Salim Ally tajiri Arusha anashangaza watanzania

Jethro

JF-Expert Member
Mar 23, 2009
2,220
370
Wana JF,

Jana katika kipindi cha njia panda - Radio Clouds FM kulikuwa na mjadala ambao ulianza tokea week iliyo pita kuhusu vijana wanao pelekwa nchi za kiarabu kufanya kazi na kujikuta kunyanyaswa na kupata mateso na kuwabidi kurudi tanzania kwa shida sana

Kwenda kwa hawa watu huko nchi za kiarabu kufanya kazi ni kutokana na kuitajika kwa wafanyakazi wa ndani na wahusika wakuu wa kuwapeleka watu au sie huku tunawaita madalali ni watanzania wenzetu wengine wana uwezo kabisa na matajiri mfano Salim ally tajiri mwenye majumba mengi hapo Arusha anahusika na sii tu kwa kupeleka wafanyakazi uarabuni bali hata kuwanyanyasa vibaruwa wake kwani twajua fika sasa kuwa Salim Ally hana mfanyakazi aliye ajiliwa wote ni vibarua na alisha waambia wafanyakazi wake kuwa waendekokote wakaseme kwani serikali hatomfanya kitu.

Salim Ally kwa sasa twajua yuko nje ya nchi pili nii kuwa anaanza kuyumba kiuchumi kwani kipindi Adv.Mwale kawekwa ndani nae alikuwa ndani kwa kesi ya kuzurumu wadhamini wake walio mfanya mpaka akafikia hapo alipo kimali na ni waitaliano ambao anataka kuwarusha mtambo wa kutengenezea ngozi za wanyama iliziweze kuzalisha ngozi ya kutengenezea viata na vitu vingine na kesi yake iko mahakamani.

Jana katika njia panda tulisikia watu wengi wakimsema salim ally kuwa anavibarua tu ambao wamefanya kazi zaidi ya miaka 5 bila ajira na anakesi Idara ya kazi ambayo mpaka sasa hajashughurikiwa, pia kuacha kazi kwake ni lazima tu akuzushia jambo yani mtaachana kwa fujo na si kwa aamani, salim ally huyo huyo anahusika na kuwapeleka watanzania uarabuni na kupata mateso na kuwatelekeza.

My Take;

Serikali yetu ndio chanzo kikubwa sana katka mambo kama haya yanapo tokea na hayafuatiliwi matajiri wengi wana kiuka sana sheria za nchi zilizopo na kuwa wahonga wafanyakazi wa hizi idara husika kama Idara ya kazi, Uhamiaji, Police hawa wote wamewekwa chini ya mikono ya hawa matajiri wasio thamini utu wa watanzania wenzao na kujifanya wao watoa misaaada sana kwa wanchi kumbe nyuma yake ni wanayama wa hali ya juu.

Serikali inapofika mahali inadhalauliwa na viongozi watendaji wake wapo makazini ni fedheha sana na aibu ni kudhihirisha kuwa serikali haipo, ni muda sasa serikali ijitambue kuwa wajibu wake ni kuwaongoza watanzania na sio kuwa beba matajiri.

Karibuni kuchangia hoja
 
Huyu ni Human Trafficker, apewe kesi hiyo ya human trafficking and enslavement. Serikali yetu vitu muhimu kama hivi inashindwa kabisa kuvifuatilia.
 
Huyu ni Human Trafficker, apewe kesi hiyo ya human trafficking and enslavement. Serikali yetu vitu muhimu kama hivi inashindwa kabisa kuvifuatilia.
Hao matajiri uchwara ndio wanaowalipa hao watumishi wa serikali wenye mishahara njiwa, unadhani watafuatlia kweli?
 
Salimu Ally ni mwarabu mwenye uraia wa Tanzania alianza kutajirika miaka ya 80s wakati huo akitumia ujanja ujanja wa fedha za kuhijji akiwapatia mahujaji fedha za kitanzania kwa ahadi ya kumwachia us dola kiasi fulani.Wakati huo hapakuwa na maduka ya kubadilisha fedha kama sasa.Kidogo akaingia biashara ya kuleta waarabu wenzake akawakamata maafisa uhamiaji kiasi kwamba kila afisa uhamiaji akitaka kufanya kazi Arusha.Maduka yote ya msikiti wa Bondeni yamejaa Waarabu,ukienda Soko kuu waarabu wamekamata maduka yote wote hawa wameletwa na Salimu Ally.

Wafanyakazi wake wote hajawapa ajira ya kudumu nawafahamu wafanyakazi wake wengine wamefanyakazi miaka 15 lakini bado wanatambuliwa kama vibarua hawana likizo,Hakuna michango ya NSSF,Hawana Overtime,hawana sikukuu isipokuwa Idd tu.
 
Haya yapo sehemu nyingi sana hapa bongo, makampuni mengi sana yanaandaa list fake za wafanyakazi afu wakaguzi wakienda wanaishia kwenye viyoyozi na kuhongwa, mwisho wa siku watz wanaendelea kukosa haki zao za msingi kwenye nchi yao. Mfano wa kiwanda kingine chenye vibarua wengi ni kiwanda cha Maji ya Africa kipo Kidamali wilaya ya Iringa vijijini. Kuna watu nawafahamu pale wamefanya kama vibarua tangu 1995 kiwanda kilipoanzishwa. Source ni mi mwenyewe naishi karibu na kiwanda na nimefanya kazi hapo kabla ya kwenda chuo.
 
Salim Ally alikuwa main sponsor wa Batilda Burian na huwa anachangia sana kampeni za CCM na huwa anakusanya michango kwa waarabu wenzie na kutoa ka mchango wao wa kampeni unafkiri sasa watamfanya nn? ndo maana huwa anadharau sana serikali na wafanyakazi wake
 
Salim Ally alikuwa main sponsor wa Batilda Burian na huwa anachangia sana kampeni za CCM na huwa anakusanya michango kwa waarabu wenzie na kutoa ka mchango wao wa kampeni unafkiri sasa watamfanya nn? ndo maana huwa anadharau sana serikali na wafanyakazi wake

Hapo ndipo Serikali yetu na viongozi wengi wa CCM wanashindwa kutambua nini maana ya uwajibikaji na kulitumikia Taifa wao ni kukalia maslahi yao wanawasahau wapiga kura wao wengi na kujari maslahi ya mmoja mmoja na ni matajiri tu na Batilda kilicho mpoza kwenye uchaguzi huko arusha ni kuwa na vikao vya mitengano matajiri kwa matajiri maskinini kwa maskini ambao ndio walikuwa wapiga kura wengi CCM kwa CCM ndio fika kabisa hao walikuwa hawapatani wao kwa wao esp UVCCM karibia nchi nzima esp Arusha ndiko kulikuwa kwafukuta sana.

Sasa katika hali hii Tajiri kama Salim Ally wategemea nini kama anadiliki kuwaambia vibarua wake nendeni mkashitaki kokote sikamatwi hii ni dhihaka na sishangai serikali na watendaji wake kuwa mabubu kwani Salim Ally alikuwa mfadhiri mkubwa wao katika kampeni za CCM.

Salim ally sasa anaanza kufirisika mtamsikia nawapeni good 2yrs mtaniambia watu wa huko Arusha alivyo wazurumu hao waitaliano wadhani wata mwachia wataahakikisha wana mweka chini na ndio walikuwa wafashili wake walio mnyanyua kiuchumi leo anataka kuwazurumu mitambo na pesa inakula kwake.

My Take;
Serikali yetu imekuwa kama jibwa koko kweli jamani hivi hizi tuhuma zote kama zilivyokuwa zikisemwa kwa radio clouds FM wanashindwa hata kumuuliza huyo jamaa na kufanya upelelezi au upelelezi wa askali wetu ni pale wakisikia maandamano ndipo utasikia kuna tatizo la kiusalama??

Matajiri wameiteka nchi hii pindi itakapo fikia pabaya haya yote tunayo yasema viongozi wajao watakuja yasema kuwa wananchi walilalamika sana viongozi waliokuwepo walipuuzi na itakuwa ni historia na kubakia ningejua maana huna neno hilo huja baaaada ya jambo kutendeka au kupita na kujutia
 
Salimu Ally ni mwarabu mwenye uraia wa Tanzania alianza kutajirika miaka ya 80s wakati huo akitumia ujanja ujanja wa fedha za kuhijji akiwapatia mahujaji fedha za kitanzania kwa ahadi ya kumwachia us dola kiasi fulani.Wakati huo hapakuwa na maduka ya kubadilisha fedha kama sasa.Kidogo akaingia biashara ya kuleta waarabu wenzake akawakamata maafisa uhamiaji kiasi kwamba kila afisa uhamiaji akitaka kufanya kazi Arusha.Maduka yote ya msikiti wa Bondeni yamejaa Waarabu,ukienda Soko kuu waarabu wamekamata maduka yote wote hawa wameletwa na Salimu Ally.

Wafanyakazi wake wote hajawapa ajira ya kudumu nawafahamu wafanyakazi wake wengine wamefanyakazi miaka 15 lakini bado wanatambuliwa kama vibarua hawana likizo,Hakuna michango ya NSSF,Hawana Overtime,hawana sikukuu isipokuwa Idd tu.

Swala la michango ya kwenda NSSF asilimia karibia 70% ya matajiri wetu hapa nchini huwa wana chakachua michango NSSF na viongozi wa NSSF hawafuatiliii chochote kuhusi hilo wanakalia kusema ukisikia njoo toa taarifa ukitoa taarifa tu huyo boss wa NSSF anakuwa mbea wa kwanza kumpigia simu huyo tajiri na wana fiksi mambo na unafukuzwa kazi au kuuwawa leo hii wanajiita ati watendaji kweli katika hii hali tutatoka kweli?

My Take;

NSSF inauliwa na Matajiri na viongozi walio pewa dhamana ya kuiongoza NSSF kwani wao wanajua fika michezo michafu yote inayochezwa na waajiri. eg Mtu anandikiwa kwa NSSF kuwa analipwa 300,000/=Tsh ikiwa na maana Boss anakutolea 15000/=Tsh na wewe ulieajiriwa unachangia 15000/=Tsh mchango kwenda kwa mfuko wa NSSF kwa account ya wewe uliyeajiriwa, lakini the relly picture ni kuwa aliye ajiriwa anapokea 600,000/=Tsh Take Home. Hapo kuna mchezo wa ajabu sana unao chezwa na NSSF hao hao wanaridia hayo mambo kweli nchi hii itasonga kweli kweli haki ya mtu inadhurumiwa na serikali inaona wazi sasa ndio hayo ya kina Salim Ally haya mamabo yapo na serikali inaya puuzia this is fact kabisa.
 
Nchi imeoza hii, wezi wa kuku ndio wanafungwa na kuozea jela, si umeona ile kesi ya yule jamaa aliyekufa kigamboni walivyo iua juu kwa juu..HATUNA VIONGozi.
 
Inasikitisha sana kiubinadamu/maadili lakini kumbukeni sheria mpya ya kazi iliyopitishwa na bunge letu haina AJIRA YA KUDUMU WALA KIBARUA IMEELEZA WAZI KUWA NI MKATABA TU na haki zote stahili ni lazima nssf, likizo,n.k. kwa maana hiyo hakuna tofauti ya kibarua na mtumishi wa muda mrefu....
 
Haya yapo sehemu nyingi sana hapa bongo, makampuni mengi sana yanaandaa list fake za wafanyakazi afu wakaguzi wakienda wanaishia kwenye viyoyozi na kuhongwa, mwisho wa siku watz wanaendelea kukosa haki zao za msingi kwenye nchi yao. Mfano wa kiwanda kingine chenye vibarua wengi ni kiwanda cha Maji ya Africa kipo Kidamali wilaya ya Iringa vijijini. Kuna watu nawafahamu pale wamefanya kama vibarua tangu 1995 kiwanda kilipoanzishwa. Source ni mi mwenyewe naishi karibu na kiwanda na nimefanya kazi hapo kabla ya kwenda chuo.

Haya yote yanatokana na kuota mizizi kwa rushwa katika utumishi wa umma. Serikali inaponunuliwa na matajiri ujue utawala wa sheria hutoweka kabisa. Utashangaa suala hili walinda sheria watakuwa wanalifahamu lakini hakuna hatua yoyote ambayo imeshachukuliwa. Mabadiliko makubwa yanahitajika ili kubadilisha mwelekeo wa mambo.
 
,

Jana katika kipindi cha njia panda - Radio Clouds FM kulikuwa na mjadala ambao ulianza tokea week iliyo pita kuhusu vijana wanao pelekwa nchi za kiarabu kufanya kazi na kujikuta kunyanyaswa na kupata mateso na kuwabidi kurudi tanzania kwa shida sana

Kwenda kwa hawa watu huko nchi za kiarabu kufanya kazi ni kutokana na kuitajika kwa wafanyakazi wa ndani na wahusika wakuu wa kuwapeleka watu au sie huku tunawaita madalali ni watanzania wenzetu wengine wana uwezo kabisa na matajiri mfano Salim ally tajiri mwenye majumba mengi hapo Arusha anahusika na sii tu kwa kupeleka wafanyakazi uarabuni bali hata kuwanyanyasa vibaruwa wake kwani twajua fika sasa kuwa Salim Ally hana mfanyakazi aliye ajiliwa wote ni vibarua na alisha waambia wafanyakazi wake kuwa waendekokote wakaseme kwani serikali hatomfanya kitu.

Salim Ally kwa sasa twajua yuko nje ya nchi pili nii kuwa anaanza kuyumba kiuchumi kwani kipindi Adv.Mwale kawekwa ndani nae alikuwa ndani kwa kesi ya kuzurumu wadhamini wake walio mfanya mpaka akafikia hapo alipo kimali na ni waitaliano ambao anataka kuwarusha mtambo wa kutengenezea ngozi za wanyama iliziweze kuzalisha ngozi ya kutengenezea viata na vitu vingine na kesi yake iko mahakamani.

Jana katika njia panda tulisikia watu wengi wakimsema salim ally kuwa anavibarua tu ambao wamefanya kazi zaidi ya miaka 5 bila ajira na anakesi Idara ya kazi ambayo mpaka sasa hajashughurikiwa, pia kuacha kazi kwake ni lazima tu akuzushia jambo yani mtaachana kwa fujo na si kwa aamani, salim ally huyo huyo anahusika na kuwapeleka watanzania uarabuni na kupata mateso na kuwatelekeza.

My Take;

Serikali yetu ndio chanzo kikubwa sana katka mambo kama haya yanapo tokea na hayafuatiliwi matajiri wengi wana kiuka sana sheria za nchi zilizopo na kuwa wahonga wafanyakazi wa hizi idara husika kama Idara ya kazi, Uhamiaji, Police hawa wote wamewekwa chini ya mikono ya hawa matajiri wasio thamini utu wa watanzania wenzao na kujifanya wao watoa misaaada sana kwa wanchi kumbe nyuma yake ni wanayama wa hali ya juu.

Serikali inapofika mahali inadhalauliwa na viongozi watendaji wake wapo makazini ni fedheha sana na aibu ni kudhihirisha kuwa serikali haipo, ni muda sasa serikali ijitambue kuwa wajibu wake ni kuwaongoza watanzania na sio kuwa beba matajiri.
 
Kaka................... Huyo cha mtoto,
huku musoma kuna tajiri anaua mpaka mchana, kundi lake linaitwa sitaki lawama wanakuuua na polisi hawafikishwi. Rpc anamjua na hata kamanda mwema namjua. Hata mzee wa kaya anamjua..... Huyu bwana ni untouchable aisee
 
saa mwalalamika nn watanzania kuweni wazalendo mkiona vyombo vya dola haviwasikizi
na jitihada za sheria kuchukua mkondo zikishindikana tumieni sheria zenu za asili nadhani
mmnenipata.kuna wajuzi wa ungo wa kuruka usiku wafanye kazi yao akiamka mara 2 akiwa amelala nje
na huku kanyolewa kila seheumu atakimbia nchi fasta na ataacha kila kitu. kazi kwenu Musoma inakuwaje bwana tunawaaminia kwa uajsiri
fanyeni kazi yenu.
 
huyo ni sehemu tu ya wanaoitwa watanzania wenye asili ya kiarabu.ipo kampuni ya kasco construction mambo ni hayo hayo.kimsingi Tanzania hakuna serikali makini wote corupt kuanzia mwenyekiti wa mtaa mpaka ikulu
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom