Wadau, mimi ni mpenzi wa kipindi cha habari kinachorushwa na BBC kuanzia saa 3 kamili usiku kupitia Star TV. licha ya habari moto moto ambazo unazipata, pia kuna huyu mtangazaji anayeitwa Salim Kikeke.. Kifupi, jamaa ni jembe sana. Huwezi kuchoka ukiwa unamsikiliza au kumwangalia anavyotangaza.
Nimegundua licha ya technolojia waliyonayo BBC, lakini ubunifu unahusika kwa kiwango kikubwa sana, kumfanya mtazamaji au msikilizaji aweze kuendelea kufatilia matangazo. Kwa watangazaji wa hapa bongo, ni vipindi vichache sana ambavyo unaweza kuvutika kiasi hicho. Mfano, hata kama unaangalia taarifa ya habari kwenye kituo flan cha television au redio, ni vigumu kuitazama yote katika shauku ileile mpaka taarifa yote iishe.
Nadhani, watangazaji wetu wa bongo, wanapaswa kuwa wabunifu katika vipindi vyao ili viweze kuvutia na kuwa vya kimataifa pia. Nakiri kuwa vipo vipindi vichache vizuri lakini vingi bado havikidhi haja ya kimataifa.
Ni mtazamo tu binafsi!
Nimegundua licha ya technolojia waliyonayo BBC, lakini ubunifu unahusika kwa kiwango kikubwa sana, kumfanya mtazamaji au msikilizaji aweze kuendelea kufatilia matangazo. Kwa watangazaji wa hapa bongo, ni vipindi vichache sana ambavyo unaweza kuvutika kiasi hicho. Mfano, hata kama unaangalia taarifa ya habari kwenye kituo flan cha television au redio, ni vigumu kuitazama yote katika shauku ileile mpaka taarifa yote iishe.
Nadhani, watangazaji wetu wa bongo, wanapaswa kuwa wabunifu katika vipindi vyao ili viweze kuvutia na kuwa vya kimataifa pia. Nakiri kuwa vipo vipindi vichache vizuri lakini vingi bado havikidhi haja ya kimataifa.
Ni mtazamo tu binafsi!