA...!tunaomba wewe au INVISIBLE mui-upload sheria ya muungano hapa!...tunaweza jadili kwa hoja za msingi

Naona unaomba kitu adimu sana juu ya muungano wetu na kwa kawaida hata ukiletewa basi utakuwaq na saini mya upande mmoja tu!
 
Hivi mbona sikuwai kuwasikia toka siku wamekamatwa samaki hawa? iweje leo? ama kweli mchuzi mtamu jaman teh, teh, teh

bila shaka wako tayari kulipia na gharama za utunzaji kwa 40%, au sio ndugu zetu?

Ilikuwa waseme hao watu wasikamatwe? au waseme kitu gani?
Ama hilo la malipo kwani hizo pesa si za Muungano? Mbona ni wagumu kufahamu?
 
waziri Hamza wa zanzibar leo kwenye Tv anasema zanzibar inastahili ipewe share ya 40% kwa sababu sheria inasema hivyo.

jee huu ni mgogoro mwengine ktk muungano?

jamaa anasema waziri magufuli alikuwa anatakiwakae na mwenziwe kabla ya kuamua lkn katumia ubabe kwa hio wao watakaa na waangalie cha kufanya

Huyu naye kituko tu! Sasa kwani kama aliliona hilo kwa nini asingemwambia kabla ya kutoa maamuzi! Au alikuwa anamtegea akishasema tu na yeye aranduke na maneno yake ili watu wamuone na yeye yupo Khaaaaa aende zake bana
 
Halafu Magufuli alisema samaki wataliwa na watanzania sio kuuzwa ila ni zile taasisi zilizopendekezwa yaani magereza, shule, mahospitali n.k au wao Zanzibar sio Watanzaniia mbona hawakupeleka hayo maombi yao basi? Au ndio hivyo kutafuta choko kila kukicha kwa kisingizio cha Muungano?

Walipokamatwa hawakusema, waliposemekana watauzwa hawakusema, kesi iko mahakamani wachangii hata mawazo hata kutoa sifa kwa Magufuli kwa kazi kubwa aliyofanya ya kukamatwa kwa hizo samaki, Taasisi zinazotaka samaki wa bure leteni maombi na muda maalumu umetolewa hatujasikia taasisi za Zanzibar zimepeleka maombi ndio kwanza nasikia wanataka mgao wa 40% kama nani? Zanzibar au Taasisi iliyopo Zanzibar au watanzania wa visiwani au tena ni masuala ya Muungano. Mmh mimi sielewi.

Una maana kuwa Zanzibar ni sawasawa na taasisi kama magereza au vipi? Huo unaozungumza wewe ni udhalilishaji kwa sehemu moja ya Muungano na halafu hiyo tani 80 iliyopelekwa na Magufuli ilipelekwa kwa misingi gani iwapo Zanzibar kama Taasisi haikufata utaratibu wa kuomba?

Hilo la kesi ulitaka kufunguliwe kesi ngapi au mawaziri wangapi wawe wasemaji wa suala moja?

Mbona mnatufanya tuanze kufikiria uwezo wa wengine kufikiri?
 
Huu Muungano una kero kweli kweli, ningekuwa na uwezo ningeuvunjilia mbali ili nchi ile cha kwao. Naanza kuona kama vile Mtikila alikuwa sahihi kudai kuwepo kwa taifa la Tanganyika ambayo ingekuwa ni njia nzuri ya kuelekea kuvunja muungano huu.

Baadaye hata Tabora nao watasema ilikuwaje samaki hao waishie Dar tu wakati Tabora nayo ni saehemu ya Tanzania? Hili dai la kutaka mtu atoke Zanzibar aje Dar kujadili swala la matumizi ya samaki wale, kitu ambacho kinaweza kutolewa maamuzi na mtu mmoja kama ilivyotokea ni kuonyesha jinsi gani tunavyopenda kutumia muda na raslimali za serikali vibaya.

Unaonaje mtu mmoja huyo angetoka Zanzibar kwanza Mnyamwezi anajuwaje jodari kuliko mtu wa Zanzibar? Ama Kambare nakubaliana nawe huyo mtu angetoka Tabora.
 
Back
Top Bottom