Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,342
- 6,467
Ukitaka kujua mambo yanavyokwenda ndani ya CCM, msikilize mama Salma, kwa jinsi asivyokuwa na uwezo mkubwa wa kupambanua mambo basi ya ndani yanatoka nje. CCM kumtumia Salma ni sawa na mwananke kwenda sokoni na nguo nyeupe ya kulalia!
Kwenye TanzaniaDaima 22/09/2010 anasema Mwantumu Mahiza amekosa nafasi ya kugombea ubunge kwa sababu ya majungu ya wanawake wenzake, sasa hii si inaonesha CCM hawafuati demokrasia bali majungu. Pili, anaji-contradict kwa kusema Mwantumu akuchaguliwa kuwa Naibu Waziri wa elimu kwa kufuata jinsia yake bali ni uhodari na uchapakazi wake, halafu anasema wanawake kukosa nafasi za uongozi 50/50 bungeni itakuwa ndoto. Sasa je, tunataka bungeni jinsia au uchapaji kazi? Je, Mahiza aliteuliwa kuwa waziri kujaza 50% ya wanawake au uchapaji kazi wake? Je, UWT imekuwa WAMA Foundation?
Kwenye TanzaniaDaima 22/09/2010 anasema Mwantumu Mahiza amekosa nafasi ya kugombea ubunge kwa sababu ya majungu ya wanawake wenzake, sasa hii si inaonesha CCM hawafuati demokrasia bali majungu. Pili, anaji-contradict kwa kusema Mwantumu akuchaguliwa kuwa Naibu Waziri wa elimu kwa kufuata jinsia yake bali ni uhodari na uchapakazi wake, halafu anasema wanawake kukosa nafasi za uongozi 50/50 bungeni itakuwa ndoto. Sasa je, tunataka bungeni jinsia au uchapaji kazi? Je, Mahiza aliteuliwa kuwa waziri kujaza 50% ya wanawake au uchapaji kazi wake? Je, UWT imekuwa WAMA Foundation?