Platnam
JF-Expert Member
- Mar 1, 2011
- 767
- 1,213
Sam Mahela-ITV
Hamjambo ndugu zangu? Poleni na shughuli za kila siku? kuna story ya abiria wa treni ya reli ya kati walokuwa wakisafiri kutoka jijini Dar es Salaam kwenda Morogoro,Dodoma,Kigoma ,Mwanza na maeneo mengine na kutelekezwa katika eneo la pugu kwa saa 16 na shirika la reli Tanzania niliyoitoa jana kupitia Itv, imesababisha kupigiwa simu na watu wawili ambao hawakutaka kutaja majina yao na kunitishia kwamba watanifundisha adabu kutokana na kuripoti habari hiyo huku wakihoji eti kwanini nilitoa habari hiyo kwenye Itv wakati vyombo vingine vya habari hawakuripoti story hiyo?
Licha ya kujitetea kwamba siwezi kuacha kufanya habari yeyote eti kwasababu vyombo vingine vya habari haviripoti habari hiyo hawakutaka kunisikiliza zaidi ya kuongeza vitisho dhidi yangu. Sasa ninachojiuliza hivi kwa hali ya abiria walivyokuwa wametelekezwa na kuachwa ktk eneo ambalo hakuna huduma za kijamii huku baadhi ya mabehewa kujaa wadudu na baadhi watoto, wazee na wagonjwa wakiwa katika hali mbaya ni sawa? Hivi sisi wanahabari tusipoonyesha haya nani ataonyesha ili jamii iweze kujua namna ambavyo shirika la reli isivyojali wateja wake?
Licha ya kutoa taarifa polisi kutokana na vitisho hivyo na nimewasilisha namba za simu walizotimia kunipigia lakini mimi binafsi kama SamMahela nikiwa nawakilisha Itv sitaacha kuripoti au kuandika habari yeyote eti kwa kuogopa kuuwawa au kwa kutishwa na mtu awaye yeyote eti kwa kufanya hivyo tutawaharibia baadhi ya watu katika nafasi zao.
Nitaendelea kufanya kazi zangu kwa mujibu wa sheria na utaratibu wa kampuni niliyoajiriwa na kwa kuwa MUNGU amenipa nafasi hii nitajitahidi kusimama katika nafasi yangu nikiwa bado hai bila uwoga wowote ili siku maisha yangu yakimalizika hapa duniani basi nami nije niende mbele zake nikisena nilitumia nafasi yangu kutetea watu,kusaidia wahitaji na hata kutumia nafasi yangu kufichua mambo, nadhani itakuwa jambo njema kuliko kutoripoti habari kama ile eti kwa kuogopa kutishwa.
Nimeona niwashirikishe hili na MWENYEZI MUNGU anisimamie mie mwanae.....
Amina