Dingswayo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 4,019
- 2,923
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Salma Kikwete, amesema ushindi wa Kikwete katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana hauna dosari kama baadhi ya vyama vya siasa vinavyotangaza.
Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akizungumza na wanachama wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Dodoma kwa nia ya kuwashukuru kwa kazi kubwa waliyoifanya wakati wa kampeni ya Uchaguzi Mkuu mwaka jana.
Mama Salma alisema baadhi ya vyama vimekuwa vikitawanya maneno ya uwongo na kuulazimisha ulimwengu uamini kuwa walishinda katika uchaguzi mwaka jana.
"Wanataka waiambie dunia kuwa wao ndio walioshinda, hivi walioshinda wana asilimia 20,"alihoji Mama Salma huku akishangiliwa na wanawake waliofurika kwenye ukumbi huo.
Alisema watu wanaoeneza uongo huo wanashangaza kwa kuwa tofauti ya kura kati ya CCM na vyama vingine ilikuwa kubwa sana.
Alibainisha kuwa uongo unaoenezwa na wapinzani umekuwa ukiwachochea wananchi kukichukia CCM wakati ukweli ni kuwa CCM ndiyo iliyoshinda uchaguzi huo.
Alisema wengi wanaoshiriki katika uzushi huo ni watoto wao kwani wamebebwa na wao migongoni lakini sasa wanawazunguka kuwachafua.
"Wasione simba kalowa wakafikiri ni paka akitoa makucha yake watakiona" alisema.
Aliitaka Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), kutokuwa wanyonge kukemea mambo yanayofanywa na baadhi ya vyama vya siasa dhidi ya Chama cha Mapinduzi(CCM).
Alisema UWT ni moja kati ya Jumiya ya CCM hivyo ina haki ya kulaani kauli zinazotolewa na Vyama hivyo.
"Msiitegemee serikali peke yake kukemea haya hata nyie mnanafasi kubwa kwani serikali ni kila mtu,"alisema
Alieleza kuwa siasa za chuki zinazoendeshwa na baadhi ya vyama vya siasa hapa nchini dhidi ya CCM ni tabia ambayo haipaswi kuachwa bila kukemewa.
Alifafanua kuwa CCM haiwezi kupoteza muda kulumbana bali itatumia muda huo kujadili mikakati yake iliyojiwekea katika mkutano mkuu uliofanyika mwaka jana.
Aidha, alisema ili jumuiya hiyo iweze kuendelea kuwa imara inahitaji kuwa na damu mpya ambayo ni vijana wasomi.
Alisema nia si kuwaoondoa wanachama ambao ni wakongwe bali ni kuweka mchanganyiko ambao utawezesha kuwepo na kasi mpya.
CHANZO: NIPASHE
Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akizungumza na wanachama wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Dodoma kwa nia ya kuwashukuru kwa kazi kubwa waliyoifanya wakati wa kampeni ya Uchaguzi Mkuu mwaka jana.
Mama Salma alisema baadhi ya vyama vimekuwa vikitawanya maneno ya uwongo na kuulazimisha ulimwengu uamini kuwa walishinda katika uchaguzi mwaka jana.
"Wanataka waiambie dunia kuwa wao ndio walioshinda, hivi walioshinda wana asilimia 20,"alihoji Mama Salma huku akishangiliwa na wanawake waliofurika kwenye ukumbi huo.
Alisema watu wanaoeneza uongo huo wanashangaza kwa kuwa tofauti ya kura kati ya CCM na vyama vingine ilikuwa kubwa sana.
Alibainisha kuwa uongo unaoenezwa na wapinzani umekuwa ukiwachochea wananchi kukichukia CCM wakati ukweli ni kuwa CCM ndiyo iliyoshinda uchaguzi huo.
Alisema wengi wanaoshiriki katika uzushi huo ni watoto wao kwani wamebebwa na wao migongoni lakini sasa wanawazunguka kuwachafua.
"Wasione simba kalowa wakafikiri ni paka akitoa makucha yake watakiona" alisema.
Aliitaka Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), kutokuwa wanyonge kukemea mambo yanayofanywa na baadhi ya vyama vya siasa dhidi ya Chama cha Mapinduzi(CCM).
Alisema UWT ni moja kati ya Jumiya ya CCM hivyo ina haki ya kulaani kauli zinazotolewa na Vyama hivyo.
"Msiitegemee serikali peke yake kukemea haya hata nyie mnanafasi kubwa kwani serikali ni kila mtu,"alisema
Alieleza kuwa siasa za chuki zinazoendeshwa na baadhi ya vyama vya siasa hapa nchini dhidi ya CCM ni tabia ambayo haipaswi kuachwa bila kukemewa.
Alifafanua kuwa CCM haiwezi kupoteza muda kulumbana bali itatumia muda huo kujadili mikakati yake iliyojiwekea katika mkutano mkuu uliofanyika mwaka jana.
Aidha, alisema ili jumuiya hiyo iweze kuendelea kuwa imara inahitaji kuwa na damu mpya ambayo ni vijana wasomi.
Alisema nia si kuwaoondoa wanachama ambao ni wakongwe bali ni kuweka mchanganyiko ambao utawezesha kuwepo na kasi mpya.
CHANZO: NIPASHE