WAZIRI Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Ahmed Salim, amemmwagia sifa mgombea wa nafasi ya urais kupitia Chama Cha Mapinduzi, Dk. Jakaya Kikwete, kuwa ana nia ya dhati ya kuwatumikia wananchi huku akilinda misingi ya amani na utulivu.
Mbali na sifa hizo, pia alitumia nafasi hiyo kuwataka Watanzania kutafakari kwa makini wakati wa kupiga kura ili kuhakikisha wanachagua viongozi wanaotokana na CCM ambacho ndicho kimejenga misingi ya amani inayoleta sifa katika nchi za Afrika.
Dk. Salim aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kimanga Jimbo la Segerea. Jamani nimepata bahati ya kuzifahamu vizuri nchi za Afrika kutokana na nyadhifa nilizokuwa nazo, nimekuwa msuluhishi wa migogoro mingi ambayo imetokana na uvunjifu wa amani, tukianza Rwanda, (DRC) na kwingine maelfu ya wananchi wanapoteza maisha yao bila sababu ya msingi, hivyo tusibeze dhana ya utulivu na amani ni jambo la msingi sana, alisema Dk. Salim. Dk. Salim hakusita kumwelezea Rais Kikwete alivyo mvumilivu na kiongozi ambaye anapata sifa kubwa kimataifa kutokana na nia yake thabiti ya kuwatetea Watanzania kila mahali anapokuwa.
Source: Tanzania Daima
Mbali na sifa hizo, pia alitumia nafasi hiyo kuwataka Watanzania kutafakari kwa makini wakati wa kupiga kura ili kuhakikisha wanachagua viongozi wanaotokana na CCM ambacho ndicho kimejenga misingi ya amani inayoleta sifa katika nchi za Afrika.
Dk. Salim aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kimanga Jimbo la Segerea. Jamani nimepata bahati ya kuzifahamu vizuri nchi za Afrika kutokana na nyadhifa nilizokuwa nazo, nimekuwa msuluhishi wa migogoro mingi ambayo imetokana na uvunjifu wa amani, tukianza Rwanda, (DRC) na kwingine maelfu ya wananchi wanapoteza maisha yao bila sababu ya msingi, hivyo tusibeze dhana ya utulivu na amani ni jambo la msingi sana, alisema Dk. Salim. Dk. Salim hakusita kumwelezea Rais Kikwete alivyo mvumilivu na kiongozi ambaye anapata sifa kubwa kimataifa kutokana na nia yake thabiti ya kuwatetea Watanzania kila mahali anapokuwa.
Source: Tanzania Daima
JAMANI WAZEE WENGINE WANGEPUMZIKA TU SASA WATUACHIE WANANCHI TUFANYE MAAMUZI